Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,183
- 10,913
Unafiki wa dunia umefikia kiwango cha juu kiasi kwamba ni wachache sana wanaoumia wenzao wanapopata shida.
Urusi ilipotishia kuzuia nafaka zisitoke Ukraine Ulaya nzima walipiga makelele wakiilaani Urusi kutumia chakula kama silaha ya vita.Urusi ikasikia na wakaachia meli ziondoke na nafaka.
Ulaya iliyolia kilio hicho si kwamba ni jangwa na nafaka zisipofika kutoka Urusi kutakuwa na upungufu tu wa vyakula wavipendavyo.Wanaweza wakala vyakula vyengine na wasife njaa.
Upande wa Gaza ni tofauti.Israel imezuia kabisa kisiingie maeneo ya kaskazini ya gaza.Kuna watu wanazuia kila gari likijaribu kuvuka mpaka kuingia Gaza wakijua kuwa Gaza hakuna kilimo cha maana cha kulisha watu ambao hata kulima nako hawajapata nafasi kujishughulisha.
Kinyume na kupiga kelele kutetea,katika hali hiyo kuna watu wanashangilia kabisa chakula kutopelekwa Gaza.Huo ni ukatili wa hali ya juu.
Tofauti na Urusi ambayo ilipata huruma na kuachia ngano ziendelee kufika Ulaya.Israel yeye kila siku ndio anakaza kamba gari zisikatishe kufika maeneo yenye ukame.
Watu walioanza kurudi makwao kaskazini ya Gaza wamechagua tena hata kufa kwa risasi warudi kusini karibu na mpaka wa Misri ili wasife kwa njaa kaskazini ambako hali ni mbaya sana
Urusi ilipotishia kuzuia nafaka zisitoke Ukraine Ulaya nzima walipiga makelele wakiilaani Urusi kutumia chakula kama silaha ya vita.Urusi ikasikia na wakaachia meli ziondoke na nafaka.
Ulaya iliyolia kilio hicho si kwamba ni jangwa na nafaka zisipofika kutoka Urusi kutakuwa na upungufu tu wa vyakula wavipendavyo.Wanaweza wakala vyakula vyengine na wasife njaa.
Upande wa Gaza ni tofauti.Israel imezuia kabisa kisiingie maeneo ya kaskazini ya gaza.Kuna watu wanazuia kila gari likijaribu kuvuka mpaka kuingia Gaza wakijua kuwa Gaza hakuna kilimo cha maana cha kulisha watu ambao hata kulima nako hawajapata nafasi kujishughulisha.
Kinyume na kupiga kelele kutetea,katika hali hiyo kuna watu wanashangilia kabisa chakula kutopelekwa Gaza.Huo ni ukatili wa hali ya juu.
Tofauti na Urusi ambayo ilipata huruma na kuachia ngano ziendelee kufika Ulaya.Israel yeye kila siku ndio anakaza kamba gari zisikatishe kufika maeneo yenye ukame.
Watu walioanza kurudi makwao kaskazini ya Gaza wamechagua tena hata kufa kwa risasi warudi kusini karibu na mpaka wa Misri ili wasife kwa njaa kaskazini ambako hali ni mbaya sana