NANDERA
JF-Expert Member
- Mar 18, 2014
- 2,023
- 2,492
Pole sana bibie. Nisisitize athari za hili jambo ni kubwa sana. Usione watu hawataki ndoa, hawatulii kwenye mahusiano, wana ndoa ngumu, ni wakatili, ni wauaji, wamejikataa ukadhani wanafanya makusudi. Si ajabu hizi habari unaskia mtu kauawa hajaporwa chochote baadhi yao ni miss chaga type wamelipiza visasi vyao au kina kaka wanalipizia dada zao au waume wanalipizia wake zao.
Nina rafiki athari za kubakwa tena kwa kulawitiwa na binamu yake aliyekuwa akilelewa kwao mara kwa mara akiwa mdogo zilikuja kujitokeza akiwa na miaka kadhaa kwenye ndoa. Ghafla tu hataki kushiriki tendo la ndoa na mumewe na hataki hata amguse. Bahati nzuri alikuwa ulaya. Mume akajaribu kumpeleka therapy kujaribu kuamsha hamu ya mgegedo ndo ukweli ukabumburuka. Mume akapiga simu kwa wazazi bongo kuwaambia hiyo issue na akawaambia hayuko tayari kulipia gharama za therapy kwa uzembe wa wazazi! (hapa sikumwelewa). Wazazi washakuwa wazee, yule binamu nae ni mtu mzima ana familia yake. Wazazi wakaita wazee, ndugu wote wa karibu wakubwa kwa wadogo bila kutaja ajenda ya mkutano. Wakaelezea yoote yaliyotokea, binamu akalowa jasho, akakiri kosa lake na kubeba mzigo wa kulipia therapy ya binamu yake ulaya. Ilimbidi kuuza viwanja vyake viwili kufanikisha hiyo kazi.
Kwa mwanaJF wa kiume aliyewahi kumnajisi/kumbaka binti yeyote wa miaka 0-21 (emotional wiring inaendelea mpaka umri huu) hata kama imepita miaka mingapi namshauri amtafute amuombe msamaha. Kwa mwanaJF wa kike aliyewahi kufanyiwa ukatili huu akaumia akakaa kimya afunue moyo wake kwa mtu anayemwamini atoe duku duku lake kama mchakato wa kuanza kuponyesha kidonda. Unaweza kutumia clinical au spiritual approach kwa kumuona mwanasaikolojia au mlezi wa kiroho mkasaidiana kukabili hii shida. Nimewahi kusoma kitabu cha Mch Kagya - Nafsi iliyoumizwa hutafuta kulipiza kisasi. Nimemuelewa sana Miss Chagga.
Nina rafiki athari za kubakwa tena kwa kulawitiwa na binamu yake aliyekuwa akilelewa kwao mara kwa mara akiwa mdogo zilikuja kujitokeza akiwa na miaka kadhaa kwenye ndoa. Ghafla tu hataki kushiriki tendo la ndoa na mumewe na hataki hata amguse. Bahati nzuri alikuwa ulaya. Mume akajaribu kumpeleka therapy kujaribu kuamsha hamu ya mgegedo ndo ukweli ukabumburuka. Mume akapiga simu kwa wazazi bongo kuwaambia hiyo issue na akawaambia hayuko tayari kulipia gharama za therapy kwa uzembe wa wazazi! (hapa sikumwelewa). Wazazi washakuwa wazee, yule binamu nae ni mtu mzima ana familia yake. Wazazi wakaita wazee, ndugu wote wa karibu wakubwa kwa wadogo bila kutaja ajenda ya mkutano. Wakaelezea yoote yaliyotokea, binamu akalowa jasho, akakiri kosa lake na kubeba mzigo wa kulipia therapy ya binamu yake ulaya. Ilimbidi kuuza viwanja vyake viwili kufanikisha hiyo kazi.
Kwa mwanaJF wa kiume aliyewahi kumnajisi/kumbaka binti yeyote wa miaka 0-21 (emotional wiring inaendelea mpaka umri huu) hata kama imepita miaka mingapi namshauri amtafute amuombe msamaha. Kwa mwanaJF wa kike aliyewahi kufanyiwa ukatili huu akaumia akakaa kimya afunue moyo wake kwa mtu anayemwamini atoe duku duku lake kama mchakato wa kuanza kuponyesha kidonda. Unaweza kutumia clinical au spiritual approach kwa kumuona mwanasaikolojia au mlezi wa kiroho mkasaidiana kukabili hii shida. Nimewahi kusoma kitabu cha Mch Kagya - Nafsi iliyoumizwa hutafuta kulipiza kisasi. Nimemuelewa sana Miss Chagga.