Tangu kuanzishwa mfumo wa vyama vingi Tz 1992 mkoa wa Kigoma umekuwa ni moja ya nguzo imara kabisa za siasa za upinzani,huku mkoa huu ukisifika kutoa wabunge na wanaharakati watetezi wa wanyonge wa maana.
Siasa za mkoa wa Kigoma mara nyingine zinachanganya,kwani wakzi wake mara zingine wamekuwa wafuasi wa mtu na si chama,unaweza shangaa kwamba wabunge wa upinzani 2010 maslani wabunge kupitia NCCR mageuzi walishinda huku chama chao kikiwa hakina wanachama wa kutosha,hakijaa enea jimbo zima na pia kikiwa hakina uongozi thabiti kulinganisha na vyama vingine kama CHADEMA na CCM,
Msingi wa maamuzi ya wananchi kuamua kuchagua wabunge wa upinzani kutoka NCCR ,ni makosa yaliyofanywa na vyama vya CDM na CCM katika kuteua wagombea ubunge wao,ilikuwa imezoeleka kwamba chama ngazi ya wilaya kuteua mgombea anaekubalika bt ngazi ya taifa kuleta jina tofauti,na hii ilitoa mwanya kwa chama kilichokuwa kimepotea kwenye siasa za mkoa wa Kigoma NCCR kushika hatamu,ikumbukwe NCCR ilikuwa imebakia Kasulu vijijini kwa Mama Buyogela,lakini kutokana na makosa ya kimkakati kwa vyama vyote vya CDM na CCM euther kutowapa fursa wagombea wanaokubalika,ama wagombea wenyewe kunulika kutoka CDM maslani na kujiunga na NCCR,ni ukweli ulio wazi,kwamba wabunge wote wa mkoa wa Kigoma ni zao la CDM kasoro Kasulu vijijini kwa mama Buyogela,unapomuongelea Serukamba,Kafulila,Machali na Mkosamali hawa wote ni zao la CDM walikimbia CDM kwa sababu mbalimbali,na ni uhakika walishinda nafasi zao kwakuwa walipambanishwa na wagombea dhaifu kutoka vyama vya CDM na CCM,na huku wengine wakichaguliwa na wananchi kwa kuwalaghai kwamba bado wapo CDM,
Mara tu baada ya uchaguzi mkuu 2010,viongozi wa CDM mkoa wa Kigoma walijipanga kuhakikisha wanashinda viti vingi vya udiwani na ubunge kwa maana waliamini ni makosa madogo ndo yaliwapoka usbindi 2010,wamekuwa wakikijenga chama katika hali ngumu hasa baada ya mwanasiasa aliyekuwa anajiona ana nguvu kubwa mkoani Kigoma na taifa ndugu Zitto Kabwe kukitelekeza chama na kuamua either kuhujumu ama kujijenga yeye binafsi,
Katika mda wote huo viongozi wa CDM na wanachama wake walikitumikia na kukijenga chama hata pale sakata la Zzk kutikisa mkoa wa Kigoma,walipambana hadharani dhidi ya propaganda za kijivu na nyeusi juu ya sakata la Zzk,walitoa elimu na wananchi wakawaelewa,na kukubari kukiunga mkono chama huku baadhi ya viongozi na wabunge wa NCCR kabla ya UKAWA wakilitumia sakata la Zzk kuihujumu CDM kwani waliungana na CCM kusambaza propaganda za ukabila,katika hili nina ushahidi,
Tuje kwenye UKAWA,ni jambo jema sana kwa wapinzani kuungana,kimekuwa kilio cha wapenda mabadiriko wengi huku wengine wakifunga na kuomba muungano huo udumu,na kamwe usivunjike,naamini kila chama ndani ya UKAWA kina maslahi na kingependa kiongoze bt kwa maslahi ya umma vyama vypte vitapoteza sehemu na kupata pengine,
Kwa sasa vyama vyote vya UKAWA vinajiandaa na uchaguzi mkuu,kila chama kikiwa tayari na watia nia wake wa ngazi mbalimbali,na huku vingozi na wanachama wa vyama hivyo wakitambua mchakato wa kumpata mgombea Ubunge/Udiwani ni kura ya maoni,binfsi leo nimeshitushwa sana na habari iliyotolewa na gazeti la mtanzani juu ya ugawanaji majimbo,hapa naomba niweke wazi,kwamba either hiyo habari iwe ya kweli ama propaganda,bt kimsingi ni ukosefu wa tafiti imara kuamini kwamba mkoa mzima wa Kigoma NCCR inawafuasi wengi na mizizi kuliko CDM,huo ni upofu,
Kwa jinsi mgawanyo wa majimbo ulivyokuwa umeelezewa na mtanzania naliona tatzo kubwa sana hapa ,na si kwa mkoa wa Kigoma pekee bali Tz nzima,
Maslani leo habari iliyotolewa na mtanzania imewakanganya sana wanaCDM hapa Kigoma na mikoa mingine,kwani wao waliamini na wanaamini kwamba kura ya maoni itakuwepo kuwapata wagombea,sasa kitendo cha kusema majimbo fulani wanaachiwa NCCR ama CUF bila kuangalia matokeo ya uchaguzi wa mitaa 2014 hilo ni kosa,maslani mkoani hapa,kwenye uchaguzi huo wa mitaa CDM ilishinda mitaa mingi kuliko chama chochote cha upinzani,CDM ilipata viti vingi maeneo yote yaliyokuwa na wabunge wa NCCR na pale walipoachiwa NCCR kama makubaliano ya UKAWA,NCCR walipoteza vibaya, sasa hizo takwimu kwamba mkoa mzima wa Kigoma ni NCCR sijajua hiyo kamati ya UKAWA imetumia vigezo gani na imepita majimbo gani,binafsi hapa jimboni sijaiona,
Kama mtazamo wa CDM taifa ndo huo,hakika watakuwa wametukosea sana wanaKigoma,kusema kati ya majimbo 8 mkoa mzima kwamba CDM ibakie na mawili tu,tena yapo ambapo ndipo kuna chimbuko la siasa za udini,ukanda na ukabila,huu ndo ulikiwa wakati mwafaka wa CDM kupambana na CCM na matawi yake hapa Kigoma,hususani tawi la CCM kupitia ACT-Kigoma.
Kamwe siamini katika utaratibu wa vyama kuachiwa majimbo kwa hoja nyepesi kwamba kutazama matokeo ya mwaka 2010 na wabunge waliopo,vpi kama mbunge aliopo hakubariki na wananchi hawamtaki ?ataachwa tu kwa kuwa yeye ni mbunge?solution hapa ni kura za maoni ,kuzingatia matokeo ya local government na wingi wa wanachama eneo husika.
Kwa wabunge waliopo sasa wa NCCR hapa Kg ni ngumu kushinda hata kama kuna UKAWA,kwa hili napendekeza tume ipite kila jimbo na ichukue maoni ya wananchi wasio na vyama,
CDM kama itaamua kuwaachia NCCR majimbo yote 6 ya mkoa wa Kigoma ni wazi kwamba wanakwenda kuifuta CDM mkoani hapa,kwani kutakuwa na vyama vya ACT ambayo inawekeza sana Kigoma,na NCCR ambao watakuwa wamzrahisishiwa kazi ya kujiimarisha,japo ni kazi iliyowashinda kwa kwa miaka 5 iliyopita that y wamepata viti vichache wakati wana wabunge na rasilimali fedha,kwani hakuna jimbo lolote hapa mkoani NCCR imepata viti zaidi ya 6.
Natambua malengo bora ya UKAWA ni kushika dora ambapo naamini fursa aitapatikana mbali na ubunge,bt kabla hawajagawana na kusema wabunge waliopo waachiwe ,inabidi wafanye tafti za kutosha ,na hii ni kwa wabunge wa vyama vyote,kwani wapo wabunge wengi wa sasa wa UKAWA hawakubariki majimboni mwao.
Kwa hapa Kigoma majimbo ambayo CDM anauhakika wa kushinda kwa urahisi bila msuri mkubwa ni majimbo ya Buyungu la Christofa Chiza,Muhambwe,Kasulu mjini,Manyovu -Buhigwe na Kigoma kaskazini.majimbo haya kabla hawajaamua kuwaachia chama flani waje kwenye majimbo husika na wafanye tafiti nyingine.
Nimalizie kwa kusema,mimi ni.mwanaCDM damu na mwenye kuutakia mema UKAWA,bt kama viongozi wetu hawatakuwa makini katika kuamua,hakika wataua baadhi ya vyama vyao(uponzani)maslani nchi nzima CDM kila jimbo ilikuwa na watia nia zaidi ya 5,ambao kwa mda mrefu wamekitumikia chama kwa uaminifu mkubwa,wametumia mda wao na gharama zao wakoamini watapewa fursa ya kugombea kupitia CDM,leo uwaambia waachieni vyama fulani vya UKAWA ambavyo mda wote havijajijenga,vyama ambavyo ili vishinde vinahtaji sapoti na huruma za wanaCDM,hakika wale wasiokuwa na moyo wa chuma,wenye kupenda chama kwa dhati na si madaraka,watakihama chama chetu,wengi watakimbilia kwenye vyama vitakavuowapa fursa ya kutimiza ndoto zao za kuwa wabunge na madiwani,
Naomba viongozi wangu walione hili na watapumbua kwa kutaka kuwaachia mkoa mzima NCCRA ni CDM kujifuta huku inajiona, na wakumbuke huku tunapambana na maadui wengi na tunakabiliana na CCM na matawi yake,chama kiwaambie watia nia watanufaikaje?coz ngazi ya urais tumeona mgawanyo mzuri,kwamba rais akitoka chama flani basi makamu na waziri flani atatoka chama kingine,vpi huku chini?tuongeze umakini ili CCM wasipige risasi moja na kuuwa upinzani coz tumeunganishana.,nachukulia habari ya jana ya gazeti la mtanzania ilikuwa ni mzaha uliolenga kuuza,the big the name,the big story,
(Kamwe siwezi kuwa adui kwa kusema ukweli)