DOKEZO URGENT: Binti wa miaka 16 ameozeshwa kwa lazima kama mke wa pili, huko Laela, Sumbawanga

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Inatakiwa busara itumike. Mazingira ya huko vijijini hakuna elimu na uelewa hivyo maisha kama haya ndiyo kawaida yao. Hawajui hata kama wanavunja sheria. Hivyo naishauri serikali isi-over react kwa kufunga watu miaka 30. Japo kutojua sheria siyo utetezi lakini itakuwa siyo vizuri kufunga watu miaka 30 kwa mazingira ya aina hiyo.

Seriously?!

Yaani tunalalamika kila kukicha kuitaka serikali na vyombo vyenye mamlaka kusimamia katiba, kufuata sheria na ku- exercise utawala bora na hapo hapo kati yetu wapo watu wanaowaza Kama wewe!


Kutokujua sheria sio kinga ya kuwajibika kisheria, na sheria haina macho ila ina mikono yenye mizani na upanga.

Watanzania ni wanafiki sana!
 
Naomba kuuliza! Hivi Ndoa za kulazimishwa huwa zinaangukia kwenye makosa gani!? Je ni Civil au Jinai!!??

Yaani unauliza Kama ni halali kujipa kibali (ndoa)kwa lazima ya kumbaka mtu hasiyekutaka kwa muda wa maisha yake yote ama mpaka tamati ya kibali chako?!
 
S

heria ya ndoa inasema wazazi wakiridhia na si mtoto akiridhia.Sheria ndio haifai nuaoaji hawana kosa hapo,kama serikali haitaki ndoa za utotoni ibadilishe sheria.Mtoto wa miaka 14 anaridhia nini kwenye suala kubwa kama ndoa? kama kupiga kura tu mtoto huyo haruhus,kunywa pombe haruhusiwi ,kuendesha gari haruhusiwi eti ndoa ndoa ndio aridhie, huu ni wendawazimu.Serikali isitufanye wote hatuna akili kama kuna makundi ya dini inayaogopa kwenye hili suala la ndoa za utotoni ni heri iache hao watoto waendelee kuolewa

Una hoja, kubwa sana.


Kama ulivyosema, mtoto wa miaka 14 hana uwezo wowote wa kufanya maamuzi sahihi kwenye jambo kubwa Kama ndoa, sasa uwezo wa kuitunza na kuihudumia hiyo ndoa anapata wapi? Ama ndio anabakwa maisha yake yote / mpaka mwisho wa hiyo ndoa?

Kweli Binaadam hana huruma.
 
Binti wa miaka 16 anaitwa Recho, yuko kijiji cha NITU, wilaya ya LAELA, Mkoa wa Rukwa.

Ameozeshwa kwa kulazimishwa na wazazi wake pamoja na kaka zake, ambao wamechukua mahari ya shilingi 700,000, tena ameozeshwa kwa mzee kama mke wa pili.

Huyo binti yeye hataki kuolewa na kwa sasa ametoroka, yupo nyumbani kwa mchungaji amejificha. Namba ya mchungaji alipo binti ni 0629 518702, mchungaji anaitwa Baba Irene. Huyu binti anahitaji msaada wa haraka sana, aokolewe kutoka katika hili janga.

Viongozi wa kijiji husika hawana msaada katika hili, kwani wao wanaona ni jambo la kawaida, wameshazoea mabinti huko huwa wanaozeshwa kilazima tu, wala si jambo la kushangaza.

NAOMBA SERIKALI IMSAIDIE HUYU BINTI.

Binti wa miaka 16 anaitwa Recho, yuko kijiji cha NITU, wilaya ya LAELA, Mkoa wa Rukwa.

Ameozeshwa kwa kulazimishwa na wazazi wake pamoja na kaka zake, ambao wamechukua mahari ya shilingi 700,000, tena ameozeshwa kwa mzee kama mke wa pili.

