Ushauri kwa waliochaguliwa UDOM

Na wale walochaguliwa computer engeneering wanapanda daladala za kwenda kitivo gani wapi?na vipi kuhusu kuhusu mavazi NAOMBA UNIFUMBUE MKUU

computer engineering panda daladala inayokwenda Education au ng'ongona, shukia info ya pili au benk, unaweza pia kushukia info ya kwanza, yote hayo ni vituo ndani ya Informatics ambayo ndiyo college yako. Mavazi sio issue sana, bado hawajabana ingawa sina hakika, labda wadau wa hapo watujuze. (NEVER: Usipande gari la social au bondeni, itakula kwako mbaya)
 
makole vp kuhusu rooms, 2nalala wangap room moja? wote ni mwaka wa kwanz or wana2changanya? room mate mnachaguana or mnapangiwa? nisaidieni plz
 
vp totoz zinapatikana lakini au ni magumashi


kabla hujauliza hilo swali ulitakiwa ujiulize kuwa ulifuata nini?
Jibu mbona unalo kabla kabla haujajbiwa!
Shule ambazo hazna totoz called bwiru byz,tabora byz nk.
Na ambazo hazina masela calld msalato girls n.k
na ulitakiwa kuuliza kama ingekuwa Udom boyz!!!
 
MAKOLE kama intakuwa sjakosea pa1 na watu kuuliza burudani na mambo mengine mengi ikiwa viwanja vya mipira,cafetarie,kuogelea ku watch Epl na burudani kibao za ndani ya chuo na hasa nje ya chuo wakiwa wamepata 'boom' na shida za usafiri na kuibiwa! Lkn kubwa ni kwamba wakumbushe wale masharobaro wanaokuja na sura za dada zao na masster duu wawe na mioyo kishujaa,kizalendo na wakupigania haki yao kama MIOYO mliokuwa nayo ya kuandamana na kugoma pale mlipoona haki yenu ya kiielimu,kijamii,maradhi nk haitendeki kwaajili yenu na wadogo zenu waliokuwa nyuma
na hata kipindi cha nyuma nilikuwa nikiuliza kwanini mgomo ukiachilia mbali madai yao walinijibu (wakati huo mabomu yapgwa vbaya mno hapa walipokuwa walipokuwa wanatakwenda bunge!) kuwa wapo kwa lolote lkn kuwajengea misingi MIZURI wadogo zao wanao kuja!!

samahani kama ntakuwa nimekosea nadhani walekebshaj watalonga! Na sio kama nachochea au kuwatisha bali wanatakiwa kujua pazuri lazma kuna vkwazo na kwenye wengi (fedha)walaji,mafisad hawakosekani na pia wapgania haki hawakosekani!
ni hayo tu!!
 
Safi, nimeona jinsi watz wanavyoweza kupeana habari, ila inaonkana UDOM ni bonge la kijiji ambacho waweza maliza miaka mi3 hujakijua chote, na hivi hadi sasa kuna stdent wangapi? maana walikuwa wanaaim elfu 40.
 
Mkuu vipi kuhusu barchelor of science in physics kwa uelewa wako unadhan iko poua hapo udom, je inalipa au ndo kuishia ualimu nadhan ipo ndan ya college of natural science naomba sana unipe maelezo ya hii college kwa upande wa chakula,mavazi,hostel,maji, usafiri na burudan zote kwa ujumla naomba msaada wenu wadau ili tujipange kwa uzuri
 

Sina uhakika kama hiyo program ni ya Ualimu. Kama ingekuwa ni ya Ualimu ingekuwa ni BED ambayo somo la kufundishia ndio physics. Pamoja na kwamba wana College yao inayojitegemea, lakini watu hao wanapatikana College of Edcation. Madarasa yao yapo miongoni mwa madarasa wanayotumia COED. Kwa maana hiyo, kila mbacho wanafanya, wanakula, wanapanda watu wa Coed, watu wa Program yako nao wanafanya, Nnao uhakika kuwa College yao inayojitegemea huenda ikawa imekamilika, ingawa hata hivyo haina Hostel. Kwa maana hiyo aidha mtaishi college of Informatics au College of Education. Then mtafanya kwenda College kwenu kusoma na kurudi. Kuhusu mavazi hapo biti sio kubwa na usafiri wake ni daladala ziendazo EDUCATION AKA Ng'ongo'na. Maji full,

Kwa mara ya mwisho Programu yako walikuwa wanatumia darasa
mfano wa hili lifuatalo kama college yao. Kulingana na uchache wao, jengo hili lilitosha kabisa kama college yao. Tazama hii picha:

 
 
Safi, nimeona jinsi watz wanavyoweza kupeana habari, ila inaonkana UDOM ni bonge la kijiji ambacho waweza maliza miaka mi3 hujakijua chote, na hivi hadi sasa kuna stdent wangapi? maana walikuwa wanaaim elfu 40.

Sina hakika kwa Idadi but wanakimbilia elf 12. Huwezi imaliza UDOM kwa kutembea siku moja, Na pia huwezi kutembea kwa miguu kutoka College moja kwenda nyingine, ingawa wakati mwingine mazingira yatasababisha utembee. Unaweza kwenda na ndugu yako na mkasoma chuoni hapo na wala msionane kabisa semista nzima, au hata miaka 3 yote msikutane mkiwa UDOM, Ni rahisi kukutana mkiwa likizo nyumbani kuliko kukutana mkiwa ndani ya UDOM
 
ivi iki chuo kinatoa masters degree?

Zipo Masterz degree program nyingi mno. Na hata Wanaosoma PHD wapo. tembelea website uangalie wale waliochaguliwa post graduate uone zilivyo nyingi
 
Zipo Masterz degree program nyingi mno. Na hata Wanaosoma PHD wapo. tembelea website uangalie wale waliochaguliwa post graduate uone zilivyo nyingi

mkuu nimekupm kuhusu kontena la mama ila hujanipa maana yake
 

Unastahili kupigiwa Like kaka, hilo nio la msingi. Kwa fresherz, mfahamu kwamba wapo watu wamepoteza chuo ili kuwawekea nyie mambo safi. Hali yoyote utakayoikuta UDOM kwa sasa ni juhudi na kujitoa mhanga kwa watu wachache wazalendo waliotangulia. Kwa mnaokwenda kuishi COED, Utakuta Simtaki kila hostel. Hiyo ni kazi kubwa ya vijana wakiongozwa na mtu anaitwa KABEHO, KELVIN na wenzao wengi ambao walihatarisha maisha yao zikapatikana Huduma zile. Nanyi mnalo jukumu pale ambapo mnadhani mnaweza kurekebisha hali (HATUCHOCHEI MIGOMO) mfanye hivyo kwa wadogo zenu watakaokuja.
 
 
kwa nini college waliziweka mbalimbali kiivyo

Sababu nnazoweza kuzitoa ni nyingi, ila ifahamike kwamba college zote zilizopo katika chuo hiki zimejengwa chini ya Vilima. Hivyo kila nyuma ya mlima iko college. Labda tunaweza kufikiri kuwa:

1. Kuweka vizuizi vya vurugu msikutane na College nyingine
2. Kwa usalama wa chuo na mali zake
3. Mandhari kwani wakati wa mvua eneo hilo linapendeza sana chini ya vilima.
4. Kupata gravity kwa ajili ya maji.
5. Kitaalam, vilima husaidia kuzuia upepo, dodoma kuna upepo mwngi na mkali.

Hizo ni sababu zangu ambazo hata hivyo sio rasmi. Mdau mwengine anaweza kuziongeza hapa.
 
makole vp kuhusu rooms, 2nalala wangap room moja? wote ni mwaka wa kwanz or wana2changanya? room mate mnachaguana or mnapangiwa? nisaidieni plz

Yote yanawezekana, Unaweza kuomba kukaa wanne mwaka wa 1 watupu. Utaratibu ni kwamba mnapangiwa na mawadern. Rum moja ni watu wanne kwa kawaida.Riooms zipo nyingi hadi kero, hamuwezi kuzijaza hata waingie wanachuo elfu hamsini leo, na hata godoro zipo za kutosha. Kimsingi, mkitaka fevor mnamuomba wadern, ila ndo ivo tena, mambo yetu yale ya kuch.....chu..a..Mikenda wote mnaohitaji kuishio rum moja ni vema sana. Pia floo nzuri za kuishi ni ya 1 na pili. ground vumbi na usalama mdogo kwani mkijisahau kufunga dirisha hatari, 3&4 mbali, lift hakuna. kwa wenzangu mimi tunaopiga simu nyumbani na kuwaeleza kuwa tunalala gorofani kama ndege hapo kwenye 3&4 zitawafaa, ingawa nazo ni nzuri kwani kumetulia sana.
 

vp hosteli kuna madarasa ya kusomea, au inakuwaje mwana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…