Urusi imeuvunja moyo wangu

mkuu unapo sema mauzo T 100 zote Mrusi katia mfukoni kwahiyo hakuna garama za uendeshaji ?halafu ikiwa tutaamini kila kitu kinacho zungumzwa na vyombo vya habari vya magharibi kuwa zote ni propaganda basi Mrus angerikuwa amesha kamilisha lengo na kumaliza vita sasa unapo ona muda unazikwenda na Putin bado hajatimiza lengo anaendelea na vita maana yake yanayo ongelewa si yote ni propaganda na unapo sema Putin alisha piga hesabu na alisha fanya uchunguzi kwenye uchunguzi kuna wakati unaweza kuwa umechunguza vibaya na mahesabu umepiga vibaya ndio kushindwa kunakuja hapo tambua wakati Putin anafanya uchunguzi na mahesabu yake na wenzie nao walikuwa wakiendesha uchunguzi na mahesabu vile vile kwahiyo atakae shindwa vita ndie alie fanya uchunguzi vibaya kwa mtazamo wangu bila kuegemea upande Putin amechemka kias flani na nahis alifikir itakuwa rahis kama alivyo ichukua Cremia na ni bora amalize vita mapema kuliko ikafika wakati mashambulizi na mapigano yakaanza kufanyikia na ndani ya Urus
 
NATO itashindwa vibaya mno hasara wanazoingia siyo za kitoto muda utaongea, Ukraine imeshashindwa, will never be the same again...yule comedian kaingizwa chaka
 
Wewe usifikiri upuuzi unaofanywa nchini kwako ndo unaofanywa na urusi.

Urusi haina sera ya kipuuzi ya ubinafisishaji kama nchi yako, Rasilimali zote zipo under full control of government hayo makampuni unayosemea niya serikali ya urusi nasiyo ya Mtu.
aya mkuu , tumekuelewa
 
Umeandika pumba Sana Kwa sababu Mrusi akachukua Maeneo mengi ya Ukraine sasa hivi Ukraine Hana Bahari.umendika kinafki Kwa taarifa yako maeneo yaliyochukuliwa na warusi hayatarudi tena.urusi anapigana na NATO nzima na bado anaendelea kuchukua maeneo huko.

Utakua haufuatilii hivi vita, Mrusi anaendelea kuachia achia maeneo, anasogezwa balaa ya kufa mtu.
 
Russia umeuvunja Moyo wangu.

Utawala wa Western ambao unategemea uchumi wa kiunyonyaji chini ya kivuli cha demokrasia na ustaarabu wa kimangharibi.

Kumezifanya nchi nyingi kuwa tegemezi na sera za Magharibi na kuziacha nchi nyingi ambazo zinafuata mifumo yao wenyewe kuachwa solemba na kuwa na changamoto kubwa za kiuchumi.
Anguko la usoviet na nchi kama North Korea ni mifano.

Nilitegemea Urusi atakuwa ndio mkombozi wa kuitoa dunia katika wimbi hili la unyonyaji wa Magharibu kutokana na kwamba

1. Urusi imejijenga kiuchumi japo sio tishio huko duniani lakini uchumi wake ameuwekeza zaidi katika maswala ya kijeshi.

2. Kijeshi pia ipo vizuri huku akimkimbiza vizuri tu Mmarekani kwa ubunifu wa technologia za kibabe (kwa mujibu wa nilivyoamini mimi)

3. maswala ya intelijensia pia kwani majasusi wa russia ndio walio sambaza formula za kutengeneza Atomic bombs zikafika russia na nchi zingine pamoja na mafanikio lukuki

4. mengineyo Ongeza mwenyewe hapa na wewe kwa mujibu wa ulivyo aminishwa.

SASA URUSSI UMEUVUNJA SANA MOYO WANGU.

nitajikita tu katika uvamizi wa taifa la UKRAINE.

Urusi baada ya kuitwaa Krimea 2014 nilitegemea wangefanya ujasusi wa kutosha na kupiga gharama yakinifu kuliko kuingia kichwa kichwa na kupata athari zisizo tarajiwa ambazo ni mbaya

haikufanya intelijensia au ilifanya kwa uchache
matokeo yake sasa.

1. mageneral wake wengi wakafia vitani

2. vifaru vya kijeshi TANKS : zaidi ya 1500 kuangamizwa kabisa (irriperable)
ngaja nikupe hii thamani ya kifaru kimoja cha urusi aina ya T-90AM kinagharimu dola milion 4.27 sawa na bilion 9 tsh zaid ya vifaru 1500 kuangamizwa hio ni zaid ya dola 6000M zaid ya trilion 12 TSH.

3 Ndege za kivita Aircrafts 200
hapa tunaongelea ndege aina ya Sukhoi Su-35 flanker E ndege moja ya aina hii inagharimu dola milion 85 sawa na zaidi ya Tsh. 197+Bilion jumla ya hasara ya ndege hizi ni zaidi ya dola bilion 17 ( TSH 40+ trilion)

3 hasara ya Armoed vehicle 2500+ ,
troops 20000+ na helcopta Tusizipigie hesabu maana huko ni kuchoshana

4 hasara ya wanajesh zaid ya 23000+ pia tusipigie hesabu zao maana hata urusi hua haithamin sana vifo vya wanajeshi nafkiri historia ya vita wanavyo pigana urusi mnaijua hasa kwenye swala la kupoteza askari wengi tangu WW2. na mara nyingi rusia wanashinda vita kwa wingi wa Askari. tuachane na tathmin za vifo hivi kwanza nikiweka wengi mtasema ni propaganda. ila kwa faida tu ujue theluthi mbili ya jeshi la ardhini la russia lipo Ukraine na vita vinavyo endelea hakuna shabaha za kijeshi zinazo lengwa kwa sasa so ni mwendawazimu tu anayejua kua PUTIN atashinda hii vita.

5 gharama za uendeshaji wa vita mishahara ya wafanya kazi penshen za wanao kufa vitani kwa familia Nk nitazipiga kwenye uzi ujao baada ya kufanya utafiti wa kina

6 vikwazo na mali zikizokua freezed na zilizo taifishwa ni matrilion ya madolari

7 kupoteza ushawishi wa kikanda na soko la silaha na bidhaa zingine kwa washirika wake tu kama india ni ma matrilion ya madolari pia.

Russia umeyvunja sana moyo wangu
wao magharibi hawana vya kupoteza katika vita hivi maana hata vikwazo walivyo muwekea mrusi wanahakikisha ni vikwazo visivyo waathiri wao kwanza na wakipata mbadala wa gesi mbona naiona urusi ikiwa kama zimbabwe

kwanza hata Ardhi yaje imeanza kushambuliwa pia yan wauni wanijipigia hadi karibu na moscow halafu wanarudi. kesho tena

Ukraine imepoteza pia askari na miundombinu yenye thamani ya matrilion ya dola. lakini Mbwa kula mbuzi sio hadithi hadithi ni Mbuzi kula Mbwa.

Yani vikwazo vya urusi kwa magharibi vinatia Aibu vikwazo kama kumzuia Biden na Boris na maafisa wengine wa serikali kutembelea russia ndo nini sasa.

Nilijua kwa trend inavyo enda sasa Russia na china ndio watakua Super power ajae lakin sasa rusia kawa kama bata.

sasa Russia hana option zaid ya kuhakikisha anashinda hii vita na Nucklea ndio las hope kwa sasa
nasema bora atumie Nuclea angalau ataurudisha moyo wangu ulio jaa mahabbat juu ya urusi lakin kwa sasa dah umeyvunja sana miyo wangu

source
Normal Millitary critical analysis
Tulia vita sio harusi, Russia anapambana na nchi zaidi ya 30, au ulifikiri Ukraine ni Iraq alieachwa yatima ? yule ni mzungu kwahiyo wenzake wamekuja kumsaidia, US alikaa miaka 20 Afghstan na alikimbia kama kashikwa ugoni, sasa Taliban kashika nchi
 
Urusi imechukua

Crimea

Donbass

Luhansk

Black sea

Ule mji wa wa kibiashara.

Unasikitika nini !?

Unajua returns gani watapiga kwenye hayo maeneo

Na usikute hivyo vifaa ni outdated

We unadhani una full vita wenzako wanaitwa operesheni.

Huwezi juu itakuaje wakianzisha operesheni engine kuimega Ukraine

Acha na fake news za Western countries.

We huoni pesa kibao zinatumwa huko ukraine kuwasaidia wako broker wamepigika.

By me

Mrusi wa ntantilyabashashi.
 
Urusi imechukua

Crimea

Donbass

Luhansk

Black sea

Ule mji wa wa kibiashara.

Unasikitika nini !?

Unajua returns gani watapiga kwenye hayo maeneo

Na usikute hivyo vifaa ni outdated

We unadhani una full vita wenzako wanaitwa operesheni.

Huwezi juu itakuaje wakianzisha operesheni engine kuimega Ukraine

Acha na fake news za Western countries.

We huoni pesa kibao zinatumwa huko ukraine kuwasaidia wako broker wamepigika.

By me

Mrusi wa ntantilyabashashi.
Nme penda kichekesho chako, kwa kweli kina chekesha
 
Umeandika pumba Sana Kwa sababu Mrusi akachukua Maeneo mengi ya Ukraine sasa hivi Ukraine Hana Bahari.umendika kinafki Kwa taarifa yako maeneo yaliyochukuliwa na warusi hayatarudi tena.urusi anapigana na NATO nzima na bado anaendelea kuchukua maeneo huko.
Maeneo gani ametangaza rasmi kuyachukua boss?
 
Kama West washajua udhaifu ya warusi mbona hawaingii vitani Rasmi?kwanini wanaingia Kwa mgongo wa nyuma wanaogopa nini?
Hakuna nchi ya magharibi yenye akili itaingia vitani rasmi iharibu uchumi wake pasina sababu ya msingi wakati uwezo wa kumdhoofisha Russia upo kwa kumsaidia Ukraine zana za kivita tu kwisha habari yake.

Yaani NATO waingie rasmi vitani unadhani Putin atahimili hata kwa wiki moja tu?

Wazungu wa magharibi lengo lao ni kumpukitisha Russia ashuke zaidi kiuchumi ndo maana wana prolong vita hali ya kiwa Putin anawasihi magharibi wamshawishi Ukraine asitishe mapigano na magharibi hawataki vita isitishwe kwasasa.
 
Hakuna nchi ya magharibi yenye akili itaingia vitani rasmi iharibu uchumi wake pasina sababu ya msingi wakati uwezo wa kumdhoofisha Russia upo kwa kumsaidia Ukraine zana za kivita tu kwisha habari yake.

Yaani NATO waingie rasmi vitani unadhani Putin atahimili hata kwa wiki moja tu?

Wazungu wa magharibi lengo lao ni kumpukitisha Russia ashuke zaidi kiuchumi ndo maana wana prolong vita hali ya kiwa Putin anawasihi magharibi wamshawishi Ukraine asitishe mapigano na magharibi hawataki vita isitishwe kwasasa.

1000% true
 
Kitambo tukiwa wadogo shuleni kuna dogo alikua anapigana huku akilia lia, hadi unayepigana naye unaonekana kama wewe ndiye unamdhulumu, ila ikichunguzwa kwa makini dogo alikua anaumiza kishenzi.
Huyo dogo lazima atakuwa na vinasabu vingi vya kike
 
Urusi imechukua

Crimea

Donbass

Luhansk

Black sea

Ule mji wa wa kibiashara.

Unasikitika nini !?

Unajua returns gani watapiga kwenye hayo maeneo

Na usikute hivyo vifaa ni outdated

We unadhani una full vita wenzako wanaitwa operesheni.

Huwezi juu itakuaje wakianzisha operesheni engine kuimega Ukraine

Acha na fake news za Western countries.

We huoni pesa kibao zinatumwa huko ukraine kuwasaidia wako broker wamepigika.

By me

Mrusi wa ntantilyabashashi.
Sisi hatuteseki, uhakika ni kuwa hiyo miji itarudi ilipokuwa zamani na tutaondoa mamluki wote wa Urusi..
Kiufupi mmeipa Ukraine nguvu maana itawekeza kwenye ulinzi zaidi
 
Kitambo tukiwa wadogo shuleni kuna dogo alikua anapigana huku akilia lia, hadi unayepigana naye unaonekana kama wewe ndiye unamdhulumu, ila ikichunguzwa kwa makini dogo alikua anaumiza kishenzi.
Dogo alikuwa anashusha ndonga kilo 5 sio?
 
Daaah ilikua hivi

Wachinjaji walienda machinjioni kuchinja Ngombe walipo fika machinjioni wakawakuta Ngombe wameshika visu wanawasubiri wachinjaji. hadithi ya wachinjaji walio chinjwa na Ngombe .

sikia hii habari ya majuzi kabla ya askari 1000+ walio kufa wakivuka mto. jana

Source BBC: Copyright: Reuters) Urusi ilipoteza wanajeshi 26,350 tangu ilipoivamia Ukraine tarehe 24 Februari, Wizara ya Ulinzi ya Ukraine ilisema katika sasisho lake la hivi punde.
Ukraine inadai jumla ya hasara iliyopata Urusi ni pamoja na:
  • Vifaru 1,187
  • Magari 2,856 ya kivita
  • Mifumo 528 ya kivita
  • Mifumo 185 ya kurushia roketi
  • Mifumo minane ya ulinzi wa anga
  • Ndege 199
  • Helikopta 160
  • Ndege 290 zisizo na rubani
  • Makombora 94 ya meli
  • Meli 12 au boti
  • Magari 1,997 na malori
  • Vitengo 41 maalum vya vifaa
Na bado
Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lyod Austin,amesema kuwa Msaada wa kifurushi kipya ( halichachi bando) GB bilion 40 us dola utajumlisha Silaha za masafa Marefu zenye Uwezo wa Kushambulia Kilometa 220+.yaaani kifurushi kinauwezo wa Kupiga Crimea..

Ikumbukwe kuwa, Kwa zaidi ya miezi 2 Sasa, Wanajeshi zaidi ya 500 wa Ukraine walikuwa Nchini Poland na Romania wakipatiwa Mafunzo ya jinsi ya Kutumia Silaha za Marekani.

Tujiulize: Kidogo
Russia hana hypersonics? ( combora ambalo halisikii rada wala cha Air defence systms ) jibu Anazo
russia hana ndege imara? jibu anazo
je rusia hana air defenc system za kulinda misafara yake? jibu anazo za kushiba zingine anauza nje
je russia hana intelligent ya kutosha? anazo.

Upande wa pili.
je ukraine misaada aliyo pewa amepewa na hypersonic bombs? HAJAPEWA

Je, kapewa yale mandege makubwa ya new generation ya Nato k.v F35 jibu Hajapewa kwanza hajui hata kuyatumia.

ukiacha javeline. je ukraine anatumia silaha yoyote ambayo mrussia hana? jibu ni hapana
tena hata misaada anayopewa ukraine ni silaha ambazo magharibi wanazidump kuziondoa kwenye stock

je haya magwaride anayooneshaga mrussi hiki ndicho tunachokiona live?

Hakika nimekata Tamaa. Urusi imenivunja moyo wangu.

sikia hii
katika Ripoti ya this week,Jeshi la Ukraine limevikomboa vijiji 7 katika mji uliotekwa na Urusi wa Kherson tangu mwezi Machi. Pia Jeshi la Ukraine limedai kuwarudisha nyuma Wanajeshi wa Urusi kwenye mji wa Kharkiv.

na ukiskia Myukraine kakomboa hata kijiji kimoja ujue russia kachapika kweli

Putin mwezi march alikiri kupoteza askar 1,500. apo bado. na vita hadi leo vinaendelea yani kama vimeanza jana.

emb tufanye kama kupoteza askar 26+ ni propaganda bas tutumie akili zetu kuchambua.

1. wakati mheshimiwa putin. anapeleka wanajeshi ukraine mwez april mwezi march russia ilikiri kupoteza askari takriban 1500/

pro warusi wenzangu hawa askari buku jero walio kufa ni ile shughuli ya pale kivy. tu. na russia ilikiri kupata hasara so tuchambue kuanzia hapo tuachane na propaganda.
na historia inaonesha
ukiona mrusi karudi nyuma vitani ujue kweli kakutana kitu kizito na hao 1500+ inaweza kua zaidi. tufanye sio zaid ya hio idadi

2. tangu mheshimiwa putin apeleke jeshi ukraine hadi leo ni miez mingap. ni miez 3+. tufanye hio idadi imeongezeka hata x 1.5ya walio kufa tutumie kigezo cha kuendelea kwa vita na kushindwa kusonga mbele na majeshi ya russia kurudishwa nyuma pale karkhiv. toka kwenye maeneo walio kuwa wamesha yatekaga.

tutumie kigezo cha russia kuto kutoa data za maendeleo ya vita na hata data akitoa yeye kazi yake ku generalize tu.
hawi spesific.
itakua ngap so idadi ya chini ukicalkulate inaweza kufika askari 1000 at least so kusema had now wamekufa 26000+ ujue kuna kaukweli fulani.

