Hapana ndugu yangu usimuhukumu mtoa hoja, ni kweli kabisa kabisa kuna baadhi ya ndege ambazo ni zile za mwanzo kabisa, usalama wake ni mdogo sana. zile ndege ni chakavu sana, hata mie nilipanda moja mwaka jana ilikuwa inapitia Musoma, ilikuwa inahangaika hata kufunga matairi, viti vilikuwa ni chakavu sana. kama wewe ni msafiri wa Mza Dar hutoweza kuzijua, ila waendao Mtwara, Musoma Shinyanga na kwingineko kusiko na abiria wengi watakuwa wanazijua.
Mleta hoja muongo kwa kweli. Miye nimepanda mara nyingi sana. Mwz - BK- Mwz, Mwz-Dar- Mwz, hata ile ya Mwz- Nairobi ni nzuri sana.Ni kweli hizo ndege zina matobo kama dala dala au mleta hoja ni mwongo?
October 2010 nilishawai kuwapelekea malalamiko kwenye ofisi zao pale NIC Building/Samora kuhusu cancellation za safari na kuhusu viti chakavu. wakadai watashughulikia. Tena wanakujibu kwa dharau kuonyesha kwamba hakuna alternative kwa local transport lazima utumie usafiri wao hata kama upendi. Natumaini moja ikianguka na kuua watu kadhaa may be watasikia.
<br />Mtoa hoja ana chuki binafsi au anatumiwa na washindani wa hii biashara kuichafua Precision Air. Mimi ni mtumiaji mkubwa wa huduma zao, ndege zao ziko katika hali nzuri sana. Nyingi ni bado mpya na hata huduma zao ndani ni za kuridhisha. Tatizo lao ni ucheleweshaji (si mara zaote) na pia ukizidisha hata kilo moja wanakulipisha.....ie hawana uhusiano mzuri na wateja ktk mzani.
<br /><font color="#0000cd"><span style="font-family: comic sans ms"><font size="4"><b>Hapo Kwenye RED Shirika letu halija shindwa ila limefilisiwa na Mataka pamoja na Viongozi wa Serikali na Precions walikuwa waiba Spare kwenye Ndege zetu, hao ndio waliochangia kufa kwa Shirika letu </b></font></span></font>
Tangia nimekuja hapa Nchini nimepata ndege za Precision mara kadhaa sasa .Lakini kama kawaida ndege hizi zinatisha na bado zinaruka .Najiuliza maswali mengi lakini nisema kuna tume itaundwa baada ya ajali kutokea maana ndiyo Tanzania yetu .Ndugu zanguni kwa wale ambao mmeshawahi kutumia ndehe hizu hebu niambieni juu ya hali ya vioo kwenye ndege hizi, viti ni chakavu ile mbaya , jana nimepanda ndege ina matobo kama daladala .Juzi nilipanda ukuta wake ukiwa unacheza kama vile waingiza upepo .Hivi kweli wana usalama wa ndege hizi wapo au wanajua ila wanafumbia macho jambo hili ? Ndege za Precision ni kama daladala kabisa na hata huhutaji uchunguzi wa kina maana ukiingia tu unaona shida zote hizo nilizo taja hapo .Kuna moja niliwahi kupanda ikawa hata haipozi hewa na uko ngani lakini joto kama uko beach na hakuna miti ya kujikinga .
Sasa wana tatizo la delays na flight cancellation .Hakuna wa kulalamika Watanzania wanachelewa mpaka matibabu lakini wao wako kimya tu.Je tunangojea litokee jambo tuunde Tume na kusema waziri ajiuzuru ?
Mwaka huu mwezi January nilipanda hiyo Precision kwenda Mwanza tiketi ikiwa kwenda nakurudi,niliyoyaona ilibidi wakati wa kurudi ni rudi na basi na nikasamehe hiyo nauli yangu,hilo ni jeneza linalopaa,ni sawa na zile ndege za DRC(kwa waliofika na kupanda ndege za DRC zikiwa zinasafiri usafiri wa ndani)Tangia nimekuja hapa Nchini nimepata ndege za Precision mara kadhaa sasa .Lakini kama kawaida ndege hizi zinatisha na bado zinaruka .Najiuliza maswali mengi lakini nisema kuna tume itaundwa baada ya ajali kutokea maana ndiyo Tanzania yetu .Ndugu zanguni kwa wale ambao mmeshawahi kutumia ndehe hizu hebu niambieni juu ya hali ya vioo kwenye ndege hizi, viti ni chakavu ile mbaya , jana nimepanda ndege ina matobo kama daladala .Juzi nilipanda ukuta wake ukiwa unacheza kama vile waingiza upepo .Hivi kweli wana usalama wa ndege hizi wapo au wanajua ila wanafumbia macho jambo hili ? Ndege za Precision ni kama daladala kabisa na hata huhutaji uchunguzi wa kina maana ukiingia tu unaona shida zote hizo nilizo taja hapo .Kuna moja niliwahi kupanda ikawa hata haipozi hewa na uko ngani lakini joto kama uko beach na hakuna miti ya kujikinga .
Sasa wana tatizo la delays na flight cancellation .Hakuna wa kulalamika Watanzania wanachelewa mpaka matibabu lakini wao wako kimya tu.Je tunangojea litokee jambo tuunde Tume na kusema waziri ajiuzuru ?
nDEGE HAIWEZI KUWA IMETOBOKA MPAKA WANAPOKAA ABIRIA IKARUHUSIWA KURUKA!!!!!. HAPA KUNA CHUMVI NYINGI IMEONGEZWA MAANA MIMI NATUMIA NDEGE HIZI KILA MARA. TATIZO LAO HASA NI CANCELLETION YA SAFARI HASA WANAPOKUWA WAMEPATA WATEJA WACHACHE. nDEGE ZAO ZA ATR ZOTE NI NZURI SANA
<br /><span style="font-family: comic sans ms"><font size="3"><b>Mi sio Mpenzi wa hizo ndege ni bora nipande basi kuliko ku-risk maisha yako na hizo ndege za mitumba</b></font></span>
Nimesafiri mara kwa mara na Precision sijaona matatizo ya kiufundi (MIMI SI FUNDI ) naona ndege zao ni nzuri na nyingi ATR ni mpya sasa hayo mengine labda tupate ufafanuzi wa wataalamu sio abiria