Nyati ushauri wangu uko namna hii:
Kama unanunua tiles kwa ajili ya nyumba yako basi sehemu zenye kutumika zaidi jipinde uweke kigae chenye ubora.
Ila kwa vile wataka maduka yenye kuuza tiles nzuri za kichina (wanaita gredi wani) nenda C&G wako Old Bagamoyo road kwa Warioba (kushoto kama wenda Kawe). Bei zao powa sana.
Tanga stones kwa ndani unahitaji fundi mzuri saaaana otherwise sebule itafanana na Pub/Bar.
Tiles za Granite za china zinapauka muda siyo mrefu. Ikiwekwa sehemu ambayo watu wanapitapita sana kama sebuleni, kwenye corridor na jikoni hazitachukua muda bila kabla hazijapauka. Porcelain ndiyo nzuri kwa nyumba zetu za kiswahili na pia bei ni nafuu sana.
Usitumie tiles za Ceremics chini (jikoni, sebuleni au chooni) kwa sababu zinanyonya maji na hivyo zitajaza uvundo sehemu hizo.
Tiles za Granite za china zinapauka muda siyo mrefu. Ikiwekwa sehemu ambayo watu wanapitapita sana kama sebuleni, kwenye corridor na jikoni hazitachukua muda bila kabla hazijapauka. Porcelain ndiyo nzuri kwa nyumba zetu za kiswahili na pia bei ni nafuu sana.
Usitumie tiles za Ceremics chini (jikoni, sebuleni au chooni) kwa sababu zinanyonya maji na hivyo zitajaza uvundo sehemu hizo.
Kwa mwenye uzoefu na tiles za Kichina toka Monalisa (GoodOne) atufahamishe. Yaani kama kuna mtu alizinunua angalau mwaka na zaidi kwa sasa na bado hazijachujuka.
Asante
Spanish Tiles and Sanitary Ware ..... Victoria karibu na sub station ya Tanesco .... good quality Spanish tiles .... ceramic, porcelain, granite both polished, rough, non slippery and mat finish
also mosaic tiles are available
kikubwa pia katika tiles ni urefu na upana uwe precisely equal .... kama upande mmoja ni umezidi mwingine kwa 2 millimeters italeta shida kwenye laying (kujenga) hii itasababisha joints na corners zitofautiane
pia katika kuweka tiles pattern ni kitu muhimu sana .... kuna aina nyingi za pattern .. kuna basket type, herringbone, staggered, zig zag etc
pia ni muhimu kutumia proprietary spacers wakati wakujenga both floor and wall tiles
Nilizikuta kwa jamaa fulani kwa kweli zinafubaa (kuchuja) hivyo mimi nilienda CTC Tiles ambao wapo Mwenge njia ya kwenda ITV wanazo tiles kutoka Afrika Kusini na Brazil, kwa kweli ni nzuri na bei siyo mbaya sana
Mkuu tiles ziko kwenye makundi matatu so far. Yaani Granite, Porcelain na ceramic. Na kwa ubora ya kwanza ni Granite, ya pili ni porcelain na ya tatu ni ceramic. Ndo maana utakuta ceramic inatumika sana kwa ukutani hasa jikoni na bafuni (sehemu ambazo hazikanyagwi). Kwahiyo ukifika dukani sisitiza granite ila ndo hivyo bei yake ni kubwa. Ukishindwa sana nunua porcelain si mbaya pia. Kwa Kariakoo ulikoelekezwa itakuwa pale GoodOne (Wachina pia) mtaa wa Swahili wanazo tile kwa kila kundi na rafiki yangu mmoja alinunua hapo na kuziweka kwenye nyumba yake tangu mwaka 2010 anasema hazijachujuka na bei zao ni nafuu sana.
Na mimi nilinunua white ceramic tiles mwaka 2008 hapo hapo GoodOne store Kariakoo swahili street na kwa kweli bado quality yake iko nzuri sana (whole house) as if nimeziweka recently hazijapauka/chujuka au kuwa na scratches bado na.. na bei yake ilikuwa nzuri tu ila sijui kwa sasa.
Mkuu hizi zilikuwa ni kwa ajili ya ukutani siyo? Maana ceramic ni za ukutani, kwa floor ni porcelain na granite. Hizi ulizonunua zilikuwa ni plain white au zilikuwa na maua kidogo?
Mkuu hapo ndo naona ntachanganya maana mie nilikuwa najua ceramic na granite ila porcelain sikuwa najua ni aina gani. Nakumbuka mabox yalikuwa yameandikwa ceramic tiles na kubwa nikaziweka chini nyeupe tupu hazina rangi nyingine au maua na kulikuwa na za ukutani pia zenyewe nlichukua za rangi mchanganyiko ila ukuta wa jikoni nimeweka nyeupe. Hizo za chini mpaka leo hazijachuja kabisa na fundi alinishauri kama nanunua floor tiles za mchina nichukue zenye rangi moja na si zenye rangi mchanganyiko maana alisema 'zinadumu' kuliko zenye rangi mchanganyiko. Nilikuwa na wasiwasi nazo lakini kwa kweli nimezifurahia. Sasa ntarudi na jibu kama ni porcelain maana hapo for now nta-mix up kwa kweli..