USAHIHI: UKAWA hawajagawana Majimbo

USAHIHI: UKAWA hawajagawana Majimbo

Lipi jina sahihi
sinema au senema?
Inaanza
:tape2:
 
Mmmh! ,ngoja waje wenyewe mi simo..
Haya , wenyewe tumeingia tayari , ni hivi , kishindo cha UKAWA na ile kashfa ya kupanga matokeo ya miss Tanzania imemtikisa Abbas Mtemvu na ccm Temeke kiasi cha kushindwa kujielewa ! ukijumlisha na ile kashfa ya kusafirisha dada zetu kwenda uarabuni kufua nepi ndio imekuwa balaa zaidi ! wameamua kutengeneza mkakati dhaifu wa kugombanisha UKAWA .
 
Kwa mbali namuona Mwenyekiti mpya wa kurasini Mivinjeni na diwani wa kurasini anayesubiri kuapishwa ndugu Matiti Toghocho .
 
Baada ya zitto kutimliwa Chama Cha Mafisi kinajifariji kwamba karata yao ya kuisambaratisha chadema wameihamishia kwenye ukawa.

Waliosoma propaganda yugoslavia, poland, cuba n.k wamepata practical work. Mtasikia kila aina ya maneno lakini nyinyi liaminini neno moja tu.

OCTOBER CCM HAWANA PA KUTOKEA.
 
Leo kumezuka taarifa katika magazeti kuwa UKAWA wamegawana majimbo 211 na bado majumbo 18,

Taarifa hiyo sio ya kweli, ni taarifa yenye lengo la kupotosha umma na kudhalilisha umoja wetu wenye nia ya kumkomboa Mtanzania dhidi ya serikali hii dharimu.

Maadhimio ya wakuu wa Ukawa mwezi jana yalikuwa ni ya pamoja, ambayo ni Vyama vyote vitapendekeze/vitateua wagombea wao wa Urais ambapo CUF itampendekeza mgombea wake, CHADEMA itampendekeza mgombea wake, NLD itampendekeza mgombea wake na NCCR MAGEUZI itampendekeza mgombea wake pia,

Kisha wagombea wote watakutanishwa na kamati kuu/wajumbe wa mkutano mkuu wa vyama vyote kwapamoja watamchagua mgombea mmoja atakaye gombea kupitia UKAWA.

Vivyo hivyo kwenye ubunge, vyama vimeruhusu watia ni wao wajitokeze kuutangazia umma kuwania majimbo,

Hatua za kumpata mgombea wa jimbo kuputia UKAWA ni sawa na zilezile zinazotumika kumpata mgombea urais. Labda pale ambapo kuna ufuasi wa chama kimoja tu basi vyama vingine vitaunga mkono tu.

Sasa propaganda zinazoendelea zinatoka mtaa wa saba kwa majoka yenye makengeza, Makamanda kuweni makini msiyumbishwe na uzandiki huo wa ccm.

Wale mnaotia nia endeleeni kujitokeza katika majimbo kwakufuata miongozo ya vyama vyenu bila kusombwa na propaganda za ccm.
Zingatieni tu kwamba kuna mtu ccm kaweka mkakati wa kuwahonga 2/3 ya wajumbe wote ili wamchague mtu anayemtaka yeye, na uwezo wa kipesa kufanya hivyo anao. Zingatieni sana hilo.
 
La uhakika ni kuwa ma jimbo yamesha gawanywa, wewe sio msemaji wa ukawa, hata hapa kuna wachangiaji walio karibu na viongozi wa vyama vinavyo ungana katika ukawa na wametuhakikishia huo mgawanyo.liko tatizo kati ya NCCR na cdm kwenye ma jimbo yao. Ndugu Yerico habari zako haziaminiki tena ile tabia ya copy past imekuvunjia heshima. One can never trust a culprit

Katika uchaguzi mkuu ujao UKAWA watasomba viti mpaka watu watashangaa.Maana CCM kuliko kuhangaikia mambo yao wanaangalia UKAWA, katibu mkuu keshasema mbunge yeyote na ajipime akiona hatoshi asichukue fomu maana atafanya CCM ishindwe bila sababu ya msingi. Najaribu kuwaangalia wale wabunge walioko bungeni sasa hivi, nawahurumia, maana kuna kazi kweli kweli. Kwanza wapambane wao kwa wao, na mpambano huo ni mkali sana kisha atakayeshinda akapambane na UKAWA kazi kweli kweli, zaidi ya nusu ya zile sura zilizoko bungeni sasa hivi hazitarudi, kitaeleweka tu.
 
UKAWA kuweni makini na mgawanyiko, itakuwa rahisi MWEWE kuwaloa mkiingia katika migongano. SISIEMU wanachungulia tu hapo na kuchekelea!!!!!
 
Mwakyembe ashinde ubunge Temeke?mnaleta utani nyie.Hilo jimbo wawaachie CUF.
 
Back
Top Bottom