Ushauri kuhusu mkopo wa gari

Habari wanajf;
mimi ni mtumishi wa umma na kipato changu ni Tsh 400000/=(take home)
nataka kukopa mojawapo ya gari hizi forester/ suzuki escudo/corona premio.
Naomba ushauri kama kuna sehemu naweza kupata mkopo wa aina hiyo(achilia mbali kukopa fedha taslimu kutoka bank)
msaada jamani nshachoka kupanda dala dala.
Kwa ushauri tafuta Collora XE/SE 110 au Collora Filieder ZNE Vvt i ni gari zinatumia mafuta kidogo (CC 1500) kulinganisha na gari kama Premio (CC 1800- 2000). Spea zake zinapatikana kwa wingi bila shida kifupi Nairobi haitakuhusu kabisa.
Taratibu za Exemption ni hizi:-

  • Mshahara wako uaanzie TGSD (kwa wewe ume qualify)
  • Kodi zinazo samehewa ni Import Duty (25% ya CIF) na Execise dut(5% kwa gari zenye CC (0-1500) na 10% kwa gari zenye (CC 1501- ). Uchakavu hausamehewi na ni 20% kabla ya VAT(18%). Uchakavu ni kwa magari yote yalitengenezwa zaidi ya miaka kumi, hivyo ukiagiza gari la mwaka 2001 kwa saizi hadi lifike litakuwa tayari limeshamaliza miaka kumi toka kutengenezwa hivyo uchakavu ni lazima ukuhusu.
  • Unaandika barua kupitia mwajiri wako kwenda Sub Treasury baada ya kujazwa fomu toka TRA ambayo inajieleza. Viambatanisho katika barua hiyo ni Salary Slip (Current), barua ya kupandishwa cheo kama ulikuwa hujafikia daraja hilo, TIN namba.
  • Gari liwe kwa matumizi ya kawaida na siyo biashara.
Kifupi huo ndiyo utaratibu lakini unahitaji ufatiliaji kidogo.
Kama unataka kukopa ni bora ukakope kwenye bank/ SACCOS (kama mnayo kwa minajili ya riba) kuliko kwenda kwenye makampuni yanayouza magari watakupiga riba kubwa sana.
Ushauri wa mwisho, kabla ya kukopa hakikisha umesave angalau 1.6m -2.0m ili ujazie hicho kiasi kingine na ubakie hata na salio kidogo la kulihidumia gari hilo kwa kuweza kulipa motorvehicles license na mingeneyo ya barabarani.
Kila la kheri katika safari yako ya kutaka kutembea huku UMEKAA.
 
Daladala ni shida wazee, unyunyu wote unaisha ukitoka unanuka mchanganyiko wa pafyumu na vikwapa
me nakushauri uchukue ka-starlet ndugu yangu kanaserve the purpose, na hako kampunga kalivyo kaduchu utamudu tu.
SWALI KWA WANAJF: kati ya CAMI(TOYOTA) na TERRIOS(DAIHATSU) ipi bora coz naona zinafanana ila sijajua ki-maintenance na spares ziko vipi, naomba msaada wenu kabla sijaangukia pua.
 
Mimi nakushauri ukope pesa bank ya wanawake, kukopa gari si rahisi itakugharimu sana afadhali kukopa fedha..
 
Kwa take home hiyo, nenda kakope mkopo wa muda mrefu, CRDB Bank.
Utatakiwa kwenda na :-
1. copy yako ya appointment letter, ili kuthibitisha wewe ni permenent pensionable.
2. Slip za miezi 3.
3.Watakupa form itakayosainiwa na mwajiri as guarantee.
4. Utakopeshwa mshahara wako wa mwezi mara miaka 4 hivyo ni 400,000 x 12 x 3 =14,400,000/=
5. Utaulipa mkopo huo ndani ya kipindi cha miaka 6 with interest ya 10%, hivyo kila mwezi utalipa 220,000/=
4. Kwa vile take home yako ni 400,000 na wewe unaweza kulipa deni la 300,000 kwa mwezi, lazima uithibitishie benki, una other source of income ili waweze kukata more than 50% ya net, kisheria, benki wanaruhusiwa kukata only 33% ya gross.
5. Kwa milioni 14,400,000 unaweza kumiliki your dream car, but think of running cost na durability, usije kumaliza kulipa deni na gari kuishia juu ya mawe.

mkuu una uhakika ?mbona huu mkopo unaonekana rahisi sana!
 
Kwa ushauri tafuta Collora XE/SE 110 au Collora Filieder ZNE Vvt i ni gari zinatumia mafuta kidogo (CC 1500) kulinganisha na gari kama Premio (CC 1800- 2000). Spea zake zinapatikana kwa wingi bila shida kifupi Nairobi haitakuhusu kabisa.
Taratibu za Exemption ni hizi:-

  • Mshahara wako uaanzie TGSD (kwa wewe ume qualify)
  • Kodi zinazo samehewa ni Import Duty (25% ya CIF) na Execise dut(5% kwa gari zenye CC (0-1500) na 10% kwa gari zenye (CC 1501- ). Uchakavu hausamehewi na ni 20% kabla ya VAT(18%). Uchakavu ni kwa magari yote yalitengenezwa zaidi ya miaka kumi, hivyo ukiagiza gari la mwaka 2001 kwa saizi hadi lifike litakuwa tayari limeshamaliza miaka kumi toka kutengenezwa hivyo uchakavu ni lazima ukuhusu.
  • Unaandika barua kupitia mwajiri wako kwenda Sub Treasury baada ya kujazwa fomu toka TRA ambayo inajieleza. Viambatanisho katika barua hiyo ni Salary Slip (Current), barua ya kupandishwa cheo kama ulikuwa hujafikia daraja hilo, TIN namba.
  • Gari liwe kwa matumizi ya kawaida na siyo biashara.
Kifupi huo ndiyo utaratibu lakini unahitaji ufatiliaji kidogo.
Kama unataka kukopa ni bora ukakope kwenye bank/ SACCOS (kama mnayo kwa minajili ya riba) kuliko kwenda kwenye makampuni yanayouza magari watakupiga riba kubwa sana.
Ushauri wa mwisho, kabla ya kukopa hakikisha umesave angalau 1.6m -2.0m ili ujazie hicho kiasi kingine na ubakie hata na salio kidogo la kulihidumia gari hilo kwa kuweza kulipa motorvehicles license na mingeneyo ya barabarani.
Kila la kheri katika safari yako ya kutaka kutembea huku UMEKAA.

nimeupenda sana ushauri wako, umejaa busara , hekima na weledi wa hali ya juu sana.
 
Habari wanajf;
mimi ni mtumishi wa umma na kipato changu ni Tsh 400000/=(take home)
nataka kukopa mojawapo ya gari hizi forester/ suzuki escudo/corona premio.
Naomba ushauri kama kuna sehemu naweza kupata mkopo wa aina hiyo(achilia mbali kukopa fedha taslimu kutoka bank)
msaada jamani nshachoka kupanda dala dala.

Kamata tuktuk tu mwisho wa matatizo. Itaendana na kipato chako.
Ukiweka wese la buku 5 unazunguka round 4
Gari kwa sasa mafuta bei juu lt1=2000 ambapo kwa wiki utatumia mafuta si chini ya 80,000 pamoja na misele yako ya hapa na pale kwa mwezi piga hesabu hapo na kipato chako ni hiyo kilo 4 + na makato ya kwenye mkopo utajikuta unapokea take home chini ya laki 4 aangalia usije ukalipaki ukawa unatembelea week end tu kwa ajili ya maumivu ya mafuta.
 
Hongera mkuu kwa kuamua kujikwamua. Ila pole pia kwa mihangaiko.

Kotokana na kipato ulichoweka hapo juu, ningekushauri utafute gari isiyozidi 1500cc kwa sababu zifuatazo.

1) Ushuru wa TRA (Road License) ni nafuu kwa gari ndogo < 1500cc
2) Uta-save pia kwenye mafuta. Matumizi makubwa ya gari yapo kwenye mafuta, na sio service wala spea.
3) Service ya engine ndogo ni bei ndogo sana, tofauti na engine kubwa.

Kwa collora Premio, sijawahi ona yenye engine ya 1500cc, ila nafahamu ipo ya 1600cc na ulaji wake wa mafuta ni mzuri sana. Spea pia zipo na bei ni nafuu sana. Ila kuna Premio za 2000cc, hizo sifahamu utumiaji wake wa mafuta ukoje, labda mdau mwingine atufahamishe.

Ila pia, unaweza jaribu Toyota Raum, ni 1500cc na utumiaji wa mafuta ni mzuri. Spea pia zipo nyingi na bei ni nafuu. (In fact, Raum inatumia spea za corrolla, na engine yake ni ile ile ya Toyota Starlet)

Mambo mengine ya jinsi ya kupata mkopo, ngoja tusubiri wadau tuone wanalipi la kuchangia.

Hapo kwenye red ndo huwa nachanganyikiwa nashindwa kuelewa which is which. Kama raum, corrola na starlet zinatumia engine aina moja iweje ziwe na cc tofauti? Mfano raum zina cc 1500 na starlet cc 1300. ufafanuzi please
 
Kwa mshahara huo sidhani utaweza kumudu gari hapa mjini ukitilia maanani kwamba on average lazima uweke petrol ya shs. 10,000.= kwa siku; bado spear na bado kula yako na wanao kutegemea. Pia bado riba ya benk ambayo on avrage ni 22% katika benki zetu hapa nchini.

Vipi pikipiki? Napona ndo size yako.
we bado uko very naive aisee, aliyekwambia ukilipwa laki nne ndo huwezi kuendesha gari mjini nani? hizo laki nne ni zinazoingia benki kila mwezi kama mshahara uliowekwa na serikali lakini in reality watu wana link za pesa nyingi tu huko serikalini kuliko huku private, unakuta ndani ya mwezi ana semina ya wiki mbili nje ya mkoa, mara kaenda swaziland training kwa miezi 2, marra sitting allowence, so usiogope mkuu, pesa ipo ndo maana akasema anawezakatwa hata laki tatu out of laki nne, au labda ana miradi yake inamlipa zaidi kuliko kazi.
 
Daladala ni shida wazee, unyunyu wote unaisha ukitoka unanuka mchanganyiko wa pafyumu na vikwapa
me nakushauri uchukue ka-starlet ndugu yangu kanaserve the purpose, na hako kampunga kalivyo kaduchu utamudu tu.
SWALI KWA WANAJF: kati ya CAMI(TOYOTA) na TERRIOS(DAIHATSU) ipi bora coz naona zinafanana ila sijajua ki-maintenance na spares ziko vipi, naomba msaada wenu kabla sijaangukia pua.
Hata mimi nasubiria jibu. Ila CAMI naona bei juu.. Tusubiri wataalam
 
Huyu anahitaji mkopo wa Gari...

Hivi kuna huduma hizo hapa TZ? Nahisi hilo gari by the tym unamaliza kulilipia inakuwa kama umenunua magari mawili

Nenda Conti-cars opposite na holiday inn mpya, walishawahi kuniambia wanafanya mikopo ya aina hiyo ila ni lazima wamshirikishe mwajiri na pia unasettle down payment hiyo nyingine ndio wanachanja taratibu...of course with high interest.
 
nitafute nikupe carina ya 2002 bei ni milioni nane unatoa asilimia 60 ya hiyo pesa alafu kila mwezi utakuwa unanipa laki tano
 
Hongera mkuu kwa kuamua kujikwamua. Ila pole pia kwa mihangaiko.

Kotokana na kipato ulichoweka hapo juu, ningekushauri utafute gari isiyozidi 1500cc kwa sababu zifuatazo.

1) Ushuru wa TRA (Road License) ni nafuu kwa gari ndogo < 1500cc
2) Uta-save pia kwenye mafuta. Matumizi makubwa ya gari yapo kwenye mafuta, na sio service wala spea.
3) Service ya engine ndogo ni bei ndogo sana, tofauti na engine kubwa.

Kwa collora Premio, sijawahi ona yenye engine ya 1500cc, ila nafahamu ipo ya 1600cc na ulaji wake wa mafuta ni mzuri sana. Spea pia zipo na bei ni nafuu sana. Ila kuna Premio za 2000cc, hizo sifahamu utumiaji wake wa mafuta ukoje, labda mdau mwingine atufahamishe.

Ila pia, unaweza jaribu Toyota Raum, ni 1500cc na utumiaji wa mafuta ni mzuri. Spea pia zipo nyingi na bei ni nafuu. (In fact, Raum inatumia spea za corrolla, na engine yake ni ile ile ya Toyota Starlet)

Mambo mengine ya jinsi ya kupata mkopo, ngoja tusubiri wadau tuone wanalipi la kuchangia.

mkuu namie nisaidie hapa; gari 1500cc ya mwaka 2000, FOB 2600USD, Je nikitaka kuinunua itani cost tsh ngapi mpa inaingia barabarani?
 
we bado uko very naive aisee, aliyekwambia ukilipwa laki nne ndo huwezi kuendesha gari mjini nani? hizo laki nne ni zinazoingia benki kila mwezi kama mshahara uliowekwa na serikali lakini in reality watu wana link za pesa nyingi tu huko serikalini kuliko huku private, unakuta ndani ya mwezi ana semina ya wiki mbili nje ya mkoa, mara kaenda swaziland training kwa miezi 2, marra sitting allowence, so usiogope mkuu, pesa ipo ndo maana akasema anawezakatwa hata laki tatu out of laki nne, au labda ana miradi yake inamlipa zaidi kuliko kazi.
kweli bana. muerezee
 
Askofu,

Corolla Spacio XG Edition zipo zenye 1800cc, hizi zinatumia engine ya 1ZZ-FE, na zipo za 1500cc ambazo zinatumia engine ya 1NZ-FE.

Engine ya 1NZ-FE inatumika kwenye Toyota IST, Corolla RunX, Toyota Allex, Corolla Fielder etc.

Kwa kifupi, engine zote za 1NZ-FE na 1ZZ-FE zinatumika kwenye magari mengi sana.

Ila, kama ilivyo kawaida, gari nyingi mpya huwa na shida ya spea kidogo na bei huwa juu. Lakini kutokana na engine ya 1ZZ na 1NZ kuwa na matumizi katika gari nyingi, hakuta kuwa na ishu ya spea sana kwenye engine. Isipokuwa, spea zitakuwa ishu kwenye Body Parts, kama vile taa, side mirrors n.k.

Engine zote zina VVT-i, hivyo tegemea matumizi mazuri ya mafuta.

Bei ya manunuzi pia ipo juu. Gari zinazotumia engine nilizozitaja hapo juu, nyingi FOB ni $3,600. Kwa mahesabu ya haraka, kuifikisha hapa home na kuitoa bandarini, andaa kitu kama 11M kwenda mbele.

Kama budget yako ni nzuri, tafuta Spacio XG Edition 1,500cc. Hii gari iko safi mzee, kuanzia interior hadi exterior design, performace and fuel economy. Ila, kutokana na suala la body parts kuwa expensive, tafuta Comprehensive Insurance, just in case umegongwa au umegonga gari ya mwenzako.

Kwa kifupi. Kama wewe ni mwendeshaji mzuri wa gari, itakuchukua mwaka mmoja na nusu au miwili (pengine hata zaidi) kabla hujaanza kutafuta spea ilala. So upatikanaji wa spea sio ishu sana kama wewe ni mtunzaji mzuri wa gari. Ishu ipo kwenye fuel consumption, maana hilo haliepukiki.

Mengineyo:

Kama budget ya Spacio XG haijakaa sawa, check Toyota Corolla Fielder XG Edition. Zote zinatumia engine hiyo hiyo, tofauti body tu! Utumiaji wake wa mafuta ni mzuri sana. Ukitoa macho sana kwenye internet, unaweza ukaingiza hichi kitu hapa nyumbani kwa 6.5M - 7.4M. Kazi kwako.

Impressive!
Inafurahisha mtu anayeelewa jambo anapochangia.Being a professional in my own field niko impressed mzee.
Thanks.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom