Invigilator
JF-Expert Member
- Aug 16, 2016
- 3,207
- 5,990
Wakuu salaam,
Awali ya yote namshukuru sana M. Mungu kwa nafasi hii adhmu niliyobahatika kupata. Kwa miaka kadhaa nimekuwa nikihangaika kuboresha maisha yangu ndani na nje ya nchi.
Mara tu baada ya kuhitimu tu masomo ya elimu ya juu, niliamua kusafiri kwenda bara la Asia nchi za Gulf kutafuta maisha, nikakaa huko kwa kipindi cha miaka miwili nikifanya vibarua vya hapa na pale hadi COVID-19 ilipoanza nikaamua kurejea nchini.
Nikafika na nikaanza maisha, maambukizi yalipopungua na mipaka kuanza kufunguliwa tena, nilijaribu mara nyingi sana kurudi kwenye kibarua changu bila mafanikio, sababu kuu ilikuwa ni kutokuwepo kwa chanjo ya COVID-19 nchi - utakumbuka wakati huo uongozi ulikuwa tofauti na huu tulionao leo (utofauti wa sera kuhusu COVID). Mwisho nikapoteza kibarua changu.
Nikakutana na changamoto kubwa ya maisha baada ya miezi kadhaa tu kupita, nikaanza kuishiwa pesa,maana sehemu ya kipato changu nilikuwa nikitumia kuhudumia wazazi na wadogo zangu wawili waliokuwa masomoni (Elimu ya juu). Kwa sasa wamehitimu wote, wapo nyumbani hawana ajira pia.
Baada ya kusota, nikaamua kiasi kile nilichobakiza (nilichokuwa napanga kutumia kwa ajili ya safari) nikiweke katika biashara, nikachukua pesa nikaweka kwenye biashara, biashara ikafa kabisa bila kupata faida yoyote.
Baada ya hapo, kuanzia mwaka jana mwezi wa tano, nikawa sina chochote kabisa hata hela ya kununua bundle.
Kidogo kidogo nikaanza kupoteza marafiki na jamaa zangu, hata wale niliokuwa nawasaidia wakanidharau kabisa, sikuwa chochote kabisa mbele yao.
Nikakataa tamaa kabisa, maana hata mpenzi wangu,niliempenda sana, niliyepanga kumuoa akaniacha akaolewa na mtu mwingine, sikuwa tena na uwezo wa kumtimizia mahitaji,na wakati alipohitaji ndoa,ndio kabisa mimi hata pesa ya kujihudumia mwenyewe sina, nikabaki mwenyewe.
Nikatoka mjini, nikaamua kurudi nyumbani wazazi wakanipa moyo sana, lakini baadae mambo yakabadilika, kwa ndugu zangu sikuwa na ile heshima niliyokuwa nayo mwanzoni,kila mtu nikaona anajitenga na mimi,nikadharaulika wakawa wananiita mchizi wa Bongo ( In Alikiba's voice).
Mwanzoni mwa mwaka huu, nikifanya maamuzi magumu, nikaamua nitoke nyumbani, baada ya kukaa huko miezi kadhaa, nikaenda mjini kwa mshikaji, bila kuwa na sent mfukoni, jamaa akanipokea maisha yakaanza, tukipata tunakula tukikoswa tunalala.(Mungu ambariki sana huyu jamaa).
Baadae nikapata wazo, nikasema kwa namna yoyote lazima nitoke hii nchi, nikaamua niende Canada au USA, mwisho wa siku baada ya kutafiti sana nakaamua USA will be the best option baada ya kuangalia baadhi ya facts.
Nikaamua kuwa niuze eneo langu, ambalo nilinunua wakati nikiwa nje, nikauza japo kwa bei ya kutupa, nikampatia mshikaji aliyenipokea Tsh 500K (nilimpatia maana maisha yake ni magumu sana na kwa kipindi nikiwa pale alinipambana sana kuhakikisha mkono unaenda kinywani, so nilimpatia kama shukran).
Nikabaki na 1.5 M, nikasafiri kuelekea Dar, huko nina mshikaji mwingine, kufika Dar mradi nina pesa nikatafuta wakala (Agent) wa kazi za Arabia (Qatar), nikaenda ofisini kwake Kariakoo, tukaandikishana, nika submit documents alizohitaji pamoja na agency fee 500K. Akaanza kunizungusha sana mwisho wa siku nikajua tu nimepigwa, nikamshukuru Mungu, nika move on, mfukoni ikabaki 900K.
Nikasema ngoja nipambane niende USA kama wazo langu la kwanza lilivyokuwa, nikamshirikisha mshikaji akaanza niambia kuwa naanza kuchanganyikiwa maana nina waza mawazo nisiyo endana nayo, nikapiga kimya nikaamua nifanye kimya kimya, nikamua aina ya visa nitakayoomba iwe ni visa ya kwenda masomoni baada ya kupata ushauri wa jamaa mmoja humu jukwaani, nikiwa huko kila kitu kitafunguka.
Nikaanza kuomba vyuo kwa fujo, course zote nilizoona nina vigezo, NOTE; lengo sio kusoma TU ila nikiwa nasoma niwe nafanya KAZI na baada ya masomo nitengeneze mazingira mazuri ya kubaki.
Mwezi wa 3 mwishoni, nikaomba vyuo sita, nikalipa application fees, ina range from 50 - 65 USD per university, nikaishiwa pesa nikakaa sasa kusubiri majibu.
Majibu yakaanza kutoka, chuo cha kwanza nimekosa, cha pili nimekosa, cha tatu vivyo hivyo, cha nne nimekosa pia . Nikahisi kuchanganyikiwa, nikawa nimepoteza kila kitu, nikasema hapa nachanganyikiwa sio muda mrefu, nikawa mtu wa kujitenga tu na kulala tu, nawaza kufa kufa tu. Kumwambia rafiki yangu siwezi, maana sikumshirikisha, nikabaki kulia na Mungu wangu.
Sababu kuu iliyosababisha nikose nilikuwa naomba, nikilipa pesa mwisho kabisa kwenye application checklist, wananiambia nitume jaribio la ujuzi wa lugha (English Language Proficiency Test - mojawapo kati ya IELTS, DUOLINGO na TOEFL) tafrani ikawa hapa, maana pesa ya kufanya IELTS pekee inaanzia 700K (laki saba) na pia wakataka niwatumie matokeo yangu ya undergraduate kwa kupita wakala ( WES - course by course evaluation ) ambao gharama zake ni 300K.
Nikaendelea hivyo hivyo, mwisho kabisa, namshukuru Mungu vyuo viwili vilivyobaki vimenikubalia, tayari vimenitumia ADMISSION LETTER na I - 20 FORM kwa ajili ya kwenda kuombea Visa - US EMBASSY.
Vyuo vyote nimepata partial Scholarship, moja ya Masters ya masomo ya DINI na nyingine ni masuala ya ELIMU, sasa nipo kwenye kuhangaika pesa kwa ajili ya visa, nauli na mambo mengine ya safari. Natakiwa kuwa MAREKANI kabla ya 16 August.
Napenda kutumia fursa hii kuwauliza wajuzi wa mambo, kunisaidia yafuatayo.
JE,
1. F 1 visa itaniruhusuruhu kufanya kazi halali?
2. Naweza kwenda USA na kufanikiwa kwa kutumia Partial Scholarship? wakati nikipambana kujilipia sehemu inayobakia kwa kufanya kazi?.(maana uchumi wangu umeyumba mno).
3. Ni vitu gani natakiwa kuzingatia wakati wa kwenda kuomba visa, ili niwe na uhakika wa kupata?
4. Nichague kusoma Masters ipi ya DINI au ELIMU? itakayonifanya nifanikiwe?
Karibuni kwa ushauri na msaada wowote tafadhali.
