Usaliti wa Dkt. Slaa ni upi?

Usaliti wa Dkt. Slaa ni upi?

Mimi kwangu nina mitazamo tofauti ni wengine kuhusu Dr. Slaa. Usipokuwa makini unaweza kumchukulia Slaa kama msaliti. Sikufurahishwa na Slaa alipoondoka cdm, tena kuondoka kwake akakutumia kama sehemu ya kuiumuza cdm kwa faida ya ccm. Ila hata ningekuwa mimi ningechukua maamuzi ambayo yangewashangaza wengi. Slaa alijiandaa kugombea urais cdm, na kweli alistahili hata kama asingeshinda lakini cdm ingebaki na msimamo wake. Lakini ninachomlaumu Slaa mpaka leo, hivi akija mtu kwenye chama chako kwakuwa humpendi ndio unaondoka. Kwangu naamini Slaa aliondoka cdm kwa kuzira baada ya kukosa nafasi aliyokuwa ameshajiandaa kuitumikia, ila kwakuwa cdm nao walifanya kosa kumpokea Lowassa ambaye alikuwa na kashfa, hapo ikawa rahisi Slaa kuhalalisha huko kuzira kwake. Hivyo mpaka sasa kwangu imebaki 50/50 kwamba Slaa aliondoka kwa kukosa nafasi ya kugombea urais, ama aliondoka kwa kutokutaka kubaki kwenye chama ambacho kimempa Lowassa nafasi adhimu ya kugombea urais wakati walimtuhumu kwamba ni fisadi. Yote mawali kwangu inaweza kuwa ni sababu ya Slaa kuondoka cdm.

Kama Slaa ni msaliti ama la, hilo linategemea na utashi wa kila mtu kulingana na uelewa wake na sababu nyingine mbalimbali. Kilichonifanya nianze kumuona Slaa hana maana ni ile sentesi yake ya jana kuhusu Lissu. Kwa kweli Lissu hakumfanyia Slaa sawa wakati kajitoa cdm kwa zile lugha alizokuwa anamtolea, lakini Slaa kama padre mstaafau alipaswa kusahau baadhi ya mambo na kuacha kutoa lugha zitakazoonyesha kwamba yaliyomkuta Lissu ni mambo ya kawaida. Ukiachia mapungufu hayo niliyoyaona kwa Slaa sioni kama ni adui sana wa cdm kulinganisha na mambo mengine yanayoendelea ndani ya cdm kwa sasa.
Mkuu tindo ni kweli. Amesema kweli tupu. Wewe ni miongoni mwa watu ambao mpo objective na constructive. Dr Slaa wa leo sio yule wa 2015.
Jiulize amepewa masharti gani hata asitoe pole ya mdomo tu kwa madhila yaliyomkuta Lissu.

Je tuamini sasa kuwa na yeye ana visasi?!
 
Ukihama CHADEMA kuna maneno haya huwezi kuyakwepa 1. Msaliti 2. Amenunuliwa 3. Anatafuta cheo 4. Hana akili, mengine ongezea
 
..hakuna usaliti wowote.

..kwanza vita ya ufisadi haikupiganwa na Dr.Slaa peke yake.

..wako wanachama wengi waliojitoa pamoja na Dr ktk kupinga ufisadi.

..Ila CDM waliamini EL atawaletea ushindi.

..hawakuamini kama Dr.Slaa angeweza kushinda uchaguzi.

..matokeo yake wakambwaga Dr na kumchukua EL and the rest is history.

..chama chochote kinapoamua kumsimamisha mgombea fulani there is a risk involved.

..mgombea huyo anaweza kushinda au kushindwa. Sasa akishindwa chama kinapaswa kujipanga upya.
Uko sahihi sana...kilichokosekana ni chadema kujipanga upya.
 
Hata hawa wabunge na madiwani wanaonunuliwa chanzo ni ujio wa Lowasa.

Hata baada ya kumpokea Lowasa Chadema walijifanya wanaweza kushindana na ccm ambacho ni chama dola.

Walimnunua Katibu wa ccm Iringa, alihama bila hata kukabidhi ofisi matokea yake akapewa ubunge viti maalum Chadema.

Tuliwaambia toka awali Chadema ifuate misingi na taratibu za chama kwenye uendeshaji wa shughuli zake sio kupimana na ccm ambacho ni chama dola.

Matokea yake ndio haya ccm wameingia miguu yote miwili kwenye ununuzi wa viongozi wa Chadema.

Ahaaa... hawa Chadema acha dhambi ya usaliti kwa watanzania iwatafune tu.
Unaelimu gani? Tuanzie hapo
 
Kumbuka tu 2010 Chadema ilisimama peke yake, halafu 2015 viliungana vyama vingapi.?

Ukitaka kujua mchango wa Dr Slaa Nenda kwenye uchaguzi wa serikali za mtaa 2014......hapo ndio utajua hata kura na mafanikio ya 2015 mizizi ni 2014.

Huyo Lowasa amekuja kwenye shamba ambalo tayari limeshalimwa.
Ku discredit influence ya lowasa 2015 ni ukengeufu....tuwe wakweli na tujifunze kuusema ukweli huo...lowasa ana mapungufu yake lakini 2015 alikuwa na influence kubwa sana
 
linganisha kura milioni mbili za mwaka 2010 na milioni sita za 2015
kama hata hujui hesabu za kujumlisha na kutoa mimi siwezi kukusaidia
Mkuu zama zinabadirika,upepo wa kisiasa 2010 ni tofaut na 2015.Hata angesimama Slaa kutokana na misimamo waliyokuwa nayo chadema kura zingeongezeka tu.Siku zingekuwa zinarud nyuma hoja yako ingekua sahh
 
NISAIDIE KUELEWA MKONO WA KUSHOTO WA MBOWE ANAITWA NANI HUYO?
ALIKUWA ANAFANYA NINI HAPO?
KAMA HAKUMKARIBISHA LOWASSA ALIKUWA ANAFANYA NINI HAPO?SI SI ASINGEKUWEPO KABISA?
MNAELEWA KUWA KILICHOMTOA CDM NI BAADA YA KUKATALIWA KUGOMBEA URAIS!!!
MMEKUWA NA NYINYI KAMA MMELISHWA LIMBWATA LA KIHAYA SHUNTAMA
d06777c9-4a07-4ef9-9ce1-bdc6202508b9-jpeg.672363
kuondoa utata ,ungeweka video clip ili tujionee kinachoendelea. kwa picha hii nina wasiwasi huo mkono umekuwafotoshopudi si kwa mikunjokunjo ile.
 
Magufuli alikuwepo kwenye list of shame?
Ndiyo, alikuwepo...
...kwa umbukumbu

Dr.Wilbrod-Slaa.jpg

Septemba 15, 2007, Dk. Willibroad Slaa akiwa wilaya ya Temeke katika viwanja vya Mwembeyanga aliwataja hadharani vigogo 11 wanaodaiwa kuwa ni mafisadi.

1. Jakaya Mrisho Kikwete
2. Benjami Mkapa
3. Edward Lowassa
4. Daniel Yona
5. Rostam Azizi
6. Andrew Chenge
7. Daudi Balali
8. Nazir Karamagi
9. Patric Rutabanzibwa
10. Nimrod Mkono
11. Basil Mramba

Apr 16, 2011, Dk. Slaa, akiwa mjini Tabora aliwataja hadharani orodha ya pili ya vigogo 6 na hivyo idadi ya watuhumiwa wa ufisadi kuongezeka hadi kufikia 17.

12. Frederick Sumaye
13. John Pombe Magufuli
14. John Samweli Malecela
15. Philip Mangula
16. John Kato
17. Bharati Goda
 
Mag3 Kwanini hii list mmeinyofoa kwenye website yenu toka EL alivyotinga Chadema? Mnajisaliti wenyewe alafu mnasingizia wengine. Kwanini hii list haipo na mkateua mtuhumiwa wenu agombee urais?
 
Dr Slaa anaitwa msaliti sio kwa sababu aliisaliti chadema, hapana.
Dr Slaa anaitwa msaliti kwa kusaliti harakati zake za kuitoa CCM madarakani na mwisho wake kujiunga nao hao hao CCM.

Kama yeye kweli anamsimamo alitakiwa aanzishe chama chake au kujiunga na chama kingine cha siasa au awe mwanasiasa huru mwenye kutetea wananchi katika kila uovu, leo anataka kutuambia CCM ni safi iungwe mkono, hahahaa huu utani..
Hivi angepewa nafasi ya kugombea Urais pale CDM angekuja leo kutuambia CCM ni safi?, CCM iliyokuwa chafu baada ya yeye kunyimwa nafasi ya ubunge karatu leo imekuwa safi baada ya kupewa ubalozi na CDM imekuwa chafu baaada ya kumnyima nafasi ya urais?, HATUHITAJI WANASIASA WA NAMNA HII TANZANIA..

Tupo wengi sana ambao hatukukubali ujio wa Lowassa lakini hatukujaribu kukaa upande wa CCM, adui yetu na adui wa taifa hili CCM, ukiiondoa CCM utakuwa umepambana na adui mkubwa ujinga maana ujinga ndio uhai wa CCM.
Ujinga ndio chanzo cha matatizo yote na umasikini wa Tanzania, Ukipambana na CCM utakuwa umepambana na ujinga.
 
..hakuna usaliti wowote.

..kwanza vita ya ufisadi haikupiganwa na Dr.Slaa peke yake.

..wako wanachama wengi waliojitoa pamoja na Dr ktk kupinga ufisadi.

..Ila CDM waliamini EL atawaletea ushindi.

..hawakuamini kama Dr.Slaa angeweza kushinda uchaguzi.

..matokeo yake wakambwaga Dr na kumchukua EL and the rest is history.

..chama chochote kinapoamua kumsimamisha mgombea fulani there is a risk involved.

..mgombea huyo anaweza kushinda au kushindwa. Sasa akishindwa chama kinapaswa kujipanga upya.

Kwanza tuujue ukweli nani aliyempeleka Lowassa Chadema?Kwanini leo Dr.Slaa hakusema ukweli Dr.SLaa,Lowassa na Gwajima walikuwa wanajuana na Dr.Slaa ndiye aliyempigia simu Mbowe wakutane kwenye kikao chao,kwanini leo hasemi kama alivyosema pale Serena?

Uongo ukizidi unakuwa ukweli ninamtaka Dr.SLaa aikane ile press conference pale Serena
 
Dr slaa atarudi CCM rasmi ..jipe miezi sita halafu na lowassa nae kufikia mwakani anarejea CCM.

Hapo nitakutaka uje na thread tena kutuonesha namna dr slaa alivyomkataa lowassa.

Dr slaa wa leo sio wa wkt ule.

Mimi nilimuunga mkono kwa hatua zote hadi alipoondoka chadema. Kitendo cha yeye kurudi CCM ndio mi naanza kuona hana jipya sasa.

Naunga mkono hoja, huwezi kujiita mtetezi wa wanyonge halafu ukawa CCM..
 
Dr Slaa anaitwa msaliti sio kwa sababu aliisaliti chadema, hapana.
Dr Slaa anaitwa msaliti kwa kusaliti harakati zake za kuitoa CCM madarakani na mwisho wake kujiunga nao hao hao CCM.

Kama yeye kweli anamsimamo alitakiwa aanzishe chama chake au kujiunga na chama kingine cha siasa au awe mwanasiasa huru mwenye kutetea wananchi katika kila uovu, leo anataka kutuambia CCM ni safi iungwe mkono, hahahaa huu utani..
Hivi angepewa nafasi ya kugombea Urais pale CDM angekuja leo kutuambia CCM ni safi?, CCM iliyokuwa chafu baada ya yeye kunyimwa nafasi ya ubunge karatu leo imekuwa safi baada ya kupewa ubalozi na CDM imekuwa chafu baaada ya kumnyima nafasi ya urais?, HATUHITAJI WANASIASA WA NAMNA HII TANZANIA..

Tupo wengi sana ambao hatukukubali ujio wa Lowassa lakini hatukujaribu kukaa upande wa CCM, adui yetu na adui wa taifa hili CCM, ukiiondoa CCM utakuwa umepambana na adui mkubwa ujinga maana ujinga ndio uhai wa CCM.
Ujinga ndio chanzo cha matatizo yote na umasikini wa Tanzania, Ukipambana na CCM utakuwa umepambana na ujinga.

Kweli kabisa na wengi tulimuomba asiondoke lakini hakutuona watanzania tuliomuomba abaki kama tunathamani akaona pesa ni bora kuliko UTU.
 
Lowassa anakuja Chadema unampokea na kuwa pamoja naye na unaendelea kuwa mwana chadema.
Lowassa anapewa nafasi ya kugombea Urais unakataa na kuikataa chadema, TATIZO NI LOWASSA AU KITI CHA URAIS?
 
Slaa hajabadilika.

Alimkataa Lowassa wakati Lowassa yupo CCM na akamkataa alipoenda CHADEMA.

Huyo ni mtu mwenye msimamo. Mtu mwenye kanuni.

Sioni kabisa usaliti wake.
Mimi namhurumia sana Lowassa. Huyu mtu na heshima zake leo yuko na genge la wahuni eti mjumbe wa kamati kuu wakati hata CCM angekuwa mjumbe wa kamati na wa kuheshimika ila kisa uroho wa madaraka na tamaa ya urais ndo anajidhalilisha kule? Lowassa kuongozwa na Mbowe ni upumbavu.
 
Slaa hajabadilika.

Alimkataa Lowassa wakati Lowassa yupo CCM na akamkataa alipoenda CHADEMA.

Huyo ni mtu mwenye msimamo. Mtu mwenye kanuni.

Sioni kabisa usaliti wake.

Lakini ndiye aliyempeleka CDM,tafuta Video zake za alivyoifanya ile press conference ya kwanza pale Serena.Kumbula Lowassa na Dr.Slaa wote hawa walikuwa wanaunganishwa na Gwajima ambaye kwake Dr.Slaa alikuwa Baba wa Kiroho.

Na muda aliomtambulisha Gwajima kama Baba yake wa Kiroho nilimdharau pale pale,maana Dr.Slaa aliwahi kuwa Padre na anaelewa vyema Baba wa Kiroho ni nani ilinishangaza,na sitoshangaa hata akija kusema hakuongea hivyo pale Serena.Nilimsikia kwa masikio yangu na nikamuona kwa macho yangu,tuache unafiki Dr.SLaa aikane kwanza ile Press Conference ndipo nitamuelewa
 
Back
Top Bottom