MwafrikaHalisi
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 1,741
- 511
Kwa jinsi ambavyo ndugu zangu, wanachama na washabiki wa CUF wanavyoupamba uprofesa wa Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF napatwa na shaka.
Sitaki kuamini kwamba uprofesa wa mtu ndio unampa kigezo cha kuwa na uwezo wa kuongoza watu au nchi. Lakini wenzetu wanataka tuamini hivyo.
Wanataka tuamini hakuna sifa nyingine inayoweza kumpiku mtu aliyebobea katika uchumi na pengine kufanya kazi na IMF.
Hii dhana inatuambia kitu kuhusu watu ama viongozi waliomo katika chama cha CUF. Inatuambia kitu kuhusu wanachama na washabiki wake. Ng'amua.
Jambo moja la msingi: UONGOZI HAUSOMEWI!
Kwahivyo ndugu zangu, kama mnataka kunishawishi nimchague Prof. Lipumba kwenye kinyang'anyiro cha Urais mwaka 2015, naomba mnipe hoja nzito zaidi ya uprofesa wake katika uchumi. Nawasilisha.
Sitaki kuamini kwamba uprofesa wa mtu ndio unampa kigezo cha kuwa na uwezo wa kuongoza watu au nchi. Lakini wenzetu wanataka tuamini hivyo.
Wanataka tuamini hakuna sifa nyingine inayoweza kumpiku mtu aliyebobea katika uchumi na pengine kufanya kazi na IMF.
Hii dhana inatuambia kitu kuhusu watu ama viongozi waliomo katika chama cha CUF. Inatuambia kitu kuhusu wanachama na washabiki wake. Ng'amua.
Jambo moja la msingi: UONGOZI HAUSOMEWI!
Kwahivyo ndugu zangu, kama mnataka kunishawishi nimchague Prof. Lipumba kwenye kinyang'anyiro cha Urais mwaka 2015, naomba mnipe hoja nzito zaidi ya uprofesa wake katika uchumi. Nawasilisha.