Ushauri: Jinsi ya kuupdate vyeti vyangu

mahwelu

JF-Expert Member
Jun 8, 2013
322
252
Wakuu nawaomba mnisamehe.. Naomba mnishauri,

Miaka sita iliyopita niliomba kazi ofisi ya serikali na kwa kuwa aliyekuwa mchumba wangu alikuwa rafiki wa mkurugenzi, haikuwa shida nikapata.

Nimeendelea kufanya kazi vizuri tu kwa miaka sita bila doa lolote.

Juzi nimeitwa kwa mkurugenzi mpya ananiambia vyeti vyangu sio halali.

Nimepewa wiki moja niwaletee vyeti original. Kusema kweli mimi sina hivyo vyeti kwani niliishia form two na mkurugenzi wa mwanzo analijua kwani yeye na Charles ndio walitafuta hiko cheti.

Nafikiria kuomba likizo isiyokuwa na malipo ili niweze kurudia mitihani ya form four.

Chondechonde, naomba mnishauri hii itawezekana? Je, kwa kuwa kazi naiweza hivi cheti kina umuhimu gani au ndio majungu yenyewe kwa kuwa nilikuwa namshabikia mgombea upinzani?

Please please nishaurini nifanyeje maana hali ngumu.Jamii itanionaje mimi mtaani mwanangu ataishije?
 
Mtumishi hewa, hapo hakuna namna kubali kupoteza na kupelekwa mbele ya vyombo vya dola.

Hiyo kazi unayofanya inahitaji elimu level ipi?
 
Mtumishi hewa, hapo hakuna namna kubali kupoteza na kupelekwa mbele ya vyombo vya dola.

Hiyo kazi unayofanya inahitaji elimu level ipi?

Mimi sio hewa kwani nafanya kazi na ukiondoa swala la cheti kazi yangu ni mzuri.
 
Hakuna namna hapo!!? Cheti cha form four ukisema urudie mtihani ni mpaka mwezi wa tisa huko kama sio wa kumi, kazini umepewa wiki moja. Na je cheti kinachohitajika ni hicho pekee?? Bado huna ujanja jiandae kuisoma namba hakuna namna Mzee mwenzangu.
 
nyie ndio mnaotafutwa na mjomba Magufuli..........form two upo kazini wakati wenye sifa ya kufanya hiyo kazi wapo mtaani............ yaani ulipata kazi kwasababu ya urafiki wa basha wako na mkurugenzi wewe jela inakuhusu................ jiandae kuwataja na wenzako wote.................MUNGU SAIDIA WATU KAMA HAWA WATUMBULIWE NA HII SERIKALI YA AWAMU YA TANO.
 
Mwambie mchumba wako ampe tena mambo huyo mkurugenzi mpya kama wamwanzo hilo swala utasolve..
zaid ya hapo hakuna namna..
 
Kama una pesa njoo nikuuzie vyeti vyangu original kafanyie kaz me nipe pesa niende Dubai kuleta mzigo wa vifaa vya ujenz niendeleze biashara yangu
 
But kwanini asiwaze kukaba wanaotaka kazi sasa? kuna haja gani kutusumbua watu ambau tumeprove kazi tunafanya?
Halafu nyie ndio mnakuwaga na dharau sana kwenye hizo ofisi..........Wacha mzee aanze na nyinyi washenzi wakubwa........!!!
 
Back
Top Bottom