Zero Hours
JF-Expert Member
- Apr 1, 2011
- 12,944
- 18,654
Tanzania tungekuwa na viongozi wenye akili Timamu wakasimamia madini yetu na maliasiri zet vizuri. Mtz angekuwa halipi hata senti kumi ya kodi yeyote.
na kama kuna tamko litakalofanyiwa kazi haraka ni hili ngoja uone mziki wake wakimezea bajeti hii ijayo limo wenye nyumba watakachofanya watapeleka hii kodi kwa mpangajiMnapendekeza vyanzo wikianza kuchip inn msianze kulialia
Maana baba nani kwa kodi yupo vyema
Wanatakiwa kulipa kodi ya mapatoWamechukua kwenye kodi ya ardhi tayari,
Hivi kwa nini watu wanapenda kujikatisha tamaa kabla hata hawajajaribu
Huu ushauri ni mzuri sana. Ndio, kuna vigogo wenye nyumba za kupagisha na wanaweza kujaribu kukwepa kulipa kodi lakini nionavyo mimi hao ni wachache sana.
Pia, huu mkondo wa kodi ukienea sehemu zote basi wanaokwepa kulipa hii kodi wataumbuliwa na majirani zao.
Huu mfumo uanzishwe halafu tutawashughulikia wale wajanja fulani wanaotaka kukwepa. Kama inavyofanywa sasa kwa biashara kutumia mashine za kulipa kodi.
Tusikatishe tamaa mawazo mazuri eti kwa sababu kuna wajanja watakwepa.
Asante kwa majibu ya kina. Anaekujibu hoja zako bila kukutusi anakupa heshima. Asante.Kifyatu,
Mkuu,
Nimekupa mifano hai ya bomoabomoa kwenye hifadhi ya barabara ,
Bomoabomoa ya nyumba za ufukweni zingine zimeachwa
Kunyang'anya mashamba yasiyoendelezwa .....
Labda, nikuulize swali, wewe na hao wananchi wengine mmechukua hatua gani kuhakikisha kuwa huo uonevu nilioutaja hapo juu unakomeshwa na wote sheria inakuwa msumeno!?
Tusidanganyane kuwa mtawaumbua wanaokwepa kodi wakati maskini na wanyonge wanaoimbwa kila siku jukwaani ndiyo wanaoteseka mfano, wajane na watoto yatima ndiyo wanaona uchungu wa hizo bomoabomoa.
Kwa nini unataka lianzishwe jambo jingine tena ambalo litaacha baadhi ya watu wengine ila wengine waonewe!?
Poise, ninazo nyumba nyingi tu za kupingisha sina Shida na kodi yoyote ile ikianzishwa ila tatizo lipo kwenye ulipishwaji,,,, itakuwa hakuna ubaguzi kama ambao tumeuona hapo kwenye mifano michache niliyoitaja !?
Any way, some ways a paved with good intentions but, unfortunately leads a driver to hell.
Asante kwa majibu ya kina. Anaekujibu hoja zako bila kukutusi anakupa heshima. Asante.
Sasa nikuulize na wewe maswali machache:
☆ Usimamizi wa ukusanyaji kodi leo ni sawa na ule kwenye miaka kabla 2015?
☆ Kuna watu hawakubomolewa nyumba zao. Je tuache kufanya mipango miji?
☆ Bado kuna ufisadi na rushwa - mfano bandarini. Je tuache kuwadhibiti mafisadi na wabadhilifu sasa?
Katika kila uongozi kutakuwa na mapungufu yake. Baadhi ya hayo mapungufu umeyataja. Lakini kama wewe ni mkweli utakubaliana na mimi kuwa Magufuli anajitahidi sana kuinyoosha hii nchi, tofauti na awamu zilizopita.
Tujitahidi kumuunga mkono, sio kwa kumsifia na kumkosoa tu bali, kwa kumpa ushauri kama huu uliotolewa ili kumsaidia.
Mkuu kama tutaogopa kumjadili kiongozi wa nchi yetu, tuliemwajiri wenyewe basi ni afadhali kuhama nchi au kufa tu.Mkuu,
Umebadilika japo tija yake bado ni ndogo.
Kuhusu mipango mji iwepo ila isiwe selective kuwa hapa bomoa ukifika eneo fulani pindisha kushoto au vuka usibomoe. Maana ile essence nzima ya mipango mji inakuwa haina maana kama itakuwa haifati master plan ya mji.
Rushwa na ufisadi wadhibitiwe. Mfano, miaka 3 hii sasa mahakama ya mafisadi imeanza kazi!?
Mafisadi umeona wanafungwa au kesi zinayeyuka!?
Pia, sijamtaja mtu kwenye comments zangu kwa jina au cheo. Hivyo wewe Kifyatu, kuweka jina kwenye aya yako hiyo ya pili kutoka mwisho unataka kunipa kesi ambayo Mimi sihusiki na sijataja jina la mtu wala cheo tangia nimeanza kuchangia huu Uzi.