Ushauri kwa CHADEMA: Japo ni Haki, lakini chondechonde Msiandamane. Mwenye Nguvu Mpishe!

Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
....ondoa hiyo 'kama'.,sema mtashikilia msimamo wenu!..
..si huwaga mnajinasibu hata Mandela alikaa jela zaidi ya miongo miwili,nendeni sasa to that extreme end KAMA kweli mna dhamira ya dhati ya ukombozi kwa wananchi maskini!
....tena na nyie viongozi viongozi muwe frontline.,sio mnatoa matamko tu huku nyie mnapigwa na viyoyozi!
 
Huu ndio wakati hasa wa CHADEMA kuionyesha dunia kuwa wao ndio chama kikuu cha upinzani Tanzania vyenginevyo wakishindwa tena huu mtihani uliopo mbele yao watakosa sifa zote za Kuwaita wao chama kikuu cha upinzani.

Niwakati muufaka wa wao kuidhihirisha kwa vitendo slogan yao ya "PEOPLE'S POWER" na waondokane na kuitamka kwa maneno tu.

Hali kama hii ya siasa iliwahi kutokezea wakati wa Mh. Mkapa baada ya uchaguzi mkuu wa 2000 pale alipozuia harakati zote za kisiasa kwa wapinzani ili aachiwe yeye na serikali yake watekeleze ilani yao.

Kwa wakati huo CUF ndio iliyokuwa chama kikuu cha upinzani hawakuikubali hii hali na ikapelekea kuja na slogan ya "JINO KWA JINO" kama ishara ya Kapinga ukandamizaji wa CCM na serikali yake.

CUF kupitia kiongozi wao SHUPAVU Professor Lipumba wakaipinga hii hali kwa maandamano ya lazima ambayo yanaruhusiwa kikatiba.

Pamoja na Mh. Mkapa na Mahita kuyapiga marufuku kwa nguvu zao zote CUF kupitia wanachama wao shupavu waliandamana na wengi wao wakauliwa, wakajeruhiwa na kupata ulemavu wa kudumu lakini walifanikiwa kuiondoa hali iliyokuwepo na siasa zikarudi kama kawaida kwa wapinzani.
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
Unadhani Magufuli kama Lowasa? Sasa jaribuni muone moto wake.
 
Pasco bado kidogo sana utang'olewa kucha au meno au vyote kwa pamoja, tena bila ganzi.
Unathubutu kumwita DICTACTOR mheshimiwa mtukufu sana rais ambaye hatakiwi kukosolewa na mtu yeyote! mark my words.
 
Wanabodi,

Kama kawaida yangu kutoa ushauri wa bure, huu ni ushauri wa bure kwa Chadema, japo kuandamana na mikutano ya kisiasa ni haki iliyotolewa kihalali ndani ya katiba, nawashauri kwa dhati kabisa, tafadhalini sana msiandamane, na kusitisha hiyo Operesheni UKUTA, ili kuutumia ule msemo wa Kiswahili "Mwenye nguvu mpishe", hata kama una haki, usitake kujipima nguvu kwa kutunishiana misuli na mtu mwenye nguvu zaidi yako, na sio tuu ana nguvu zaidi yako, na tayari, umeishajua ni dikiteta, bali ndio mwenye nguvu ya dola mikononi mwake!.

Misingi ya Katiba na The Rule of Law
Tanzania ni nchi inayofuata misingi ya katiba na sheria, (the rule of law) ambapo inapaswa kuendeshwa kwa mujibu wa sheria, taratibu na kanuni, na sio kwa matamko ya viongozi yanayokwenda kinyume cha katiba!.

The Separation of Powers & Check and Balance .
Nchi yetu ina mihimili mikuu mitatu, Serikali, (the executive), Bunge (The Legislature) na Mahakama (The Judiciary). Mihimili hii mitatu, ilipaswa kufanya kazi kwa kujitegemea bila mhimili mmoja kuingilia mhimili mwingine (independence), huki kila mhimili uki act as a watchdog wa muhimili mwingine usivuke mipaka ya madaraka au mamlaka yake yaani (The sepaation of powers check and balance).

