Ushauri: Ana mgogoro wa muda mrefu na jirani yake

Ushauri: Ana mgogoro wa muda mrefu na jirani yake

Ni ngumu sana kuhukumu kesi ambayo haujasikiliza pande zote mbili. Lakini kwa ushahidi wa kimazingira na maelezo tulinayo mpaka sasa na jinsi picha zinavyojionyesha inaonekana huyo mwenye nyumba nyeupe ana matatizo sana japo kuna watu wanajaribu kumtetea. Watu wa aina hiyo ukipakana nao wanapenda sana kuangalia muonekano wa mtu na kumdharau hasa akishatangulia kujenga anakuona wewe huna kitu kwa sababu unakuja "site" na kuondoka miaka na miaka kwa hiyo anazidisha nyumba akijua huna ujanja utamuuzia taka usitake. Kumbe masikini ya Mungu una mipango yako mingine kabisa labda kuja kujenga hapo mahali baada ya miaka hata 10. Viwanja vyenyewe hivi "20 x 20" mara nyingi tunanunua kipindi tunaanza anza kazi/biashara. Sasa tukija kupata hela kidogo tunatamani kiwanja hicho hicho yatokee mazingaombwe kiwe "40 X 40" lazima tu yatatukuta yaliyomkuta huyo mwenye nyumba nyeupe. Kitu cha msingi kipato kikiongezeka nenda kanunue shamba kabisa huko Kibaha, Mkuranga, Kisarawe, n.k. kuepuka aibu hiyo ya kuja kejengewa ukuta dirishani halafu picha zinazunguka kwenye mitandao yote ya kijamii dunia nzima.

Kikubwa kwenye maisha tufanye mambo yatakayotupa amani ya roho sasa hivi na hata baadae na kuangalia faida na hasara ya maamuzi tunayofanya sasa hivi kwani maisha yenyewe haya mafupi sana. Unaweza kukuta huyo jamaa mwenye nyumba nyeupe alijenga wakati huo ana uwezo/nafasi sasa mambo yamebadilika unaweza kukuta huo uwezo/nafasi tena hana. Maana yake hata kurekebisha nyumba yake kwa kuweka hata AC hawezi si atakufa na joto maana mjenga ukuta kashaliziba . Mbaya zaidi unakuta walijenga wazazi na wameshatangulia mbele za haki si unawaachia msala watoto wako ambao hauwahusu kabisa.
 
Ni ngumu sana kuhukumu kesi ambayo haujasikiliza pande zote mbili. Lakini kwa ushahidi wa kimazingira na maelezo tulinayo mpaka sasa na jinsi picha zinavyojionyesha inaonekana huyo mwenye nyumba nyeupe ana matatizo sana japo kuna watu wanajaribu kumtetea. Watu wa aina hiyo ukipakana nao wanapenda sana kuangalia muonekano wa mtu na kumdharau hasa akishatangulia kujenga anakuona wewe huna kitu kwa sababu unakuja "site" na kuondoka miaka na miaka kwa hiyo anazidisha nyumba akijua huna ujanja utamuuzia taka usitake. Kumbe masikini ya Mungu una mipango yako mingine kabisa labda kuja kujenga hapo mahali baada ya miaka hata 10. Viwanja vyenyewe hivi "20 x 20" mara nyingi tunanunua kipindi tunaanza anza kazi/biashara. Sasa tukija kupata hela kidogo tunatamani kiwanja hicho hicho yatokee mazingaombwe kiwe "40 X 40" lazima tu yatatukuta yaliyomkuta huyo mwenye nyumba nyeupe. Kitu cha msingi kipato kikiongezeka nenda kanunue shamba kabisa huko Kibaha, Mkuranga, Kisarawe, n.k. kuepuka aibu hiyo ya kuja kejengewa ukuta dirishani halafu picha zinazunguka kwenye mitandao yote ya kijamii dunia nzima.

Kikubwa kwenye maisha tufanye mambo yatakayotupa amani ya roho sasa hivi na hata baadae na kuangalia faida na hasara ya maamuzi tunayofanya sasa hivi kwani maisha yenyewe haya mafupi sana. Unaweza kukuta huyo jamaa mwenye nyumba nyeupe alijenga wakati huo ana uwezo/nafasi sasa mambo yamebadilika unaweza kukuta huo uwezo/nafasi tena hana. Maana yake hata kurekebisha nyumba yake kwa kuweka hata AC hawezi si atakufa na joto maana mjenga ukuta kashaliziba . Mbaya zaidi unakuta walijenga wazazi na wameshatangulia mbele za haki si unawaachia msala watoto wako ambao hauwahusu kabisa.
Umeongea point sana mkuu
 
Habari wana jamvi, jamaa amekua na mvutano wa muda mrefu na jiran yake juu ya mipaka yao ya viwanja. Kutokana na mvutano huo jamaa kaamua kujenga fensi mwisho wa kiwanja chake. Je ni sahihi kwa maamuzi haya kama inavyoonekana katika picha hizi?View attachment 1510186View attachment 1510187View attachment 1510188View attachment 1510189
Mnaokoteza picha Facebook mnaleta hapa mkijifanya ni tukio la kweli. Hizi picha zinatembea sana si Facebook, si WhatsUp na kila mmoja ameitungia story yake na anajifanya ni jamaa yake au jirani yake.
 
Kwa hio mkuu huamin kama hilo tukio limetokea?
Mnaokoteza picha Facebook mnaleta hapa mkijifanya ni tukio la kweli. Hizi picha zinatembea sana si Facebook, si WhatsUp na kila mmoja ameitungia story yake na anajifanya ni jamaa yake au jirani yake.
 
Ingekua ni Mimi, nadhani ningeacha walau mita mbili kutoka kwenye ukuta wa nyumba ya huyo jirani mkorofi na kisha ningeweka ukuta.
Mkuu, ubaya hua haulipwi kwa ubaya. Na kosa huwa halifutwi kwa kutenda kosa tena.
Kuna mtu anaweza kufanya kosa halafu akawa nadharau siami kama huyo mwenye fensi amekosa kabura hata kidogo
 
Huyo aliyejenga Ukuta akaziba madirisha ili familia yangu ikose hewa. Hata afuge chochote ni mwendo wa kutupa sumu uani kwake
 
Safi tu na ikiwezekana ajenge hata juu ya hiyo nyumba wauane tu, tumewachoka na vituko vyao vya kijinga/kitoto
 
Hyo anaejenga ukuta pimbi kweli Kama ni Mimi nisingeangaika ningetumia huo huo ukuta wa nyumba ya jirani nikuunganisha tu.
Akikwambia nataka kuzunguka nyuma yanyumba yangu itakuwaje dawa ni hiyo amejenga kamaliza naww unamaliza
 
Back
Top Bottom