kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 12,313
- 12,607
Wacha wabunge wa wapinzani washiriki vikao vya bunge lijalo, na ikiwezekana wapeleke majina ya watu wa ubunge wa viti maalumu. Maana kuhudhuria au kutokuhudhuria hakusaidii kuimarisha demokrasia wala vyama vya upinzani wala kubadilisha siasa za Tanzania.
CUF walifanya hivyo mara nyingi bila kuzaa matunda yoyote. Wabunge wa upinzani wamekuwa wakisusia vikao vya bunge mara kadhaa lakini sikuona walichofanikisha sanasana kujinufaisha wao wenyewe kiuchumi.
Itakuwa ni kuwanyima fursa wabunge wa upinzani waliochaguliwa kama tutasema wasihuhudhurie pia bunge. Hata wakisusia hawana uzito wowote wa kubalidisha mambo zaidi ya kuwakosesha fursa yao ya kiuchumi, kisiana na kijamii.
Vyama vijipange upya kwa 2025 kwa kufanya yafuatayo:
1. Kueneza vyama vyao hadi vitongojini.
2. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanajiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kupiga kura wakati utakapowadia.
3. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanakwenda kupiga kura wote siku ya kupiga kura.
4. Wahakikishe kuwa wakati wa kujaza fomu za kugombea kuna watu maalumu wanaohakiki ujazaji na urudishwaji wa fomu hizo kwa usahihi.
5. Hakikisheni kuwa kuanzia sasa na kabla ya 2025 mnapata muafaka kuhusu Tume Huru ya uchaguzi na wasimamizi wake. Kama mkishindwa kuipata Tume huru ya uchaguzi tafadhali sana msiwasumbue na kuwarubuni wananchi kwa kuwapa matumaini ya uongo. Tunafahamu kuwa wanasiasa wanawatumia wananchi kama mtaji wao wa kuichumi wa kuwafikisha kwenye posho, mshahara, magari makubwa na kiinua mgongo bungeni na wapenzi wao wa viti maalum na kujipatia ruzuku. Na hii ndiyo maana walikuwa wakishiriki chaguzi za vyama vingi bila kujali Tume imekaakaaje.
Wanasema Tume ni mbaya kila siku lakini Tume hiyohiyo ilikuwa ikiwatangaza kushinda Ubunge. Naishukuru sana Tume safari hii kwa kuacha kuwatangaza hawa jamaa ili waufahamu ukubwa wa shughuli.
Tuwaache waliotangazwa kushinda nao wakafaidi kama vile nyie mlivyofaidi kwa miaka 10 kwa kutumia Tume ya aina hiihii.
Nitawashangaa wale walioshinda kama watasikiliza porojo za kuwaambia wasiende kupata mpunga bungeni, hata 2015 malalamiko yalikuwa hayohayo kwa Tume lakini walikwenda bunge kilafi pamoja na malalamiko ya Lowassa kuibiwa kura.
Kwakuwa wao safari hii wametemwa basi wanataka walioshinda wasiende bungeni. Huu ni utoto.
CUF walifanya hivyo mara nyingi bila kuzaa matunda yoyote. Wabunge wa upinzani wamekuwa wakisusia vikao vya bunge mara kadhaa lakini sikuona walichofanikisha sanasana kujinufaisha wao wenyewe kiuchumi.
Itakuwa ni kuwanyima fursa wabunge wa upinzani waliochaguliwa kama tutasema wasihuhudhurie pia bunge. Hata wakisusia hawana uzito wowote wa kubalidisha mambo zaidi ya kuwakosesha fursa yao ya kiuchumi, kisiana na kijamii.
Vyama vijipange upya kwa 2025 kwa kufanya yafuatayo:
1. Kueneza vyama vyao hadi vitongojini.
2. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanajiandikisha kwa wingi kwenye daftari la kupiga kura wakati utakapowadia.
3. Kuhakikisha kuwa wanachama wao na wapenzi wanakwenda kupiga kura wote siku ya kupiga kura.
4. Wahakikishe kuwa wakati wa kujaza fomu za kugombea kuna watu maalumu wanaohakiki ujazaji na urudishwaji wa fomu hizo kwa usahihi.
5. Hakikisheni kuwa kuanzia sasa na kabla ya 2025 mnapata muafaka kuhusu Tume Huru ya uchaguzi na wasimamizi wake. Kama mkishindwa kuipata Tume huru ya uchaguzi tafadhali sana msiwasumbue na kuwarubuni wananchi kwa kuwapa matumaini ya uongo. Tunafahamu kuwa wanasiasa wanawatumia wananchi kama mtaji wao wa kuichumi wa kuwafikisha kwenye posho, mshahara, magari makubwa na kiinua mgongo bungeni na wapenzi wao wa viti maalum na kujipatia ruzuku. Na hii ndiyo maana walikuwa wakishiriki chaguzi za vyama vingi bila kujali Tume imekaakaaje.
Wanasema Tume ni mbaya kila siku lakini Tume hiyohiyo ilikuwa ikiwatangaza kushinda Ubunge. Naishukuru sana Tume safari hii kwa kuacha kuwatangaza hawa jamaa ili waufahamu ukubwa wa shughuli.
Tuwaache waliotangazwa kushinda nao wakafaidi kama vile nyie mlivyofaidi kwa miaka 10 kwa kutumia Tume ya aina hiihii.
Nitawashangaa wale walioshinda kama watasikiliza porojo za kuwaambia wasiende kupata mpunga bungeni, hata 2015 malalamiko yalikuwa hayohayo kwa Tume lakini walikwenda bunge kilafi pamoja na malalamiko ya Lowassa kuibiwa kura.
Kwakuwa wao safari hii wametemwa basi wanataka walioshinda wasiende bungeni. Huu ni utoto.