Huyo binti yeye hataki kuolewa na kwa sasa ametoroka, yupo nyumbani kwa mchungaji amejificha. Namba ya mchungaji alipo binti ni 0629 518702, mchungaji anaitwa Baba Irene. Huyu binti anahitaji msaada wa haraka sana, aokolewe kutoka katika hili janga.

Viongozi wa kijiji husika hawana msaada katika hili, kwani wao wanaona ni jambo la kawaida, wameshazoea mabinti huko huwa wanaozeshwa kilazima tu, wala si jambo la kushangaza.

NAOMBA SERIKALI IMSAIDIE HUYU BINTI.
Mrejesho.

Ndugu zangu, timu ya maafisa iliwajibika kuchukua hatua za kwenda hadi kwa huyu aliyetajwa kama Baba Irene mwenye simu iliyoandikwa hapo kwenye taarifa.

Mara baada ya kufika huko, Baba Irene aliwajulisha maafisa hao kuwa yule Binti ametoroka. Kilichofuata ni taarifa hiyo kuwasilishwa Polisi na jalada la kufunguliwa Ili upelelezi ufanyike juu ya taarifa hii. Hivyo, tumeacha suala hili mikononi mwa vyombo. RB na. 802/2023 kituo cha Polisi Laela.

Siku ingine karibuni pia kituo chetu cha huduma kwa wateja namba 0734986503 au 026 2160250 siku za kazi au 116 siku zote saa 24.

Ahsanteni sana na Mungu awabariki. 🙏🏽 Pamoja, inawezekana kukomesha ukatili wa kijinsia na kwa watoto.
 
Mrejesho.

Ndugu zangu, timu ya maafisa iliwajibika kuchukua hatua za kwenda hadi kwa huyu aliyetajwa kama Baba Irene mwenye simu iliyoandikwa hapo kwenye taarifa.

Mara baada ya kufika huko, Baba Irene aliwajulisha maafisa hao kuwa yule Binti ametoroka. Kilichofuata ni taarifa hiyo kuwasilishwa Polisi na jalada la kufunguliwa Ili upelelezi ufanyike juu ya taarifa hii. Hivyo, tumeacha suala hili mikononi mwa vyombo. RB na. 802/2023 kituo cha Polisi Laela.

Siku ingine karibuni pia kituo chetu cha huduma kwa wateja namba 0734986503 au 026 2160250 siku za kazi au 116 siku zote saa 24.

Ahsanteni sana na Mungu awabariki. Pamoja, inawezekana kukomesha ukatili wa kijinsia na kwa watoto.
Kazi njema Madam Gwajima. Mapendekezo yangu naona muanzishe kampeni ya kutokomeza unyanyasaji wa watoto wa kike hasa kwenye mikoa ambayo imekithiri suala hili, watu wapatiwe elimu na adhabu kali kwa yeyote atakayehusika na unyanyasaji huo. Natanguliza shukurani madam. Uwe na majukumu mema
 
Mrejesho.

Ndugu zangu, timu ya maafisa iliwajibika kuchukua hatua za kwenda hadi kwa huyu aliyetajwa kama Baba Irene mwenye simu iliyoandikwa hapo kwenye taarifa.

Mara baada ya kufika huko, Baba Irene aliwajulisha maafisa hao kuwa yule Binti ametoroka. Kilichofuata ni taarifa hiyo kuwasilishwa Polisi na jalada la kufunguliwa Ili upelelezi ufanyike juu ya taarifa hii. Hivyo, tumeacha suala hili mikononi mwa vyombo. RB na. 802/2023 kituo cha Polisi Laela.

Siku ingine karibuni pia kituo chetu cha huduma kwa wateja namba 0734986503 au 026 2160250 siku za kazi au 116 siku zote saa 24.

Ahsanteni sana na Mungu awabariki. Pamoja, inawezekana kukomesha ukatili wa kijinsia na kwa watoto.
Hongereni sana for quick response Muheshimiwa Gwajima, vp kuhusu Wazazi wake team yako ilifanikiwa kuwaona na kuwasikia na wao wanasemaje kuhusu swala la Mtoto kuolewa!!??
 
S

heria ya ndoa inasema wazazi wakiridhia na si mtoto akiridhia.Sheria ndio haifai nuaoaji hawana kosa hapo,kama serikali haitaki ndoa za utotoni ibadilishe sheria.Mtoto wa miaka 14 anaridhia nini kwenye suala kubwa kama ndoa? kama kupiga kura tu mtoto huyo haruhus,kunywa pombe haruhusiwi ,kuendesha gari haruhusiwi eti ndoa ndoa ndio aridhie, huu ni wendawazimu.Serikali isitufanye wote hatuna akili kama kuna makundi ya dini inayaogopa kwenye hili suala la ndoa za utotoni ni heri iache hao watoto waendelee kuolewa
Ji-update mkuu

Sidhani kama sheria bado inasema hivyo
 
Ji-update mkuu

Sidhani kama sheria bado inasema hivyo
Uliibdili wewe? Haya sema hiyo sheria mpya ni ya lini na inasemaje?


Mgongano wa Sheria katika kufafanua Tafsiri ya Mtoto kwa muktadha wa NdoaKama ilivyoelezwa hapo awali, Sheria ya Ndoa ni Sheria ambayo inasimamia maswalayote ya ndoa nchini Tanzania. Sheria ya Ndoa inapingana na Sheria zingine ambazozinafafanua tafsiri ya mtoto. Wakati Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, inamwelezeamtoto kama mtu mwenye umri chini ya miaka 18, Sheria ya Ndoa bado inamruhusumtoto mwenye umri wa miaka 15 kuolewa kwa ruhusa ya wazazi. Tafsiri ya mtoto chiniya Sheria ya Mtoto haijabatilisha kifungu cha 13 ya Sheria ya Ndoa ambacho kinawekaumri wa chini wa ndoa kuwa miaka 15 kwa wasichana na 18 kwa wavulana. mwaka2019, Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ilithibitisha uamuzi wa Mahakama Kuu katika kesiya Rebeca Gyumi dhidi ya MwanaSheria mkuu wa Serikali, kuwa vifungu vya 13 na 17vya Sheria ya Ndoa ambavyo vinaruhusu mtoto kuolewa na umri wa miaka 15 kwa idhiniya wazazi na 14 kwa ruhusa ya mahakama ni vya kibaguzi dhidi ya mtoto wa kike na nikinyume na Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo, vinapaswakurekebishwa katika kipindi cha miezi 12, hata hivyo Sheria ya ndoa, haijabadilishwampaka sasa. Mara kwa mara Serikali imekua ikikiri kwamba kushindwa kubadili kifunguhicho ni kutokana na unyeti wa kitamaduni na wa kidini juu ya jambo hilo.
 
Uliibdili wewe? Haya sema hiyo sheria mpya ni ya lini na inasemaje?


Mgongano wa Sheria katika kufafanua Tafsiri ya Mtoto kwa muktadha wa NdoaKama ilivyoelezwa hapo awali, Sheria ya Ndoa ni Sheria ambayo inasimamia maswalayote ya ndoa nchini Tanzania. Sheria ya Ndoa inapingana na Sheria zingine ambazozinafafanua tafsiri ya mtoto. Wakati Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009, inamwelezeamtoto kama mtu mwenye umri chini ya miaka 18, Sheria ya Ndoa bado inamruhusumtoto mwenye umri wa miaka 15 kuolewa kwa ruhusa ya wazazi. Tafsiri ya mtoto chiniya Sheria ya Mtoto haijabatilisha kifungu cha 13 ya Sheria ya Ndoa ambacho kinawekaumri wa chini wa ndoa kuwa miaka 15 kwa wasichana na 18 kwa wavulana. mwaka2019, Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ilithibitisha uamuzi wa Mahakama Kuu katika kesiya Rebeca Gyumi dhidi ya MwanaSheria mkuu wa Serikali, kuwa vifungu vya 13 na 17vya Sheria ya Ndoa ambavyo vinaruhusu mtoto kuolewa na umri wa miaka 15 kwa idhiniya wazazi na 14 kwa ruhusa ya mahakama ni vya kibaguzi dhidi ya mtoto wa kike na nikinyume na Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania. Hivyo, vinapaswakurekebishwa katika kipindi cha miezi 12, hata hivyo Sheria ya ndoa, haijabadilishwampaka sasa. Mara kwa mara Serikali imekua ikikiri kwamba kushindwa kubadili kifunguhicho ni kutokana na unyeti wa kitamaduni na wa kidini juu ya jambo hilo.
Hapana sijabadili mimi.

Ila ni mahakama za hapa hapa Tanzania zilibadili baada ya kampeni mbalimbali zilizofanywa na wanaharakati pamoja na kituo cha LHRC

Serikali ikakata rufaa na wakasema wanakata rufaa ili kuhakikisha hukumu inakazwa hatotokea mtu wa kuipinga.

 
Hapana sijabadili mimi.

Ila ni mahakama za hapa hapa Tanzania zilibadili baada ya kampeni mbalimbali zilizofanywa na wanaharakati pamoja na kituo cha LHRC

Serikali ikakata rufaa na wakasema wanakata rufaa ili kuhakikisha hukumu inakazwa hatotokea mtu wa kuipinga.

Ndicho nilichosema lakini mahakama haina uwezo wa kubadili au kutunga sheria isipokuwa Bunge kwa Muswada utakaopelekwa na serikali kitu ambacho serikali imeshindwa kufanya tangu iliposhindwa Mahakamani kwenye kesi ya Rebecca Gyumi na kuambiwa na Mahakama ikarekebishe hicho kifungu cha miaka 14 mtoto kuolew kwa ridhaa ya wazazi ili umri wa kuolewa uwe miaka 18m lakini serikali imeshindwa kutokana na shinikizo la imani za kidini ambapo kwenye baadhi ya dini kwao ni sahihi mtoto kuolewa kwa umri huo wa miaka 14,hivyo serikali inaogopa mgogoro na makundi ya dini kuweka umri miaka 18 hivyo inachofanya serikali ni kurukaruka tu na kufanya maigizo ya kujifanya wanapinga hizo ndoa
 
Mrejesho.

Ndugu zangu, timu ya maafisa iliwajibika kuchukua hatua za kwenda hadi kwa huyu aliyetajwa kama Baba Irene mwenye simu iliyoandikwa hapo kwenye taarifa.

Mara baada ya kufika huko, Baba Irene aliwajulisha maafisa hao kuwa yule Binti ametoroka. Kilichofuata ni taarifa hiyo kuwasilishwa Polisi na jalada la kufunguliwa Ili upelelezi ufanyike juu ya taarifa hii. Hivyo, tumeacha suala hili mikononi mwa vyombo. RB na. 802/2023 kituo cha Polisi Laela.

Siku ingine karibuni pia kituo chetu cha huduma kwa wateja namba 0734986503 au 026 2160250 siku za kazi au 116 siku zote saa 24.

Ahsanteni sana na Mungu awabariki. 🙏🏽 Pamoja, inawezekana kukomesha ukatili wa kijinsia na kwa watoto.
Hongera sana@Dr.Gwajima D.
 
Mrejesho.

Ndugu zangu, timu ya maafisa iliwajibika kuchukua hatua za kwenda hadi kwa huyu aliyetajwa kama Baba Irene mwenye simu iliyoandikwa hapo kwenye taarifa.

Mara baada ya kufika huko, Baba Irene aliwajulisha maafisa hao kuwa yule Binti ametoroka. Kilichofuata ni taarifa hiyo kuwasilishwa Polisi na jalada la kufunguliwa Ili upelelezi ufanyike juu ya taarifa hii. Hivyo, tumeacha suala hili mikononi mwa vyombo. RB na. 802/2023 kituo cha Polisi Laela.

Siku ingine karibuni pia kituo chetu cha huduma kwa wateja namba 0734986503 au 026 2160250 siku za kazi au 116 siku zote saa 24.

Ahsanteni sana na Mungu awabariki. Pamoja, inawezekana kukomesha ukatili wa kijinsia na kwa watoto.
Dkt Dorothy Gwajima, binafsi nikushukuru sana Kwa hatua ulizo chukua , lakini nikupongeze Kwa jinsi ulivyo jibainisha waziwazi kwenye jukwaa hili, Kwani wengine tumekuwa na uhakika kuwa kupitia JF baadhi ya taarifa zetu Huwa zinawafikia viongozi wetu. Tutaendelea kutoa ushirikiano kwenye wizara yako ili tuweze kukomesha kabisa ukatili wa kijinsia hasa Kwa watoto wetu. Hakika nimekuelewa sana. Mungu akubariki.
 
Dkt. Gwajima D , umefeli kutatua jambo dogo kama Hilo.

Maafisa uliowatuma wamechotewa mgao kwenye Mahari wewe ukaambiwa ametoroka. Hiyo RB haitadaidia, hata mtuhumiwa na mkewe wakikamatwa watoa maokoto na kuachiwa..

Next time ukipatiwa taarifa za namna hiyo tumia watu wenye weredi na sio hao maafisa maendeleo ya jamii.

Kumbuka, ulimwaguza sirro amkamate gwajiboy akakugomea na hili vijana wako wamekugomea na Kuna dalili wamepigia noti.


Naomba ujiuzulu Kwa kuwa unatoa amri zisizotekelezeka.

Mchizi amesema mtoto aolewe wazaz wakiridhia, sheria haisema waziri akiridhia.


Rekebisheni kwanza sheria mnawasumbua polisi Bure, na watawagomea kistaarabu.



Umeshindwa, jiuzulu uwaziri Dr Gwajima d
 
Hapo shida sio umri pekee, shida ni kwamba binti mwenyewe hajaridhia na hayuko tayari kuolewa!
Sheria ya ndoa inasema Wazazi wakiridhia na si mtoto akiridhia.Halafu mtoto ambaye haruhusiwi kupiga kura, kuendesha gari kunywa pombe iweje awe na ridhaa kwenye suala kubwa kqma ndoa? Tukubali tu sheria ya ndoa ni mbovu. Tunajua serikali inaogopa kufanya mabadiliko ya hicho kifungu kutokana na shinikizo toka kwenye makundi ya dini ambayo kwa mujibu wa viongozi hao wa dini binti wa miaka 14 ni sahihi kuolewa k
Hapo shida sio umri pekee, shida ni kwamba binti mwenyewe hajaridhia na hayuko tayari kuolewa!
Sheria ya ndoa inasema Wazazi wakiridhia na si mtoto akiridhia.Halafu mtoto ambaye haruhusiwi kupiga kura, kuendesha gari kunywa pombe iweje awe na ridhaa kwenye suala kubwa kama ndoa? Tukubali tu sheria ya ndoa ni mbovu. Tunajua serikali inaogopa kufanya mabadiliko ya hicho kifungu kutokana na shinikizo toka kwenye makundi ya dini ambayo kwa mujibu wa viongozi hao wa dini binti wa miaka 14 ni sahihi kuolewa kwa mujibu wa sheria za dini.Hivyo serikali imeufyata inaogopa mgogoro na na wana dini kwani hata ilipotungwa sheria hiyo ya ndoa mwa 1971 lengo lilikuwa kuwaridhisha wana dini ambao dini yao imeruhusu kitu hicho,..ndio maana tangu serikali iliposhindwa kwenye kesi ya Rebecca gyumi na kuambiwa ibadili umri wa mtoto kuolewa hadi miaka 18 serikali imepata kigugumizi kupeleka muswada bungeni wa mabadiliko ya sheria hiyo.
 
Back
Top Bottom