Urais CHADEMA it's like a death sentence!


Tunavitazama vyama vyote bila kuiacha chadema pembeni humu ndani,usivunje kioo ndio sura yako ilivyo,namaanisha usituchukiea sisi kwa kuiweka hadharani sura halisi ya chama chako,unachotakiwa ni kujiuliza mara mbili kwanini hali hiyo inakikumba chama chako?ni wazi kuna tatizo,shiriki kulitokemeza ili kurejesha demokrasia ya kweli nadani ya chama cha demokrasia..!
 
Urais wa CDM 2015 HAUEPUKIKI. Soma alama za nyakati. Hata mabwana zako CCM wameshaliona ndo maana wanajiandaa kuwa wapinzani. Au hufuatilii yanayojadiliwa kwenye vikao vyenu?

CHADEMA NI KAMA CHELSEA!
kwanini mnawaziba midomo wanachama wenu wanapojaribu kusema mipango yao ya kisiasa ya huko mbele?ndio hoja ya msingi hapa
 
Kwani nyie mlimkata jina eti alitaka kupora urais wa JK?.Si mngemwacha atumie haki yke kidomokrasi
Hakuambiwa aondoe jina lake kama zitto,vikao vya maamuzi ndio hujadili na kumpitisha mgombea anaeonekana kuwa bora,shibuda alikua bora ccm lakini bahati mbaya kwake kulikua na mgombea alionekana bora zaidi yake,kwanini na nyie msimuache then mkaenda kumchinjia kwenye vikao vyenu vya maamuzi,si mnavyo?mlikua na haraka gani?
 

Kwa hiyo wewe unajifanya huoni kama yanafanana na ni muendelezo wa yale yale ya liyowakuta zitto na marehemu chacha wangwe?

chadema kubalini kwamba kuna tatizo hapo ili muweze kulitatua,ubishi hautowasaidia kamwe
 
Hoja sio Shibuda kutaka kugombea urais,bali Shibuda kukidhalilisha chama mbele ya viongozi wa ccm,kwa kusema kuwa hakuna chama ambacho kinaweza kushika dola zaidi ya ccm,Je anafanya nini ndani ya CHADEMA kama anaamini ccm ni bora?

Hata lowassa huwa anaikosoa ccm hadharani na nyie huwa mnakenua wakati sisi huwa tunaamini anatimiza wajibu wa kukipa chama chake challlenge ili kijiimarishe,the same to bwana magale shibuda john,haitasaidia kumfukuza bali kuifanyia kazi kauli yake kwa kubadilika
 
Uroho wa madaraka na kukariri kuwa rais lazima awe fulani ndo' kunaondoa Demokrasia!
CDM tumekuwa tunapambana ili wananchi wawe na demokrasia ya kweli, ya nin kupiga kelele kwa sababu tu ni shibuda?
Kwani yeye hana haki kikatiba kugombea?
Tuache Demokrasia ifanyekazi cyo kubwabwaja kama Heche ili kuwafurahisha wakubwa.
 
Nilifungua post yako kwa spidi saaana, alafu nakutana na mambo ya nafsi ya m2 ilio megeka!! wewe ni 1 wawalio sema CDM itashindwa vibaya arumeru leo tena unakuja na mengine, hisia haziwekwi hewani kizembe hivi ndugu, peleka kwenye udaku kuuule!!
 

Ebwana siku hizi kuna mpaka kuoteshwa kuwa Rais ( please Refer Mr membe )
 
Ni nani asiye jua kuwa Shibuda ni kada nambari wani wa ccm? Shibuda kaja cdm kwa malengo yake makuu nayo ni kuivuruga cdm lakini anapaswa elewe kuwa cdm ina watu makini na waelewa zaidi yake hivyo hawezi kitu ameshtukiwa. Njama zenu twazijua kitambo
 
Lema anasema akina Lowasa, Sita na Mwakyembe wanaenda CDM sasa hao watapewa nafasi gani? kama mtu akitangaza urais inakuwa shida namna hiyo?
 
Wewe kama si gamba, basi hujui maana ya kanuni na taratibu. Soma vizuri hotuba ya mwenyekiti wa bavicha arusha na singida. Kama huelewi uliza.
 
Shibuda ana haki ya kutangaza nia ya kugombea uRais wa JMT .Huu ni mwaka 2012 bado miaka mitatu kufikia mwaka 2015 mwaka wa uchaguzi Tanzania.

Mpaka sasa Mheshimiwa Shibuda amekosa umakini/mikakati ya dhati katika mipango yake ya kugombea urais kupitia CDM.Mtu makini mwaka 2012 si mwaka wa kutangaza nia ya kugombea uRais toka sasa hadi kufika mwaka 2015 yatatokea mambo mengi yamkini kufikia 2015 CDM kama chama kinaweza kupoteza mvuto uliyonayo sasa.

Njia aliyotumia Mh Shibuda si sahihi hata kidogo sana sana namwona anatafuta umaarufu/anatumiwa ili kufikia malengo fulani ambayo kwa mtu makini au chama makini hakita angaika/jishuhulisha naye hata kidogo.Bahati mbaya CDM kimekosa umakini na umahiri kitaangaika na Mh Shibuda na mwisho wa siku kitasahau ajenda zake muhimu kwa waTanzania.Ajenda muhimu wakati huu ni katiba mpya masuala ya uRais yawekwe kando.
 
Weweee acha kauli makamasi kama hizi. Unapoongelea tazama nyakati na namna watu hao wanapotangaza kufanya hivyo, uwa ni kama wana ajenda ya siri ya kuvuruga jambo fulani. Tazama Zitto Kabwe, yeye alitangaza kuutaka uraisi wakati chama kipo kwenye mapambano ya uchaguzi kule Arumeru Mashariki na kwenye uchaguzi wa madiwani kwenye karibia kata 9. Haiwezekani watu wapo vitani wewe unakaa kuwaza namna ya kuuchukua uraisi. Hii ingeweza leta mgawanyo na makundi wakati wakati ule umoja ulikuwa ni wa muhimu sana kuliko wakati mwingine wowote.
Haya huyu Shibuda yeye ndio katoa kali ya mwaka, anakwenda kutangaza kuutaka uraisi akiwa kwenye kikao cha CCM, na anawaambia wana CCM kuwa hakuna chama kingine chenye uwezo wa kushika dola zaidi ya CCM, na anaomba Jakaya Kikwete awe kampeni manager wake. Hivi kama hakuna chama chenye uwezo wa kuongoza zaidi ya CCM anataka kugombea CDM kwanini? Kwanini asigombee kwa kupitia CCM?
Sasa mazingira na nyakati ambapo watu hawa walitoa matamko yao ndio tatizo na watu wanawapinga zaidi kwa hilo na sio kauli ya kuutaka uraisi, ukitazama tamko la BAVICHA linasema wazi kuwa wanaumia kwasababu ya Shibuda kwenda kutoa kauli akiwa kwenye vikao vya CCM na tena akaenda mbali kudai kuwa CCM ndio chama imara kwasasa hapa nchini. Demokrasia sio vurugu na kutofata utaratibu.

VIVA CHADEMA.
 
Na ile ya chacha wangwe na zitto kabwe je?

Unataka kwenda nyuma Jinsi CCM kugombea Urais? Haujui ni Cult? Haukumbuki yaliyompata Paul Sozigwa? Salim A. Salim

Majina ni Marefu haswa, na wameapishwa wakiondoka hiyo Cult au kuisema vipaya yatawapata ya Sozigwa
 
jaman tusiwe mashabiki wa sias kama mpira hata cdm wanakuwa wrong muda mwingine kwa hiyo msimvamie mtu katoa idea yake aand he is right
 
Sioni shida Shibuda kutangaza nia ya kugombea urais. Ila sidhani kama alikuwa serious na tangazo lake hilo hasa ukizingatia kuwa alilihusisha na wapinzani wakuu wa chama chake yaani CCM.

Ila sipendi jinsi washabiki wa chadema wanavyokuwa mstari wa mbele kumrushia maneno na hata matusi yeyote anayehoji maaamuzi ya chama chao. Sidhani kama hii ni njia nzuri ya kuwashawishi wafuasi wa vyama vingine na hasa wale wasio wafuasi wa chama chochote cha siasa kuwa chama chao ni makini.

Ujumbe kwa wana CHADEMA: Sio kila anayehoji mambo ya CHADEMA ni CCM au Gamba kama mnavyopenda kuwabatiza. Kuna wengine ni wazalendo wa nchi hii na wangependa mabadiliko ya kweli. Ila wanahitaji assurance kuwa kweli CHADEMA inasimamia hayo mabadiliko wanayoyahitaji.
 

Hii Tata ni gari au tata baba kwa kikurya? Mkuu umenena vyema sana hasa hapo kwenye ujumbe. Assurance kwamba CDM ni chama makini kuliko vyama vyote nchi ni muhimu sana siyo tu kwamba CDM ni kimbilio la Watanzania. Isije ikawa kwamba vyote vibaya lakini afadhali CDM hawajatawala tuwajaribu. Waonyeshe kwamba siyo chama cha kujaribiwa bali chama tofauti na CCM.
 
Last edited by a moderator:
Bahati mbaya sana niko tofauti na wengi,sipo hapa ku win applouse but to speak the truth na yale ambayo watu hawapendi kusikia,that's my principle since day one najiunga jf
Hawa wasema kweli wa karne hii bwana, yaani watu wasichopenda kusikia ndio the truth?
 

umetumwa?
 
kwani si shibuda huyuhuyu alitangaza kupitia ccm, mbona aliomba msamaha? Kwa nini aliomba msamaha? Halafu ndugu, cdm ni watu kama wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…