Upotoshwaji Kuhusu ya Mahakama za Kadhi

Mimi swali langu ni moja ni moja tu, nimeelewa kiasi umuhimu wa mahakama ya kadhi:
kama mtu aliwahi kuwa muislamu, atafanya vipi kama hataki kuhukumiwa na hio sheria, mfano ameamua kuacha dini hio na kubadili dini au kuwa mpagani.
Je familia zenye mchanganyiko wa dini mojawapo ikiwa ya kiislamu, zinahusishwa vipi na hii mahakama


A kama ninaa mzazi mmoja muislamu, mwingine mpagani, ninahusika na hii mahakama?
Yani kwa maneno mengine nauliza hii mahakama inachaguaje watu wa kupokea kesi zao? je hata ndugu, marafiki, maadui wanaweza kuamua kunishtaki katika hii mahakama simply tu kwa kuwa nilishawahi kuwa na historia ya kiislamu? Yani mahakama itafanyaje kazi katika nchi hii ambako tumejichanganya na wengi tumeacha dini zetu?

.........ulipata wapi maelezo kuwa Mahakama hiyo itawashurutisha watu !
Tukisema kuwa 'Mahakama ya kadhi' ni ibada hamuelewi !.............hivi kuna Waislaam wangapi wa kuzaliwa Baba na Mama, Bibi na Babu lakinini hawafanyi 'ibada ya kuswali' !?
Halazimishwi mtu yeyote kujihusisha na Mahakama hiyo kama hataki 'ibada' hiyo kama mtu mwingine anavyokwepa ibada ya kuswali.

Kiislaam ndoa inayotambulika ni ya Muislaam kwa Muislaam mwenziwe, na imefungwa kwa taratibu za Kiislaam.
Muislaam anayesema kaoa asiye Muislaam huyo ni mzinifu period !
Uislaam hauhangaiki (katika taratibu zake) na asiye Muislaam ! Haika
 
Last edited by a moderator:
Nimefikiria kwa kina sana kuhusu hiyo Kadhi. Achilia mbali kugharamiwa na Serikali, inaweza ikasambaratisha waislamu wenyewe kwa wenyewe badala ya kuwaweka pamoja. Na isitoshe inaweza kusababisha ndoa nyingi za waislamu na wakristo zikavunjika.
Na hii inaweza kuwafanya hata kwa baadhi ya walio waislamu kwa sasa wakakimbia dini yao wakiona hiyo mahakama inawanyima uhuru wa baadhi ya vitu walivyokuwa wanafanya hapo awali bila bughudha.

Kwa kuhitimisha ni kwamba hii Mahakama inafaa kwa nchi ambazo wakazi wake wengi ni Waislamu, ndo itafanya kazi vizuri. Lakin kwa hapa Bongo, mtu akichoshwa na masharti ya Kadhi, ana hamia Ukristo, anaendelea kupata uhuru wake wa awali

.........kwa hiyo wewe ndio unajua zaidi kuhusu Waislaam kuwa 'ibada' yao ya kupitia Mahakama ya Kadhi ni kero !?
Uislaam unahusika vipi na ndoa ya Muislaam na Mkiristu wakati katika Uislaam ndoa hiyo haitambuliki na hao watu wana hadhi ya 'wazinifu' !?
Unajua unacho ongea au unaropoka tuu ! CPU
 
Last edited by a moderator:
1. Zimekuwa zikitolewa kauli mara kwa mara kwamba kuna watu wasiowatakia mema waislamu kiasi kwamba hawataki wawe na Mahakama za Kadhi ambazo ni sehemu ya Ibada zao! Kauli hizo zimekuwa zikipotosha ukweli ama kwa makusudi au kwa kutokujua juu ya jambo hilo. 2. Mara kwa mara linapotokea suala la Kadhi utasikia suala la Ubalozi wa Vatican likijitokeza kama vile Ubalozi huo unagharimiwa na Serikali ya Tanzania. Hata hivyo suala la Balozi nyingine ambazo nchi zao au Serikali zao ni za Kidini halizungumzwi kabisa, it is a one sided story! 3. Suala kubwa toka kwa watu wasio Waislamu ni kwamba Mahakama hizo ziruhusiwe, kwa kuwa ni haki kwa Waislamu kuwa nazo, hata hivyo sijui kama wameangalia kwa marefu na mapana juu ya mahakama hizo! (a) Tumesikia kwamba Mahakama za Kadhi zitahusu Ndoa, Talaka na Mirathi tu. Ukiangalia kwa haraka haraka ni kama vitu vyenyewe si vizito sana kuingizwa kwenye Sheria zetu za kawaida na kushughulikiwa na Majaji wetu kama zilivyoingizwa Sheria nyinginezo. Hata hivyo katika kuonesha kwamba hii ni sehemu ya Ibada ya Kiislamu hawataki suala hili kushughulikiwa na watu wasiokuwa Waislamu! Kwa uelewa wangu mdogo ni kwamba waislamu wanataka kufanya mambo yao bila kuingiliwa na Serikali. (b) Hata hivyo, inavyoonekana mambo sivyo yalivyo. Ukiangalia Mahakama za Kadhi kwa Zanzibar, Chief Kadhi huteuliwa na Rais wa Zanzibar. Kwa Zanzibar sina neno sana kwa kuwa 99% ya Wazanzibari ni Waislamu, kwa hiyo probability ya kuwa na Rais mwislamu ni kubwa. Hata hivyo akitokea Rais ambaye ni Mkristo itabidi amteue huyo CK bila kupenda! (c) Kwa upande wa uendeshaji wa Mahakama hizo kwa upande wa gharama, Waislamu wanataka Serikali ndiyo igharamie Mahakama hizo! Hapo ndio matatizo yanapoanzia! Kama nilivyosema kwamba Mambo ya Mahakama za Kadhi ni Ibada ya Waislamu. Ibara ya 19 (2) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 inasema kwamba "Kazi ya kutangaza dini, kufanya Ibada na kueneza dini itakuwa ni huru na jambo la hiari la mtu binafsi na shughuli na uendeshaji wa jumuiya za dini zitakuwa nje ya shughuli za mamlaka ya nchi." Kwa hiyo Serikali itakapotia mguu kugharamia Mahakama za Kadhi itakuwa imejiingiza kutangaza dini ya Kiislamu ambapo itakuwa ni kuvunja Katiba! (d) Pamoja na kwamba Mahakama za Kadhi zitajihusisha na ndoa kama nilivyosema hapo mwanzo, suala la ndoa ni pana. Ndio maana tumeona kwamba kuna Sheria za Kiislamu za KUPIGA WATU MAWE hadi kufa kwa kosa la uzinzi! Yapo pia makosa ambayo yanasema kwamba ni kosa kwa wanaume kuchanganyika na wanawake (haya yapo kwenye nchi za kiislamu, lakini msingi wake ndio huo). Suala la kujiuliza ni kwamba kama Mahakama za Kadhi zinaweza kuachiwa BAADHI YA MAMBO tu na mengine kushughulikiwa na Serikali (eg adhabu za kupiga mawe zisiwepo), Je, Mahakama hizo kwa nini ziwepo? Wasio Waislamu wanaona kwamba haya mambo ya Mahakama ya Kadhi ni NJIA YA KUISILIMISHA nchi baadaye! 4. Wasio Waislamu wanachotaka ni kwamba Waislamu waachiwe mambo yao wenyewe na Serikali isijiingize kwa namna yoyote ile katika kumteua Kadhi Mkuu (KM) au kuyagharamia! 5. Nchi za Nigeria, Somalia, Sudan na nyinginezo zimeingia katika migogoro ya kidini na hata kufikiria kuzigawanya baadhi ya nchi hizo ili Wakristo wakae peke yao, pia Waislamu wawe hivyo hivyo peke yao. Mauaji yasiyokoma, uchomaji Misikiti na Makanisa umetokea ili mradi tu kuonesha hasira walizonazo baadhi ya watu wa dini moja dhidi ya dini nyingine. 6. Zipo hoja ambazo zimetolewa kwamba baadhi ya nchi zina Mahakama za Kadhi lakini hakuna fujo za aina yoyote! Kwa mwenye macho ya kutazama na masikio ya kusikia hawezi kubishana na mimi kwamba kama Serikali itaamua kuibeba dini moja kwa maslahi ya dini hiyo tunao mgogoro mkubwa wa kidini katika siku za mbeleni, kwa sababu dalili zote zipo. Kila iitwapo leo amani ya nchi yetu inazidi kutoweka taratibu! Tutazame nchi yetu mambo yanavyokwenda badala ya ku-copy n' paste mambo ya nchi nyingine! Tukilazimisha mambo tutakuja kulia siku moja na hakuna pa kukimbilia maana kwa majirani zetu si wakarimu kama sisi, wanachukia mno wageni! 7. Amani yetu ni kama barafu, tusiiruhusu ikaanza kupigwa na jua itaanza kuyeyuka taratibu na mwisho wa siku tutakuwa na maji ya moto badala ya barafu! 8. Wasio Waislamu wanawatakia mema Waislamu, ndio maana wanataka Waislamu washughulikie mambo yao ya kiibada bila kuingiliwa na Serikali kiuendeshaji au kwa gharama kwa manufaa yao na bila kuvunja Sheria za Nchi, ikiwemo Sheria mama, Katiba! Naomba kuwasilisha, kwa mjadala zaidi, kama upo!
hapo juu umepatia! Ila hiyo signature yako pana utata mkubwa tu! Ndio sababu Mungu ametusisitiza kwamba 'wafu hawana sehemu kati ya walio hai!' kama ilivyo kwa wanadamu woote hatujakamilika ndivyo alivyo Nyerere, Mazuri mengi kayafanya pia mabaya mengi kayafanya! Basi tuendeleze yale mazuri yake na yale mabaya aliyo fanya, kama ameomba toba Mungu atamsamehe!
 
Hawa jamaa janja sana! Wanakupa mkono, ukiwapa, wanashika bega! Mwanzoni kabisa walianza na Mahakama ya Kadhi. Siku hazijaenda mbali wameshaongeza pia Mwaka Mpya wa Kiislamu ili uwe publis holiday. Wataenda taratibutaratibu... na hatimaye kuanza kukama watu mikono na kuwapiga mawe hadi kufa maana kwao si tatizo kufanya hivyo bali ndiyo kuishi dini yao.

...........kwani nyinyi ndio mnao toa hizo siku kuu !?.........tupeni basi kama na nyinyi mlivyo na yakwenu ya mwaka mpya ! Tatizo nini, uchoyo !? Magobe T
 
Last edited by a moderator:
Mkuu upo sahihi sana. Hawajui wafanyalo. Mimi ninaona ni kama aina ya kiubaguzi fulani. Na kama wanasema ni moja ya ibada za dini ya kiislam kuna haja gani ya kuhusisha serikali ili hali serikali yetu haifungamani na dini yoyote? Huko nigeria isijeonekana walianza tofauti sana na sisi. Tumshukuru mwl kwa kuliona mapema na kulifanya liwe lilivyo. Dini na serikali viwe tofauti. Kwani mbona wakristu wakikorofishana mume na mke huenda kwa padre au askofu? Kwa nini kadhi asiwepo but awe chini ya bakwata na si serikali? Kuna kitu kingine naona kinatafutwa underground ambacho hatukijui. Ningeomba watz tusicheze na hii amani iliyopo. Tukumbuke kuna watu wameoa waislam na wengine wakristu na kuolewa the same. Itakuwaje kama watakuwa wameanza kubaguliwa? Kama kuna mtu alieona sinema iitwayo sometimes in april au picha yoyote ile ya mauaji ya rwanda angejumbuka watusi walooa wahutu au the opp walivyoteseka. Kupewa panga umuue mwanao au mkeo ni kitu kigumu jamani. Na kama viongozh wetu wa serikali wanakujaga jf walifanzie kazi hili kwa haraka na bila kumuangalia mtu usoni. Hatufiki 2050 salama.[/QUOTE]

..........viongozi wako wamelifanyia kazi na Pinda kaahidi inakuja Mahakama ya Kadhi !
 
.........ulipata wapi maelezo kuwa Mahakama hiyo itawashurutisha watu ! Tukisema kuwa 'Mahakama ya kadhi' ni ibada hamuelewi !.............hivi kuna Waislaam wangapi wa kuzaliwa Baba na Mama, Bibi na Babu lakinini hawafanyi 'ibada ya kuswali' !? Halazimishwi mtu yeyote kujihusisha na Mahakama hiyo kama hataki 'ibada' hiyo kama mtu mwingine anavyokwepa ibada ya kuswali. Kiislaam ndoa inayotambulika ni ya Muislaam kwa Muislaam mwenziwe, na imefungwa kwa taratibu za Kiislaam. Muislaam anayesema kaoa asiye Muislaam huyo ni mzinifu period ! Uislaam hauhangaiki (katika taratibu zake) na asiye Muislaam ! Haika
wewe ni al buhtan! Allah anakwambia; 'it is not for us to speak of this. Praise to thee; this is awfull slender!' Q. al nuur.6! kama uislamu hauhangaiki ktk taratibu zake za ibada wala kulazimisha! Kwa nini mnalazimisha Serkali isio amini muumini, iwalipe mshahara wanaoendesha ibada yenu? Huoni huo ni ukafir?
 
Last edited by a moderator:
Kwakifupi waislam ni wabaguzi! Ubaguzi ni sehemu ya dini yao, bila ubaguzi hakuna uislam.......hawana wanachowaza kwenye rasim ya katiba zaidi ya mahakama ya kadh.......wanahis hii tanzania ni yao peke yao
 
Mwanzisha mada Aksante sana, maana hakuna hata mmoja aliyejibu hoja, zaidi ya kutapatapa, hii ina maana dawa imewaingia na sasa wenye "akili" wameishaelewa. Wao wanakuwa wa kwanza kupinga upendeleo kwa watu wengine, na hapo hapo wanakuwa wa KWANZA kutaka kupendelewa. Kinacho wazuia kuanzisha wenyewe ni nini? Maana kama kuna mmojawapo atakataa kukubaliana na hukumu zao, basi ijulikane hana imani katika ibada hiyo, simple. Kama wanataka hukumu zao zitambulike kwenye sheria za mahakama, hiyo ni hoja nyingine lakini serikali kuanzisha Kadhi court , ama cout zingine za dini yoyote, ni kitanzi kwa mstakabali wa amani ya nchi yetu.
 
.........kwa hiyo wewe ndio unajua zaidi kuhusu Waislaam kuwa 'ibada' yao ya kupitia Mahakama ya Kadhi ni kero !? Uislaam unahusika vipi na ndoa ya Muislaam na Mkiristu wakati katika Uislaam ndoa hiyo haitambuliki na hao watu wana hadhi ya 'wazinifu' !? Unajua unacho ongea au unaropoka tuu ! CPU
kama wewe huropoki, tubandikie humu Hukumu ya mzinifu na anae uacha uislamu!
 
Last edited by a moderator:
Hapo ndipo nawashangaa waislamu wa aina hii. Nani kakwambia mwaka mpya ni sherehe ya dini fulani? Au kinachowapumbaza ni kuona Wakristo wakisherehekea mwaka mpya kwa kufanya maombi na tamasha? Wametumia fursa hiyo tu, kumshukuru Mungu kwa kumaliza siku 395 basi no more. Ni kama unavyomshukuru Mungu kwa kumaliza siku moja. Hata na ninyi ni kosa kumshukuru Mungu kumaliza siku 395, nakuliombea Taifa? Siku serikali ikiifuta siku ya mwaka mpya, hakuna mkristo ataathirika maana si siku ya kidini upo? Basi kawaambie na wenzio, achene wivu wenzenu wanapotumia fursa ambayo hata ninyi mnayweza kuitumia bila shida.
...........kwani nyinyi ndio mnao toa hizo siku kuu !?.........tupeni basi kama na nyinyi mlivyo na yakwenu ya mwaka mpya ! Tatizo nini, uchoyo !? Magobe T
 
mbona wakatolic wana mahakama zao ndani ya kanisa kuanzia ngazi ya jumuia hadi ngazi ya mwisho vatican. na wala hazipo kikatiba na hazigharamiwi na kodi za wananchi. kwa nini waislam wasiwe na mahakama hiyo chini ya bakwata? mmmh i can smell something fishy down here.
 
Back
Top Bottom