Serikali yenye Nguvu, Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo!.
Mihimili hii, inaongozwa na viongozi ambao wana mamlaka kuu kuhusu mihimili yao. President ndio mkuu wa the executive, Spika ndio mkuu wa The Legistlatue, na Jaji Mkuu, ndie mkuu wa The Judiciary, lakini pamoja na nia njema kuwa mihimili yote inamamlaka na hakuna mhimili wowote uliokuwa unapaswa kuwa na mamlaka kuliko mhimili mwingine, lakini kiukweli, mhimili wa the executive ndio mhimili mkuu unaomiliki vyombo vya dola na kuitawala mihimili mingine yote!, hivyo mkuu wa the executive, yaani rais, ndio kila kitu!, akisema!, amesema!.

Rais Magufuli na Uvunjaji wa Katiba.
Tuambiane ukweli, tangu rais Magufuli ameingia madarakani, sio mara moja au mbili amekuwa akitoa kauli tata, zinazokwenda kinyume cha katiba, mhimili wa Bunge na Mahakama ilipaswa kuingilia kati kwa kumcheck mkuu wa the executive, lakini vyombo hivyo vimekaa kimya hivyo kumfanya rais ajisikie kuwa he is always right! kwa kanuni ya "the boss is always right!".

Udikiteta wa Magufuli.
Hoja kama Magufuli ni dikiteta au la, haina mjadala, Magufuli ni dikiteta wa ukweli ambaye hana msalie mtume, na alipoingia tuu madarakani, alianza kuonyesha udikiteta wake right away kwa kuliingilia bunge na mahakama kuziweka chini ya amri zake!. Lile katazo lake la watumishi wa umma hawaruhusiwi kusafiri safari za nje bila kibali chake kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, liliwahusu watumishi wote wa serikali, likiwemo bunge na mahakama!, just imagine Jaji Mkuu na Spika wa bunge wakapige magoti kwa rais kuomba kutimiza wajibu wao!.

Baada ya katazo lile, checks and balance zingepaswa kuanzia hapo kwa Jaji Mkuu kumweleza rais huko ni kuingilia uhuru wa mahakama (the independence of the judiciary) hivyo muhimili wa mahakama haukupaswa kujisubmit chini ya the executuve, bali mamlaka hayo ya kuzuia safari za nje, Spika alipaswa kuwa nayo kudhibiti safari za mhimili wa bunge, na Jaji Mkuu alipaswa kuwana nayo kudhibiti safari za mhimili wa mahakama, lakini mihimili hii ilikaa kimya kwa kujisubmit chini ya the executive, hivyo kumfanya rais ndio kila kitu!.

Hivyo sasa rais Magufuli ndio kila kitu, hakuna cha bunge, mahakama, wala katiba, amri ya rais ndio kila kitu na ndio sheria kuu!, hivyo nawashauri Chadema kwa dhati kabisa, wasitishe maandamano yao, wasifanye kabisa mchezo wa kumjaribu Ngosha, wataumia bure!.

Hili la udikiteta wa rais Magufuli, tumeisha lizungumza sana humu
Magufuli ni Dikiteta!, Tanzania Ilihitaji Dikiteta, Tumempata ...
Rais Magufuli, Waliomchagua Wanajuta!, Wasiomchagua Wanamshangilia ...
Kama sio udikteta, Mhe. Rais futilia mbali utawala wa sheria ...
Utumbuaji Majipu wa Rais Magufuli: Is It A Right Thing, At The ...
Je, Hizi Terorizing za Ziara za Kushtukiza, Hakutajenga Nidhamu ya ...
Rais hana mamlaka ya kupunguza mshahara wa mtumishi yeyote | Page ...
Nimetishwa, Kushitushwa na Kuogopeshwa na Kauli Hii ya Rais ...
Hili la Polisi kuruhusiwa 'kuwanyanganya' silaha majambazi na ...
Mnatambua kuwa baadhi ya Maamuzi ya Magufuli yanaligharimu Taifa ...

Ila kitu kimoja kuzuri kuhusu udikiteta wa rais wetu, ni Rais Magufuli ni dikiteta mzalendo!, mwenye uchungu na umasikini wa nchi hii, mwenye nia njema ya kusafisha uozo wote wa uzembe, rushwa na ufisadi, na kulikomboa taifa letu toka kwenye lindi la umasikini uliotopea na kuwa nchi ya maziwa na asali kupitia uchumi wa gesi na viwanda.

Mungu mbariki Magufuli!.

