Ushauri kwa Waziri wa fedha: Serikali inapoteza zaidi ya bilioni 200 kila mwaka kwa kupotezea chanzo hiki cha kodi

Mtini

JF-Expert Member
Apr 28, 2011
1,487
2,344
Kwa muda mrefu Serikali imeshindwa kusimamia kwa ukamilifu ukusanyaji wa kodi katika majengo ya kibiashara. Kuna nyumba nyingi sana mijini na vijijini zinafanya biashara ya upangishaji ila hazilipi kodi kutokana na kipato inachoingiza. kwa hesabu za haraka bei ya nyumba za kujitegemea za kupanga mijini ni kuanzia sh. 150,000 hadi 400,000 kwa mwezi kwa nyumba za kawaida na hizi ndio nyingi, ingawa zipo nyumba zinaenda hadi sh. 6,000,000 kwa mwezi.Nyumba nyingine zinapangishwa kwa vyumba, chumba kimoja sh. 20,000 hadi 50,000 kwa mwezi na unakuta nyumba moja inavyumba kama 4 hadi 10+. Kuna vyumba vya biashara bei yake ni sh. 50,000 hadi 500,000 kwa mwezi.

Nashauri yafuatayo:

1. Serikali iachane na ukusanyaji wa hizi kodi kwa mfumo wa withholding tax

2. Kila nyumba ilipe kodi ya 10% kama inavyotozwa kwenye withholding tax

3. Serikali ibadirishe sheria ya ukusanyaji kodi, kuwa biashara zenye mauzo chini y ash. 4,000,000 zisilipe kodi, nyumba za biashara ziondolewe kwenye hii sheria

4. Kila nyumba inayofanya biashara ya kupangisha ipewe TIN

5. TRA iongezewe nguvu ya ukusanyaji wa hizi kodi
 
Kwa hesabu za haraka bei ya nyumba za kujitegemea za kupanga mijini ni kuanzia sh. 150,000 hadi 400,000 kwa mwezi kwa nyumba za kawaida na hizi ndio nyingi
Kusanya nyumba zote Dar es salaam zinazopangishwa kwa hiyo gharama lakini idadi yake haiwezi kufikia hata nyumba za Mbagala (na vitongoji vya jirani) peke yake ambazo zinapangishwa kwa Sh.50,000 kushuka chini!
 
Tatizo huwajui wamiliki au unajisahaurisha kwa makusudi!?

Jiulize, ni kwa nini nyumba zingine zinabomolewa zingine hazibomolewi!?
Mfano, zilizo kwenye fukwe za bahari au hifadhi za barabarani!?

Kwa nini, mashamba ya wengine yasiyoendelezwa yalichukuliwa tena kwa/mbwembwe na matarumbeta wakati baadhi ya watu mashamba yao hayakuchukuliwa na hadi leo hajaendelezwa!?

Kazi njema mkuu.
 
Kusanya nyumba zote Dar es salaam zinazopangishwa kwa hiyo gharama lakini idadi yake haiwezi kufikia hata nyumba za Mbagala (na vitongoji vya jirani) peke yake ambazo zinapangishwa kwa Sh.50,000 kushuka chini!
nimerekebisha andiko langu hope litafit ulicho comment
 
Mnapendekeza vyanzo wikianza kuchip inn msianze kulialia
Maana baba nani kwa kodi yupo vyema
 
safi sana mkuu..Hizi ndio aina za siredi ninazozipenda humu JF!Unajenga hoja mpaka mtu akisoma anatikisa kichwa
 
wafanyakazi wa TRA wale mabosi ndio wamiliki wa hizo nyumba nyingi wanaanzia wapi kuweka utaratibu utakaowabana..

unajua mawaziri, makatibu wakuu, wakurugenzi ndio wamiliki wa nyumba nyingi za kupanga... so hili jambo kufanikisha ni ngumu kuliko unavyofikiri
 
Anzia kwenye madini how come government owns nil%
Madini yanatosha kabisa kuendesha nchi.
Vile vile futa kabisa chaguzi za miheusho.
Mwisho punguza kodi za vileo na vinywaji baridi ili viwanda viongeze uzalishaji na kukusanya mapato makubwa ya kodi ya serikali.Ili kufanikisha mlokole au ustadhi asipange kodi ya vilevi.
 
Mtu afirike kujenga afu we uchukue kodi hata ela yangu ya ujenzi haijarudi.
Hicho ndio umeona chanzo kikubwa kuliko vingine vinavyopewa exempted kama makanisa na misikiti
 
Back
Top Bottom