Awali ya yote namshukuru sana M. Mungu kwa nafasi hii adhmu niliyobahatika kupata. Kwa miaka kadhaa nimekuwa nikihangaika kuboresha maisha yangu ndani na nje ya nchi.
Mara tu baada ya kuhitimu tu masomo ya elimu ya juu, niliamua kusafiri kwenda bara la Asia nchi za Gulf kutafuta maisha, nikakaa huko kwa kipindi cha miaka miwili nikifanya vibarua vya hapa na pale hadi COVID-19 ilipoanza nikaamua kurejea nchini.
Nikafika na nikaanza maisha, maambukizi yalipopungua na mipaka kuanza kufunguliwa tena, nilijaribu mara nyingi sana kurudi kwenye kibarua changu bila mafanikio, sababu kuu ilikuwa ni kutokuwepo kwa chanjo ya COVID-19 nchi - utakumbuka wakati huo uongozi ulikuwa tofauti na huu tulionao leo (utofauti wa sera kuhusu COVID). Mwisho nikapoteza kibarua changu.
Nikakutana na changamoto kubwa ya maisha baada ya miezi kadhaa tu kupita, nikaanza kuishiwa pesa,maana sehemu ya kipato changu nilikuwa nikitumia kuhudumia wazazi na wadogo zangu wawili waliokuwa masomoni (Elimu ya juu). Kwa sasa wamehitimu wote, wapo nyumbani hawana ajira pia.
Baada ya kusota, nikaamua kiasi kile nilichobakiza (nilichokuwa napanga kutumia kwa ajili ya safari) nikiweke katika biashara, nikachukua pesa nikaweka kwenye biashara, biashara ikafa kabisa bila kupata faida yoyote.
Baada ya hapo, kuanzia mwaka jana mwezi wa tano, nikawa sina chochote kabisa hata hela ya kununua bundle.
Kidogo kidogo nikaanza kupoteza marafiki na jamaa zangu, hata wale niliokuwa nawasaidia wakanidharau kabisa, sikuwa chochote kabisa mbele yao.
Nikakataa tamaa kabisa, maana hata mpenzi wangu,niliempenda sana, niliyepanga kumuoa akaniacha akaolewa na mtu mwingine, sikuwa tena na uwezo wa kumtimizia mahitaji,na wakati alipohitaji ndoa,ndio kabisa mimi hata pesa ya kujihudumia mwenyewe sina, nikabaki mwenyewe.
Nikatoka mjini, nikaamua kurudi nyumbani wazazi wakanipa moyo sana, lakini baadae mambo yakabadilika, kwa ndugu zangu sikuwa na ile heshima niliyokuwa nayo mwanzoni,kila mtu nikaona anajitenga na mimi,nikadharaulika wakawa wananiita mchizi wa Bongo ( In Alikiba's voice).
Mwanzoni mwa mwaka huu, nikifanya maamuzi magumu, nikaamua nitoke nyumbani, baada ya kukaa huko miezi kadhaa, nikaenda mjini kwa mshikaji, bila kuwa na sent mfukoni, jamaa akanipokea maisha yakaanza, tukipata tunakula tukikoswa tunalala.(Mungu ambariki sana huyu jamaa).
Baadae nikapata wazo, nikasema kwa namna yoyote lazima nitoke hii nchi, nikaamua niende Canada au USA, mwisho wa siku baada ya kutafiti sana nakaamua USA will be the best option baada ya kuangalia baadhi ya facts.
Nikaamua kuwa niuze eneo langu, ambalo nilinunua wakati nikiwa nje, nikauza japo kwa bei ya kutupa, nikampatia mshikaji aliyenipokea Tsh 500K (nilimpatia maana maisha yake ni magumu sana na kwa kipindi nikiwa pale alinipambana sana kuhakikisha mkono unaenda kinywani, so nilimpatia kama shukran).
Nikabaki na 1.5 M, nikasafiri kuelekea Dar, huko nina mshikaji mwingine, kufika Dar mradi nina pesa nikatafuta wakala (Agent) wa kazi za Arabia (Qatar), nikaenda ofisini kwake Kariakoo, tukaandikishana, nika submit documents alizohitaji pamoja na agency fee 500K. Akaanza kunizungusha sana mwisho wa siku nikajua tu nimepigwa, nikamshukuru Mungu, nika move on, mfukoni ikabaki 900K.
Nikasema ngoja nipambane niende USA kama wazo langu la kwanza lilivyokuwa, nikamshirikisha mshikaji akaanza niambia kuwa naanza kuchanganyikiwa maana nina waza mawazo nisiyo endana nayo, nikapiga kimya nikaamua nifanye kimya kimya, nikamua aina ya visa nitakayoomba iwe ni visa ya kwenda masomoni baada ya kupata ushauri wa jamaa mmoja humu jukwaani, nikiwa huko kila kitu kitafunguka.
Nikaanza kuomba vyuo kwa fujo, course zote nilizoona nina vigezo, NOTE; lengo sio kusoma TU ila nikiwa nasoma niwe nafanya KAZI na baada ya masomo nitengeneze mazingira mazuri ya kubaki.
Mwezi wa 3 mwishoni, nikaomba vyuo sita, nikalipa application fees, ina range from 50 - 65 USD per university, nikaishiwa pesa nikakaa sasa kusubiri majibu.
Majibu yakaanza kutoka, chuo cha kwanza nimekosa, cha pili nimekosa, cha tatu vivyo hivyo, cha nne nimekosa pia . Nikahisi kuchanganyikiwa, nikawa nimepoteza kila kitu, nikasema hapa nachanganyikiwa sio muda mrefu, nikawa mtu wa kujitenga tu na kulala tu, nawaza kufa kufa tu. Kumwambia rafiki yangu siwezi, maana sikumshirikisha, nikabaki kulia na Mungu wangu.
Sababu kuu iliyosababisha nikose nilikuwa naomba, nikilipa pesa mwisho kabisa kwenye application checklist, wananiambia nitume jaribio la ujuzi wa lugha (English Language Proficiency Test - mojawapo kati ya IELTS, DUOLINGO na TOEFL) tafrani ikawa hapa, maana pesa ya kufanya IELTS pekee inaanzia 700K (laki saba) na pia wakataka niwatumie matokeo yangu ya undergraduate kwa kupita wakala ( WES - course by course evaluation ) ambao gharama zake ni 300K.
Nikaendelea hivyo hivyo, mwisho kabisa, namshukuru Mungu vyuo viwili vilivyobaki vimenikubalia, tayari vimenitumia ADMISSION LETTER na I - 20 FORM kwa ajili ya kwenda kuombea Visa - US EMBASSY.
Vyuo vyote nimepata partial Scholarship, moja ya Masters ya masomo ya DINI na nyingine ni masuala ya ELIMU, sasa nipo kwenye kuhangaika pesa kwa ajili ya visa, nauli na mambo mengine ya safari. Natakiwa kuwa MAREKANI kabla ya 16 August.
Napenda kutumia fursa hii kuwauliza wajuzi wa mambo, kunisaidia yafuatayo.
JE,
1. F 1 visa itaniruhusuruhu kufanya kazi halali?
2. Naweza kwenda USA na kufanikiwa kwa kutumia Partial Scholarship? wakati nikipambana kujilipia sehemu inayobakia kwa kufanya kazi?.(maana uchumi wangu umeyumba mno).
3. Ni vitu gani natakiwa kuzingatia wakati wa kwenda kuomba visa, ili niwe na uhakika wa kupata?
4. Nichague kusoma Masters ipi ya DINI au ELIMU? itakayonifanya nifanikiwe?
Karibuni kwa ushauri na msaada wowote tafadhali.