Usalama wa Taifa hutangaza nafasi za kazi ila sio direct kama watu tuvyofikiria

The meaning of being secrete Agent with special Task is to know the The Risk ahead. Katika kucalcute risk ahead APA watu wengi wanashindwa ndo uwa wengi wanajikuta kuwa na profile fb/ insta kupost picha basii...
Kuwa secrete agent ukiamua kuweka nia ukataka uwe uko unaweza kuwa...


Kazi yenyewe kama inavyojieleza ni secrete agent katika maisha yako usitegemee kuna proper way recruitment kwa watu ambao amko katika majeshi yetu..

Sababu unamuajiri MTU toka nje ukamuweka usalama moja kwa moja the risk is very high ikiwa uyo MTU Serikali aina faili lake ya maisha aliyoishi tofauti na mama...ndugu kati yenu alikuwa anafanya kazi uko kupata inakuwa raisi..


So kama unataka kufanya usalama do impossible thing to challenge them
 
Habari wanajamvi, kumekuwa na ulinganishi,ukosoaji na maulizo kwa nini nchi zilizoendelea mashirika yao ya kijasusi hutangaza nafasi za kazi kwa uwazi kabisa kama zinavyotangazwa kazi nyingine kwenye vyombo mbalimbali kama magazetini,mitandaoni n.k. lakini ni tofauti kwa nchi zetu. Baadhi ya wakosoaji huwa ni watu walio katika nchi hizi zilizoendelea hivyo kwao huona kitu cha kawaida ila hushangaa kwetu halipo hilo jamabo na kutoa mifano ya mashirika kama CIA, MI6 n.k wakitangaza nafasi za kazi kwa uwazi kabisa

Ukweli ni kwamba kazi hizi hutangazwa kama kawaida ila tu hazitangazwi direct kabisa kwa kuambiwa unajiriwa na idara ya ujasusi. Utakuta tangazo linahitaji wapishi, wafagiaji n.k lakini unachoenda kukifanya unafanya ukiwa mwajiriwa wa idara. Hii hutokea kulingana na mahitaji ya wakati huo. ila sisemi wote huajiriwa hivyo hapana,ila ikitokea kwa mfano idara ina uhitaji wa madereva,ina maana zinaweza kutangazwa tu nafasi za kazi za udereva.

Ngoja nitoe mifano hai, majuma kadhaa nyuma kulitangazwa nafasi kwa ajili ya kuwapata vijana wa kuwapa mafunzo ya upigaji picha ili wazunguke mashuleni nchi nzima kwa ajili ya kupiga picha, lakini tangazo lilionesha ni kazi ya mda mfupi na ukilipwa kwa kila kichwa kiasi fulani tu cha kawaida, lakini kweli ilikuwa ni idara. Je vijana wa ngapi wenye degree unaweza ukawaambia kuwa ukapatiwe mafunzo ya kupiga picha alafu azunguke nchi nzima kwa kila kichwa elfu moja wakakubali? Aliyekubali maana yake yupo tayari kufanya kazi yeyote mahala popote bila kujali kwamba ana elimu gani.

Mfano wa pili kulitangzwa kazi kwa watu wenye Diploma ya IT lakini walikuwa wanaenda kuwa waajiriwa wa idara, imagine usawa huu wa masuala ya IT yaliyovyopamba moto lakini unasikia wanahitajika wa Diploma. Kwangu tafsiri yake kwanza matarajio ni kwamba wengi wao watakuwa ni vijana wadogo, kwa hiyo watakuwa ni watiifu kwani wengi wao hawajaanza maisha,wengi wao watakuwa hawajaingia kwenye masuala ya ndoa, wengi wao watakuwa wana njaa na kiu ya mafanikio lakini pia miili yao inaweza kuhimili mikiki mikiki ya mafunzo kwa urahisi zaidi.

Ni mawazo yangu binafsi, karibuni kwa michango
[/QUOT
Napingana na wewe.Hawa watu si wa mchezo mchezo.Wana watu wao mashuleni na vyuoni,mwalimu anakuangalia tokea ukiwa darasa la tatu,ukienda sekondari unapokelewa na mwalimu mwingine hivyo hivyo mpaka watakapoamua kukuchukua.
Njia nyingine ni kutumia wazee wastaafu kuleta vijana wao.
Hawawwezi kuweka matangazo hovyo,na njaa hii waliokuwa nayo vijana,wanaweza kujikuta wanamuajiri Salary Slip!itakuwa hatari tupu idarani
 
Kwani hata ukiwa na hiyo 45 lakini ni ' Talented and Charismatic ' kama GENTAMYCINE sitowafaa katika majukumu yao?

Duuuh,
Mimi nimeona wachangiaji wengi wanasema kuwa ni vijana Wadogo wanachukuliwa kwa hiyo sikuelewa kuwa inawezekana hadi vibabu //vikongwe na vibibi / ajuza wakachukuliwa na kuwa huko aisee
 
Aman iwe nanyi wapendwa katika bwana

Husika na kichwa cha habari hapo juu

Nataka kuwa usalama wa taifa
Ni wapi nikaombe hii kazi ya usalama wa taifa?
Ni wapi nitapata mafunzo ya usalama wa taifa?

Naombeni msaada wenu wanajukwaa

LONDON BABY
 
Unataka kua mtu usiye julikana, kuna kijana namfahamu yeye alikwenda CCP alipokua huko alikua akichunguzwa tabia yake kuanzia pale mapaka shule aliposoma mapaka nyumbani mtaani tulikuja kuulizwa maswali kuhusu yeye.

Wakati wa kumaliza mafunzo akachukuliwa akapelekwa huko kwenye vitengo vyao Leo hii namuona na Earphone sikioni
 
Aman iwe nanyi wapendwa katika bwana

Husika na kichwa cha habar hapo juu

Nataka kuwa usalama wa taifa
Ni wapi nikaombe hii kaz ya usalama wa taifa?
Ni wapi nitapata mafunzo ya usalama wa taifa?

Naomben msaada wenu wanajukwaa


LONDON BABY
Kazi za Usalama wa Taifa hazitangazwi kama ajira nyingine za majeshi.

Kama nia yako ni ya kweli ya kizalendo kuilinda nchi yako unaweza kuifanya hiyo kazi kwa kujitolewa kama informer kama una taarifa zenye mashiko zifikishe kwenye ofisi ya DSO hapo unapoishi na utatambulika rasmi kama informer wao.
 
Back
Top Bottom