Ushauri: Chalamila aondolewe Dar es Salaam, Atasababisha Machafuko

Ushauri: Chalamila aondolewe Dar es Salaam, Atasababisha Machafuko

Angekuwepo makonda mda huu tungekua tumekaa kwenye tv tunaangalia watu wanatoa hoja zao na kujibiwa na mamlaka sasa huyo anakuja kutisha watu congo na kkooo wapi na wapi zero brain kabisa km huyu ndo mkuu wa mkoa sishangai hii nchi kushindwa bajeti na uganda
 
Natoa ushauri kwa Mamlaka ya Uteuzi kwamba, ipo haja ya dharula ya kumuondoa Mkuu wa Mkoa Albert Chalamila baada ya Kushindwa kutumia Ushawishi kumaliza mgomo wa Wafanyabiasha wa Dar es Salaam na badala yake anatoa vitisho.

View attachment 3024750

Mgomo wa Wafanyabiashara hautamalizwa kwa vitisho vya namna yoyote ile, hii kwa sababu Biashara za watu ndio Maisha yao, ndio uwekezaji wao, ni mitaji yao, walizianzisha wao wenyewe kwa kufuata sheria za nchi, sasa zinapochomekwa sheria za mfukoni wafanyabiashara hawatakubali hata ikibidi kwa gharama ya damu

Cheo alichonacho Chalamila ni dhamana ya hisani tu, tena ni dhamana ya muda mfupi mno, anapaswa kutenda haki, Amos Makalla tulihakikisha ang'olewa Dar es Salaam kwa mambo haya haya anayoleta leo Chalamila, Taarifa tulizonazo ni kwamba Chalamila hajawahi kufanya biashara hata ya kuuza Mapera, kwahiyo hajui lolote kuhusu matatizo ya Wafanyabiashara, huyu alikuwa Mwl tu na baadaye akaanza kupewa hivi vyeo, anapaswa kuangalia na kufikiri kwa kina kuhusu jambo hili na hasa akizingatia kwamba Serikali yake imeshindwa kufanya biashara yoyote kutokana na changamoto, SGR, MWENDOKASI na Mashirika kadhaa ya umma uwe mfano kwake, Chama chake cha CCM kimeshindwa kuendeleza SUKITA , kikabaki kupora mali za Umma na kujimilikisha, vikiwemo viwanja vya soka na Majengo kadhaa

View attachment 3024761

Tunashauri Kero na Malalamiko ya Wafanyabiashara yasikilizwe na yatatuliwe, na kwa vile huyu kashindwa basi aletwe mtu mwingine haraka

View attachment 3024765
Tunaye Sana!
 
Natoa ushauri kwa Mamlaka ya Uteuzi kwamba, ipo haja ya dharula ya kumuondoa Mkuu wa Mkoa Albert Chalamila baada ya Kushindwa kutumia Ushawishi kumaliza mgomo wa Wafanyabiasha wa Dar es Salaam na badala yake anatoa vitisho.

View attachment 3024750

Mgomo wa Wafanyabiashara hautamalizwa kwa vitisho vya namna yoyote ile, hii kwa sababu Biashara za watu ndio Maisha yao, ndio uwekezaji wao, ni mitaji yao, walizianzisha wao wenyewe kwa kufuata sheria za nchi, sasa zinapochomekwa sheria za mfukoni wafanyabiashara hawatakubali hata ikibidi kwa gharama ya damu

Cheo alichonacho Chalamila ni dhamana ya hisani tu, tena ni dhamana ya muda mfupi mno, anapaswa kutenda haki, Amos Makalla tulihakikisha ang'olewa Dar es Salaam kwa mambo haya haya anayoleta leo Chalamila, Taarifa tulizonazo ni kwamba Chalamila hajawahi kufanya biashara hata ya kuuza Mapera, kwahiyo hajui lolote kuhusu matatizo ya Wafanyabiashara, huyu alikuwa Mwl tu na baadaye akaanza kupewa hivi vyeo, anapaswa kuangalia na kufikiri kwa kina kuhusu jambo hili na hasa akizingatia kwamba Serikali yake imeshindwa kufanya biashara yoyote kutokana na changamoto, SGR, MWENDOKASI na Mashirika kadhaa ya umma uwe mfano kwake, Chama chake cha CCM kimeshindwa kuendeleza SUKITA , kikabaki kupora mali za Umma na kujimilikisha, vikiwemo viwanja vya soka na Majengo kadhaa

View attachment 3024761

Tunashauri Kero na Malalamiko ya Wafanyabiashara yasikilizwe na yatatuliwe, na kwa vile huyu kashindwa basi aletwe mtu mwingine haraka

View attachment 3024765
Albert Chalamila Hana sifa hata moja ya kuongoza binadamu, lablda wanyama pori au wanyama wa kufungwa.
Rais anapaswa kutengua uteuzi wake Mara moja ili kuepusha nchi kuingia kwenye Mgogoro wa machafuko ya kijamii (civil unrest) kutokana na kauli zake chafu na za kibabe.
 
Leo nilikuwa na diaspora mmoja wa Kenya hapa TX tunazungumzia EA siasa za Afrika mashariki.

Ama kweli watanganyika walijichimbia kaburi 2014-2015, ile ndio ulikuwa miaka ya mageuzi .

Nchi ingepata katiba mpya 2015 na ingeingia uchaguzi mkuu bila uwepo wa wahuni.

Mawe mawili ya watanganyika yakashindwa kuua ndege mmoja.

Poleni sana huenda nchi ikarudi kwenye mstari miaka 20+ kutoka sasa.
 
Nadhani hapa kwa hali ilivyo,RC aondolewe au asiondolewe haiweza kutatua matatizo ya wafanyabiashara waliyonayo!
Serikali iji commit kusikiliza madai ya wafanyabiashara na kuwa tayari kuyatatua! Yale ambayo yameshindikana kwa sababu yako nje ya uwezo wa serikali yawepo maelewano kifanyike kipi ili kukabiliana na matatizo hayo!
 
Back
Top Bottom