witnessj
JF-Expert Member
- Mar 22, 2015
- 28,710
- 47,099
Hii ndo point sasaKaombe kazi za chapu chapu sehemu kama ukuli, kumenya chipsi, deiwaka saloon, kusaidia fundi ujenzi, deiwaka boda boda au bajaji, nenda minadani muuzie mtu vitu vyake kama mitumba, vyombo, mazao halafu kamisheni atakulipa huku unaweka akili yako sawa.
Usiuze kiwanja, anza kujengea mabati kama mdau alivyo sema hapo.
Adui yako mkubwa ni status quo, ngoja nikwambie ukweli sisi binadamu tulikuja uchi na tutaondoka bila chochote, usijionee aibu uko uchi tayari usiangalie kushoto wala kulia pambana kianaume, acha wakuseme wala hutomeguka.