Mkwavingwa
Member
- Jul 26, 2020
- 87
- 37
LISU hata akiyasema hayo hayatakuwa yakitoka katika dhati ya moyo wake, kiongozi kama jpm at least unaweza kuyaona machoni pake anayokusudiaMkuu hiyo kazi kaifanyia wapi? Hoja ya mleta uzi iko wazi kuwa ajenda ziwe za wananchi, na wala mgombea asiwe ajenda. Mfano mrahisi kwa sasa mwenye nyota ndani ya cdm ni Lisu. Hivyo anatakiwa akisimama aongee matakwa ya wananchi zaidi, na sio matatizo yake. Anatakiwa akimaliza kuongea mahitaji ya wananchi, hayo yakwake aongee kama ziada.
Kwa mvuto alionao Lisu akisimama na kusema kipaombele chake cha kwanza itakuwa ni kutoa ajira kwa vijana, kukuza kilimo na kuboresha masoko, akisema atashusha vifaa vya ujenzi ili kila mtu ajenge nyumba bora, akisema atashusha gharama za matibabu nchini ili kila aweze kutibiwa, huoni hapo atavuta wapiga kura wengi wa ukweli?