USAHIHI: UKAWA hawajagawana Majimbo

USAHIHI: UKAWA hawajagawana Majimbo

Tumezigundua ila zao kutwa kupost utumbo,hizi tunaziita akili za matakoni ukijamba tu zinapungua,,ukawa bado hawajapata mgombea yeyote wa kila nyanja ila vyama ndo watangaza nia wameanza na bado hawajapitishwa na vyama vyao kwa utaratibu walizojiwekea
 
uclazimishe wewe jisemee peke yako inatosha..
Subirini kichapo chenu october

Unapofika wakati kama huu, huwa mna kauli kuu mbili.
1)-Subiri kichapo october
2)-(october ikipita), Tumeibiwa Kura.

Halafu na Nchi inasonga kama kawaida. So,kelele za chura...........
 
Sasa huu uzi waliuleta hapa wa nini?


Ajabu, by the wy huyo nyerere fake ni sisimizi tu ndani ya chama
wakati zitto anakikuza chama yeye alikuwa kijijini analima viazi, hata mjini hajui kunafananaje!
 
Magazeti siku hizi yamekuwa ya kimangumashi kuelekea uchaguzi, sijui kudanganya ni kwa faida ya nani?
 
Mkuu sijaelewa vyema. Kwamba wajumbe wa mkutano mkuu wa CUF, wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CDM, wajumbe wa mkutano mkuu wa NCCR na wajumbe wa mkutano mkuu wa NLD watakutana pamoja kumchagua mgombea Urais wa UKAWA. Idadi yao kwa kila chama inalingana kweli? Kwa sababu naona wale ambao watakuwa na wajumbe wengi wa mkutano mkuu wataweza kumpitisha mgombea toka chama chao. Hii mtaifanyaje ili iwe na uwakilishi sawa kwenye huo mkutano mkuu wa mikutano mikuu ya vyama?

Utaratibu utawekwa ili kukidhi uwiano ikiwa kutakuwa na mapungufu hayo,
 
Kuna tetezi zinaenea kwenye mitandao kuwa
majimbo fulani yamepewa chama hiki na majimbo
fulani yamegawiwa kwa chama kile n.k. Taarifa
nilizozipata hivi punde kutoka chanzo sahihi ni
kwamba kazi ya vikao vya UKAWA ya kufanya
tathmini juu ya vigezo na ugawaji wa majimbo
inaendelea na watatoa taarifa rasmi kazi yote
ikishakamilika.


Ni muhimu wanachama wa vyama vya UKAWA
wakawa watulivu na kusubiri maelekezo ya
mwisho ya viongozi juu ya namna ya kuachiana
majimbo au kushindanisha wagombea wa vyama
vyote kuliko kuendelea kujenga hoja juu ya
taarifa za 'kusadikika'.


Na ni vema wagombea watarajiwa wakawa tayari
kwa lolote, kwamba ungependa kwenda jimbo
fulani au ulijipanga jimbo fulani lakini sasa
jimbo hilo limekwenda kwa chama kingine.
Tujiandae kwa yote mawili na tusijiwekee
uhakika kuwa chama changu lazima kipewe jimbo
fulani au mimi lazima niwe mgombea wa jimbo
fulani.

Waachieni viongozi wamalize kazi yao na kisha
wanachama wa vyama vyetu waamue nani
atawawakilisha kwenye uchaguzi mkuu.
Haya ni maoni binafsi tu.

.........
kilaza
 
Leo kumezuka taarifa katika magazeti kuwa UKAWA wamegawana majimbo 211 na bado majumbo 18,

Taarifa hiyo sio ya kweli, ni taarifa yenye lengo la kupotosha umma na kudhalilisha umoja wetu wenye nia ya kumkomboa Mtanzania dhidi ya serikali hii dharimu.

Maadhimio ya wakuu wa Ukawa mwezi jana yalikuwa ni ya pamoja, ambayo ni Vyama vyote vitapendekeze/vitateua wagombea wao wa Urais ambapo CUF itampendekeza mgombea wake, CHADEMA itampendekeza mgombea wake, NLD itampendekeza mgombea wake na NCCR MAGEUZI itampendekeza mgombea wake pia,

Kisha wagombea wote watakutanishwa na kamati kuu/wajumbe wa mkutano mkuu wa vyama vyote kwapamoja watamchagua mgombea mmoja atakaye gombea kupitia UKAWA.

Vivyo hivyo kwenye ubunge, vyama vimeruhusu watia ni wao wajitokeze kuutangazia umma kuwania majimbo,

Hatua za kumpata mgombea wa jimbo kuputia UKAWA ni sawa nau zilezile zinazotumika kumpata mgombea urais. Labda pale ambapo kuna ufuasi wa chama kimoja tu basi vyama vingine vitaunga mkono tu.

Sasa propaganda zinazoendelea zinatoka mtaa wa saba kwa majoka yenye makengeza, Makamanda kuweni makini msiyumbishwe na uzandiki huo wa ccm.

Wale mnaotia nia endeleeni kujitokeza katika majimbo kwakufuata miongozo ya vyama vyenu bila kusombwa na propaganda za ccm.

dharimu=dhalimu
 
Utaratibu utawekwa ili kukidhi uwiano ikiwa kutakuwa na mapungufu hayo,
Mkuu najua hii ni hatua ngumu sana na kwa uzoefu wangu kwenye hatua hii ndio umoja wa upinzani huwa unaparaganyika. Wanachama wa vyama wanafahamu kwamba ukipata ubunge chama chako kinajulikana na kuimarika pia kuna ruzuku. Hivyo hii ni hatua ngumu sana na ushahidi upo kwamba huko nyuma hatua hii imesababisha kuvunjika kwa umoja. Hata hapa nimeanza kuona watu wanasema wamejijenga na kukijenga chama hivyo haiwezekani watu wengine watumie UKAWA kujineemesha kwa jasho la wengine. Mwanzo wa ngoma ni lele, na hapa kuna lele.
 
Mkuu najua hii ni hatua ngumu sana na kwa uzoefu wangu kwenye hatua hii ndio umoja wa upinzani huwa unaparaganyika. Wanachama wa vyama wanafahamu kwamba ukipata ubunge chama chako kinajulikana na kuimarika pia kuna ruzuku. Hivyo hii ni hatua ngumu sana na ushahidi upo kwamba huko nyuma hatua hii imesababisha kuvunjika kwa umoja. Hata hapa nimeanza kuona watu wanasema wamejijenga na kukijenga chama hivyo haiwezekani watu wengine watumie UKAWA kujineemesha kwa jasho la wengine. Mwanzo wa ngoma ni lele, na hapa kuna lele.

Tusiishi kwa tabiri za akina Shekhe Yahya, Kamati ya ukawa inaendelea na kazi yake
 
mwakyembe.JPG

CHADEMA Temeke leo wakanusha propaganda za kuwa jimbo la Temeke wapewa CUF akizungumza mwenyekiti wa CHADEMA Temeke, mh. Benard mwakyembe kwa niaba ya kamati tendaji ya jimbo amesema jimbo aligawiwi kama pipi kwani tunaamini viongozi wa UKAWA watashusha muongozo ambao kila chama kitatoa mgombea na baada ya hapo kutakuwa na kura ya maoni ya pamoja na kuchagua mgombea mwenye sifa anayekubalika na pande zote na sio kama ilivyoandikwa na wahuni wa Mtazania na Mwananchi leo.

CHADEMA Temeke ni tishio kubwa kwa CCM kwani watangazania wa ubunge na udiwani wote wananguvu kubwa hivyo CCM ina hofu ya kupoteza jimbo na hasa Mwakyembe anamsumbua sana Mtevu ndio maana zinatengenezwa propaganda juu ya Temeke kupewa CUF.
 
Back
Top Bottom