Msaada: Nifanye biashara gani kukuza mtaji wangu? Nipo Chunya Makongorosi

Yohimbe bark

JF-Expert Member
Sep 1, 2019
1,050
2,581
Habari wakuu, ni week sasa nipo chunya makongolosi kuchungulia fursa.

Kipindi natoka mbeya kuja huku nilipanda gari moja na mdada mmoja tulikaa seat za upande mmoja nikaanza kumdadisi anafanya shughuli gani huku Makongolosi akaniambia hua anaenda Soko la Mwanjelwa (anajumua) ndio lugha wanatumia akimaanisha anatafuta vipochi vya mitumba vya elfu 5&7 then analeta huku Makongolosi anauza kwa elfu 10 mpaka 15 kwa kuzungusha mtaani.

Nikamuomba aniongoze na mimi nifanye hiyo biashara nikiendelea kuzoea mazingira, dada wa watu hakua na shida akakubali so tukaweka appointment ya juzi tukutane town twende tukanunue mzigo.

Kweli siku ikawadia tukakutana nikanunua mzigo wa laki moja vipochi kama 16 hivi vya elfu 5 na elfu 7 na yeye akachukua mzigo wake safari ikaanza kwenda Makongolosi kuuza.

Aisee, tumefika kila mtu akabeba mzigo wake, tukaanza kukatiza mitaani huku namfata nyuma, mind you tulianza kuzunguka mida ya saa 7 mchana lakini mpaka saa moja usiku nilikua nimeuza vipochi viwili tuu tena kwa elfu 8000 each.

Yeye mwenyewe biashara haikua nzuri, dah nilikua nimechoka balaa yani kule kuna jua na vumbi balaa ikabidi tulale huku huku ili leo tukimbize tena, ila mpaka sasa bila bila mpaka nimechoka hapa nimekaa sehem nimepimzika nawaza tuu.

Wakuu naombeni ushauri nifanye biashara gani kwa huku ili nikuze mtaji? Lengo langu ni kufanya biashara Zambia huku nipo kukuza mtaji tuu hela iliyobaki ni 1M tuu balance.

Je, kwa mtaji huu naweza kununua dhahabu kidogo kidogo nikuze mtaji? Au nifanye nini ili mtaji ukue at least nipate profit ya 20k per day, najua biashara ni uvumilivu ila hii hapana nipo ready kufanya biashara nyingine ila hii imenishinda wakuu.

Kuna watu walinipa muongozo wa kufika huku Mungu awabariki sana na kuna wengine walinifata DM kupata abc za huku msihofu mje mjaribu na nyie penye watu hela ipo msiogope karibuni.

Mtanisamehe kwa kuandika bila kutumia paragraph coz am totally confused naombeni ushauri wakuu.
 
Biashara haiendi ivo. Yaani umekutana na mtu kwenye gari masaa kadhaa umeshaamua kufanya biashara anayofanya yeye.

Kwa ufupi haukufanya research.

Jipe muda, fanya kwanza research ujue biashara unayoshauriwa, tafuta changamoto zake, hafu kua mvumilivu. Kwa maana biashara ya pochi siku 2 tu umeanza lalamika.

Cha kufanya, pokea ushauri wa wadau, angalia mazingira, fanya research ata ya week moja.

Ila iyo biashara ya madini ACHA.
 
Biashara haiendi ivo. Yaani umekutana na mtu kwenye gari masaa kadhaa umeshaamua kufanya biashara anayofanya yeye.

Kwa ufupi haukufanya research.

Jipe muda, fanya kwanza research ujue biashara unayoshauriwa, tafuta changamoto zake, hafu kua mvumilivu. Kwa maana biashara ya pochi siku 2 tu umeanza lalamika.

Cha kufanya, pokea ushauri wa wadau, angalia mazingira, fanya research ata ya week moja.

Ila iyo biashara ya madini ACHA.

Shukrani mkuu.
 
Kununua dhahabu inatosha lakini kama dhahabu huzijui utapigwa ndani siku moja. So kama vipi ingia machimbo ungana na buyo demu wauzie supu ya mbuzi na chapati unaweza usiende zambia komaa mzee.
ume give up on the second day? kaza upige ata wiki chunya pesa ipo pia biashara ya chakula uhakika sana huko
Mkuu Yohimbe bark ukifungua kijiwe cha supu ya mbuzi na chapati ukawa serious unaweza toboa.

Ebu fanya research, ona wanaoendesha biashara ya chakula wapoje. Wewe jishikirie kwenye small "niche" ya chapati na supu ya mbuzi mdogo mdogo unakuja kwenye chips, nyama choma, ugali etc.

Tumesema chapati na supu kwasababu inahitaji vitu vichache vya kuanzia. Sio kama chips.

Ila nakukumbusha, research kwanza.
 
Sina lengo la kukuvunja moyo ila kufanya biashara Chunya sio kazi rahisi hata kidogo.

Tena biashara ya aina hiyo kama nguo ndio usiseme.

Kuna rafiki yangu alikuwa anasoma chuo pale MUST, akafanikiwa kupata rafiki ambaye ni mkazi wa DSM

Yule jamaa wa DSM aliporudi home likizo akakusanya mitumba mingi akaja nayo pale Mbeya.

Jamaa yangu akamshauri kuwa hii mitumba ipeleke Chunya kule utauza.

Matokeo yalikuja kama yako, ila ye alichokifanya aligawa zile nguo.

Biashara ambayo Chunya unaweza kuwa na hakika nayo we fungua Grocery jaza miponbe mikali halafu weka mademu warembo hapo utawashika.

Ila nguo nguo hizi vijana wala hata hawashoboki.
 
Habari wakuu, ni week sasa nipo chunya makongolosi kuchungulia fursa kipindi natoka mbeya kuja huku nilipanda gari moja na mdada mmoja tulikaa seat za upande mmoja nikaanza kumdadisi anafanya shughuli gani huku makongolosi akaniambia hua anaenda soko la mwanjelwa (anajumua) ndio lugha wanatumia akimaanisha anatafuta vipochi vya mitumba vya elfu 5&7 then analeta huku makongolosi anauza kwa elfu 10 mpaka 15 kwa kuzungusha mtaani nikamuomba aniongoze na mimi nifanye hiyo biashara nikiendelea kuzoea mazingira dada wa watu hakua na shida akakubali so tukaweka appointment ya juzi tukutane town twende tukanunue mzigo kweli siku ikawadia tukakutana nikanunua mzigo wa laki moja vipochi kama 16 hivi vya elfu 5 na elfu 7 nayeye akachukua mzigo wake safari ikaanza kwenda makongolosi kuuza aisee tumefika kila mtu akabeba mzigo wake tukaanza kukatiza mitaani huku namfata nyuma, mind you tulianza kuzunguka mida ya saa 7 mchana lakini mpaka saa moja usiku nilikua nimeuza vipochi viwili tuu tena kwa elfu 8000 per each yeye mwenyewe biashara haikua nzuri dah nilikua nimechoka balaa yani kule kuna jua na vumbi balaa ikabidi tulale huku huku ili leo tukimbize tena ila mpaka sasa bila bila mpaka nimechoka hapa nimekaa sehem nimepimzika nawaza tuu. Wakuu naombeni ushauri nifanye biashara gani kwa huku ili nikuze mtaji? lengo langu ni kufanya biashara zambia huku nipo kukuza mtaji tuu hela iliyobaki ni 1M tuu balance je kwa mtaji huu naweza kununua dhahabu kidogo kidogo nikuze mtaji? au nifanye nini ili mtaji ukue at least nipate profit ya 20k per day, najua biashara ni uvumilivu ila hii hapana nipo ready kufanya biashara nyingine ila hii imenishinda wakuu. Kuna watu walinipa muongozo wa kufika huku Mungu awabariki sana na kuna wengine walinifata DM kupata abc za huku msihofu mje mjaribu na nyie penye watu hela ipo msiogope karibuni. Mtanisamehe kwa kuandika bila kutumia paragraph coz am totally confused naombeni ushauri wakuu.
Pole sana .
Kumbe safari yako ya Tunduma to Chunya ndiyo imekufikisha kwenye vipochi ?

Umekurupuka bwana mdogo , mambo hayaendi hivyo yaani mtu akupe story za biashara anayofanya na wewe bichwa bichwa mpaka kufanya hiyo biashara serious ? Usirudie mdogo wetu .

Basi sasa uko Chunya ila naona kuwa pamekushinda kwa maelezo yako na sitakuwa na dhambi kukueleza kuwa hata huko Tunduma ni kama palikushinda ukapakimbia kijanja sivyo ?

Basi pole sana mdogo wangu , tafuta sehemu kula ushibe , then kunywa na maji mengi ukimaliza tafuta sehemu ya kulala , jitulize alafu asubuhi ingia mtaani Chunya utapata sehemu ya kujiweka .

Mind you , usiwe karibu na wageni wa kule kuwa karibu na wenyeji maana chunya inabeba watu wengi
 
Mkuu Yohimbe bark ukifungua kijiwe cha supu ya mbuzi na chapati ukawa serious unaweza toboa.

Ebu fanya research, ona wanaoendesha biashara ya chakula wapoje. Wewe jishikirie kwenye small "niche" ya chapati na supu ya mbuzi mdogo mdogo unakuja kwenye chips, nyama choma, ugali etc.

Tumesema chapati na supu kwasababu inahitaji vitu vichache vya kuanzia. Sio kama chips.

Ila nakukumbusha, research kwanza.

Nifungulie hapa makongolosi center au nifungulie kule machimboni?
 
Pole sana .
Kumbe safari yako ya Tunduma to Chunya ndiyo imekufikisha kwenye vipochi ?

Umekurupuka bwana mdogo , mambo hayaendi hivyo yaani mtu akupe story za biashara anayofanya na wewe bichwa bichwa mpaka kufanya hiyo biashara serious ? Usirudie mdogo wetu .

Basi sasa uko Chunya ila naona kuwa pamekushinda kwa maelezo yako na sitakuwa na dhambi kukueleza kuwa hata huko Tunduma ni kama palikushinda ukapakimbia kijanja sivyo ?

Basi pole sana mdogo wangu , tafuta sehemu kula ushibe , then kunywa na maji mengi ukimaliza tafuta sehemu ya kulala , jitulize alafu asubuhi ingia mtaani Chunya utapata sehemu ya kujiweka .

Mind you , usiwe karibu na wageni wa kule kuwa karibu na wenyeji maana chunya inabeba watu wengi

Shukrani mkuu barikiwa.
 
Nifungulie hapa makongolosi center au nifungulie kule machimboni?
Dah mi sio mwenyeji. Ebu angalia wewe fanya research ila nahisi Machimboni ndio kutakua na vibe la watu. Ebu jaribu kutafuta kama siku mbili tatu za kuzunguka.

Kua unique, kua msafi eneo lako la kazi, bei andika kabisa na unaweza weka ata offa mfano chapati 3 kwa supu bure (supu bila nyama, yaan mchuzi).
 
Sina lengo la kukuvunja moyo ila kufanya biashara Chunya sio kazi rahisi hata kidogo.

Tena biashara ya aina hiyo kama nguo ndio usiseme.

Kuna rafiki yangu alikuwa anasoma chuo pale MUST, akafanikiwa kupata rafiki ambaye ni mkazi wa DSM

Yule jamaa wa DSM aliporudi home likizo akakusanya mitumba mingi akaja nayo pale Mbeya.

Jamaa yangu akamshauri kuwa hii mitumba ipeleke Chunya kule utauza.

Matokeo yalikuja kama yako, ila ye alichokifanya aligawa zile nguo.

Biashara ambayo Chunya unaweza kuwa na hakika nayo we fungua Grocery jaza miponbe mikali halafu weka mademu warembo hapo utawashika.

Ila nguo nguo hizi vijana wala hata hawashoboki.
Uko sahihi mkuu. Ila hapo kwenye grocery nawaza kaa budget yake itaweza?
 
Biashara ambayo Chunya unaweza kuwa na hakika nayo we fungua Grocery jaza miponbe mikali halafu weka mademu warembo hapo utawashika.
Hapa umenena kwenye migodi peleka pombe kali

Au jenga lodge fungua danguro, malaya wawe wanakulipa kwa siku chumba atakachotumia

Mitumba inalipa Mbeya mjini tu tena uwe na location nzuri

Maeneo ya migodi biashara za dhambi dhambi ndio huwa zinalipa
 
Back
Top Bottom