Urais CHADEMA it's like a death sentence!

Hivi kuna shida gani mtu kutangaza kwamba anataka kugombea Urais. Kuna watu ambition yao ni Urais hivyo wakati wote wanaota kuwa Marais. Zile habari za kwamba muda wa kutangaza bado zimepitwa na wakati. CDM na hata CCM ziwaache watu wenye nia watangaze nia zao ili tupate muda mrefu wa kuwapima na kuwajadili kwa mapana na marefu. Masuala ya kuutaka Urais kwa staili ya nataka sitaki ni uzandiki. At least kwa sasa najua kuna watu wawili CDM wametamka kwamba watagombea kwa kufuata utaratibu wa chama wengine wanaotaka nao watamke na siyo kujiundia makundi kimyakimya. Hayo makundi siku yakilipuka utakuwa ndio mwisho wa chama.
 
Uko sawa mkuu! Mimi nashangazwa sana Na hizi kelele... Sijui wanamtaka mtu wa aina gani? Hawataki challenge kabisa....
 
hivi ccm nbona mna maneno, wenyewe kwa vijembe mnaongoza tukiangalia tukio linalokuja la 2015 mnababaika kwa kuwa na majungu mnawasabisha LOWASA NA SITTA kwa kutokuwa na amani mbona hilo hamlizugumzii na hata MWAKYEMBE akawa hatiani hivi hili hamlioni ?
 
Africa yote ni sawa, viongozi wote wa Africa wanafanana. Ni waroho wa madaraka, ni wagumu kuwajibika. Kama ilivyo kwa nchi zingine, tumeshuhudia vyama vya upinzania vikichukua nchi vinafanya yale yale ya chama kilichokuwa madarakani, muda wa kutoka ukikaribia ni vurugu na mfano wa karibu ni jirani zetu wa-Kenya.

Pia kuna kitabia cha mpinzani akishindwa analalamika, akipewa madaraka ya umakamu, au uwaziri mkuu hukaa kimya na huasi mapambano dhidi ya serikari. Tuna mifano rahisi Kenya-Odinga, Zanzibar-Seif, Zimbabwe etc.

Huwa sielewi hii yote ni kwa sababu ya umaskini, ujinga au ulimbukeni? Chadema unayoiona leo, siyo Chadema utakayoiona itakapochukua madaraka.
 
Urais wa CDM 2015 HAUEPUKIKI. Soma alama za nyakati. Hata mabwana zako CCM wameshaliona ndo maana wanajiandaa kuwa wapinzani. Au hufuatilii yanayojadiliwa kwenye vikao vyenu?

CHADEMA NI KAMA CHELSEA!
 
Mkuu Kanigini upo sahihi. CDM inabidi wakubali challenge na wawe wapambanaji wanaopalilia demokrasia. Kwenda ikulu sawa lakini tusije kuishia kusema afadhali wakati wa ukoloni (CCM). Ninachokiona ni watu kuichoka CCM lakini huko wanakokimbilia nako sioni usalama wowote. Namkumbuka Mathew Kerekou aliruhusu vyama vingi nchini kwake wakafanya uchaguzi wakamuondoa kwa hasira tu. Waliochukia wakaka miaka minne watu wakamkumbuka Gen. Kerekou wakamtaka agombee, akagombea akashinda na kirudi ikulu. Wananchi wale waliponzwa na hasira. CDM ijitofautishe na CCM ili kiwe chama kimbilio. Hii hali ya sasa ya kusema huyu si kiongozi bora alishinda tu kwa sababu alisimamishwa CDM. Hii inaonyesha kuwa huko CDM hakuna viongozi makini bali wanachaguliwa tu kwa sababu ya watu kuichoka CCM. Angalia comments kuhusu Diwani Matata na huyu Shibuda.
 
Last edited by a moderator:
Nimefurahi watu walivyokupuuza tangu asubuhi ni watu 10 tu wamechangia huu uchafu wako na wote wamekupinga.
Hatujampinga kasema ukweli ukitaka kuwadhi CDM gombea ngazi ya juu mfano Wangwe Zito Shibuda km ni demokrasia mnakasirika nini sio mara ya kwanza Shibuda kuomba nafasi ya urais hata alikokuwa alifanya hivyo na demokrasia ilimruhusu
 
Hatujampinga kasema ukweli ukitaka kuwadhi CDM gombea ngazi ya juu mfano Wangwe Zito Shibuda km ni demokrasia mnakasirika nini sio mara ya kwanza Shibuda kuomba nafasi ya urais hata alikokuwa alifanya hivyo na demokrasia ilimruhusu

NI mara mia ukamchezea simba sharubu kuliko kutangaza au kuonyesha nia ya kugombea urais au umwenyekit na hasa kama siyo wa ukanda huo
 
Lkini shibuda kasema atamuomba slaa awe meneja wake wa kampeni za urais,kuna dhambi gani?kwanini msimuache atumie haki yake then mkutane nae kwenye vikao vya kuchuja wagombea?Heche na genge lake walikua na haraka gani nae kama sio uoga tu?

