USHAURI: kwa wasioamini maswala ya time travel

Rejea niliyo andika huko juu.
Baada ya kurejea ndo nimeandika hayo.

Kiufupi ni kuwa hauwezi kumfanya mtu awe makini kwa lugha za kejeli na ususuavu.

Zaidi lugha hizo zinamfanya mtu aonekane kituko mbele ya wengine.
 
Mbona mnabishania jambo dogo /tatizo lenu wote mnashindwa kutofautisha kati ya Muda Na Wakati...kubalianeni kwanza mnachoshindania ni Muda au Wakati?
Pengine tukapata uelewa kupitia wewe mkuu.

Kwa uonavyo tofauti ya muda na wakati ni upi mkuu
 
Pengine tukapata uelewa kupitia wewe mkuu.

Kwa uonavyo tofauti ya muda na wakati ni upi mkuu
muda na wakati ni vitu 2 tofauti,mara zote watu tulio wengi hua tunauongelea wakati tukiwa na maana ya muda.kuuelezea muda katika maneno ya kawada ni ngumu,ila nikupe mifano michache unaweza ukapata mwanga,Muda ni kiumbe ambacho mfano wake ni kama mnyororo {chain},na katika umbo la mduara{cicle},na ndani ya muda ndio tunapata WAKATI NA MATUKIO.na kazi kubwa ya wakati ni kututunzia kumbukumbu za matukio yanayotokea ndani ya muda.Tuje kwenye mada husika ambayo ni Time travel,inawezekana au haiwezekani?Kwa mujibu wa Albert Einsten jambo hili linawezekana kwa sababu ya uwepo wa vitu 3.ambavyo ni 1.space 2.speed 3.dimention. Ufafanuzi wake ni kwamba ,space ni lile eneo la katikati la hio chain [muda],ambalo lipo wazi ,lakini kuna nyenzo kuwezesha kusafiri.
Speed ndio jambo kubwa la kuweza kufanikisha jambo hili la kutembea katika muda.na hapa ndipo ufafanuzi wa ndugu Einsten unawapa watu mashaka juu ya uwepo wa jambo hili la kutembea katika muda.kwa sababu alisema ili ufanikiwe kutembea katika muda ni lazima uwe na speed ya mwanga au zaidi ya speed hio ya mwanga.Kwenye akili yakawaida ni kwamba jambo hili haliwezekani.ukweli ni kwamba kwa akili ya wenye kutafiti jambo hili linawezekana ila wakati haujafika.
Dimention ni uelekeo ambao upo katika chain[muda] hio, na kuna sehemu kuu 4 za uelekeo.ambazo ni,Mashariki,magharibi,kusini na kaskazini.Katika muktadha Einsten akasema kwamba ili utoke mashariki kwenda magharibi ni lazima uwe na speed ya mwanga ila kama hutoweza kutembea kwa speed hio ya mwanga basi wewe utabaki present na kwako past na future litakuwa ni jambo la muhali kulielezea.,
Baada ya maelezo hayo nadhani sasa mtakua mmepata picha kua nyinyi mnabishana kwenye wakati na sio muda,kwasababu mnaongelea idadi ya miaka ambayo inapimwa kwa nyenzo za wakati,ambazo ni..
Milenium,karne,decan,year,month,week,day,hour,minute,second,mill second etc,.
Kwa kumalizia inapaswa kufaham WAKATI una uelekeo wa aina moja tuambao ni clockwize direction,Tofauti na muda ambao una uelekeo zaidi ya mmoja,mnaweza mkaniomba ushahidi juu ya kauli hii..ushahidi ni ROHO YA MWANADAMU, yenyewe haifi,hua inatenganishwa na mwili na hurejeshwa past,bi maana sehemu ya awali kabla ya kuunganishwa na mwili ndani ya tumbo la uzazi.
Mwisho natoa ushauri tu ,katika ulimwengu huu kuna mambo ambayo unapotaka kuyafaha,kuyajadili na hata kuyafanyia maamuzi ,haitakiwi utumie akili ya kawaida,NI LAZIMA,uwe na VIINI VYA AKILI..yaani uwe extra ordinar person.
 
muda na wakati ni vitu 2 tofauti,mara zote watu tulio wengi hua tunauongelea wakati tukiwa na maana ya muda.kuuelezea muda katika maneno ya kawada ni ngumu,ila nikupe mifano michache unaweza ukapata mwanga,Muda ni kiumbe ambacho mfano wake ni kama mnyororo {chain},na katika umbo la mduara{cicle},na ndani ya muda ndio tunapata WAKATI NA MATUKIO.na kazi kubwa ya wakati ni kututunzia kumbukumbu za matukio yanayotokea ndani ya muda.Tuje kwenye mada husika ambayo ni Time travel,inawezekana au haiwezekani?Kwa mujibu wa Albert Einsten jambo hili linawezekana kwa sababu ya uwepo wa vitu 3.ambavyo ni 1.space 2.speed 3.dimention. Ufafanuzi wake ni kwamba ,space ni lile eneo la katikati la hio chain [muda],ambalo lipo wazi ,lakini kuna nyenzo kuwezesha kusafiri.
Speed ndio jambo kubwa la kuweza kufanikisha jambo hili la kutembea katika muda.na hapa ndipo ufafanuzi wa ndugu Einsten unawapa watu mashaka juu ya uwepo wa jambo hili la kutembea katika muda.kwa sababu alisema ili ufanikiwe kutembea katika muda ni lazima uwe na speed ya mwanga au zaidi ya speed hio ya mwanga.Kwenye akili yakawaida ni kwamba jambo hili haliwezekani.ukweli ni kwamba kwa akili ya wenye kutafiti jambo hili linawezekana ila wakati haujafika.
Dimention ni uelekeo ambao upo katika chain[muda] hio, na kuna sehemu kuu 4 za uelekeo.ambazo ni,Mashariki,magharibi,kusini na kaskazini.Katika muktadha Einsten akasema kwamba ili utoke mashariki kwenda magharibi ni lazima uwe na speed ya mwanga ila kama hutoweza kutembea kwa speed hio ya mwanga basi wewe utabaki present na kwako past na future litakuwa ni jambo la muhali kulielezea.,
Baada ya maelezo hayo nadhani sasa mtakua mmepata picha kua nyinyi mnabishana kwenye wakati na sio muda,kwasababu mnaongelea idadi ya miaka ambayo inapimwa kwa nyenzo za wakati,ambazo ni..
Milenium,karne,decan,year,month,week,day,hour,minute,second,mill second etc,.
Kwa kumalizia inapaswa kufaham WAKATI una uelekeo wa aina moja tuambao ni clockwize direction,Tofauti na muda ambao una uelekeo zaidi ya mmoja,mnaweza mkaniomba ushahidi juu ya kauli hii..ushahidi ni ROHO YA MWANADAMU, yenyewe haifi,hua inatenganishwa na mwili na hurejeshwa past,bi maana sehemu ya awali kabla ya kuunganishwa na mwili ndani ya tumbo la uzazi.
Mwisho natoa ushauri tu ,katika ulimwengu huu kuna mambo ambayo unapotaka kuyafaha,kuyajadili na hata kuyafanyia maamuzi ,haitakiwi utumie akili ya kawaida,NI LAZIMA,uwe na VIINI VYA AKILI..yaani uwe extra ordinar person.
Asante sana mkuu.

Hii comment inabidi nitulie vizuri niisome.

Lakini bwana zurri hajajibu mambo ambayo nimemuuliza ametokomea gizani.
 
Kuna eneo nililiona ndani ya ndoto miaka mingi.Basi jana nimebahatika kufika urambo kwa mara ya kwanza,lile eneo nimeliona vile vile kama nishawahi kufika.
Huwa inanitokea. inaogopesha. Inawezekana kweli kuna vitu vinaendelea ambavyo hatuna uwezo wa kuvijua.
 
Naomba niingie kwenye maada mojakwamoja,

Ni baada ya kupitia mijadala kadhaa ya kitu kinachoitwa time travel nimeona watu wengi wakipingana na hii kitu, mimi binafsi bila ya lengo ya kujinufaida na faida yeyote ile napenda nikupe shuhuda na kukuomba pia uamini na ufanyie kazi kuwa hii kitu IPO.

