Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 141,569
- 284,101
Natoa ushauri kwa Mamlaka ya Uteuzi kwamba, ipo haja ya dharula ya kumuondoa Mkuu wa Mkoa Albert Chalamila baada ya Kushindwa kutumia Ushawishi kumaliza mgomo wa Wafanyabiasha wa Dar es Salaam na badala yake anatoa vitisho.
Mgomo wa Wafanyabiashara hautamalizwa kwa vitisho vya namna yoyote ile, hii kwa sababu Biashara za watu ndio Maisha yao, ndio uwekezaji wao, ni mitaji yao, walizianzisha wao wenyewe kwa kufuata sheria za nchi, sasa zinapochomekwa sheria za mfukoni wafanyabiashara hawatakubali hata ikibidi kwa gharama ya damu
Cheo alichonacho Chalamila ni dhamana ya hisani tu, tena ni dhamana ya muda mfupi mno, anapaswa kutenda haki, Amos Makalla tulihakikisha ang'olewa Dar es Salaam kwa mambo haya haya anayoleta leo Chalamila, Taarifa tulizonazo ni kwamba Chalamila hajawahi kufanya biashara hata ya kuuza Mapera, kwahiyo hajui lolote kuhusu matatizo ya Wafanyabiashara, huyu alikuwa Mwl tu na baadaye akaanza kupewa hivi vyeo, anapaswa kuangalia na kufikiri kwa kina kuhusu jambo hili na hasa akizingatia kwamba Serikali yake imeshindwa kufanya biashara yoyote kutokana na changamoto, SGR, BANDARI, MWENDOKASI na Mashirika kadhaa ya umma uwe mfano kwake, Chama chake cha CCM kimeshindwa kuendeleza SUKITA , kikabaki kupora mali za Umma na kujimilikisha, vikiwemo viwanja vya soka na Majengo kadhaa
Tunashauri Kero na Malalamiko ya Wafanyabiashara yasikilizwe na yatatuliwe, na kwa vile huyu kashindwa basi aletwe mtu mwingine haraka
Mgomo wa Wafanyabiashara hautamalizwa kwa vitisho vya namna yoyote ile, hii kwa sababu Biashara za watu ndio Maisha yao, ndio uwekezaji wao, ni mitaji yao, walizianzisha wao wenyewe kwa kufuata sheria za nchi, sasa zinapochomekwa sheria za mfukoni wafanyabiashara hawatakubali hata ikibidi kwa gharama ya damu
Cheo alichonacho Chalamila ni dhamana ya hisani tu, tena ni dhamana ya muda mfupi mno, anapaswa kutenda haki, Amos Makalla tulihakikisha ang'olewa Dar es Salaam kwa mambo haya haya anayoleta leo Chalamila, Taarifa tulizonazo ni kwamba Chalamila hajawahi kufanya biashara hata ya kuuza Mapera, kwahiyo hajui lolote kuhusu matatizo ya Wafanyabiashara, huyu alikuwa Mwl tu na baadaye akaanza kupewa hivi vyeo, anapaswa kuangalia na kufikiri kwa kina kuhusu jambo hili na hasa akizingatia kwamba Serikali yake imeshindwa kufanya biashara yoyote kutokana na changamoto, SGR, BANDARI, MWENDOKASI na Mashirika kadhaa ya umma uwe mfano kwake, Chama chake cha CCM kimeshindwa kuendeleza SUKITA , kikabaki kupora mali za Umma na kujimilikisha, vikiwemo viwanja vya soka na Majengo kadhaa
Tunashauri Kero na Malalamiko ya Wafanyabiashara yasikilizwe na yatatuliwe, na kwa vile huyu kashindwa basi aletwe mtu mwingine haraka