Kwani nyie mlimkata jina eti alitaka kupora urais wa JK?.Si mngemwacha atumie haki yke kidomokrasi
 
wasaidizi wa ghadafi hata walipoona utawala unazama waliendelea kujitia moyo mpaka walipoanguka puuuu. si ccm endeleeni kujitia moyo.mimi ni msukuma nipo magu cdm ipo juuu sana wala hakun uchaga hapo

Mimi pia Msukuma asili ya Kishapu ila naishi mbeya.Sisi huku CDM ni mlima Everest.
 
Tusipende siasa za fitina na majungu, chadema hawamuandami shibuda sababu katangaza nia ya kugombea urais, kikubwa mimi ninacholiona hapa ni matamshi yake ya kusema hakuna chama chochote kinachoweza kutawala tanzania isipokuwa ccm, hapohapo anatangaza kugombea kwa tiketi ya chama cha chadema.

Hayo mambo ya marehemu chacha wangwe na zito yanahusika vipi na mada hii ya shibuda?.
 
shibuda sifa mojawapo ya kuwa rais chadema hana. anatoka shinyanga.

hata zitto anajisumbua, hana sifa, anatoka kigoma. kazi yao ya juu ni ubunge na kuongeza ruzuku ya chama.
 
Hoja sio Shibuda kutaka kugombea urais,bali Shibuda kukidhalilisha chama mbele ya viongozi wa ccm,kwa kusema kuwa hakuna chama ambacho kinaweza kushika dola zaidi ya ccm,Je anafanya nini ndani ya CHADEMA kama anaamini ccm ni bora?
 
Lkini shibuda kasema atamuomba slaa awe meneja wake wa kampeni za urais,kuna dhambi gani?kwanini msimuache atumie haki yake then mkutane nae kwenye vikao vya kuchuja wagombea?Heche na genge lake walikua na haraka gani nae kama sio uoga tu?

Shibuda halaumiwi kwa kutangaza nia ya kugombea Urais (kwanza kila mmoja anajua kuwa hakuna uwezekano katika ulimwengu huu Shibuda kuwa Rais kwa kupitia chama chochote!), bali analaumiwa kwa kudharau vyama vya upinzani kuwa havina uwezo wa kuongoza Taifa, na wakati huo huo kwa upungufu wa kichwani kwake, anasema atagombea Urais kupitia vyama hivyo hivyo vya siasa alivyosema havina uwezo wa kuongoza Taifa. Huyu anavikejeli vyama vyama vya upinzani, nafasi ya Urais na Watanzania. Jambo la muhimu ni kwa CHADEMA kukubali kuwa wana mbunge ambaye hakustahili kuwa mbunge wa chama chochote, njia nzuri ni kumpuuza. Kosa lilikwishafanyika la kumpa huyu Bwana nafasi ya kugombea ubunge kupitia CHADEMA. Hili ni funzo kwa CHADEMA juu ya umuhimu wa kuyachunguza na kuyachuja vizuri magamba yanayotaka kugombea nafasi za uongozi kupitia chama makini kama CHADEMA. Watu kama akina Shibuda wanashusha hadhi ya chama.
 
Dua la CCM haliipati CHADEMA na dua la Kim humpata mwenyewe. Mawazo mengine hata kama ni haki kuwa nayo yana taabu tu. Anyway huenda uko sawa ingawa nina wasi wasi.
 
SUALA SIO SHIBUDA KUTANGAZA NIA YA KUGOMBEA URAISI
SOMENI HILI TAMKO LA BAVICHA VIZURI:
BAVICHA imepokea kwa mshituko mkubwa kauli ya ndugu Shibuda kuwa yeye atagombea Urais na Meneja wake wa Kampeni atakuwa Mwenyekiti wa CCM ndugu Jakaya Kikwete, na alitoa kauli hiyo kwenye kikao cha NEC ya CCM.
MAMBO YAFUATAYO YEMETUSHTUA;
1. Katoa Kauli hiyo kwenye kikao cha NEC ya CCM
2. Meneja wa kampeni zake amemtangaza kuwa ni Mwenyekiti wa CCM taifa Jakaya Kikwete
3. Amesema kuwa hakuna chama kingine chenye uwezo wa kuiongoza nchi kwa sasa
4. Alitoa tamko hilo kwa niaba ya APRM .
Mambo hayo manne ndio yametushtua na kutufedhehesha sana sisi vijana wa CHADEMA na ndio maana tumelazimika kutoa kauli kuhusiana na suala hili , na kauli yetu ni kama ifuatavyo;
1. Kamwe BAVICHA hatutaruhusu mgombea Urais wa CHADEMA meneja wake wa kampeni awe ni Mwenyekiti wa CCM hata siku moja kwani tunao watu wa kutosha na wenye uwezo wa kutosha kuifanya kazi hiyo na hatuhitaji msaada huo .
2. Kamwe hatutaruhusu mgombea urais wa CHADEMA awe anatangaza nia kwenye vikiao vya CCM kwani hawana mamlaka ya kumteua mgombea wa CHADEMA na kama Shibuda alikuwa halijui hilo anapaswa kulifahamu kuanzia sasa kuwa vijana wa CHADEMA hatuchaguliwi mgombea na NEC ya CCM kwani CHADEMA kuna vikao na taratibu zetu za kuteua wagombea.
3. Kusema kuwa hakuna chama kingine chenye uwezo wa kuongoza nchi ni kutudhalilisha sisi vijana wa CHADEMA na watanzania wote ambao leo wanaiona CHADEMA kama tumaini pekee la kuwakomboa, kauli hii tunaamini kama vijana wa CHADEMA kuwa mamlaka za nidhamu hazitakaa kimya na kuiachia kauli ya namna hii iachwe bila kutakiwa maelezo ya kina , tutaitisha kikao cha BARAZA na tutaijadili kauli hii na kuwasilisha mapendekezo yetu kwenye vikao halali vya chama .
4. Tunapenda kumwambia kuwa kama anaona kuwa yeye haendani na utamaduni wa chama chetu na anakiona kuwa hakina uwezo wa kuongoza dola anafanya nini kwenye chama ambacho anona kuwa hakiwezi kuongoza dola? Kwanini atafute urais kwenye chama ambacho anaona hakiwezi kuongoza dola ? anawatania watanzania? Ni heri akaenda kwenye hicho ambacho anaamini kuwa kinaweza kuongoza dola , kwani lengo la chama chochote kile ni kuchukua dola na sio vinginevyo.
5. Mwisho tunapenda kuwahakikishia vijana wote wa Tanzania na wananchi kwa ujumla kuwa tayari CHADEMA kimejiandaa kikamilifu kuongoza dola na wasiwe na hofu na maneno yaliyotamkwa na Mbunge huyu .
6. Natoa wito kwa Vijana wenzangu wote wa CHADEMA kuwa sasa tujiandae kikamilifu katika kukabiliana na mtu yeyote yule ambaye ataonekana kuwa kikwazo kwa chama chetu na wananchi kwa ujumla wake katika kuelekea kuchukua dola 2015 .
Nawatakia kila la kheri katika ujenzi wa chama na tuendeleze operesheni ya ‘Vua Gamba, Vaa Gwanda’ popote pale tulipo nchini.
Imetolewa leo Dar es Salaam, Mei 16, 2012 na;
John Heche
Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa.
 
Huu ni ukweli ambao wengi wenu humu hamtaki kuusikia!!! Umesema sawa kabisa. Chadema pale kila mtu ana personal interest yake.. Soon utaona kila mtu anachukua chake akalale.. Chadema njaa tupu!!! Na tupo hapa mtasikia tu mpasuko wa chama cha demokrasia na maendeleo kwaajili ya vijimambo vyao hivi hivi... Kwanza majembe ni machache sana pale wengi wa wabunge wao ni ma mediocre... Wameoana wenyewe kwa wenyewe, wanakulana wenyewe kwa wenyewe yani na nchi sasa wanategemea kuindesha kienyeji enyeji.. They need to strategise theIr priorities and objectives if they seriously want to be the #change
 
Hivi kuna shida gani mtu kutangaza kwamba anataka kugombea Urais. Kuna watu ambition yao ni Urais hivyo wakati wote wanaota kuwa Marais. Zile habari za kwamba muda wa kutangaza bado zimepitwa na wakati. CDM na hata CCM ziwaache watu wenye nia watangaze nia zao ili tupate muda mrefu wa kuwapima na kuwajadili kwa mapana na marefu. Masuala ya kuutaka Urais kwa staili ya nataka sitaki ni uzandiki. At least kwa sasa najua kuna watu wawili CDM wametamka kwamba watagombea kwa kufuata utaratibu wa chama wengine wanaotaka nao watamke na siyo kujiundia makundi kimyakimya. Hayo makundi siku yakilipuka utakuwa ndio mwisho wa chama.

Tatizo watu wanapenda kusikia ule uongo wa "nimeombwa nigombee"..mambo hayo hayana nafasi kwa kuwa unakuwa ni unafiki.
 
Back
Top Bottom