Last Seen
JF-Expert Member
- Jun 7, 2013
- 223
- 549
Habari wana JF,
Kwa awamu nyingi Kigoma imekuwa miongoni mwa Mikoa michache inayozalisha wabunge wengi vijana wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na hatimaye kujipatia umaarufu mkubwa nchi nzima.
Baadhi yao huanza kuwa na kiburi Mara wanapojihisi wamefanikiwa zaidi kisiasa na kuanza kuwakejeli waliowafanya wafike hapo walipofika.
Uroho wa madaraka pia imekuwa kikwazo kwa viongozi wengi Vijana, Hutamani kufanikiwa zaidi kisiasa kuliko kufanya kazi walizoagizwa na wananchi Bungeni,Kafulila ni mmoja kati ya vijana walioingia Bungeni (2010-2015) kwa kasi na kupata umaarufu wa haraka kwa umahiri wake wa kufichua maovu mbali mbali katika Serikali hadi kufikia hatua ya kuitwa "tumbili".
Aliwahi kumkashifu ZZK aliyemshika mkono na kufanikiwa kuwa Mbunge wa JMT.
Licha ya kuwa mwanasiasa mzuri Amekuwa kijana mwenye Kiburi kwa viongozi wake na mwenye uroho wa madaraka vilivyompelekea kutimuliwa na Chama chake Cha Awali Cha CHADEMA na kutimkia NCCR-MAGEUZI ambako alipewa nafasi ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika ngazi ya ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini na Kushinda, Alihudumu kwa Kipindi Kimoja na hatimaye katika Uchaguzi wa mwaka 2015 akashindwa na Mwana-mama Hasna Mwilima. Alikimbilia mahakani na kushindwa Mara kadhaa.
Akahamia CCM, Mheshimiwa Rais akamteua kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe kutokana na utendaji Kazi wake wa Awali... 2020 akajivua cheo Cha U-RAS na kutia Nia ya kuteuliwa na Chama chake kugombea nafasi ya Ubunge na Akapigwa kipigo Cha mbwa Koko.
MH. Rais aliwaonya wateuliwa wake na kuwakumbusha kuhusu Kisa Cha Mwananzila aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora ambaye alipotea Kisiasa kutokana na uroho wa madaraka. Kafulila amepotea tayari, Kafulila tumsahau Kabisa,Kapewa nafasi na mheshimiwa Rais kaona haifai asitarajie miujiza yoyote ya kupata nafasi ya Kuteuliwa na Mh. Rais.
Kwa awamu nyingi Kigoma imekuwa miongoni mwa Mikoa michache inayozalisha wabunge wengi vijana wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na hatimaye kujipatia umaarufu mkubwa nchi nzima.
Baadhi yao huanza kuwa na kiburi Mara wanapojihisi wamefanikiwa zaidi kisiasa na kuanza kuwakejeli waliowafanya wafike hapo walipofika.
Uroho wa madaraka pia imekuwa kikwazo kwa viongozi wengi Vijana, Hutamani kufanikiwa zaidi kisiasa kuliko kufanya kazi walizoagizwa na wananchi Bungeni,Kafulila ni mmoja kati ya vijana walioingia Bungeni (2010-2015) kwa kasi na kupata umaarufu wa haraka kwa umahiri wake wa kufichua maovu mbali mbali katika Serikali hadi kufikia hatua ya kuitwa "tumbili".
Aliwahi kumkashifu ZZK aliyemshika mkono na kufanikiwa kuwa Mbunge wa JMT.
Licha ya kuwa mwanasiasa mzuri Amekuwa kijana mwenye Kiburi kwa viongozi wake na mwenye uroho wa madaraka vilivyompelekea kutimuliwa na Chama chake Cha Awali Cha CHADEMA na kutimkia NCCR-MAGEUZI ambako alipewa nafasi ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika ngazi ya ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini na Kushinda, Alihudumu kwa Kipindi Kimoja na hatimaye katika Uchaguzi wa mwaka 2015 akashindwa na Mwana-mama Hasna Mwilima. Alikimbilia mahakani na kushindwa Mara kadhaa.
Akahamia CCM, Mheshimiwa Rais akamteua kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe kutokana na utendaji Kazi wake wa Awali... 2020 akajivua cheo Cha U-RAS na kutia Nia ya kuteuliwa na Chama chake kugombea nafasi ya Ubunge na Akapigwa kipigo Cha mbwa Koko.
MH. Rais aliwaonya wateuliwa wake na kuwakumbusha kuhusu Kisa Cha Mwananzila aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora ambaye alipotea Kisiasa kutokana na uroho wa madaraka. Kafulila amepotea tayari, Kafulila tumsahau Kabisa,Kapewa nafasi na mheshimiwa Rais kaona haifai asitarajie miujiza yoyote ya kupata nafasi ya Kuteuliwa na Mh. Rais.