SASA kuna wanao sema askar kufa vitani ni kawaida sana. oky fresh ni kawaida
lakini
mnakufaje askar 20000+ kufa vitani within 3 month ? daaah tena askar wa superpower nilie mtegemea.
mwenye zana za kutosha. apana kwa kweli

UKRAINE Ilikua sehem ya russia zaman so hakuna sehemu russia asipo pajua pale ukraine jumlisha na silaha za panasonic anazotutambia katika magwaride yake yan kashindwa kujua Mr. comedian yupo wapi amuagizie kombora moja tena sio la nyuklia bali la panasonik lile kubwa kubwa. amalize vita.
yani mnataka kuniambia putin hajui kwenye geographia ikulu ya Ukraine ipo wapi kweli?
kombora halina tiba wala kinga dhidi ya mifumo ya ulinzi na accuracy yake ni 98%.
jamani ee tuache unazi rusiia sio kama tulivyo mdhania.


siongelei waukraine walio kufa vitani wala sitaki kuchambua huko kwa sababu.

chukua mfano waukraine askari walio kufa lets say wamekufa askari laki tatu
hoja ni kuwa supapawa unapotezaje askari elfu 20000+ ????
unapotezaje majenerali?
unasema oparation tu halafu unatumia had moscova
oparation unatumia 1/3 ya askari wa ardhini wanao linda taifa la rusia wanaenda ukraine
operation unatumia hadi silaha zilizo kwenye akiba?
operesion unatumia ICBM? kombora la kuvuka mabara unalitumia dhidi ya jirani yako wachumba cha pili tu apo halaf unasema oparation. apana kwa kweli.

sipati jibu.

rusia imenivunja moyo.

hoja kusema ukraine anasaidiwa silaha sidhan kama ina mashiko

mfano
mtoto anapigwa na mtu mzima kwa kutumia fimbo na visu halafu watu wakamsaidia mtoto kumpa japo na yeye fimbo imsaidie asinyamaze kimya apigane. hio itakua ni big inshu jaman?
ukraine hakuwa anasaidiwa silaha nzito

sasa majuzi kati
Waziri wa Ulinzi wa Marekani Lyod Austin,amesema kuwa Msaada wa kifurushi kipya ( halichachi bando) GB bilion 40 us dola utajumlisha Silaha za masafa Marefu zenye Uwezo wa Kushambulia Kilometa 220+.yaaani kifurushi kinauwezo wa Kupiga Crimea..

pro Russia sote tuungane kuomba vita viishe Russia anatutia Aibu

technique kubwa ya Ukraine ukiwa unavamia mji fulani huwa dizain kama wanakuacha uingie na ili kukupoteza maboya wanakuonesha kaupinzani feki ili ujisifu na kujihakikishia
then wanajua kabisa sehemu mlipo pateka ndipo patakua kituo cha kujikisanya na kukusanya silaha nzito hapo sasa zile silaha zaid zinapokua njiani kwa sababu zinakuja kutoa backup na zina kuja kimsafara inakua rahisi kuziona kwenye satelite sababu ni nyingi apo zikishambuliwa askari walio teka mji wanashikwa na kihoro kisha nawao wanaanza kushambuliwa mbaya zaid mashambulizi ya ukraine ni vigumu kujua yanatokea wapi maana huwa hawajirundiki kama warussia
hii ina maana ili kuangamiza kikosi cha askari wa ukraine 1000 utahitaji makombora 1000
lakini ili kuangamiza kikosi cha askari 1000 wa russia utahitaji makombora mawili tu.
kitaalamu tunasema mbuzi kala Mbwa.

Mwisho

sijaongea kishabiki nimeamua kutoa tu hisia zangu zidi ya Taifa ambalo nililiamin ndio namba moja duniani interms of Military power Rusia

* ITAENDELEA*
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom