Kaka naomba nikuambie kitu hapa
Kuna watu wanakushauri vema lakini wanaongeza na Bias zao lakini ukweli ni huu:
Kwanza nimeona mdau mmoja amekuambia kuwa TPDC wapo lumumba, hapana. Interview mnafanyiwa Ofisi za Mikocheni karibu na ROSE GARDEN (ULIZA BRAJEC) Kwenye makazi ya Watumishi wa TPDC mule ndani kuna Ofisi. Mimi nimefanya hapo interview.
Pili suala la kwenda wapi, yote yapo ndani ya uwezo wako. Hiyo saa 6 mchana si kwamba ndio utaitwa kuna karatasi utaandika na baadae wanafanya logistics zao ndipo wanaanza kuita mmoja mmoja. Nakumbuka niliitwa saa 2 asubuhi lakini nilifanyiwa interview saa 10 jioni (Japo si lazima iwe kwako)
Tatu. TANESCO hapa naomba niongee kwa uzoefu wangu na ninavyowafahamu kwa ukaribu. TANESCO KUMETAWALIWA NA UJAMAA WA KUTOSHA. Si kwa wote bali kwa kiasi kikubwa sana. Nina ushahidi wa wazi wazi. Nilifanya usahili na mmoja wa watoto wa wakuu wa bodi ya tanesco na ninamfahamu vema na hata nafasi aliyoitwa hafai hata kwa vigezo (narudia namfahamu huyo mtu) Hatima yake yeye aliitwa na yupo kazini hata sasa YAANI TANESCO = UHAMIAJI. Japo napenda kukutia moyo kuwa Mungu yupo na alitakalo huwa hata kama watafanya njama gani
Nne. TPDC wako fare kuliko wadau wanavyowadhania. Namna wanavyoendesha usahili. Usitegemee kukaa ndani ya chumba cha usahili Dk. ishirini, zikizidi sana ni dakika 6 mpaka kumi. Wapo specific sana
Nikutakie kila la kheri Mungu akipenda tutakutana kazini. Usiogope