TUKANA UONE
JF-Expert Member
- Jan 3, 2018
- 1,816
- 5,153
Ukihitaji salamu nenda uswahilini, kwangu utaula wa Chuya!
Sikutishi Sikupangii lakini huu ndiyo uhalisia wenyewe, ipo siku utalia na kusaga meno.
Yaani binti mzima mwenye umri kuanzia 18 - 30, hufanyi shughuli yeyote na huwezi kuzitumia nguvu zako kwenye uwekezaji wa maisha yako na mwanao, wewe kutwa kwenye Night club, kutwa kunywa pombe, kutwa kutoka "out", kutwa kutumikishwa kwenye ngono, kutwa kuvaa nusu uchi, kutwa kujisinapu, kutwa kuiga mitindo ya mavazi ya kihuni, kutwa kuvuta shisha, kutwa kubadili wanaume.
Kila weekend wewe umekuwa wa kubadili bar, hakuna Bar au kiwanja cha starehe ambacho hapa mjini hukijui!
Yaani umesoma lakini huna plan yeyote kila siku bora liende, umezaa mtoto ukaamua umrudishe huko kijijini kwenu ili uje uangaike na mji, umezaa mtoto umeamua kumtupia sista wako wewe ukaona uje mjini uruke ruke, umezaa mtoto umemtelekeza kwa shangazi yako ukaona uje mjini upuyange.
Utakuja kushituka umefikisha miaka 40 ndugu yangu na huna mbele wala nyuma kazi yako itakuwa kulaumu watu.
USHAURI
1. Achana na mambo ya kwenye bar, siyo ujanja kila kiwanja cha starehe wewe kukifahamu, unapoteza muda wako bure, huo muda ni heri upambane na maisha yako na ujiwekee savings zitakazokuja kukusaidia wewe na mwanao.
2. Muombe Mungu (fanya Ibada kwa imani yako).
3. Vaa vizuri na kwa heshima.
4. Jali Afya yako, kama unakunywa pombe kunywa kiasi au acha kabisa, acha kuvuta shisha ni hatari kwa afya yako.
5. Acha ngono.
6. Acha Tamaa.
7. Panga chumba/nyumba ambayo unaweza kuzimudu gharama.
8. Usipende Show-off itakuja kukigharimu kwasababu unaigiza maisha.
9. Ishi kwenye uhalisia.
10. Ishi maisha halisi kwasababu 'MAISHA HALISI NI MAISHA RAHISI".
11. Kama una marafiki ambao hawajielewi kila siku wanataka starehe tu WAPIGE CHINI, kuanza upya si dhambi.
12. Badili tabia ili uwashangaze wengi.
13. Tafuta shughuli ya kufanya.
14. Tunza kidogo kidogo tu pesa twako.
15. Ukipata kikubwa jitahidi utafute kieneo nje ya mji ununue.
16. Anza ujenzi kidogo kidogo kwa kudunduliza,Mungu atakusaidia utaweza kwasababu penye nia pana njia.
Ukiendelea kurukaruka siku ukipata matatizo watu wasipokujali utawaona wabaya tu, mwenye kuyaharibu au kuyatengeneza maisha yako ni wewe mwenyewe.
Hao ndugu uliowaachia mtoto wako nao ushawachosha kwa tabia zako inapaswa ubadirike. Wewe endelea kusema "Nakula ujana" wakati umri unaenda na huna mbele wala nyuma.
Siku ukifa mwanao utamuacha kwenye mazingira gani? Je, unawaamini ndugu zako au mwanao nae aje arukeruke kama wewe? Muda wa kutengeneza maisha yako ni sasa, achana na anasa, hazitokupeleka popote zaidi ya kukuharibia fyucha!
Sikutishi Sikupangii lakini huu ndiyo uhalisia wenyewe, ipo siku utalia na kusaga meno.
Yaani binti mzima mwenye umri kuanzia 18 - 30, hufanyi shughuli yeyote na huwezi kuzitumia nguvu zako kwenye uwekezaji wa maisha yako na mwanao, wewe kutwa kwenye Night club, kutwa kunywa pombe, kutwa kutoka "out", kutwa kutumikishwa kwenye ngono, kutwa kuvaa nusu uchi, kutwa kujisinapu, kutwa kuiga mitindo ya mavazi ya kihuni, kutwa kuvuta shisha, kutwa kubadili wanaume.
Kila weekend wewe umekuwa wa kubadili bar, hakuna Bar au kiwanja cha starehe ambacho hapa mjini hukijui!
Yaani umesoma lakini huna plan yeyote kila siku bora liende, umezaa mtoto ukaamua umrudishe huko kijijini kwenu ili uje uangaike na mji, umezaa mtoto umeamua kumtupia sista wako wewe ukaona uje mjini uruke ruke, umezaa mtoto umemtelekeza kwa shangazi yako ukaona uje mjini upuyange.
Utakuja kushituka umefikisha miaka 40 ndugu yangu na huna mbele wala nyuma kazi yako itakuwa kulaumu watu.
USHAURI
1. Achana na mambo ya kwenye bar, siyo ujanja kila kiwanja cha starehe wewe kukifahamu, unapoteza muda wako bure, huo muda ni heri upambane na maisha yako na ujiwekee savings zitakazokuja kukusaidia wewe na mwanao.
2. Muombe Mungu (fanya Ibada kwa imani yako).
3. Vaa vizuri na kwa heshima.
4. Jali Afya yako, kama unakunywa pombe kunywa kiasi au acha kabisa, acha kuvuta shisha ni hatari kwa afya yako.
5. Acha ngono.
6. Acha Tamaa.
7. Panga chumba/nyumba ambayo unaweza kuzimudu gharama.
8. Usipende Show-off itakuja kukigharimu kwasababu unaigiza maisha.
9. Ishi kwenye uhalisia.
10. Ishi maisha halisi kwasababu 'MAISHA HALISI NI MAISHA RAHISI".
11. Kama una marafiki ambao hawajielewi kila siku wanataka starehe tu WAPIGE CHINI, kuanza upya si dhambi.
12. Badili tabia ili uwashangaze wengi.
13. Tafuta shughuli ya kufanya.
14. Tunza kidogo kidogo tu pesa twako.
15. Ukipata kikubwa jitahidi utafute kieneo nje ya mji ununue.
16. Anza ujenzi kidogo kidogo kwa kudunduliza,Mungu atakusaidia utaweza kwasababu penye nia pana njia.
Ukiendelea kurukaruka siku ukipata matatizo watu wasipokujali utawaona wabaya tu, mwenye kuyaharibu au kuyatengeneza maisha yako ni wewe mwenyewe.
Hao ndugu uliowaachia mtoto wako nao ushawachosha kwa tabia zako inapaswa ubadirike. Wewe endelea kusema "Nakula ujana" wakati umri unaenda na huna mbele wala nyuma.
Siku ukifa mwanao utamuacha kwenye mazingira gani? Je, unawaamini ndugu zako au mwanao nae aje arukeruke kama wewe? Muda wa kutengeneza maisha yako ni sasa, achana na anasa, hazitokupeleka popote zaidi ya kukuharibia fyucha!