Urafiki umeisha kisa gari

Urafiki umeisha kisa gari

Apendeki2

Senior Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
161
Reaction score
77
Mtu siku zote ukiwa mkweli unakuwa huru.
Nilikuwa zangu kwenye daladala natoka town nikakutana na baba mmoja wa makamo.

Tukapiga stori tukapeana namba za simu.
Tulipofika mwisho wa gari akaniambia ngoja nikafuate gari langu nililiacha sehemu. Nikamwambia poa

Tumeendelea kuwasiliana ila kila nikimchokoza khs gari anakuwa mkali. Nikimwambia nataka twende wote mjini visingizio.

Akiwa mjini akakwambia yupo na gari ukimwambia na wewe upo mjini akusubiri anapotea hewani. Na mifano mingi nisiwachoshe.

Sasa kubwa ni pale aliponiambia yupo njiani anaenda mjini nikamuona kapanda daladala kiti cha mbele kaweka kushoka tangu hapo no communication.

Jamani kuwa mkweli ili uwe huru.
 
jinsia yako kama ni Ke hizo zilikuwa swaga za kukuingiza tunduni tu kwa hiyo umekatiza mawasiliano kisa hana gari hahaa ulimpendea gari ndo iliyokuvutia eeeh
 
Nshamaliza mie.
Unajua kawimbo flani; 'mbuzi karanga bei ganiiiii? Chuma beeee'

Ha ha haaaaaa we mi ndio mana nakupenda bure saaanaaaa!!!

Kwanini unauza chuma bee??!!!
Nisameheee!!!

Umenifanya siku hii niianze kwa furaha ya enzi za utoto!!!
 
Awe na gari au asiwe na gari kinachokukera wewe ni kipi?

Btw mbona mara ya kwanza aliposhuka kwenye daladala kufuata gari lake wala hukumtilia shaka....

Lakini uliponyimwa lifti na kumuona kwenye daladala ndio waanza zogo, je unajuaje kama mzee huyo hutumia utaratibu uleule kama aliokuambia siku mwakutana!!!
 
jinsia yako kama ni Ke hizo zilikuwa swaga za kukuingiza tunduni tu kwa hiyo umekatiza mawasiliano kisa hana gari hahaa ulimpendea gari ndo iliyokuvutia eeeh

Siyo kuwa mimi ndo nimekata mawasiliano. Yaani tangu aliponiambia yupo njiani anakwenda mjini na anadrive ghafla tukaonana yy mwenyewe ndo kakata mawasiliano. Ukipiga apokei ndo maana nikasema anakosa uhuru.
Mimi sina gari kwa hiyo awe na gari asiwe nalo mimi sina shida kwani si kigezo cha urafiki
 
Hiyo para ya mwisho mbona alikujibu vizuri tu, acha kulalamika. Au kila kitu amekukopa? Kama Apendeki2 kelele za nini?

Yawezekana hujajua ninachokilalamikia.
Niaminivyo mimi km asingesema ana gari huyu mtu angekuwa na uhuru zaidi. Ila amekosa kuwa huru kutokana na hofu hiyo.
Na kitendo cha kunibia anadrive nikamuona kwenye daladala kilimfedhehesha sana. Kwa misingi hiyo ndo maana nasema akakata na communication ukipiga hapokei.
 
Last edited by a moderator:
Ndugu mleta mada wewe ni Jinsia gani?

Itakuwa jinsia ya kike, na alikuwa ameshamkubali jamaa! Ila sasa inashindikana kwa sababu swaga za jamaa zimefeli na jamaa anaona soo kuendeleza mawasiliano.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom