Usaliti wa Dkt. Slaa ni upi?

Usaliti wa Dkt. Slaa ni upi?

Anyway basi tuseme hivi ili stori yako inoge ...Dr Slaa alimleta Chadema ikamkubali siyo? Umewahi kuilaumu Chadema na mwenyekiti Mbowe kwahili kama unavyomtukana Dr Slaa? ....naomba walau mstari wako mmoja humu ukikosoa kipindi kile tunahangaika kukosoa chama kishtuke ....

How old are you? You sound childish, I'm sorry to say this.
Kwa hiyo kuilaumu CHADEMA na Mbowe ndiyo kutahalalisha lawama zangu kwa Slaa?

Unataka nikupe mstari wangu mmoja? You sound not only childish, but also naive. Yaani nikiweka mstari wangu mmoja ndiyo utaniamini ama? Ni sawa na huyo aliyekutuma umtetea alivyosema ati Lowassa ajisafishe na tuhuma zake!!
 
Ni kweli Dr Slaa sio tu ana mchango ktk kuujenga upinzani ila ni kwamba ameujenga kweli kwa damu na jasho. Hilo lipo wazi.
Na kwangu mimi alikuwa sahihi kuondoka baada ya chadema kumpokea fisadi lowassa.

Ila nikutahadharishe kuwa Dr Slaa wa leo sio yule wa 2015.
Mimi nilikuwa mfuasi wake na nilikubaliana nae kuiacha Chadema ..
Iko hivi Dr Slaa atarudi CCM rasmi. Nakupa miezi 6 . Lingine ni kwamba Lowassa nae atarudi CCM na utakachoshangaa ni kwamba this time Dr Slaa hatasimamia msimamo wake wa kuondoka CCM wkt Lowassa akirejea.

Sasa nasubiri hiyo thread cku Dr Slaa na Lowassa wakiwa wote huko CCM.
Kwa hiyo lowasa akirudi ccm anakwenda kuachiwa nafasi ya kugombea urais 2020?!
 
Usaliti mwingine wa msaliti Lipumba ni huu hapa. Mara baada ya hawara yake kumjia juu kuhusu kuruhusu fisadi lowassa achukue nafasi yake kama mgombea wa Urais alionekana meza moja na Mwigulu mtu ambaye mara nyingi alimsema vibaya sana kutokana na matendo yake mbali mbali dhidi ya Chadema. Mwigulu alifanya kipi cha kumfanya Slaa asahau kauli zake dhidi ya Mwigulu hata kukaa meza moja na Mwigulu?







Usaliti wa Slaa ni huu hapa na hadi hii leo hajajibu hizi tuhuma za Gwajima. Siku zote alijua kwamba lowassa ni fisadi ilikuwaje tena akubali kukaa naye meza moja na kumkaribisha Chadema!? Angekataa tangu mwanzo wengi wangemuona ni mtu mwenye msimamo usioyumba lakini hadi hawara yake alipokuja juu kwa kujua Dr Slaa si mgombea tena wa Urais Chadema ndipo alipoanza kubadili Gia angani.

Fisadi lowassa hakustahili kupewa muda wa kuwa meza moja na kiongozi yeyote yule wa Chadema wala kukaribishwa Chadema.

 
Na wewe umeshakuwa MNAFIKI uliyebobea. Huwezi ukajenga upinzani huku unawakumbatia wale wale ambao uliahidi Watanzania kwamba kama ungechaguliwa ungemtia ndani kutokana na ufisadi mkubwa wa wizi wa nyumba za Serikali!!! Huwezi kukaa meza moja na mwizi Mwigulu meza moja kama hii picha inavyoonyesha hapa chini. Ulikuwa kichwa sana miaka michache iliyopita sasa nawe umekuwa moja ya MAZWAZWA wakubwa sana nchini. Sijui kitu gani kilichokupata hadi ubadili msimamo wako kiasi hiki cha kuandika upuuzi humu tena wa hali ya juu..







Itawachukua muda mrefu sana hawa ndugu zetu kutambua hili na kukubali upekee wa mchango wa Dkt. Slaa katika kujenga upinzani. Sasa hivi wamekuwa kama kondoo wasio na mchungaji!
 
Ni kweli Dr Slaa sio tu ana mchango ktk kuujenga upinzani ila ni kwamba ameujenga kweli kwa damu na jasho. Hilo lipo wazi.
Nyie watoto wadogo mna taabu sana...hebu rudi darasani usome historia ya mageuzi Tanzania. Uliza kitu gani kilimkimbiza Dr. Slaa huko CCM na kusetiriwa na Chadema!

Kwa ufahamisho zaidi ni kwamba Dr. Slaa aliikimbia CCM baada ya jina lake kukatwa akiutafuta Ubunge na kukimbilia Chadema na hivyo kuweza kuukuwaa Ubunge!

Alichofanya Lowassa mwaka 2015 hakina tofauti na alichofanya Dr. Slaa mwaka 1995. Wapo walioijenga Chadema kwa damu zao na siyo Dr. Slaa aliyekuwa mdandiaji tu.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mimi kwangu nina mitazamo tofauti ni wengine kuhusu Dr. Slaa. Usipokuwa makini unaweza kumchukulia Slaa kama msaliti. Sikufurahishwa na Slaa alipoondoka cdm, tena kuondoka kwake akakutumia kama sehemu ya kuiumuza cdm kwa faida ya ccm. Ila hata ningekuwa mimi ningechukua maamuzi ambayo yangewashangaza wengi. Slaa alijiandaa kugombea urais cdm, na kweli alistahili hata kama asingeshinda lakini cdm ingebaki na msimamo wake. Lakini ninachomlaumu Slaa mpaka leo, hivi akija mtu kwenye chama chako kwakuwa humpendi ndio unaondoka. Kwangu naamini Slaa aliondoka cdm kwa kuzira baada ya kukosa nafasi aliyokuwa ameshajiandaa kuitumikia, ila kwakuwa cdm nao walifanya kosa kumpokea Lowassa ambaye alikuwa na kashfa, hapo ikawa rahisi Slaa kuhalalisha huko kuzira kwake. Hivyo mpaka sasa kwangu imebaki 50/50 kwamba Slaa aliondoka kwa kukosa nafasi ya kugombea urais, ama aliondoka kwa kutokutaka kubaki kwenye chama ambacho kimempa Lowassa nafasi adhimu ya kugombea urais wakati walimtuhumu kwamba ni fisadi. Yote mawali kwangu inaweza kuwa ni sababu ya Slaa kuondoka cdm.

Kama Slaa ni msaliti ama la, hilo linategemea na utashi wa kila mtu kulingana na uelewa wake na sababu nyingine mbalimbali. Kilichonifanya nianze kumuona Slaa hana maana ni ile sentesi yake ya jana kuhusu Lissu. Kwa kweli Lissu hakumfanyia Slaa sawa wakati kajitoa cdm kwa zile lugha alizokuwa anamtolea, lakini Slaa kama padre mstaafau alipaswa kusahau baadhi ya mambo na kuacha kutoa lugha zitakazoonyesha kwamba yaliyomkuta Lissu ni mambo ya kawaida. Ukiachia mapungufu hayo niliyoyaona kwa Slaa sioni kama ni adui sana wa cdm kulinganisha na mambo mengine yanayoendelea ndani ya cdm kwa sasa.
Mkuu tindo ni kweli. Amesema kweli tupu. Wewe ni miongoni mwa watu ambao mpo objective na constructive. Dr Slaa wa leo sio yule wa 2015.
Jiulize amepewa masharti gani hata asitoe pole ya mdomo tu kwa madhila yaliyomkuta Lissu.

Je tuamini sasa kuwa na yeye ana
Kwa hiyo lowasa akirudi ccm anakwenda kuachiwa nafasi ya kugombea urais 2020?!
Anaenda kukutana na Dr Slaa na JPM na maisha ya kupambana na ufisadi yanaendelea.
 
Alikuwa ni zaidi ya mwanachama, alikuwa Katibu Mkuu (mtendaji mkuu) wa chama. Angekuwa principled asingekubali ombi la Gwajima na kwenda kuanza kujadili uwezekano wa Lowassa kuhamia CHADEMA. Kimsingi yeye ndiye aliyewezesha hata uwezekano wa Lowassa kuhamia CHADEMA. Bila ya yeye kutumiwa na Gwajima kuwezesha Lowassa kuhamia CHADEMA, pengine Lowassa asingehamia huko.

Ni heri angekataa ombi la Gwajima. Na hata kama Gwajima angetumia kiongozi mwingine, Slaa angekuwa ana mikono safi katika hilo.
Mkuu hapa pia tunatofautiana..who is gwajma...? Yaan nmwamn mtu asie kuwa na msaada kwangu halafu nishindwe kumwamin MTU aliekua kabeba mstakabal Wa dhana ya demokrasia yenye mising ya utu na hak...I mean unachotaka niamn maneno ya mwendawazm kama gwajima nishndwe kumwamn kiongoz na mwanaharakat alie kua amebeba jukum na tumain la kupambana unyonyaji na ubakaz Wa democrasia nchin...?
 
alitakiwa ajitoe baada tu ya kujua anajiunga cdm
hii inaonyesha angepitishwa kugombea urais asingekuwa na tatizo lowassa kuwa ndani ya cdm
Unafkr kwa nn hakuonekana tena kwenye ulingo wa siasa since lowassa alivyoingia cdm...? (Unapaswa kufkr vizur swal hil).

Kukaa kimya huku kulikua na maana kubwa..mind u Dr. Alikua sio mtu wa kukurupuka...cku zote wataalam Wa saikolojia wanadai mda ndo kila...nafkr mda ndo ulio mpa jibu la kufanya maamz....atabak kua great man ever kwenye siasa za bongo..hakka ameacha legacy ambayo wanasiasa wachanga kama kina mnyika, makamba,zzto pamoja na vijana mnaoingia kwenye ulingo wa siasa za kidemokrasia kufuata nyayo zake...
 
Mzee mwanakijiji said:
Itawachukua muda mrefu sana hawa ndugu zetu kutambua hili na kukubali upekee wa mchango wa Dkt. Slaa katika kujenga upinzani. Sasa hivi wamekuwa kama kondoo wasio na mchungaji!
Hili ndilo tatizo la nyie wengi ambao hamkupokea na hivyo hamkushiriki kabisa katika harakati za mageuzi nchini yaliyoanza late 1980s!

Wako watu waliumia, walifilisiwa, walitengwa na ndugu zao na walitengwa na serikali ya chama cha majizi CCM kwa kuwa tu na mawazo tofauti kuhusu mfumo wa siasa.

Dr. Slaa hakuwa peke yake, wako watu kama Augustino Lyatonga Mrema na wengineo wengi tu ambao waliungana na status quo kupiga vita mageuzi kwa kutumia vyombo vya dola. Hawakujua kabisa kuwa iko siku yatawakuta na wao wapate pa kukimbilia.

Kinachoniudhi na kunikasirisha ni hawa watu baadaye kuonekana kwamba ndio walitoa mchango mkubwa katika kuleta hayo mageuzi. Mrema amewahi kuitwa kinara wa mageuzi, Dr. Slaa amewahi kuitwa nguzo katika kujenga upinzani na leo anatokea mtu na akili timamu anadai eti, nanukuu;

Kwa sababu tu wadandiaji hao wamerudi walikotoka, wapinzani wamekuwa kama kondoo wasio na mchungaji!

Kama huu si uenda wazimu tafadhali niambieni, ni nini? Hata huyo Lowassa leo hii akirudi CCM atakuwa anarudi nyumbani kwao kuungana na wenzi wake! Hajui gharama ya kupigania mageuzi, tupo tunajua!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Nyie watoto wadogo mna taabu sana...hebu rudi darasani usome historia ya mageuzi Tanzania. Uliza kitu gani kilimkimbiza Dr. Slaa huko CCM na kusetiriwa na Chadema!

Kwa ufahamisho zaidi ni kwamba Dr. Slaa aliikimbia CCM baada ya jina lake kukatwa akiutafuta Ubunge na kukimbilia Chadema na hivyo kuweza kuukuwaa Ubunge!

Alichofanya Lowassa mwaka 2015 hakina tofauti na alichofanya Dr. Slaa mwaka 1995. Wapo walioijenga Chadema kwa damu zao na siyo Dr. Slaa aliyekuwa mdandiaji tu.
Mag 3 hivyo vyote tunavijua sana...lakn. Historia hyo ya mageuz ina tofout kubwa sana na siasa za ujana zilivyoanza kukomaa...pia miaka hyo tulikua na maisha ya ki primitive haswaa... Ukubal ama ukatae...Dr .ndie alikua mwiba mkal kwa utawala Wa kizaz hik ..nikimanisha since 2005
 
Mag 3 hivyo vyote tunavijua sana...lakn. Historia hyo ya mageuz ina tofout kubwa sana na siasa za ujana zilivyoanza kukomaa...pia miaka hyo tulikua na maisha ya ki primitive haswaa... Ukubal ama ukatae...Dr .ndie alikua mwiba mkal kwa utawala Wa kizaz hik ..nikimanisha since 2005
Dr. Slaa yupi? Je, ni huyu anayesema Mh. Tundu Lissu kumiminiwa risasi ni kitu cha kawaida? Come on mr.sparon, you are joking, aren't you? Au ni huyu anayemsifia dikteta uchwara? Kama kuna hekima, busara na uadilifu wowote aliowahi kuwa nao it's gone and there's nothing left there...ameamua kuungana na watesi wetu tusio na unafiki.
 
Nimekuwa nikisoma soma humu tokea 2015 kutoka kwa baadhi ya watu kuwa eti aliyekuwa katibu mkuu wa CHADEMA na mgombea urais wa chama hicho mwaka 2010, Dkt. Wilbroad Slaa ni msaliti.

Eti ni msaliti kwa sababu aliamua kuachana na siasa baada ya CHADEMA kuamua kubadili gia angani. Pia, baada ya kuachana na siasa akakataa pia kumuunga mkono mgombea wa UKAWA, Edward Lowassa.

Sioni kabisa usaliti wa Dkt. Slaa hapo. Ninachokiona ni mtu mwenye msimamo na uadilifu na anayeongozwa na kanuni.

Hivi kweli kabisa mtu na akili yako timamu, kati ya Slaa na CHADEMA, unaweza kumwona Slaa ndiye msaliti?

Kama kuna msaliti basi msaliti huyo ni CHADEMA na si Dkt. Slaa.

CHADEMA walisaliti karibu kila kitu walichokipigania wakiongozwa na Dkt. Slaa. Ni CHADEMA ndiyo waliobadilika. CHADEMA ndiyo wasaliti.

Nyie wote mnaodiriki kumuita Dkt. Slaa kuwa ni msaliti ni vifuu tundu msiojielewa kabisa.

Dr. Slaa alieikataa CCM. Leo hii yupo CCM mulemule. Haitaji kupewa Kadi anayo hata kabla hajaenda CCM. Unatafuta usaliti Upi mwingine zaidi ya huo?.

Tukisema aliosaliti CDM kwasababu CCM walimnunua baada ya kugundua ametofautina nao utakataa?

Yeye na Mwakyembe si ndio walikutana Serena Hotel kwa siri?

Yeye na Mwakyembe si ndio waliaminisha Kua Lowasa ni Fisadi?

Mbona leo hii wamekalia makabrasha yao ya kesi za ufisadi?
Mbona kila ufisadi unaoibuliwa hatusikii Jina la Lowasa?
And yet, bado hauoni sanii.!!?.

Je bado Unahitaji PHD kuwaelewa wanasiasa?
 
Nyani Ngabu Mimi binafsi nina tatizo kubwa sana na Dkt. Slaa. Nakubaliana kwamba CHADEMA walifanya kosa kubwa la kimkakati, kwa maslahi ya muda mfupi, kumpokea na kumpa kifimbo cha kugombea Urais, Edward Lowasa. ijapokuwa pia naweza kuelewa hoja yao, kwamba kwa kuwa na Lowasa kungekuwa na uwezekano mkubwa zaidi wa kushinda urais.

Lakini tukubaliane kwamba lilikuwa kosa kubwa. sasa lakini Dkt. Slaa alifanya nini? kujiondoa CHADEMA inaeleweka, kama response ya mtu makini asiyekubaliana na kilichofanyika. Lakini kilichofuatia, kwenda live kwenye TV na kutumia hoja mbalimbali kuiponda CHADEMA, tena kwa kusaidiwa na CCM, hapo ndiyo simuelewi kabisa Dkt. Slaa.

Inaonekana zoezi lote liliandaliwa na CCM. yeye alikubali kutumika kama chombo cha kuiangamiza CHADEMA. Inaonekana Dkt. Slaa alikasirika, aliumizwa binafsi, na alikusudia kulipa kisasi. aliamua kuiharibu CHADEMA tena kwa nguvu zote, Shock and Awe. Kwa gharama za CCM, na kwa faida ya CCM. Inakuwaje, kosa moja la CHADEMA limfanye ajiunge na chama alichopambana nacho kwa miaka nenda rudi? kwa hiyo kwa kosa hilo la CHADEMA, CCM imekuwa safi?

Na kwa kweli, kwa kuangalia ile TV presence yake pale Clouds TV, unaweza kuona kwamba amebaba madhambi yote ya CCM. hana cha kukemea kwa nguvu katika CCM isipokuwa katika Upinzani. alifanya kile kinachoitwa "a tactical defence of CCM" alijificha nyuma ya "uchambuzi" , "umakini" lakini kwa uhalisia, alikuwa ni kama kada yoyote wa CCM.

Kuna swali aliulizwa, kuhusu maoni yake kwa shambulio la Tundu Lissu, na hoja kwamba hajatoa pole. Alijibu kwamba kuna mashambulio mengi tu yanafanyika kila mahali, So what? Lakini ni kama mtu anapata taarifa za rafiki yake kupata majanga, halafu hatoi pole. akiulizwa anajibu kwamba wengi tu wanapata majanga, so what. haiwagi hivyo. Slaa na Tundu Lissu wamepigana na kupambana side by side kwa miaka nenda rudi. wamejenga uhusiano mkubwa sana kama udugu vile. makamanda vitani sasa kwa mtu makini kama Slaa, ilikuwa ni jambo jema kuonesha ushirikiano na CHADEMA katika hali hiyo ngumu. kwamba hata kama walitofautiana huko nyuma, lakini bado nia yake ni kuona mapambano ya kudai haki yanaendelea vema, tena siyo Tanzania tu, bali Afrika Mashariki, Afrika na popote duniani.

Ningetarajia hayo kwa mtu wa calibre ya Slaa. lakini mwenyewe amejishusha chini sana. anastahili kuitwa MSALITI. hajaisaliti CHADEMA tu, bali amesaliti mapambano ya kudai haki toka kwa serikali kandamizi. amekuwa mshiriki wa serikali mojawapo katika kukandamiza haki za raia. hiyo ni changeover kubwa sana, eti kwa kisingizio cha CHADEMA kubadili gia angani! Actually, yeye pia amebadili gia angani. kutoka mtetezi wa wanyonge, hadi kuwa comrade in arms na serikali kandamizi. na yeye ndiye aliyefanya mabadiliko makubwa zaidi kuliko hata CHADEMA
Well said Mkuu.
 
Nimekuwa nikisoma soma humu tokea 2015 kutoka kwa baadhi ya watu kuwa eti aliyekuwa katibu mkuu wa CHADEMA na mgombea urais wa chama hicho mwaka 2010, Dkt. Wilbroad Slaa ni msaliti.

Eti ni msaliti kwa sababu aliamua kuachana na siasa baada ya CHADEMA kuamua kubadili gia angani. Pia, baada ya kuachana na siasa akakataa pia kumuunga mkono mgombea wa UKAWA, Edward Lowassa.

Sioni kabisa usaliti wa Dkt. Slaa hapo. Ninachokiona ni mtu mwenye msimamo na uadilifu na anayeongozwa na kanuni.

Hivi kweli kabisa mtu na akili yako timamu, kati ya Slaa na CHADEMA, unaweza kumwona Slaa ndiye msaliti?

Kama kuna msaliti basi msaliti huyo ni CHADEMA na si Dkt. Slaa.

CHADEMA walisaliti karibu kila kitu walichokipigania wakiongozwa na Dkt. Slaa. Ni CHADEMA ndiyo waliobadilika. CHADEMA ndiyo wasaliti.

Nyie wote mnaodiriki kumuita Dkt. Slaa kuwa ni msaliti ni vifuu tundu msiojielewa kabisa.

Hivi ilikuwaje Dr. Slaa akaishia kuishi uhamishoni muda mfupi sana baada ya “kujiuzulu siasa za vyama”? Kule Canada anaishi kama mkimbizi wa kisiasa? Serikali ilihusika kuratibu (facilitate) mchakato wa Dr. Slaa kwenda kuishi uhamishoni?

Nasikia sasa ameteuliwa kuwa balozi kwa kuwa serikali ya Canada imeanza kuuliza maswali kuhusu uhalali wa Dr. Slaa kuishi Canada. Sasa itakuwa rahisi kwa kuwa amekuwa diplomat na pengine atafanya kazi kama mwambata katika ubalozi wa Tanzania nchini Canada. Ni ngumu kama ni Dr. Slaa yuleyule aliyekuwa mwiba kwa maCCM anakarimiwa kiasi hiki.
 
Mkuu hapa pia tunatofautiana..who is gwajma...? Yaan nmwamn mtu asie kuwa na msaada kwangu halafu nishindwe kumwamin MTU aliekua kabeba mstakabal Wa dhana ya demokrasia yenye mising ya utu na hak...I mean unachotaka niamn maneno ya mwendawazm kama gwajima nishndwe kumwamn kiongoz na mwanaharakat alie kua amebeba jukum na tumain la kupambana unyonyaji na ubakaz Wa democrasia nchin...?
Umejikumbushia lakini ile video ya press ya Slaa kung’atuka? Ni dhahiri hujajikumbushia na umesahau Gwajima alihusika vipi. Angalia ile video, nimeiweka mara 2 humu.
 
Kupinga wazi wapi? Mzee unadhani mimi ni nani CHADEMA? I'm a nobody CHADEMA. Mimi ni mwananchi wa kawaida tu aliye concerned na mambo yanavyoenda, na upotoshaji mnaoufanya nyiye fanatics wa Slaa. Ingawa ni kweli ni mpenzi wa CHADEMA, kwani ninaichukia CCM kuliko ninavyomchukia shetani.

Hivyo, kuhusu kupinga harakati za kumpokea fisadi Lowassa, hata ningepinga nisingesikilizwa, kwani hata kadi ya chama sina. Ingawa, kwenye maisha yangu binafsi na watu wanaonizunguka, nilimpinga, nimempinga na ninaendelea kumpinga Lowassa mpaka kiama. Hafai kama ambavyo Magufuli na mtu yeyote mwenye chembechembe za CCM asivyofaa. Nimeandika sana humu juu ya CHADEMA kufanya big blunder katika hilo la Lowassa. But, hey I'm a nobody, with no influence within CHADEMA.



Huu ndiyo usanii ninaousema wa huyo aliyekutuma kumtetea hapa. Kwa kashfa na tuhuma ambazo Slaa na CHADEMA walimwelekezea Lowassa, ni kosa kubwa sana hata kumjadili ati juu ya yeye kuwa mwana CHADEMA. Hakuna mkakati wowote wenye tija in long term katika hili.

Yaani unafikiri kuna uovu gani ambao CCM imefanya tungestahili kujua kutoka kwa Lowassa zaidi ya kile ambacho tunajua hadi sasa? Hakuna uovu ambao angeutaja na kuleta tija kwetu watanzania. Tunajua vya kutosha, kama haya tunayoyajua hadi sasa hayatoshi kutufanya tuone how evil CCM and its crooks of members, including Magufuli, basi hakika Lowassa asingeongeza lolote la maana.

Binafsi sihitaji kujia uovu zaidi wa CCM kutoka kwa mtu yeyote yule. I know enough to hate CCM; not vote for them; and never associate with none of them CCM crooks. Nina ndugu humo serikalini na ni maCCM, uwa nawaambia haya on their faces.




Hujajibu swali langu hadi sasa: taratibu zingefuatwa, ufisadi wa Lowassa ungefutika? Uhai wa chama utalindwaje kwa chama kuchukua lifisadi likubwa kabisa kwenye taifa letu?




Slaa should have been straight from the get go, kwamba he doesn't roll with Lowassa. He should have told Gwajima that. Kama Gwajima angetafuta kiongozi mwingine kumsaidia kufanikisha Lowassa kuingia CHADEMA, hakika leo Slaa angepata sifa kutoka kwangu. But, Slaa ndiye kimsingi aliyefanikisha Lowassa kuingia CHADEMA, kwani yeye ndiye aliyewezesha wazo hilo kufika kwa chama na Mwenyekiti.



Hata nikisema, it doesn't change anything. Inabaki kuwa kelele tu. Ingawa, rekodi yangu humu ipo wazi kwamba CHADEMA walichemsha katika hili la Lowassa. Kwani nchi hii imefika hapa ilipo kwa sababu ya CCM. Mtu yeyote mwenye chembechembe za CCM hawezi kuwa mtu wa kulitoa taifa hili lilipo sasa.



This proves how shallow you are. Yes, ninakipenda chama, ingawa sina uanachama. Hivyo, kinachotokea huko kimsingi hakina madhara yoyote katika kile ninachokiamini. Na nitaendelea kusema kwamba, kama ilivyo kwa Magufuli, Lowassa naye alistahili kuwa jela na siyo mtaani. Lakini nani wa kumfunga paka kengele CCM?
Mzee kupinga ushindwe kwasababu wewe ni "no body" na huna kadi ya chama lakini kumpinga Dr Slaa uweze na kumtetea Mbowe na Chadema kila tulipopaza sauti uweze!!! Unafurahisha sana .....hata mimi ni "no body" na sijawahi kumiliki kadi ya chama chochote lakini nina wajibu kwa nchi yangu.....kusema Dr Slaa asingeruhusu hata kujadiliana na Lowasa naona unajisahaulisha mzee .....Dr Slaa ameeleza hata kikao chenyewe kilivyoitishwa .....zaidi ya Gwajima kumpigia Dr Slaa juu ya uwezekano wa kumpokea El na Dr Slaa kumueleza azungumze na Mwenyekiti ili watafakari hakuna tena kilichofuata ( ni dhahiri mazungumzo yalishafanywa walikuwa wanamtega) .....then procedures zingine hata katibu hakujua kinachoendelea ikiwemo swala la kikao na ajenda zake .....haya yote yapo kwenye maelezo ya Dr Slaa pale Serena ndio maana naona watu kama wewe mnapindisha hili makusudi ....kwanini hujawahi kuandika kero yako hii ya Chadema kumpokea Lowasa lakini kila akitajwa Dr Slaa unaibuka na kauli za usaliti? Anyway tuseme ni msaliti basi tungeona ukilaumu wote ....lakini comments zenu toka El anapokelewa zipo humu ....wengine sasa hivi ndio walau mmeanza kusema japo kidogo EL haikufaa kupokelewa ....huku mkikwepa kutaja makosa haya ya mwenyekiti aliyebadili gia angani mkashangilia ....rekodi zenu zipo humu
 
Back
Top Bottom