Ushauri, natokaje hapa?

Ncha Kali

JF-Expert Member
Sep 19, 2019
14,523
27,021
Wakuu, yamenifika hapa

Nimekuwa nikiishi na binti wa watu kinyemela kwa takribani miezi MINNE sasa. Tulianza kama masikhara, mwisho nikamruhusu ahamie ili nijihakikishie tunda kila nikiwa na KIU.

Stori iko hivi:

Nilikutana na binti ambaye yupo kwenye kupambana aanze maisha. Alikuwa akiishi kwa dada’ke kipindi hicho. Katika stori za hapa na pale, binti akagusia hitaji lake la kujitegemea kimaisha. Japo kwa chumba kimoja tu, ili aondokane na kuishi kwa dada (shemeji).

Kumuuliza mipango yake ipoje, kasema anahitaji kiasi cha kodi tu. Na itamchukua miezi MITATU ikiwa ataitafuta kupitia kazi anayofanya.

Wakati huo tulishawahi kujadili lengo lake la kuanzisha ofisi yake ili tu awe na kazi yake. Hapa aliomba 'sapoti' yangu na nilimuahidi.

Basi bwana! Nikaona kitonga si hii, nikamwambia ahamie kwangu ili tuishi kwa hiyo miezi MITATU huku akijiandaa kupanga. Maaweee! Mtoto bila hiyana akafungasha, kaaga kwa dada’ke ya kuwa amepata chumba anahamia. Kapewa jiko dogo la gesi, na beseni kama zawadi ya kuanzia maisha. Huyu hapa.

Basi maisha yakaanza, yakasonga. Ahadi yangu nikatimiza akafungua ofisi yake, ikawa sasa kila anachopata anaboresha ofisi yake. Siku nikigusia kuhusu maandalizi yake ya kupanga anakuwa mkali balaa, nimvumilie hajaanza kupata faida, nikisema nimlipie kodi utasikia ooh nimemchoka nataka kuleta MKE mwingine!

Kumbe mwenzangu alisha-update STATUS, alishakuwa MKE tayari. Mwanzo nikadhani utani, siku zinasonga AKILI inazidi kunirudi.[emoji15. Sasa nawaza namna gani ya kuondokana naye kwa amani, sitaki kuoa wala sitaki kumuumiza kwa kumpotezea muda. Ingawa kwa hili labda aamue tu kunigeuka.

Hakuna namna ataweza kunishawishi kwenye mtazamo wangu juu ndoa, na hata msimamo wangu juu yake nilimweka wazi tangu mwanzo.

Jibu lake lilikuwa kama langu, kwamba hata yeye hahitaji kuolewa saivi anatafuta MAISHA kwanza. Ni wasiwasi wangu tu, naishije na mtu kinyemela muda wote huu. Japo hatuombei ya kutokea, God forbid!

Naombeni ushauri wenu ndugu zangu, hii ni tukio halisi linaloendelea sasa mubashara kwa ndugu yenu.

Natanguliza shukrani.

Ncha Kali.
 
Hama wewe lakini uwe unarudi kugonga mzigo mara mojamoja sana.
Atakuchoka na atatafuta mchepuko kisha ataanza kukusahau mdogomdogo(angalizo wanaume hapa wanaanzaga kuona wivu )

Isije ukawa huoni anafaa kwa ndoa kwasababu umeshaizoe k yake. Akipata bwana na wewe kukupotezea huenda ukaanza usumbufu.

Au nipe namba yake nikusaidie kumsahaulisha wewe.
 
Mkumbushe sababu ya siku ya kwanza kukutana na sababu iliyofanya Aishi kwako.

Mimi ningekuwa wewe,ningetafuta chumba kizuri nikampangia,nikamwekea kitanda na godoro..then siku ya siku mnatoka sehemu iliyotulia mnazungumza na kumkumbusha Kwanini alikuja kukaa kwako.

Inawezekana kwa mwanamke ikawa ni ngumu kukuelewa lakini ni bora umuumize kumwambia ukweli akae akijua.
Baada ya kumkumbusha ukweli unamwambia nimeshakutafutia chumba na umelipa kwa miezi kadhaa na kitanda kipo ndani kwaajili ya kuanza maisha.wewe akuache kwenye nyumba yako kama alivyokukuta.

