HARUFU
Platinum Member
- Jan 21, 2014
- 31,704
- 48,140
Pole sana.
Linapokuja suala la kupewa ushauri uende nchi gani/ipi ni ngumu sana, ujue kwanini?
Kila mtu (namaanisha wale wanaosema kweli wanapokuwa nje) atakujibu kutokana na Maisha yalivyo kwa upande wake.
Tunapokuja kwenye uhalisia ni kwamba, hakuna maisha rahisi popote hapa Ulimwenguni, nenda popote utakapoenda hapa Ulimwenguni changamoto za maisha/kimaisha ni zile zile na zinafanana.
Na ugumu unaongezeka zaidi pale linapokuja suala la Vibali, iwapo hukufanikiwa kupata Vibali vya kuishi hiyo Nchi husika.
Kitu cha kwanza utakapoingia Nchi yoyote ya Ugenini, changamoto kubwa ni Kibali kwanza.
Kwahiyo utakapofanikiwa kuingia popote hapa Ulimwenguni, kaa ukijua changamoto kubwa ni Kibali.
Maisha yamebadilika, Ulaya ya sasa tofauti na Ulaya ya zamani, Vibali vimekuwa vigumu, na machafuko yanayoendelea pande nyingine tofauti, tofauti za Ulimwengu yamechangia kwa kiasi kikubwa kufanya maisha ya Ulaya kuwa magumu, na Wahamiaji wamekuwa wengi sana.
Sikukatishi tamaa, wewe jaribu popote usiogope, kufanikiwa au kutokufanikiwa ugenini kupo, na ni sehemu ya maisha.
Muhimu wewe mwenyewe utakapofanikiwa kuingia Nchi yoyote jitahidi sana kuwa mpiganaji, mafanikio utayaona.
Kila la Kheri
Linapokuja suala la kupewa ushauri uende nchi gani/ipi ni ngumu sana, ujue kwanini?
Kila mtu (namaanisha wale wanaosema kweli wanapokuwa nje) atakujibu kutokana na Maisha yalivyo kwa upande wake.
Tunapokuja kwenye uhalisia ni kwamba, hakuna maisha rahisi popote hapa Ulimwenguni, nenda popote utakapoenda hapa Ulimwenguni changamoto za maisha/kimaisha ni zile zile na zinafanana.
Na ugumu unaongezeka zaidi pale linapokuja suala la Vibali, iwapo hukufanikiwa kupata Vibali vya kuishi hiyo Nchi husika.
Kitu cha kwanza utakapoingia Nchi yoyote ya Ugenini, changamoto kubwa ni Kibali kwanza.
Kwahiyo utakapofanikiwa kuingia popote hapa Ulimwenguni, kaa ukijua changamoto kubwa ni Kibali.
Maisha yamebadilika, Ulaya ya sasa tofauti na Ulaya ya zamani, Vibali vimekuwa vigumu, na machafuko yanayoendelea pande nyingine tofauti, tofauti za Ulimwengu yamechangia kwa kiasi kikubwa kufanya maisha ya Ulaya kuwa magumu, na Wahamiaji wamekuwa wengi sana.
Sikukatishi tamaa, wewe jaribu popote usiogope, kufanikiwa au kutokufanikiwa ugenini kupo, na ni sehemu ya maisha.
Muhimu wewe mwenyewe utakapofanikiwa kuingia Nchi yoyote jitahidi sana kuwa mpiganaji, mafanikio utayaona.
Kila la Kheri