Nakumbuka wakati nikiwa mdogo huko kijijini kwetu (....) Mkoa wa pwani. "Kijiji kimezungukwa na mito, vichaka mabonde na misitu mikubwa.
Kulikuwa na kawaida ya kupotea kwa watu mara kwa mara huku imani ya wengi ikiwa ni wachawi ndo wahusika wa kupotea kwa watu. Na hii nahisi wenda si kijijini kwetu tu bali hata kijijini kwenu wenda kuna haka ka tabia ka kupotea kwa watu ila niseme tuu sio watu wote wanapotelea kwa wachawi ila baadhi yao ni time travel. kwanini nasema ni time tlavel iliwahi nitokea pia ilikuwa hivi;-
(Shuhuda ya kwanza)::;
mimi na vijana wenzangu tulikuwa tunakwaida ya kusaka wanyama wadogowadogo kwa kutumia mbwa. Siku moja shambani kwetu waliingia ngedere kama kawaida nikafungulia mbwa na kuanza kimbiza ngedere (tumbili) kimbiza yangu ikaishia kwenye msitu mdogo ulioko mbali kidogo. Nikafika mahali na kupumzika nakumbuka ilikuwa kama majila ya saa saba mchana kwendea saa nane nikakaa chini ya mti mmoja aina ya mtopetope na kuanza kula matunda ya mti huo. Hada kufika saa 11 jioni ndio safari ikaanza ya kurudi home ile nafika home napata taarifa kuwa nilikuwa nimepotea tena siku mbili na watu walishapiga mpaka nyanga.
nikaanza kuwaelezea na hakuna aliyeniamini kuwa nimetumia kama masaa manne tu hivi kuwa msituni wala sio siku mbili nikaenda shambani kuhakiki baadhi ya mazao waliyokuwa wameharibu ngedere siku ile ni kweli nilikuta ni mazao yaliyoalibiwa kama siku mbili zilizopita nyuma. Kwa wakati ule niliamini kweri wenda ikawa ni wachawi ila baada ya kufika JF na kukutana na hii kitu time travel. Imenifanya niamini kuwa hata hapa dunianibkuna maeneo ukifika ukitoka hapo unaeza ona umetumia dakika mbili ila ukitoka kwenye hilo eneo unakuta hata masaa saba yameahapita. Na hata kama unasaa ya kimwekumweku itakulazimu uilekebishe.
(Shuhuda ya pili)
Wakati nasoma pia shule ya msingi ilikuwa inanilazimu nilekebishe saa yangu kila ninapopita njia flani yaani saa yangu imekuwa imechelewa hata dakika tano na saa wenzie.
HITIMISHO
time travel ni yakweli na ipo na hata kuna baadhi ya maeneo hapa hapa ndani ya dunia.

i will give you a very honest answer, time travel is only theoretically possible but practically its almost getting impossible: i will explain

for you to achieve time travel you have to travel at-least slightly more than the speed of light, the speed of light is ~ 299 792 458 m / s
- i agree that there are some galaxies moving away each other more than the speed of light but here is the issue:

- As a human the faster you get , the more mass you add and when you have more mass you need more energy , and when you need more energy you add more weight to yourself, at the end of the day you only add much mass than you can move forward, thats 1

2. light is made of photons whih dont have weight, there is no any human who doesnt have weight, the best way atleast possible can be through worm holes
 
Hayo ni matukio tu kama matukio mengine wala hayana uhusiano wowote na iyo Time Travel.kama izo sehemu ambazo walipita kuna sehemu jua lina mwendo wa 0 degree, basi ukipita tena njia iyo lazima usafiri tena.wazungu wamezirudia izo njia na hamna kitu chochote kile kilichotokea.

Eistern na wanaoendelea kufatilia ili jambo wote wanapoteza muda tu
 
Hiyo ya kwenda kuwinda wanyama na kuchelewa kurudi nyumbani haiwezi kuwa time travel wewe sema ulikuwa umesinzia vichakani ulivyoamka ukapata wazo la kurudi nyumbani.
kwa nini wengi wetu huwa hivi? kwa nini umpangie mtu cha kusema, kwa nini uone kama ulichokusudia wewe ndio sahihi....kwa nini aseme alisinzia wakati yeye anahakika hakufanya hivyo...unajua hali hii ya kuwa na majibu yetu katika hoja nyingi za watu imeharibu vitu vingi na kuwaingiza wengi katika madhara.
 
kwa nini wengi wetu huwa hivi? kwa nini umpangie mtu cha kusema, kwa nini uone kama ulichokusudia wewe ndio sahihi....kwa nini aseme alisinzia wakati yeye anahakika hakufanya hivyo...unajua hali hii ya kuwa na majibu yetu katika hoja nyingi za watu imeharibu vitu vingi na kuwaingiza wengi katika madhara.
Kuwaingiza wengi katika madhara gani ndugu?
Kwa hiyo wewe ukianzisha mada hata kama ulichokisema ni ndoto ya abunuasi unataka tukukubalie tu umeona sisi mazezeta ama?
Kupewa uhuru wa kuanzisha uzi isikufanye uwe unajiandikia tu hata vitu ambavyo haviingii kabisa akilini.
 
Mwaka 2002 mjomba wngu alikuw anaendesha magari makubwa, akiwa ametoka kukusanya mzigo wa kahawa akiwa na konda wake, walifika sehemu akaegesha gari pembeni ilikuwa usiku akaenda chimba dawa. Kwenye gari alikuwa kaambatana na tingo wake. Tingo alisubiri jamaa hakurejea. Ikabidi aanze kumtafuta akamtafuta sana vichakani akaita lakini jamaa hakuwepo. Yani ni kama vile e just vanished into thin air without a trace.
Kesho yake habari zikafika nyumbani, na kwa mke wake kazini na kwa marafiki pamoja na vyombo vya dola. Alitafutwa sana lakini hakuwahi kupatikana kabisa mpaka baadae msako ukakoma maana hakukuwa na habari yake kabisa.
Ikapita miaka 3, ndipo habari ikaja kuwa kapatikana. Ajabu alikuwa kavaa nguo zile zile alizopotea kavaa na hazijachakaa, ni kama vile yuko vile vile, kuanzia nywele zake ziko kama zilivyokuwa yuko kama alivyokuwa wakati anapotea.
Jambo la kushangaza yeye alikuwa anadai kapaki gari kaenda chimba dawa karudi hakulikuta ndipo akaanza tembea tembea barabarani kulitafuta mpaka alipokutana na wananchi wakamsaidia kumfikisha serikali ya kijiji. Kwake ilikuwa ni tukio la muda mchache hakujua kama kapotea miaka mitatu.
Hakuna aliyeweza kuelewa nini kinaendelea, watu wakahusisha na ushirikina. Na bahati mbaya alifariki kwa kuugua baad ya miaka miwili toka apatikane.
Sijui nini kilitokea mpaka leo hakuna anayeelewa.
Dah, hii inafikirisha sana, hakika wanadamu kuna mambo mengi sana hatuyajui.
 
Kuwaingiza wengi katika madhara gani ndugu?
Kwa hiyo wewe ukianzisha mada hata kama ulichokisema ni ndoto ya abunuasi unataka tukukubalie tu umeona sisi mazezeta ama?
Kupewa uhuru wa kuanzisha uzi isikufanye uwe unajiandikia tu hata vitu ambavyo haviingii kabisa akilini.
kama haviingii akilini kwako huo ndio ukomo wa akili yako....lakini wengine huenda yanaingia....so usichore mstari kisa kwako hayapiti
 
na wewe usiponielewa comment yangu ujue ndio ukomo wako umeishia hapo hauna sababu ya kinilaumu au kunizia nisicomment.
kama haviingii akilini kwako huo ndio ukomo wa akili yako....lakini wengine huenda yanaingia....so usichore mstari kisa kwako hayapiti
 
na wewe usiponielewa comment yangu ujue ndio ukomo wako umeishia hapo hauna sababu ya kinilaumu au kunizia nisicomment.
sijakuzuia kutoa mawazo yako boss....ila nimeshangaa pale unapochora mstari wa hitimisho....wakati bado asubuhi na chochote kinaweza kutokea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom