Messenger RNA
JF-Expert Member
- Jul 24, 2022
- 1,103
- 3,023
Jeshi la Ukraine linasema kuwa lilidungua ndege tatu za kivita za Urusi kusini mwa nchi hiyo siku ya Ijumaa.
Ndege tatu za kivita aina ya Su-34 zilidunguliwa katika eneo la Kherson, jeshi la wanahewa la Ukraine lilitangaza.
Rais Volodymr Zelensky aliwashukuru wanajeshi walioangusha ndege hizo, akisema tukio hilo lilifanyika katika Mkoa wa Kherson wenye vita.
Urusi haijatoa maoni yoyote kuhusu kupotea kwa ndege zake, lakini Fighterbomber, mwanablogu mashuhuri wa vita vya Urusi, aliripoti kupotea kwa idadi isiyojulikana ya ndege, akisema labda ziliangushwa na makombora ya Patriot yaliyotengenezwa na Amerika.
Wafanyakazi wote walionusurika na waliokufa walipatikana, mwanablogu aliongeza.
Ukraine inakabiliwa na uhaba wa risasi huku ikiendelea kupambana na majeshi ya Urusi, kufuatia uvamizi kamili wa Moscow mnamo Februari 2022.
Kyiv ilisitisha makabiliano ya kujibu mashambulizi mwanzoni mwa majira ya baridi, huku Marekani - ambayo ni mfadhili mkuu wa kijeshi wa Ukraine – ikipunguza ufadhili zaidi juhudi za vita vya Ukraine.
Katika mkutano na waandishi wa habari wa mwisho wa mwaka wiki hii, Bw Zelensky alisisitiza kwamba Ukraine haishindwa katika vita vyake dhidi ya Urusi.
BBC swahili
Ndege tatu za kivita aina ya Su-34 zilidunguliwa katika eneo la Kherson, jeshi la wanahewa la Ukraine lilitangaza.
Rais Volodymr Zelensky aliwashukuru wanajeshi walioangusha ndege hizo, akisema tukio hilo lilifanyika katika Mkoa wa Kherson wenye vita.
Urusi haijatoa maoni yoyote kuhusu kupotea kwa ndege zake, lakini Fighterbomber, mwanablogu mashuhuri wa vita vya Urusi, aliripoti kupotea kwa idadi isiyojulikana ya ndege, akisema labda ziliangushwa na makombora ya Patriot yaliyotengenezwa na Amerika.
Wafanyakazi wote walionusurika na waliokufa walipatikana, mwanablogu aliongeza.
Ukraine inakabiliwa na uhaba wa risasi huku ikiendelea kupambana na majeshi ya Urusi, kufuatia uvamizi kamili wa Moscow mnamo Februari 2022.
Kyiv ilisitisha makabiliano ya kujibu mashambulizi mwanzoni mwa majira ya baridi, huku Marekani - ambayo ni mfadhili mkuu wa kijeshi wa Ukraine – ikipunguza ufadhili zaidi juhudi za vita vya Ukraine.
Katika mkutano na waandishi wa habari wa mwisho wa mwaka wiki hii, Bw Zelensky alisisitiza kwamba Ukraine haishindwa katika vita vyake dhidi ya Urusi.
BBC swahili