Mungu ibariki Tanzania.

Wasalaam.

Pasco
Rejea za shauri za bure
Ushauri wa Bure Kwa Lowassa: Kwa Vile ni Magufuli, Kubali Matokeo ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Hata kama ni kweli uliibiwa kura; Kaa ...
Ushauri wa Bure kwa CCM: Hope for the best but get prepared for ...
Ushauri wa Bure kwa Mhe. Lowassa: Ili kuilinda Heshima yako ...
Ushauri wa Bure kwa ZZK!-Congratulations..But,,,!, Be Calm!, Keep ...
Ushauri wa Bure Kwa Hon Dr. Harison Mwakyembe (Mb)-Kwa Hili la ...
Ushauri wa Bure Kwa Mhe. Zitto on Escrow Report: Please Keep Quite ...
Ushauri wa Bure kwa CHADEMA: Heri Nusu Shari Kuliko Shari Kamili ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Magufuli, Futilia Mbali Utawala wa Sheria ...
Ushauri wa Bure kwa Rais Kikwete, muombe msamaha Lowassa kabla ya ...
Ushauri wa Bure kwa Lowassa: Usikanyage Arumeru!, Atamponza Sioi!.
Ushauri wa Bure kwa Dr. Shein: Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar ...
Ushauri wa Bure kwa Magufuli, DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es ...


Pasco kuna tofauti kati ya kuandamana na kufanya mikutano. CHADEMA wamedhamiria kufamya mikutano na sio kuandamana!
 
Pasco nadhani elimu yako inatosha Ila ushauri kwa CHADEMA waambie waliokutuma pamoja na ngosha mwenzio pelekeni maziwa makuu inaeleweka
 
Unajua kwa tanzania elimu ya siasa na uraia kuna mapungufu sana........
Kiukweli wapinzani pamoja na serikali wote wanamaeneo wanakosea pia wanapatia.........
Nikianza na wapinzani........hawa mlengo wa hoja zao zimekaa kukosoa serikali sio kwa lengo la kuijenga bali kuiharibia ili nao wapate ridhaa ya wananchi katika kuliongoza taifa.....hili si jambo zuri hata kidogo.......huu ni usanii kabisa....

Nitawapa mfano wa inshu ya sukari.........wabunge wengi wa upinzani walichachamaa sana kwa kuwaambia wananchi kuwa serikali haiwatakii mema kwa kuzia uagizaji wa sukari usio fuata taratibu za kisheria za biashara katika manunuzi........nakumbuka walituhadaa wananchi kuwa sukari haitokuja kushuka maana serikali inakosea......leo hapa mimi nipo kilimanjaro nimetoka kununua sukari kilo 1800. Tokea ilipokuwa 3000. Sasa najiuliza huwa wapinzani wakiongea wanatumia taarifa za wapi.......maana ni kama wanapotosha uma.........mimi naona ni kama wanaweka jitihada nyingi kubeza jitihada zinazofanywa na kupotosha uma wa watanzania.......na asilimia kubwa ya watanzania si wafuatiliahi huwa wanajiridhisha na story za kusadikika ama za mtaani au post za facebook ambazo huwa wanaozipost hawajulikani ni akina nani plus wanamalengo gani.......

Swala la elimu......wanabeza sana maamuzi ya kuweka vigezo ambavyo vitarejesha thamani ya elimu sio kama sasa kila mtu anadegree uchwara halafu uwezo zero kazi kupiga domo tu.....wapinzani wanakazana kuropoka tu ili wapate hii popularity kama ya akina wema na diamond kwa kuropoka.......

Me nasema mh.raisi yupo sahihi kukataza hizi kelele zisizo na tija yeyote ........hawa wapinzani si muda wote.wapo sahihi......wanayohaki ya kuikanya......kuirekebisha na kuikosoa serikali.......ila sio kwa staili hii wanavyofanya ya kuibeza na kuikejeli badala ya kuishauri.............wapinzani hawaongei jipya kazi yao ni kubeza .Unapomkosoa mtu......toa suggestion ......au wazo mbadala ila sio unangojea mwenzako akosee ndipo povu likutoke........tena unatoa kauli za kuhatarisha amani na usalama wa raia........

serikali ni kweli inakosea kuwazuia wapinzani kuongea na uma lakini ni kwasababu wamegundua mnaitumia fursa hiyo kuongea vijembe.....na kukejeli serikali ndio maana wanawabana kwa kila namna .......hata ningekuwa mimi nisingeruhusu mtu ambaye hauna ridhaa ya kuendesha nchi uongee maneno ya uchochezi badala ya kutoa ushauri.......hii kitu alishaifanyaga mbatia mara moja tu......aliishauri serikali kuhusu kuhamisha maofisi yao maeneo ya posta na kuyasambaza maeneo mengine ili kupunguza msongamano wa foleni za magari asubuhi watu wanapokwenda makazini maana msongamano huu unaitia serikali hasara kila siku ya mabilioni......na ndio maana kikwete akamkubali sana akampa nafasi ubunge viti maalumu.........mrema huyo hapo amepewa nafasi anashirikiana na serikali......huo ndio upinzani wa ukweli unatakiwa kuwa sio hawa wakina zitto wanakwenda kusoma vitabu na notes za shule wanakuja kutuletea theory za utabiri hapa.....wanaboa sana......
 
Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!

Hii kauli inaqualify kuitwa mkakati wa uhaini.

Rais aliyechaguliwa kikatiba hakuna njia isiyo ya kihaini ya kumtoa madaraka kabla ya uchaguzi.
 
Kwahiyo unatushauri tuwe kama Bunge Butu na Mahakama Kibogoyo ili ajiskie always Right.

Huyo Mungu uliemuomba ambariki huyo mvunja katiba ungeanza kwa herufi ndogo jina lake isomeke 'mungu' na sio "Mungu"


Tena tuliosema atakua one term president tulikosea hata term moja hatamaliza kama tutashikilia msimamo wetu Septemba mosi na tunaweza kuigeuza ajenda ikawa ya kumng'oa ikulu.

He should be careful of what he wish for!
Watch out.. Mnataka ku over through the government... Watanzania wazalendo tumempa kura Magufuli na tunamwamini.. Nyie subirini 2020 muonekano anavoshinda kwa kishindo.. Watanzania wana akili na niwaelewa msidhani mashabiki wa ukawa bado mpo Milion 6..mmepungua sana mpo million 3
 
Uzuri wa kitu ninachopenda kwa Magufuli....atafanya anachokisema,hana msalia mtume kwa vichwa maji na wenye viburi na alishasema ana mkataba wa miaka mitano na wananchi wake tu basi.....sasa nyie Warombo mnataka mkaandamane kahama huku majimbo yenu yako salama tu

Ajaribu kufanya
The world is watching......na Tanzania ni sawa na tone la maji katikati ya maji ya bahari!!
I hope, umenipata.....
 
Unadhani magufuli mjinga kama Lowasa? Sasa jaribuni muone moto wake.

Mbona nyinyi WAGALATIA huwa hamna hekima ya kuheshimu wakubwa ambao wanaweza wakawa na umri sawa sawa na wazazi wenu!!!????

Hivi akitokezea mtu akamwita baba au mama yako "MJINGA" wewe utaridhika na hiyo hali!!??? Kama haoutoridhika basi vivyo hivyo watoto wa Mh. Lowassa hawafurahii kuona baba yao anatukanwa hivyo.

Mimi nadhani CCM wengi wenu ni wanawaharamu maana hii tabia yako ndio tabia ya wanachama na wapenzi wengi wa CCM.

Ukienda Zanzibar wako watu kama wewe ambao tabia zenu mnafanana "AKINA SHAKA HAMDU, BORAFYA NA MAREHEMU ASHA BAKARI"

hivi haitoshi kupingana na mpinzani wako kwa maneno na vitendo vya heshima!!!!!!???????????

JIFUNDISHE KUWEKA AKIBA.
 
Watch out.. Mnataka ku over through the government... Watanzania wazalendo tumempaTa kura magufuli na tu namwamini.. Nyie subirini 2020 muonekano anavoshinda kwa kishindo.. Watanzania wana akili na ni waelewa msidhani mashabiki wa ukawa bado mpo Milion 6..mmepungua sana mpo million 3

KAMA CCM wanajiamini kuwa wananchi wanawapenda basi waweke tume huru za uchaguzi na waruhusu katiba ya warioba ipigiwe Kura.

Vyenginevyo wanajitekenya na kucheka wenyewe
 
Back
Top Bottom