Kumezuka jitihada za kupotosha juu ya kilichotokea. Ila tunashukuru uwepo wa kumbukumbu za kivideo na maandishi. Kama hiyo video inavyoonyesha, Slaa mwenyewe alikiri kushiriki maongezi ya kujadili ujio wa Lowassa CHADEMA. Slaa alienda mbele na kusema alitoa masharti ya Lowassa kufanya kabla ya yeye kukubali ujio wake. Mtu aliye principled, hata nafasi ya kumjadili mtu aliyemtuhumu kuwa ni fisadi asingeipata.
Usaliti wake mkubwa ni yeye kukubali kutumika na CCM katika wakati ambao mapambano yalikuwa yamepamba moto. Kwa kuheshimu harakati zake, angeweza kuondoka chamani, kusubiri uchaguzi uishe na kisha kusema aliyoyasema. Ila yeye kukubali kutumiwa na CCM (kulipiwa gharama za press, kukutana na Mwakyembe n.k.) wakati kama ule, ndiyo sababu ya yeye kuitwa msaliti. Alisaliti harakati alizoshiriki kuzianzisha.