Uchaguzi 2020 Ushauri kwa CHADEMA kuelekea Oktoba 2020

Tuachane na siasa za kukariri ajenda za nchi zilizo endelea, wao wamesha endelea hivyo hawashughuliki sana na shida tunazosumbuka nazo sisi nchi maskini. Tunashirikiana tatizo moja tu la ajira lakini hayo mengine kwetu siyo ipaumbele chetu watanzania ambao bado tunapigania uhakika wa matibabu , mavazi na chakula.
Pamoja na kukubaliana na uliyoandika hapo juu kuhusu ajenda zinazowagusa wananchi kwa haraka na moja kwa moja, sikubaliani kabisa na kipande hiki nilichokinyanyua hapo juu.

Huwezi kuniambia kwamba mwanakijiji au mzee mjini haoni thamani ya kura yake anapokwenda kupiga kura, na kwa hiyo mshindi yeyote atakayetangazwa kwake ni sawa tu.

Kwa nini udhani tu kwamba huyo mzee mjini au raia kijijini hataki kusikia michango anayotoa mwakilishi wake bungeni kutetea waliyomtuma kuyawasilisha?

Kwa nini wewe unadhani watu hawa wanapoonewa huko walipo, na hata wakabambikiziwa makesi ya hovyo, kwao isiwe mhimu kuondoa ukiritimba huo, wewe unaona hayo ni yale yanayowahusu binaadam tofauti kabisa na wao wanaoishi nchi zingine?

Kila binaadam anataka atendewe HAKI, awe ni wa nchi zilizoendelea au hizi zetu za kiafrika.

Hizi mbinu mnazotumia kuwatishia ndizo mnazozigeuza kueleza kwamba wao haki zao sio mhimu kwao?

Hizo ajenda za mazao na mengineyo uliyotaja utazitenganisha vipi na hizi ajenda za msingi unazoona wewe kwamba sio mhimu kwa wananchi?

Kiongozi akiamua tu kwa hiari yake bila hata kujua taratibu zilizopo, akaingilia manunuzi ya mazao ya wakulima, kwa madaraka yake tu bila kufikiri madhara yanayoweza kuwapata wakulima kwa kukosa kabisa faida ya mazao yao, wewe hilo huoni kabisa kwamba ni ajenda inayostahili kufikisha kwa wananchi waelimishwe na wafanye maamuzi sahihi wasiendelee kupata hasara ya kazi zao?

Ajenda za msingi katika kampeni hii ni kuwaelimisha wananchi wajue haki zao, wasinyimwe haki kwa mabavu tu ya mtu mmoja kwa kutumia majeshi.
Wananchi wakizijua haki zao watakataa kuendelea kuonewa.

Tuachane na "siasa za kukariri..." - Hebu nieleze kama uliyoandika katika mstari huo sio mambo ya kukariri tu na kutumia mipasho unayoisikia ikitumika bila kuipa uzito wa fikra nyuma yake!
 
Labda nikukumbushe tu kuwa CDM kina sera mbadala, umefanikiwa kusoma? Ama unabwabwaja tu. CDM tayari imeshaandaa ilani ya uchaguzi, subiri itoke ndipo useme. Vyote hivi, vinahitaji wataalam wa kuelezea, sasa ndiyo tuna kuja kuchagua. Nani asiyejua kuwa Lissu ni mtaalam wa kujenga hoja? Labda niseme tu kuwa hata kama angekuwa hakipigwa risasi, Lissu angesimama dhidi ya Magufuli, na cha moto kiko pale pale mjipange.

Mimi nimeshauri. Hakuna sehemu nimesema hakina sera. Acha kuhemka.
 
Chadema ina wanachama hai 6.7m plus mashabiki CCM chalii usubuhi tuu ✌🏻
Mkuu umewahi kuangalia vizuri takwimu za waliopiga kura upinzani ndani ya chama chao kuchagua wawakili na wale wa CCM walipiga kura kuchagua wawakili ndani ya chama chao?
Umehesabu jumla kila upande kwa jimbo husika walikuwa wangapi?

Kwa mfano Mbeya wajumbe wa CDM walipiga kura kuwachagua akina Sugu (Mbilinyi) na wajumbe wa CCM waliowachagua akina Tulia walikuwa wangapi?

Kama CDM wapo 6.7M basi CCM wapo wengi sana, ila hiyo isiwatishe maana Kinana kasema ukweli siri ya wapiga kura ipo rohoni, anaweza kuwa CDM akampigia wa CCM au kinyume chake inawezekana pia.
 
Ushauri wako mzuri sana ILA sijui kama kwa mazingira haya watakuwa na AJENDA YOYOTE kwani zote zimeisha shughulikiwa na Rais Magufuli! Kero zao zote, nasema kero zao zote na vihoja vyao vyote vimesha pewa majibu muafaka na sahihi. Hawana hoja mpya this time, we ngoja uone!
Hili la ajira nalo limeshatatuliwa??
 
Hili la ajira nalo limeshatatuliwa??
Utatuzi wa tatizo la "ukosefu wa ajira" lazima kwanza uendane na mabadiliko ya mtazamo (MINDSET) ya mtafuta ajira au asiye na ajira! Suala la ajira ni SUBJECTIVE, wewe kwako ajira inaweza kuwa ni kupata "white collar job" huko maofisini ukiwa na tai yako; kwa mwingine ajira ni kazi inayompatia "mkate wake wa kila siku" iwe kufyeka nyasi kwa jirani yake, kulima shamba lake au la mwingine na kadhalika. Hivyo basi suala la KUTATUA ukosefu wa ajira ni PROCESS. haliwezi kuisha overnight! Hata hao CDM wangekuwa Ikulu wasingeweza kulimaliza overnight au for that for 50 years kwani kuna watu kama nyie mnaodhani ajira IKO MAOFISINI TU.
 
Utatuzi wa tatizo la "ukosefu wa ajira" lazima kwanza uendane na mabadiliko ya mtazamo (MINDSET) ya mtafuta ajira au asiye na ajira! Suala la ajira ni SUBJECTIVE, wewe kwako ajira inaweza kuwa ni kupata "white collar job" huko maofisini ukiwa na tai yako; kwa mwingine ajira ni kazi inayompatia "mkate wake wa kila siku" iwe kufyeka nyasi kwa jirani yake, kulima shamba lake au la mwingine na kadhalika. Hivyo basi suala la KUTATUA ukosefu wa ajira ni PROCESS. haliwezi kuisha overnight! Hata hao CDM wangekuwa Ikulu wasingeweza kulimaliza overnight au for that for 50 years kwani kuna watu kama nyie mnaodhani ajira IKO MAOFISINI TU.
Nakuona kama msomi kumbe huna lolote!!
Kupatika ajira ni kuboresha uchumi, ukibomoa uchumi kama ilivyofanyika usitegemee kuongeza ajira!!
Wafanya biashara wamekimbia maana Tz sio friendly kibiashara.
Makampuni viwanda maduka vimefungwa taxs sio friendly, hakuna mbinu nzuri ya kukusanya hiyo kodi ni dhuluma na unyanganyi watu wanakimbia!!
Ubabe umezidi busara na hekima, hali ya watanzani ni dhohofu bin hali!!
Muulize mtu wa Bank kama BoT au mwingineo upate ukweli!!
Nenda vijijini uone ukweli acha kujidanganya kwenye keyboard!!
 
Pamoja na kukubaliana na uliyoandika hapo juu kuhusu ajenda zinazowagusa wananchi kwa haraka na moja kwa moja, sikubaliani kabisa na kipande hiki nilichokinyanyua hapo juu.

Huwezi kuniambia kwamba mwanakijiji au mzee mjini haoni thamani ya kura yake anapokwenda kupiga kura, na kwa hiyo mshindi yeyote atakayetangazwa kwake ni sawa tu.

Kwa nini udhani tu kwamba huyo mzee mjini au raia kijijini hataki kusikia michango anayotoa mwakilishi wake bungeni kutetea waliyomtuma kuyawasilisha?

Kwa nini wewe unadhani watu hawa wanapoonewa huko walipo, na hata wakabambikiziwa makesi ya hovyo, kwao isiwe mhimu kuondoa ukiritimba huo, wewe unaona hayo ni yale yanayowahusu binaadam tofauti kabisa na wao wanaoishi nchi zingine?

Kila binaadam anataka atendewe HAKI, awe ni wa nchi zilizoendelea au hizi zetu za kiafrika.

Hizi mbinu mnazotumia kuwatishia ndizo mnazozigeuza kueleza kwamba wao haki zao sio mhimu kwao?

Hizo ajenda za mazao na mengineyo uliyotaja utazitenganisha vipi na hizi ajenda za msingi unazoona wewe kwamba sio mhimu kwa wananchi?

Kiongozi akiamua tu kwa hiari yake bila hata kujua taratibu zilizopo, akaingilia manunuzi ya mazao ya wakulima, kwa madaraka yake tu bila kufikiri madhara yanayoweza kuwapata wakulima kwa kukosa kabisa faida ya mazao yao, wewe hilo huoni kabisa kwamba ni ajenda inayostahili kufikisha kwa wananchi waelimishwe na wafanye maamuzi sahihi wasiendelee kupata hasara ya kazi zao?

Ajenda za msingi katika kampeni hii ni kuwaelimisha wananchi wajue haki zao, wasinyimwe haki kwa mabavu tu ya mtu mmoja kwa kutumia majeshi.
Wananchi wakizijua haki zao watakataa kuendelea kuonewa.

Tuachane na "siasa za kukariri..." - Hebu nieleze kama uliyoandika katika mstari huo sio mambo ya kukariri tu na kutumia mipasho unayoisikia ikitumika bila kuipa uzito wa fikra nyuma yake!
Kweli Kuna vitu vinategemeana, Ila vinahitaji kutolewa elimu ili wapiga kura waelewe

Mfano ili kufikia maendeleo endelevu tunahitaji Katiba Bora, kwa hiyo anatakiwa mgombea anayeweza kulink ubora wa Katiba na upatikanaji wa maendeleo kwa kila watu wa Calibre tofauti,

Ni jukumu la mgombea kutoa elimu kwa wapiga kura. Mfano Je Katiba mbovu, ukosefu wa haki, ufisadi rushwa, kutokuheshimu utawa Sheria na Katiba, ukosefu wa demokrasia na Uhuru vinawezaje kuchangia kushuka au kupanda kwa uchumi ambako kunapelekea matatizo mengi sugu vijijini na mijini

Kuwaambia wapiga kura kuwa utaondosha tatizo Fulani bila kuelezea chanzo Cha tatizo na mkakati mbadala ni utapeli tuliouzoea
 
Kweli Kuna vitu vinategemeana, Ila vinahitaji kutolewa elimu ili wapiga kura waelewe

Mfano ili kufikia maendeleo endelevu tunahitaji Katiba Bora, kwa hiyo anatakiwa mgombea anayeweza kulink ubora wa Katiba na upatikanaji wa maendeleo kwa kila watu wa Calibre tofauti,

Ni jukumu la mgombea kutoa elimu kwa wapiga kura. Mfano Je Katiba mbovu, ukosefu wa haki, ufisadi rushwa, kutokuheshimu utawa Sheria na Katiba, ukosefu wa demokrasia na Uhuru vinawezaje kuchangia kushuka au kupanda kwa uchumi ambako kunapelekea matatizo mengi sugu vijijini na mijini

Kuwaambia wapiga kura kuwa utaondosha tatizo Fulani bila kuelezea chanzo Cha tatizo na mkakati mbadala ni utapeli tuliouzoea
Mkuu 'mliberali', 'bottomline' ni hii: kuwepo kwa haki za wananchi na utawala bora kunazuia vipi kuwepo maendeleo?

Kwa nini watu wanyimwe haki, wakandamizwe kwa kisingizo cha kuleta maendeleo.
Hili sioni mantiki yake kabisa.
 
Yap wakishindwa waombe .msaada tupo watanzania wapenda mabadiliko ambao tupo tayari kuwafanyia hii kazi bure,

Na Mimi Ni muumin wa hayo mabadiliko... Natarajia wapinzani wakichukua nchi mabadiliko makubwa yatafanyika ktk nyazifa za serikali, taasisi na mashirika ya serikali.... Maana tumezoea kusikia majina na sura zilezile ktk uwaziri, makatibu wa kuu, ma dc na ma rc, wajumbe wa bodi za mazao nk..

Japo chadema wakati mwingine wanakera hasa kususia vikao vya bunge na uchaguzi mdogo... Hapo napata mashaka na maamuzi ya Hiki chama.

Chadema wapunguze kukosoa Kila Jambo la CCM... Waeleze raia umuhimu wa mabadiliko, Nini watawafanyia raia ktk maendeleo na mbadala kwa Yale yaliyofanywa na CCM.
 
Utatuzi wa tatizo la "ukosefu wa ajira" lazima kwanza uendane na mabadiliko ya mtazamo (MINDSET) ya mtafuta ajira au asiye na ajira! Suala la ajira ni SUBJECTIVE, wewe kwako ajira inaweza kuwa ni kupata "white collar job" huko maofisini ukiwa na tai yako; kwa mwingine ajira ni kazi inayompatia "mkate wake wa kila siku" iwe kufyeka nyasi kwa jirani yake, kulima shamba lake au la mwingine na kadhalika. Hivyo basi suala la KUTATUA ukosefu wa ajira ni PROCESS. haliwezi kuisha overnight! Hata hao CDM wangekuwa Ikulu wasingeweza kulimaliza overnight au for that for 50 years kwani kuna watu kama nyie mnaodhani ajira IKO MAOFISINI TU.
Mbona enzi za Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete tatizo hili halikuwa kubwa kama sasa??
 
Back
Top Bottom