Wasalaam , kuna hii simu yangu tajwa hapo juu ilianguka na kufa display nimekiweka tu ndani kwa mda sasa .Nataka kuifufua nimejaribu kupita kkoo bei nimetajiwa 280k mpaka 300k hapo ikijumuisha na ufundi . kwa maoni yangu nimeona ni risk kuitengeneza kwa gharama hio na isirudi kama awali . naomba ushauri /msaada.
1. Je gharama hizo ni sahihi au walitaka kunilamba
2.Je naweza pata display used kwa bei rafiki?
3. Je nikiitengeneza itarudi vizuri kama mwanzo au niachane na wazo hili
Nawasilisha