Ushauri katika utata huu

Ushauri katika utata huu

CharmingLady

JF-Expert Member
Joined
Apr 16, 2012
Posts
18,304
Reaction score
12,997
Habari zenyu binafsi wanajamvi…… Natumaini mko pouwa!!!!!!

Kutokana na kufahamiana mpaka kukutana na baadhi ya memberwa JF, nimekuwa nikipata shida katika kuomba ushauri wa baadhi ya mambo. Mfano1: Nina tatizo la kiafya na ninataka kuomba ushauri, nashindwa kufanya hivyokwa sababu unakuta flani ananifahamu kiuhalisia. Atajua kwamba nasumbuliwa natatizo Fulani la kiafya kitu ambacho sitopenda mtu mwingine afahamu zaidi yamshauri (Daktari).

Mfano 2: NInaweza kuwa na tatizo katika mahusiano yangu auhata kifamialia na ninahitaji ushauri , nashindwa kuomba ushauri kwani kila anayenifahamu kiuhalisia atajuakuwa nina tatizo katika mahusiano yangu au familia yangu.

Wadau, nifanyeje ili nisijulikane wakati Mods wanapingaissue ya kuwa na multiple IDs???????

(Nahisi pia kuna watu watakuwa na tatizo kama langu)

Wabheja sana!!!!! :A S angel:
 
Usiogope watu. Omba ushauri bila kuwa na shaka. Tatizo laweza kuwa kubwa kama utashndwa kuomba ushauri kwa sababu ya kuogopa watu.
 
Mficha maradhi kifo humuumbua,hakuna mwanadamu asiyekuwa na tatizo hivyo kuweka wazi matatizo yako ni jambo litakalokusaidia wewe katika maisha yako si hao wanaukufahamu.
 
Mficha maradhi kifo humuumbua,hakuna mwanadamu asiyekuwa na tatizo hivyo kuweka wazi matatizo yako ni jambo litakalokusaidia wewe katika maisha yako si hao wanaukufahamu.

Ukweli.. charminglady usiogope watu.
 
Last edited by a moderator:
Umekosea sana! Ulitakiwa hilo tatizo lako! Ulisemee mwingine!! Liwe tatizo lako lakini ukimuhusisha mwingine!!! Sasa hivi jf unaweza kumuongelea jamaa yako wa karibu sana! Kumbe naye yumo humu!!,, tumia PM kwa watu unaoona hapa jamvini wana upeo na hilo tatizo lako!!@charminglady weka aibu pembeni my dada
 
hapa naona akili ya mama/baba USHAURI iliwaza mbali sana sana. hili ni tatizo kwa mtu mwenye aibu ingawa kwa mtu free kama mm sio ishu kabisaa ingawa jamvini nusu yao wananijua na nimewah kuonana nao ila nikipata gumu huwa nalirusha live. na hata majuzi tu nimetoka kuomba ushauri hapa licha ya kwamba niliyoyaeleza wengine walibahatika nikiwa kwenye hali hiyo.

ushauri wangu kwako m-pm USHAURI atakusaidia na kama ni wa kitabibu pia anaweza kukusaidia.
 
Last edited by a moderator:
hapa naona akili ya mama/baba USHAURI iliwaza mbali sana sana. hili ni tatizo kwa mtu mwenye aibu ingawa kwa mtu free kama mm sio ishu kabisaa ingawa jamvini nusu yao wananijua na nimewah kuonana nao ila nikipata gumu huwa nalirusha live. na hata majuzi tu nimetoka kuomba ushauri hapa licha ya kwamba niliyoyaeleza wengine walibahatika nikiwa kwenye hali hiyo.

ushauri wangu kwako m-pm USHAURI atakusaidia na kama ni wa kitabibu pia anaweza kukusaidia.
unasema ukweli kabisa, kuna watu wa aina yako ambao wanawaza kutatua matatizo yao tu, haijalishi nani anajua....
lakini kuna watu kama hao akina charminglady inakuwa ngumu kidogo. nadhani USHAURI lilishamtokea hilo ndo maana akaamua kuanzisha ile ID ili watu kama huyu na wengine watupie matatizo yao kwake.
 
Last edited by a moderator:
Mficha maradhi kifo humuumbua,hakuna mwanadamu asiyekuwa na tatizo hivyo kuweka wazi matatizo yako ni jambo litakalokusaidia wewe katika maisha yako si hao wanaukufahamu.

Ni kweli mkuu... Mficha maradhi kifo humuumbua ila si kila tatizo kila mtu alifahamu. Kuna wakati mtu anaweza kupost tatizo lake mwingine anamcrash hata kumtukana. sio jambo jema kutukanwa kama mtoto na watu wanakufahamu... Kuna wakati hata nahitaji ushauri wa kina kuhusu kazi na wafanyakazi wenzangu hata boss ni member humu, unadhani ni busara wao kuhafamu may be nataka kuacha kazi, au nimefanya kosa flani kazini lakini sijajulikana ila natafuta mbinu ya kurekebisha.. Au mchumba wangu yupo humu na ninahitaji ushauri juu yake, unadhani nitaweza kuomba ushauri???
 
Multiple ID'S naona kama inahusika sana hapa .. japo mods wanalipinga...

Ni kweli mkuu.... ila unaweza pata aibu ya mwaka kama ilivyomtokea member flan humu... Pale ambapo mods walimerge IDs zake lol!!!!
 
Sharing ni nzuri sana, ila kama wewe kwa binafsi yako utakosa amani kwa watu wanaokufahamu kujua ukubwa au tatizo lako, ni muhimu sana kuchunga privacy yako, vinginevyo itakusumbua psychologicaly na kukunyong'onyeza.

Tafuta wawili watatu uwashirikishe, naamini utapata pa kuanzia kama itakupendeza. nakupendekezea huyu mmojawapo [gfsonwin]. LoL
 
Umekosea sana! Ulitakiwa hilo tatizo lako! Ulisemee mwingine!! Liwe tatizo lako lakini ukimuhusisha mwingine!!! Sasa hivi jf unaweza kumuongelea jamaa yako wa karibu sana! Kumbe naye yumo humu!!,, tumia PM kwa watu unaoona hapa jamvini wana upeo na hilo tatizo lako!!@charminglady weka aibu pembeni my dada

Mkuu... PM inamaana utakuwa umeomba ushauri kwa mtu mmoja... Wengi wetu huwa tunahitaji maoni ya watu mbalimbali ili tupime. Unaweza kuta mtu anakushauri "huyo achana naye" ila unapoweka katika public unapata maoni ya watu mbalimbali then unachagua na kuchanganya na zako ndiposa unaamua....

Issue ya kumuongelea mtu mwingine huku story yakuhusu wewe ni ngumu. Let say kuna issue imetokea kazin kwako then ukaibadili na kuifanya imetokea kwa mtu mwingine, wakati huo huo wafanyakazi mwenzio wako humu lazima watakufahamu tu!
 
hapa naona akili ya mama/baba USHAURI iliwaza mbali sana sana. hili ni tatizo kwa mtu mwenye aibu ingawa kwa mtu free kama mm sio ishu kabisaa ingawa jamvini nusu yao wananijua na nimewah kuonana nao ila nikipata gumu huwa nalirusha live. na hata majuzi tu nimetoka kuomba ushauri hapa licha ya kwamba niliyoyaeleza wengine walibahatika nikiwa kwenye hali hiyo.

ushauri wangu kwako m-pm USHAURI atakusaidia na kama ni wa kitabibu pia anaweza kukusaidia.

Kwanza shikamoo dada mkubwa..Pili nakubaliana na ushauri wako.. ila kumbuka kuwa kuna issue ambazo ulishawahi kusema kwa njia moja ama nyingine hukuwahi kuzipitia.

Na zile ambazo umekuwa ukifunguka hapa jukwaani ni za kawaida sana ambazo hata.mimi naweza kufunguka.

Hapo mwishoni naona ndiyo pana faa zaidi kuwa niMPM USHAURI kisha yeye ndie anaweza kuileta jukwaan....
 
Last edited by a moderator:
Pole miss lady, but once a mistake is done, u gatta live with it positively.. Hata ka umejulikana lakini itabaki kuwa ni wewe na si mwingine, live your life, be free,.we only live once.
 
Hili nalo geni..huyu USHAURI ndio nani??ni ngumu kuwin trust yake kirahisi humu jamvini labda mpka tumzoee kwanza kama ambavyo imekuwa kwa baadhi ya member kama@ashadii .
 
Last edited by a moderator:
Pole miss lady, but once a mistake is done, u gatta live with it positively.. Hata ka umejulikana lakini itabaki kuwa ni wewe na si mwingine, live your life, be free,.we only live once.

Mkuu.... Nahisi hii issue sio nyepesi kama unavyoifikiria. Si vyema kila mtu afahamu tatizo lako hata kama ni lako... Naomba nikutolee mfano.. samahani lakini...

Imagine wewe umefumaniwa na mke/mme wa mtu huko mtaani kwenu, wanaofahamu ni watu wachache wa huko mtaani kwenu. . Kisha ukaja hapa jamvini kuomba ushauri ilihali asilimia kubwa ya member wanakufahamu. Will u be happy ati kwa kuwa kosa lishatendeka, wafanyakazi wenzio wajue, boss ajue, member wengine pia wajue????
 
Back
Top Bottom