Uroho wa madaraka unavyomgharimu Kafulila

Last Seen

JF-Expert Member
Jun 7, 2013
223
549
Habari wana JF,
Kwa awamu nyingi Kigoma imekuwa miongoni mwa Mikoa michache inayozalisha wabunge wengi vijana wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na hatimaye kujipatia umaarufu mkubwa nchi nzima.

Baadhi yao huanza kuwa na kiburi Mara wanapojihisi wamefanikiwa zaidi kisiasa na kuanza kuwakejeli waliowafanya wafike hapo walipofika.

Uroho wa madaraka pia imekuwa kikwazo kwa viongozi wengi Vijana, Hutamani kufanikiwa zaidi kisiasa kuliko kufanya kazi walizoagizwa na wananchi Bungeni,Kafulila ni mmoja kati ya vijana walioingia Bungeni (2010-2015) kwa kasi na kupata umaarufu wa haraka kwa umahiri wake wa kufichua maovu mbali mbali katika Serikali hadi kufikia hatua ya kuitwa "tumbili".

Aliwahi kumkashifu ZZK aliyemshika mkono na kufanikiwa kuwa Mbunge wa JMT.

Licha ya kuwa mwanasiasa mzuri Amekuwa kijana mwenye Kiburi kwa viongozi wake na mwenye uroho wa madaraka vilivyompelekea kutimuliwa na Chama chake Cha Awali Cha CHADEMA na kutimkia NCCR-MAGEUZI ambako alipewa nafasi ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika ngazi ya ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini na Kushinda, Alihudumu kwa Kipindi Kimoja na hatimaye katika Uchaguzi wa mwaka 2015 akashindwa na Mwana-mama Hasna Mwilima. Alikimbilia mahakani na kushindwa Mara kadhaa.

Akahamia CCM, Mheshimiwa Rais akamteua kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe kutokana na utendaji Kazi wake wa Awali... 2020 akajivua cheo Cha U-RAS na kutia Nia ya kuteuliwa na Chama chake kugombea nafasi ya Ubunge na Akapigwa kipigo Cha mbwa Koko.

MH. Rais aliwaonya wateuliwa wake na kuwakumbusha kuhusu Kisa Cha Mwananzila aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora ambaye alipotea Kisiasa kutokana na uroho wa madaraka. Kafulila amepotea tayari, Kafulila tumsahau Kabisa,Kapewa nafasi na mheshimiwa Rais kaona haifai asitarajie miujiza yoyote ya kupata nafasi ya Kuteuliwa na Mh. Rais.
 
Ujue mimi nimejiuliza mpaka nashindwa kuelewa hawa wateule wa Rais huwa wanafikiria nini. Hivi kweli mtu inaacha u RAS unaenda kupata kura 64? Serious kabisa unaenda kuwa mshindi wa nne, RAS...


yani hata kufanya tathmini ndogo umeshindwa? Yupo aliyeacha u DC kaenda kupata kura 12
 
Habari wana JF,
Kwa awamu nyingi Kigoma imekuwa miongoni mwa Mikoa michache inayozalisha wabunge wengi vijana wenye uwezo mkubwa wa kujenga hoja na hatimaye kujipatia umaarufu mkubwa nchi nzima.

Baadhi yao huanza kuwa na kiburi Mara wanapojihisi wamefanikiwa zaidi kisiasa na kuanza kuwakejeli waliowafanya wafike hapo walipofika.

Uroho wa madaraka pia imekuwa kikwazo kwa viongozi wengi Vijana, Hutamani kufanikiwa zaidi kisiasa kuliko kufanya kazi walizoagizwa na wananchi Bungeni,Kafulila ni mmoja kati ya vijana walioingia Bungeni (2010-2015) kwa kasi na kupata umaarufu wa haraka kwa umahiri wake wa kufichua maovu mbali mbali katika Serikali hadi kufikia hatua ya kuitwa "tumbili".

Aliwahi kumkashifu ZZK aliyemshika mkono na kufanikiwa kuwa Mbunge wa JMT.

Licha ya kuwa mwanasiasa mzuri Amekuwa kijana mwenye Kiburi kwa viongozi wake na mwenye uroho wa madaraka vilivyompelekea kutimuliwa na Chama chake Cha Awali Cha CHADEMA na kutimkia NCCR-MAGEUZI ambako alipewa nafasi ya kupeperusha bendera ya chama hicho katika ngazi ya ubunge wa Jimbo la Kigoma Kusini na Kushinda, Alihudumu kwa Kipindi Kimoja na hatimaye katika Uchaguzi wa mwaka 2015 akashindwa na Mwana-mama Hasna Mwilima. Alikimbilia mahakani na kushindwa Mara kadhaa.

Akahamia CCM, Mheshimiwa Rais akamteua kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe kutokana na utendaji Kazi wake wa Awali... 2020 akajivua cheo Cha U-RAS na kutia Nia ya kuteuliwa na Chama chake kugombea nafasi ya Ubunge na Akapigwa kipigo Cha mbwa Koko.

MH. Rais aliwaonya wateuliwa wake na kuwakumbusha kuhusu Kisa Cha Mwananzila aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora ambaye alipotea Kisiasa kutokana na uroho wa madaraka. Kafulila amepotea tayari, Kafulila tumsahau Kabisa,Kapewa nafasi na mheshimiwa Rais kaona haifai asitarajie miujiza yoyote ya kupata nafasi ya Kuteuliwa na Mh. Rais.
Nasema hivi 'TUMBILI NI TUMBILI TU' 'acha arudi msituni tu, yaani kwa akili yake alidhania kuwa kwenye kura za maoni angetoboa?!! Wakati huko kuna wajumbe kindakindaki wamezeekea kwenye chama hata ukatibu tu hakuna!! Leo uje mtu umepata fever ya jiwe, utake kutuzidi!! Sasa kwenye u RAS, alikuwa anakosa nini? Na yule mwingine aliyekuwa DC, dodoma?!!
 
Ujue mimi nimejiuliza mpaka nashindwa kuelewa hawa wateule wa Rais huwa wanafikiria nini. Hivi kweli mtu inaacha u RAS unaenda kupata kura 64? Serious kabisa unaenda kuwa mshindi wa nne, RAS...


yani hata kufanya tathmini ndogo umeshindwa? Yupo aliyeacha u DC kaenda kupata kura 12
Makubaliano ya kuunga juhudi ilikuwa ni kuwawezesha kuwa wabunge na sio Ma -RAS na Ma-DC.

Ukweli ni kwamba mkuu ameenda kinyume na makubaliano!

Sent from my VFD 301 using JamiiForums mobile app
 
Ujue mimi nimejiuliza mpaka nashindwa kuelewa hawa wateule wa Rais huwa wanafikiria nini. Hivi kweli mtu inaacha u RAS unaenda kupata kura 64? Serious kabisa unaenda kuwa mshindi wa nne, RAS...


yani hata kufanya tathmini ndogo umeshindwa? Yupo aliyeacha u DC kaenda kupata kura 12

Walikaririshwa eti upinzani hakuna atakayerudi bungeni, wakawahi siti
 
Nafuu Kafulila aliambulia kura 64. Kuna mtu anaitwa Vincent Mashinji ambaye alifight kwa jasho na damu na kupata kura 2.

Huyu Mashinji sijawahi kumuelewa tangia akiwa KM Chadema, sijui mbowe alimuokotea wapi maana hata uteuzi wake wengi sana walitilia shaka.
Ogopa sana watu wakina John kisomo wale unakuta ana CV ndefu kasoma degree kama 4, Diploma 3, mara PHd etc hawa wengi wao huwa ni wasaka fursa, mara nyingi hutamani kupata fursa kupitia elimu yao.
 
Nafuu Kafulila aliambulia kura 64. Kuna mtu anaitwa Vincent Mashinji ambaye alifight kwa jasho na damu na kupata kura 2.

Huyu Mashinji sijawahi kumuelewa tangia akiwa KM Chadema, sijui mbowe alimuokotea wapi maana hata uteuzi wake wengi sana walitilia shaka.
Ogopa sana watu wakina John kisomo walebunakuta ana CV ndefu kasoma degree kama 4, Diploma 3, mara PHd etc hawa wengi wao huwa ni wasaka fursa, mara nyingi hutamani kupata fursa kupitia elimu yao
 
Back
Top Bottom