Atalia ,ataumia,atakulaumu,atakuona mbaya sana tena mkatili..kwakuwa hisia za kimapenzi kwake zimeshika hatamu lakini siku akija kurudi kwenye mhimili wa akili,atakushukuru sana na kukuombea(inawezekana asikwambie kuwa anakushukuru nakumuomba Mungu kwa ajili yako)lakini ukweli atakuwa na shukrani.

Maisha Haya hayatabitiki hakuna sababu ya kuachana vibaya wakati unaweza kutumia njia ya kiustaarabu na kiuungwana kuachana na mtu🥂
 
Wakuu, yamenifika hapa!

Nimekuwa nikiishi na binti wa watu kinyemela kwa takribani miezi MINNE sasa. Tulianza kama masikhara, mwisho nikamruhusu ahamie ili nijihakikishie tunda kila nikiwa na KIU.

Stori iko hivi:

Nilikutana na binti ambaye yupo kwenye kupambana aanze maisha. Alikuwa akiishi kwa dada’ke kipindi hicho.

Katika stori za hapa na pale, binti akagusia hitaji lake la kujitegemea kimaisha. Japo kwa chumba kimoja tu, ili aondokane na kuishi kwa dada (shemeji).

Kumuuliza mipango yake ipoje, kasema anahitaji kiasi cha kodi tu. Na itamchukua miezi MITATU ikiwa ataitafuta kupitia kazi anayofanya.

Wakati huo tulishawahi kujadili lengo lake la kuanzisha ofisi yake ili tu awe na kazi yake. Hapa aliomba 'sapoti' yangu na nilimuahidi.

Basi bwana!
Nikaona kitonga si hii, nikamwambia ahamie kwangu ili tuishi kwa hiyo miezi MITATU huku akijiandaa kupanga.

Maaweee! Mtoto bila hiyana akafungasha, kaaga kwa dada’ke ya kuwa amepata chumba anahamia. Kapewa jiko dogo la gesi, na beseni kama zawadi ya kuanzia maisha. Huyu hapa.

Basi maisha yakaanza, yakasonga. Ahadi yangu nikatimiza akafungua ofisi yake, ikawa sasa kila anachopata anaboresha ofisi yake.

Siku nikigusia kuhusu maandalizi yake ya kupanga anakuwa mkali balaa, nimvumilie hajaanza kupata faida, nikisema nimlipie kodi utasikia ooh nimemchoka nataka kuleta MKE mwingine!

Kumbe mwenzangu alisha-update STATUS, alishakuwa MKE tayari. Mwanzo nikadhani utani, siku zinasonga AKILI inazidi kunirudi.

Sasa nawaza namna gani ya kuondokana naye kwa amani, sitaki kuoa wala sitaki kumuumiza kwa kumpotezea muda. Ingawa kwa hili labda aamue tu kunigeuka.

Hakuna namna ataweza kunishawishi kwenye mtazamo wangu juu ndoa, na hata msimamo wangu juu yake nilimweka wazi tangu mwanzo.

Jibu lake lilikuwa kama langu, kwamba hata yeye hahitaji kuolewa saivi anatafuta MAISHA kwanza. Ni wasiwasi wangu tu, naishije na mtu kinyemela muda wote huu. Japo hatuombei ya kutokea, God forbid!

Naombeni ushauri wenu ndugu zangu, hii ni tukio halisi linaloendelea sasa mubashara kwa ndugu yenu.

Natanguliza shukrani.

Ncha Kali.

Umeshamla mtoto wa watu unataka kubadili kikojoleo kingn saiv ndio unajidai kushtuka!mzee ulishakosea pale ulipomruhusu tu kuleta virago vyake kwako ila km kipato kinaruhusu na unaplan nae bhas vumilia tu huwez jua mtatoka vp kimaisha ila km hukumpenda mtoto wa watu ww ni kuzama chumvini bhas mwambie tu ukwel ila ni ngumu sana kwa upande wa binti kukuelewa kirahis
 
Kichwa cha chini kikisimama,, kichwa kikubwa cha juu huwa hakifanyi kazi. alisikika muuza UKWAJU akimshauri Bitozi mmoja.

Mkuu wewe hapo ulikosea sana,, hakukuwa na ulazima wa kusogeza papuchi ghetto kwa ajili ya hizo kabichi za mpito..

Kaa nae mueleze,, japo sio rahisi.. AU kama vipi endeleza migegedo hadi pale atakapoondoka yeye..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom