US Election Coverage 2008


Hebu soma hapa then think again before you dismiss the race factor in American politics.Kwa vile sijui uko wapi,siwezi kukulaumu kwa kuwashangaa wanaodhani race inamkwaza Obama.Any sensitive Black person in the West anaweza kubaini kwamba racism ipo (kwa vile racists wapo) na itaendelea kuwepo.Kwanini Obama halalamiki kuhusu hilo?Well,ili ku-win hearts&minds of middle-of-the-road Whites,he must avoid ishu ya race.Mind you,Blacks ni percentage ndogo tu ya wapiga kura...

Nakubaliana nawe kwamba suala sio kulalamika tu,inabidi ku-confront...je wewe ungekuwa mgombea mweusi katika sehemu ambayo ni predominantly White how would have confronted racist voters?
 


That is the thing; sisi tunaofanya kazi na haya majamaa tunajua inapokuja swala la white vs black, hawawezi kuishinda ile wanasaikolojia wanaita cognitive dissonance: wanachosema na wanachofanya ni tofauti kabisa. Wanasema watampigia Obama lakini inapokuja kwenye kutenda wanampigia Hillary. Hope Koba atasoma hiyo article. Pia anaweza kusoma kidogo theory ya cognitive dissonance aone jinsi inavyofanya kazi US na nchi zingine za wazungu kwenye mambo ya racism.

Ndo nasema tena miaka 16 sio mingi ambapo hawa wazungu wanaojifanya leo hawana ubaguzi wa rangi waliwa-support wenzao wa south africa kuwakandamiza akina Mandela kwa sababu ya ngozi zao. Tena tunasahau mapema kabisa kwamba juzi tu hapa Ian Smith alitamka mbele ya kadamnasi kuwa hatarajii katika uhai wake kwamba mwafrika anaweza kujitawala (soma kutawala)! Kujua kahistoria kidogo inasaidia sana kuyaona haya majambo. Hawa jamaa usipokuwa makini watacheka ukifikiri mnacheka pamoja kumbe wanakucheka!

Najua Obama analijua hili vizuri sana ndio maana ameweza kuli-handle vizuri so far. Lakini subiri ashindwe (Mungu apishe mbali) ndipo umsikie kama hataweka sababu ya racism kama one of the reasons.
 
well,hapa tutabishana mpaka yesu arudi lakini kitu kimoja tunakubaliana racism ipo na Obama hatakiwi kuplay race card maana akianza tuu ujue uchaguzi umekwissha hata kabla vote moja haijapigwa,Kitila ubaguzi upo sana tuu lakini sio kama ule wa miaka ya nyuma,kidogo mambo yanabadilika(naongelea America) maana atleast unaweza uka confront racism legally sio maneno tuu au makelele na sehemu nyingi ina work vizuri tuu,ubaguzi unapungua sio kwa sababu ya morals & sympathy za watu,ni laws zilizopo ndio zinasaidia kuondoa ubaguzi
 

Sasa kama ubaguzi haupo kwa nini ktk seneti ya na majimbo ya Marekani kuna seneta na gavana mmoja tu mweusi? Hivi unadhani kunakuwaga hakuna weusi wenye sifa wanaogombeaga?
 
Sasa kama ubaguzi haupo kwa nini ktk seneti ya na majimbo ya Marekani kuna seneta na gavana mmoja tu mweusi? Hivi unadhani kunakuwaga hakuna weusi wenye sifa wanaogombeaga?

...nani kasema ubaguzi haupo? ndio yale yale ukiona mzungu tuu all you see is racism,na hayo mambo ya numbers of senators/governors unataka kusema ni ubaguzi au vipi? wewe kiboko naona unataka affirmative action kwenye senate.
 
Honestly what I see katika mama na Obama, nadhani Obama kwa kweli yuko ahead ya mama kabisa hata anavyoarticulate issues (though these arent the qualities rank and file voters care about!). Infact kama kweli conventional wisdom ikifanya kazi vizuri kwamba Obama akiwa nominee wa Dems blue states zote zitampa kura, then the way it seems here, huyu bwana can win independents than HRC or any other dem and this will assure dems another 4 years in WH.

But this can only work, if and only if, Conventional wisdom works well kwamba Dems WOTE wawe solidly behind him na aweze kuattract independent voters wengi (na hizi huge rallies zinazomsikiliza kila siku-ziwe translated into votes)! Though sadly, siku hizi siasa hazitabiliki kama ambavyo bado nashangaa kuona mama kashinda juzi NH!

Kama Koba alivyosema, ubaguzi upo, lakini ukiufikiria sana, huwezi kufanya kitu cha maana! Na Obama ameweza kuprove hilo kwa kuingia kwenye ligi hii ya urais! Hivi mnafikiri, tukiendelea na hizi stereo type which is a truth sometimes, what can we Africans ever do? maana whites have conquered us in every aspect. So we have to be more pragmatic to dream the impossibles. Hivi jamani ni njia gani ya kuelekea kwenye mafanikio ya kweli ambayo haina milima na mabonde??

I dont trust American press, the same press which had coronated HRC as the inevitable President is the same which is hounding her now! So Obama awe very careful, honeymoon na hawa jamaa ikiisha ndo hao hao watakaomuona ni villain! Na usishangae mama akishinda Nevada au SC... jamaa wakamgeuka Obama kama walikuwa hawamjui vile.

Na what I think Obama akipata nomination kwanza inabidi awe very smart ku-unite Democratic party KABLA YA UCHAGUZI between the young turks and the old guard! Kwa sababu naona this is a very big problem kwenye hiki chama. Na kama ukiangalia vizuri Wengi wanaomsupport Obama ni watu ambao naturally wanamchukia Clinton NA KIFUPI HAWATAKI TENA THIS DYNASTY. But as we may all agree hawa wazee wa chama waga hawaondoki kirahisi hivi kwa dissilusionment za vijana wanaotaka mabadiliko na wao wapate nafasi ya kula- ndiyo, kula! hawa wazee ambao almost wote wako in late fiftees na early sixtees wana deep roots kwenye organization ya Chama. Kifupi Clinton na jamaa zake ni establishemnt iliyokamilika. Obama akipata nomination inabidi achukue running mate from Old Guard na asifanye kosa la kumualianate Bill Clinton na old guards wengine. Awatumie vizuri sana. (leo polls zinasema the man has 83% of dems voters viewing him favourably! Should he do otherwise, it will be political suicide. I guess.

But kweli kabisa much as this guy is not "white enough", I hope he can heal the scar of racial injustice in the history OF USA.

Again, I must complement HRC kwa political fight ambayo ameidisplay mpaka leo! I can argue with surelty kwamba mama knows what she is doing! Iam sure every intelligent woman somewhere must be smiling for her audacity to challenge that high office. Ni wachache wanaoweza kuwa scrutinized like her na bado wakashinda! as she has done so far!

But the fight is still on! Yaani

Those are my wishes which may not necessarily be politically correct. But that is the way I see it.

Better try and fail, but never fail to try!
 
Happening now............John Kerry juniour senator from MA, endorses Obama.!!! its a very huge endorsement indeed!.
 
YourNameisMine,

..John Edwards alikuwa runningmate wa John Kerry.

..Since Kerry is from Mass he would have been more helpful if he had endorsed Obama before NH caucas.

..This is HUGE for Obama, and a big snub to Edwards campaign.

..Watch how it is going to be spinned against Hillary Clinton.

..I am very curious who Al Gore is going to endorse.
 
ubaguzi unapungua sio kwa sababu ya morals & sympathy za watu,ni laws zilizopo ndio zinasaidia kuondoa ubaguzi

true indeed; tatizo ni kwamba wanapoenda kupiga kura kinachowaongoza hapo tena sio sheria bali mioyo yao ambayo haifungwi na sheria yeyote. Yaani hapa tunaongea mambo mawili tofauti: wewe unasema ubaguzi hakuna kwa sababu ya sheria-well and good, hiyo tunaita extrinsically influenced not to be racist because of fear for being punished, but the problem is, it is overt behaviours that are punishable. You cannot punish covert behaviours-and unforunately it is these that are more relevant when it comes to voting!
 

Well said Kitila! No one could have said it better. And sadly, you can't punish anyone for voting or not voting for a person based on their race. Even more unfortunate (or fortunate) you can't legislate people's feelings....
 


Al gore na vingunge wengine wa dems are very smart mkuu! lazima wabaki juu ya hizi fray kusudi waangalie who is a likely winner. Kila mtu anapenda kuji-associate na ushindi. Kama Obama akiendeleza hii momentum mpaka Feb 5 Iam sure the powers that be will shower him endorsement. Kwa sasa it is too soon for them maana mama hatabiliki kabisa and they are intelligent enough to know that. Sio wote wanaompenda mama, lakini mkuu, kumbuka siasa ni kulipa fadhila! Kama mtanzania unalijua hili.

Harafu waungwana mi mnisaidie, what is wrong with American press? yaani ilivyomgeuka HRC mpaka naona kama cinema. Do you think the turn of Obama will come? Iam afraid iko siku wanaomsifia leo watamfanyia kitu mbaya. But what Iam sure of ni kwamba kama Obama akiface barrage za mama anazokutana nazo, sidhani kama ata survive. Press ya US ina influence kubwa sana katika kushape mawazo ya watu.
 

One can't trust the American press. Obama is getting a pass at this moment but I have a sneaky suspicion something is cooking somewhere. It's just a matter of time...Halafu endorsement hazimaanishi lolote na hazimletei mtu kura.
 
Mzee Joka,
Al Gore atachelewa kidogo kujimwaga ukumbini, lakini wakti ukifika atamwi-endorse Obama!!! Gore na Clintons wana bonge la beef......the clintons, are terrible human beings if and only if you studied 'em closely.

Lose ya Obama in NH ina mambo mengi sana, including kujilizaliza kwa bibie, some pple became anti-media na kuamua kuwa-defiance. Kuna wanaosema kisogezwa(takriban wk 3 mbele) ya uchaguzi kumefanya Obama kushindwa. This is true because, UNH in Durham and other colleges kama vile in Exeter zilikuwa bado zimefungwa na wanafunzi/professors wapo out of town, mind you kwamba hizi ndio zilikuwa strongholds za Obama na potential voters kama 8000!!!!.............so mapambano bado yanaendelea. Argument ya ubaguzi ni weak kinomanoma yaani, kwani in NH population ya minorities ni less than 3 per ilihali wengi ni immigrants wa kisomali na sudan ambao si voters. Now hizo asilimia 36 za kura Obama kazipata wapi???
 

Hoja ya race unaweza kuiona haina nguvu sasa hivi kwa sababu mambo bado hayaja-"cottonfire". Subirini basi apate hiyo nomination...hamtauona ubaguzi waziwazi kwani unawafanya wazungu waonekane wabaya. Utakuwepo siku ya kupiga kura kumchagua rais wa taifa kubwa na lenye nguvu kuliko yote duniani. Hapo ndio itakuwa ni sawa na kufa na kupona.
 
Ngabu,
Ubaguzi upo, lakini ni muhimu sana kuwa positive na ku-ignore hiyo fact. Mie naamini wakisubiri mpaka apate nomination itakuwa too late..........wazungu wengi hasa wasomi wanaona hii ni opportunity ya ku-turn page to a new chapter in racial relations na mambo mengine in America. Plus Obama si Jesse au Sharpton, is a man of great talents na wewe mwenyewe (ngabu) unajua kwamba wazungu, regardless huwa wana-appreciate kama kweli unajua/kuweza jambo!!.
 

Hivi unaamini kwamba mtu akiwa msomi ndio anakuwa less-mbaguzi? Mimi nadhani anabadilisha tu mbinu zake lakini hisia za kujiona yeye ni bora zaidi zinabaki na kuna vitu hawako tayari kuvi-concede na mojawapo ni uraisi wa Marekani. Sasa sisemi kwamba wazungu wote ni wabaguzi lakini ninachosema ni kwamba, watu unaocheka nao kila siku, wanaokualika nyumbani kwao n.k hao ndio wabaya zaidi kwa sababu hujui haswa kilicho moyoni mwao. Ni bora nijue unasimama wapi ili nijue jinsi ya kudili na wewe. Mimi nawashemu sana KKK na wengineo kama wao kwa sababu ni wakweli. Sitakatiza anga zao na wao hopefully hawatakatiza anga zangu na tutakuwa pouwa tu.

Sasa msinielewe vibaya hapa. Mimi napenda sana kumwona Obama anafanikiwa ktk kampeni yake hii lakini kwa wakati huo huo sitapuuzia vizingiti alivyonavyo. Pamoja na hivyo vizingiti haina maana kwamba watu wasijaribu na kuthubutu. Bila hivyo kusingekuwa na maendeleo yeyote hapa duniani
 
..kama ilivyokuwa kwa dr.martin luther king,obama anaibadili marekani taratibu,hata kama hatapata nomination.

..the guy is showing fellow americans how to live the "american dream".
 
Mzee Joka,
Al Gore atachelewa kidogo kujimwaga ukumbini, lakini wakti ukifika atamwi-endorse Obama!!! Gore na Clintons wana bonge la beef......the clintons, are terrible human beings if and only if you studied 'em closely.

Ama kweli siasa ni unafiki wa hali yajuu! All of the sudden Bill Clinton aliyekuwa anaonekana Masiha leo amekuwa inhuman na all kinds a demon can be? You guys kweli siasa waachieni akina Kingunge na Makamba wacheze, maana at times na elimu yangu nashindwa kuelewa what is politics...This is the man viewed favourably by 83% wapiga kura wa democrat! Guys Clinton EARNED his political capital by working for it, it was not awarderd to him on silver plate! so you think it will dissapear overnight? and why not if he can use it to help his partner? wouldnt you? I would ofcourse!


As far as I know Clintons family wameingia madarakani kwa kura za halali (sio kama Kibaki), iweje leo waonekane inhumans? au walio/wanaowapigia kura nao ni wajinga kama sisi na CCM? Nadhani siasa ni ngumu! I salute the likes of Zitto na Slaa.

Hivi kweli wewe leo mke wako akiwa anagombea uongozi si utafanya uwezalo kumsaidia? nani kati yetu hapa ataacha kumsaidia mke wake/au atamwambia aache kwa sabau watu watasema mbovu?? Sasa whats wrong with Bill helping his wife? I guess Bill is fulfilling his spousal obligations-just like any other responsible partner. what happened to that famous phrase uttered in Church?..for better or worse? Lets get real! Hata mke wa Obama/Edwards angekuwa na uwezo Iam sure angetumia role yake kumsaidia mume wake. Just as Oprah did!

Iam not a fun of mama Clinton, lakini mi naona we are extremely being unafair kwa ajili tuu ya ushabiki wetu! Clinton mke wake survived barrage of criticim to win NY senate, against all odds, she defied pundits... yaani kinachotokea hapa between these two people ni opportunity ilijitokeza, kwani walioana wakiwa na ambitions za kuwa maraisi? au mwanamke ni kiazi kwamba hajui kitu? Bill might be a charismatic leader, but I guess her wife is fighting her own battle and should be treated as such.

Na maisha ni plan, as long these folks Bill and his wife knew what they wanted in their lives, it remains their mission to accomplish it and as such kama wapiga kura wakimkataa that will be the end! But kuwa na malengo sio kitu kibaya, she is fulfilling her dreams just as Obama is doing, just as you and me are doing (if you are).
 
...Ngabu kwa kweli mambo ya kukaa chini na kuanza cry baby ya race ni kujirudisha nyuma sana,na vipi kama kina Dr king wangekubali separate but equal,leo wewe ungekuwa unaozea ghetto,hata slavery kuna waliamini haitaisha lakini sasa slavery ukiongelea unaonekana kichaa tuu na hao KKK wanaonekana wendawazimu tuu hata kwa wazungu wenzao,sijui unakaa wapi wewe lakini najua lots of blacks living in affluent neighborhoods na heshima mbele kama kawaida na hii ni kutokana wamekataa stereo type ya black belongs to the ghetto,siku hizi hata Wall street blacks CEOs wapo kwenye forbes500 na kumbuka historically Wall street ilikuwa ni exclusive club ya whitemen,sasa unafikiri jamaa wangebaki wanalia lia ingekuwaje...tunaenda mbele haturudi nyuma ngabu na Obama anandelea akishindwa poa tuu lakini sio kukaa nje na kusema no way for a black president.
 
Mzee Joka,
the clintons, are terrible human beings if and only if you studied 'em closely.

uhuuu, usije ukawa unaimba nyimbo za wengine; in so far as Africa is concerned, huyu ndiye Rais wa US ambaye ameingia kwenye record kwamba alikuwa genuinely concerned na shida za bara hili na kujaribu kusaidia kutatua. na hadi leo ameendelea kutumia nguvu nyingi tu za akili na mwili wake kwa ajili ya maendeleo ya watu wa Afrika.

Sio lazima uwakandie akina Clinton ili uonekane unampenda Obama.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…