Urusi: Hatutishwi na blah blah za Trump na Magharibi

Urusi: Hatutishwi na blah blah za Trump na Magharibi

Jikite kwenye mada kijana,issue ya dini inahusikaje hapa?

Kama huu uzi upo nje ya uwezo wako wa uelewa na kuchanganua mambo,pita kimya tu.
Mkuu mchango wangu unahusu jinsi kobazi walivyo na akili finyu. Hayo memgine tuyaache
 
Mkuu mchango wangu unahusu jinsi kobazi walivyo na akili finyu. Hayo memgine tuyaache
Na wagalatia wanaoshobokea LGBTQ mpaka kuruhusiwa kwenda kubarikiwa na Papa,ndio kua na akili huko?

Kuuziwa udongo na chumvi na mafuta ili uwe tajiri kimiujiza,ndio akili zenu hizo wagalatia?
 
Mkuu wa baraza la ulinzi la Urusi Dmitry Medvedev amesema Urusi haitishwi na kauli ya raisi wa Marekani Donald Trump kuhusu vikwazo zaidi kwa nchi hiyo endapo itagoma kusaini mkataba wa kusitisha vita huko Ukraine ndani ya siku 50 (49 sasa 😁) zijazo.

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X, Medvedev amesema Urusi kamwe haitishwi na vitisho vya Donald Trump kwa kuwawekea vikwazo vya kiuchumi wale wote wanaonunua gesi, mafuta pamoja na uranium kutoka nchini humo.

Medvedev aliongeza kuwa ulimwengu lazima utegemee kutetemeka huku baadhi ya nchi za ulaya zimechukizwa na kauli ya Donald Trump kwa sababu nishati kutoka nchini Urusi ndiyo nishati nafuu zaidi kwao. Hata hivyo Urusi haitishiki kwa vitisho vya Trump.

Kauli hii ya Dmitry Medvedev inakuja mara baada ya raisi wa Marekani Donald Trump kutangaza kupeleka silaha zaidi nchini Ukraine ili kuifanya Urusi irejee kwenye mazungumzo ya kutafuta suluhu ya mgogoro uliopo ulaya mashariki baina ya Urusi na Ukraine.

NB: Niliwahi kusema humu kuwa hakuna mtu yeyote kutoka nje ya Urusi ambaye anaweza kuamua hatima yao kwenye huu mgogoro uliopo ulaya mashariki baina ya Urusi na Ukraine isipokuwa ni warusi wenyewe. Licha ya vitisho na kauli nyingi za Donald Trump kuhusu Urusi, wanaume wamemjibu kwa kauli moja tu kuwa hawatishiki na kauli zake.

Halafu Urusi angekuwa anaziogopa nchi za magharibi ungeona yeye ndiye anahangaika kutafuta suluhu ya huu mgogoro. Lakini cha ajabu licha ya kulundikiwa vikwazo lukuki vya kiuchumi ndio kwanza anazidi kupigana na wala hajaonekana kwenda kuwapigia magoti watu wa magharibi ili warudi kwenye meza ya mazungumzo. Sasa uoga wa Urusi uko wapi?


Hakuna la kujivunia kwa Urusi. Urusi kupambana muda wote huu na Ukraine ambayo ilikiwa ni jimbo tu la Urusi ya zamani, ni aibu kubwa. Hata Urusi yenyewe haiamini uanayoendelea. Vita hii ya Urusi na Ukraine ndiyo iliyoithibitishia Dunia kuwa uwezo wa kijeshi wa Urusi ulikuwa exagerated sana. Urusi iliamini ingeimaliza Ukraine ndani ya siku mbili, na kwa muda huo ingekuwa tayari ingefanikiwa kuiondoa mpaka Serikali, na kuisimika serikali kibaraka. Lakini mpaka leo, hakuna hata dalili. Inaendelea tu kuua raia kwa drones za kupewa na Iran.
 
Hakuna la kujivunia kwa Urusi. Urusi kupambana muda wote huu na Ukraine ambayo ilikiwa ni jimbo tu la Urusi ya zamani, ni aibu kubwa. Hata Urusi yenyewe haiamini uanayoendelea. Vita hii ya Urusi na Ukraine ndiyo iliyoithibitishia Dunia kuwa uwezo wa kijeshi wa Urusi ulikuwa exagerated sana. Urusi iliamini ingeimaliza Ukraine ndani ya siku mbili, na kwa muda huo ingekuwa tayari ingefanikiwa kuiondoa mpaka Serikali, na kuisimika serikali kibaraka. Lakini mpaka leo, hakuna hata dalili. Inaendelea tu kuua raia kwa drones za kupewa na Iran.
Labda nikuhoji kidogo, hivi Jeshi la Merikani iliwachukua miaka mingapi wakipigana huko VietNam na wakashindwa vibaya sana hilo mbona huwa hamlisemi? Afghanistan,je, na huko mambo yalijirudia hivyo hivyo, jeshi LA Merikani lilitimuka bila ya kuvaa hata viatu wakiwakimbia Wateliban akina Mulla Omari - tukija huko Ukraine licha ya kupewa silaha pia na askari/wanajeshi wakukodishwa kutoka mataifa ya magharibi, nawambieni licha ya msaada huo wote (narudia): WA silaha,manajeshi na fedha kutoka magharibi - Ukraine haiwezi kumaliza mwaka huu bila ya kushindwa VITA na jeshi la Urusi, na siku 50 ambazo Trump ameipa Urusi kwamba sijui wasitishe vita na kuja kwenye meza ya mazungumzo, mtu ungetegemea kauli hiyo angemwambia Zelensky na siyo Putin - Trump akumbuke kwamba Urusi si taifa la kutishwa tishwa na Amerika, kijeshi Urusi ndilo Taifa pekee Duniani la kuiweza Merikani, neck to Neck,hivyo Warusi wasichukuliwe poa hata kidogo.
 
Trump ataanza kuwanunulia magaidi iwasumbue kwanza.
 
Uislam Unahusianaje hapa???

Nyie wa Galatia mna chuki sana.. Hata samia mnam chukia coz ni dini
Hao wakristo usihangaike nao mbona hata kwenye qur an wametajwa kasome qur an 2:120 chuki yao dhidi ya waislam haiwezi kuisha kamwe mpaka dunia inafika mwisho maana christians walitakiwa wawachukie wayahudi waliyomsulubisha yesu lakini imekuwa kinyume chake wanawapenda wayahudi wanawaona watakatifu lakini waislam ambao wanamtambua yesu na kumuheshimu ndio wamekuwa na chuki nao ndio maana unaona hata km mada haihusiani na dini mtu atajitahidi mpk ahakikishe waislamu wanakashifiwa ndio moyo wake unakuwa na amani anapata usingizi hao wanatimiza tu maandiko waache wakitukana uislamu ww usitukane dini yao.
 
Labda nikuhoji kidogo, hivi Jeshi la Merikani iliwachukua miaka mingapi wakipigana huko VietNam na wakashindwa vibaya sana hilo mbona huwa hamlisemi? Afghanistan,je, na huko mambo yalijirudia hivyo hivyo, jeshi LA Merikani lilitimuka bila ya kuvaa hata viatu wakiwakimbia Wateliban akina Mulla Omari - tukija huko Ukraine licha ya kupewa silaha pia na askari/wanajeshi wakukodishwa kutoka mataifa ya magharibi, nawambieni licha ya msaada huo wote (narudia): WA silaha,manajeshi na fedha kutoka magharibi - Ukraine haiwezi kumaliza mwaka huu bila ya kushindwa VITA na jeshi la Urusi, na siku 50 ambazo Trump ameipa Urusi kwamba sijui wasitishe vita na kuja kwenye meza ya mazungumzo, mtu ungetegemea kauli hiyo angemwambia Zelensky na siyo Putin - Trump akumbuke kwamba Urusi si taifa la kutishwa tishwa na Amerika, kijeshi Urusi ndilo Taifa pekee Duniani la kuiweza Merikani, neck to Neck,hivyo Warusi wasichukuliwe poa hata kidogka
 
Hao wakristo usihangaike nao mbona hata kwenye qur an wametajwa kasome qur an 2:120 chuki yao dhidi ya waislam haiwezi kuisha kamwe mpaka dunia inafika mwisho maana christians walitakiwa wawachukie wayahudi waliyomsulubisha yesu lakini imekuwa kinyume chake wanawapenda wayahudi wanawaona watakatifu lakini waislam ambao wanamtambua yesu na kumuheshimu ndio wamekuwa na chuki nao ndio maana unaona hata km mada haihusiani na dini mtu atajitahidi mpk ahakikishe waislamu wanakashifiwa ndio moyo wake unakuwa na amani anapata usingizi hao wanatimiza tu maandiko waache wakitukana uislamu ww usitukane dini yao.
kWeli
 
Hakuna la kujivunia kwa Urusi. Urusi kupambana muda wote huu na Ukraine ambayo ilikiwa ni jimbo tu la Urusi ya zamani, ni aibu kubwa. Hata Urusi yenyewe haiamini uanayoendelea. Vita hii ya Urusi na Ukraine ndiyo iliyoithibitishia Dunia kuwa uwezo wa kijeshi wa Urusi ulikuwa exagerated sana. Urusi iliamini ingeimaliza Ukraine ndani ya siku mbili, na kwa muda huo ingekuwa tayari ingefanikiwa kuiondoa mpaka Serikali, na kuisimika serikali kibaraka. Lakini mpaka leo, hakuna hata dalili. Inaendelea tu kuua raia kwa drones za kupewa na Iran.
Wewe huna akili..samahani lakini.....Ukraine anasaidiwa na NATO .....ndo maana zeleiski kila siku anavinjari tu Ulaya kutafuta namna ya kupambana na urusi....
 
Wewe huna akili..samahani lakini.....Ukraine anasaidiwa na NATO .....ndo maana zeleiski kila siku anavinjari tu Ulaya kutafuta namna ya kupambana na urusi....
Kiufupi Urusi anapigana na mataifa ya NATO na sio Ukraine pekee
 
Back
Top Bottom