machafuko jr
JF-Expert Member
- Sep 7, 2017
- 798
- 1,681
- Thread starter
- #21
Mkuu umeongea vizuri sana hasa ulipo gusia mambo ya mikataba maana hapo ndio sehemu tunapo anzia kupigwa.Kaka hakuna Mkataba usiokuwa na kipengele cha kuvunja Mkataba.
Kila Mkataba lazima HICHO kipengele kiwepo, Mbona enzi za JPM wale Barrick walibanwa mpaka wakakubali kulipa fidia ya mamilioni ya Dola na Mkataba mpya ukaandaliwa na Sasa hivi Tanzania tuna hisa ya 16% kwa Barrick na tuna watu wetu ndani ya Barrick KUSIMAMIA hilo.
Na hiyo 16% ni ya kuanzia lakini Kila baada ya miaka 5 inaongezeka hiyo asilimia kwa asilimia 3% hadi 10% kadri Hali itakavyokuwa inaruhusu na bado Barrick walidhia hilo.
Ni kichaa pekee ndiye atashindwa KUSIMAMIA RASIMALI za nchi ili ziwanufaishe wananchi na kuondokana na umasikini tulionao na kupunguza ugumu wa maisha badala ya kukimbilia tozo.
Kwa kifupi Tozo yeyote itakayowekwa na Serikali itaongeza ugumu wa Maisha kwa Mwananchi masikini wa Tanzania.
Tafuta Blueprint document iliandaliwa enzi za JPM iliangazia sekta zote za uchumi na utitiri wa Kodi, ushuru, Tozo, n.k. ulikuwepo na ilivyomshauri JPM kuondoa hizo Tozo na Kodi zilizokuwepo enzi hizo JPM akiwa Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Biashara nchini
Je viongozi wakuu hawaoni namna ambavo wanaweza kurekebisha hii mikataba ili inufaishe watanganyika wote.
Tubadili ushauri kwamba selikali iuze mlima Kilimanjaro pesa itakayo patikana watu watibiwe bure