g vizy
JF-Expert Member
- Jan 5, 2016
- 896
- 977
Habari wakuu poleni na majukumu mbalimbali ya Kila siku
Mama yanguamekumbwa na tatizo ambalo hata sisi binafsi kama watoto wake tumeshindwa kumuelewa
Labda nianze Kwa kusema mama ni mwathirika wa virusi vya ukimwi Kwa Muda mrefu na amekua akitumia vidonge vya ARVS Kwa Muda mrefu sana. kipindi cha nyuma tulikua tukiishi nae vizuri tu tukiwa wote nyumbani kabla ya sisi watoto wake kutawanyika Kila mmoja kuishi katika mji wake na familia yake (baba yetu alifariki Muda mrefu sana tangu mwaka 1994)
Sasa mnamo mwaka 2018 baada ya sisi watoto kutawanyika nyumbani tulimwacha mwenyewe pale nyumbani na ikawa tunamuhudumia Kwa matumizi ya hapa na pale,ilipofika mwezi wa 11 kuelekea mwezi wa 12 mwaka huo ndipo tatizo hili lilipoanza
Akawa anatuambia wanangu hapa nyumbani naona Kuna watu wanakuja wananifatilia wanataka kuniua Mimi siwaelewi tukawa tuna muuliza ni watu gani hao mbona sisi wakati tunaishi hapo hatukuwai kuwa na tatizo na mtu,akazidi kusisitiza kwamba Mimi siwezi kuendelea kuishi hapa naomba mje mnichukue
Basi dada yetu mkubwa ikabidi apange safari aende akamchukue mana yeye ndiye anaeishi nae karibu zaidi kuliko sisi wengine mana tupo mikoa ya mbali, baada ya kumchukua na kuanza kuishi nae lile tatizo likawa kama limemtoka la kuhisi watu wanamfatilia wanataka wamuue.... Bas ikaenda Kwa Muda kama wa mwaka mmoja hivi akadai anataka aende kijijini kukaa Kwa madai yake kwamba anataka kubadilisha mazingira haikua tatizo
Tukampeleka Kwa mama yetu mdogo nae alisema ngoja nijaribu kuishi nae mana mama mdogo ni mtu wa maombi sana kanisani masaa 24
Yaan tulivyompeleka kule ndo kama tukawa tumeongeza tatizo ikawa Kila Muda tunaambiwa kwamba mama yenu anataka kujinyonga ety amechoka kuishi anaona Kila mtu mbaya kwake Hana Nia njema juu yake ikawa ni kulalamika Kila Leo kwamba mama yenu mdogo ananichukia,mara watoto wake hawanieshimu yaani ikawa taflani
Mpaka kufikia hatua mamdogo kusema mje mumchukue mama yenu Mimi amenishinda inafikia hatua anataka ajinyongee nyumbani kwangu tena mbele ya watoto wangu Mimi Kwa kweli hapana
Dada ikabidi aende akamchukue amrudishe tena nyumbani kwake mana ni mama yetu hatuna namna inabidi tuishi nae hvyo hvyo
Sasa baada ya kumrudisha yaan ndo kama tatizo limezidi kua kubwa zaidi mpaka dada nae ameanza kuhofia juu ya uhai wake mana amekua ni mtu wa kulaumu Kila mtu hamna mtu anaefanya jema kwake imefikia hatua anadai sisi tunapanga njama za kumuua kwanza hatumthamini kitu ambacho sio kweli mbaya zaidi anadai Mimi Bora nife tu Sina nilichobakiza Dunian,wakati mwingine anaongea vitu havieleweki,avielezeki yaan
Amekua ni mtu wa kuwaza tuuuu Muda wote Yani halali usingizi,ni kama mtu mwenye uwoga
Muda mwingine anatukana mpaka watoto wa dada kwamba nao Wana njama za kutaka kumuua,Sasa unajiulizan watoto wadogo hawa akili ya namna hiyo waitolee wapi
Kifupi ni kama mtu aliyechanganyikiwa,analaumu Kila anaemuona mbele yake kwamba ni sababu ya yeye kua hivyo.
Sasa wakuu hii tatizo linaniumiza sana kichwa changu sijui tunafanyaje kutibu hili tatizo.mana kama ni kuombewa ameshaombewa sana tu tangu kule Kwa mamdogo lakini wapi Mambo yamekua magumu
Najiuliza uenda ni issue ya phycology tumtafutie wanasaikolojia wakae nae wazungumze nae sisi tulishaongea nae mara nyingi sana hamna kitu tumeambulia
Sasa ndugu zangu nimeleta kwenu mnishauri nifanyaje kutibu tatizo halilonalo mama angu
Sipendi awe kwenye hali hii inatuchanganya familia nzima hatuelewi la kufanya we are so confused Kwa kweli
Natanguliza shukrani wakuu
Mama yanguamekumbwa na tatizo ambalo hata sisi binafsi kama watoto wake tumeshindwa kumuelewa
Labda nianze Kwa kusema mama ni mwathirika wa virusi vya ukimwi Kwa Muda mrefu na amekua akitumia vidonge vya ARVS Kwa Muda mrefu sana. kipindi cha nyuma tulikua tukiishi nae vizuri tu tukiwa wote nyumbani kabla ya sisi watoto wake kutawanyika Kila mmoja kuishi katika mji wake na familia yake (baba yetu alifariki Muda mrefu sana tangu mwaka 1994)
Sasa mnamo mwaka 2018 baada ya sisi watoto kutawanyika nyumbani tulimwacha mwenyewe pale nyumbani na ikawa tunamuhudumia Kwa matumizi ya hapa na pale,ilipofika mwezi wa 11 kuelekea mwezi wa 12 mwaka huo ndipo tatizo hili lilipoanza
Akawa anatuambia wanangu hapa nyumbani naona Kuna watu wanakuja wananifatilia wanataka kuniua Mimi siwaelewi tukawa tuna muuliza ni watu gani hao mbona sisi wakati tunaishi hapo hatukuwai kuwa na tatizo na mtu,akazidi kusisitiza kwamba Mimi siwezi kuendelea kuishi hapa naomba mje mnichukue
Basi dada yetu mkubwa ikabidi apange safari aende akamchukue mana yeye ndiye anaeishi nae karibu zaidi kuliko sisi wengine mana tupo mikoa ya mbali, baada ya kumchukua na kuanza kuishi nae lile tatizo likawa kama limemtoka la kuhisi watu wanamfatilia wanataka wamuue.... Bas ikaenda Kwa Muda kama wa mwaka mmoja hivi akadai anataka aende kijijini kukaa Kwa madai yake kwamba anataka kubadilisha mazingira haikua tatizo
Tukampeleka Kwa mama yetu mdogo nae alisema ngoja nijaribu kuishi nae mana mama mdogo ni mtu wa maombi sana kanisani masaa 24
Yaan tulivyompeleka kule ndo kama tukawa tumeongeza tatizo ikawa Kila Muda tunaambiwa kwamba mama yenu anataka kujinyonga ety amechoka kuishi anaona Kila mtu mbaya kwake Hana Nia njema juu yake ikawa ni kulalamika Kila Leo kwamba mama yenu mdogo ananichukia,mara watoto wake hawanieshimu yaani ikawa taflani
Mpaka kufikia hatua mamdogo kusema mje mumchukue mama yenu Mimi amenishinda inafikia hatua anataka ajinyongee nyumbani kwangu tena mbele ya watoto wangu Mimi Kwa kweli hapana
Dada ikabidi aende akamchukue amrudishe tena nyumbani kwake mana ni mama yetu hatuna namna inabidi tuishi nae hvyo hvyo
Sasa baada ya kumrudisha yaan ndo kama tatizo limezidi kua kubwa zaidi mpaka dada nae ameanza kuhofia juu ya uhai wake mana amekua ni mtu wa kulaumu Kila mtu hamna mtu anaefanya jema kwake imefikia hatua anadai sisi tunapanga njama za kumuua kwanza hatumthamini kitu ambacho sio kweli mbaya zaidi anadai Mimi Bora nife tu Sina nilichobakiza Dunian,wakati mwingine anaongea vitu havieleweki,avielezeki yaan
Amekua ni mtu wa kuwaza tuuuu Muda wote Yani halali usingizi,ni kama mtu mwenye uwoga
Muda mwingine anatukana mpaka watoto wa dada kwamba nao Wana njama za kutaka kumuua,Sasa unajiulizan watoto wadogo hawa akili ya namna hiyo waitolee wapi
Kifupi ni kama mtu aliyechanganyikiwa,analaumu Kila anaemuona mbele yake kwamba ni sababu ya yeye kua hivyo.
Sasa wakuu hii tatizo linaniumiza sana kichwa changu sijui tunafanyaje kutibu hili tatizo.mana kama ni kuombewa ameshaombewa sana tu tangu kule Kwa mamdogo lakini wapi Mambo yamekua magumu
Najiuliza uenda ni issue ya phycology tumtafutie wanasaikolojia wakae nae wazungumze nae sisi tulishaongea nae mara nyingi sana hamna kitu tumeambulia
Sasa ndugu zangu nimeleta kwenu mnishauri nifanyaje kutibu tatizo halilonalo mama angu
Sipendi awe kwenye hali hii inatuchanganya familia nzima hatuelewi la kufanya we are so confused Kwa kweli
Natanguliza shukrani wakuu