Usaili wa kazi uliyokuwa unafanya mwanzo kabla ya kushushwa cheo

Dilas

Member
Jul 24, 2012
80
67
Habari wakuu,

Ninaomba ushauri wa jambo hili. Miaka miwili iliyopita niliashushwa cheo kutokana na kutoelewana na mfanyakazi mwenzangu ambaye hayupo tena kwenye kampuni yetu.

Sasa nafasi hiyo imetangazwa tena ila kwa mkoa mwingine.

Na mmoja kati ya wahusika wa usahili ni kiongozi aliyekuwepo wakati huo kwenye mkoa wangu na alikuwepo wakati wanafanya maamuzi ya kunishusha cheo.

Je, nina haki ya kuwa na wasiwasi na huu usaili?

Na je ni vipi nitajibu swali la kwanini naitaka tena hiyo nafasi wakati mwanzo ilinifanya nikashuka cheo?

Natanguliza shukrani.
 
Back
Top Bottom