Upinzani ujipange, Huyu hafai kupewa tena miaka mitano

Mimi sijawahi kuwa mkabila, ila ikitokea mtu yoyote wa kabila lolote anafanya mazuri, nitamkubali na kumpongeza.

Mwalimu Nyerere alituhusia tusimchague mtu hana sifa lakini ni kabila letu, ila pia tusimkatae mtu, ana sifa zote, tatizo "mkara", kumaanisha sio kabila langu.

Mambo ambayo rais Magufuli anayafanya yanaonekana with naked eyes, hivyo tusimpongeze kwa vile tutaonekana wakabila?.

Kiukweli nimeguswa sana na uchapakazi wa Rais Magufuli!. Je, kuna uhusiano kati ya kabila la mtu, na uchapakazi wake?. Je, 2020 kuna haja ya... - JamiiForums

P
Ukimpa kibarua jembe na kumpangia kazi ya kufanya kwa malipo huwa mkataba ule umekamilika endapo atatimiza kulima.
Endapo kalima sawa sawa ndo katimiza wajibu wake,na endapo kalipua ndo kashajihalalishia kutopata kibarua kingine.
Kumsifu kwa kumwambia wewe ni mkulima bora ,kuna uwezekano wa kuomba nyongeza ya malipo.
Sasa kinyume chake Mgema akisifiwa Tembo hulitia maji.
Hivi Magu anastahili sifa kwa lipi ambalo hatukumtuma ila yeye kalifanya kwa ihsani? na ndio kwa hilo tumpogeze?
 
Mkuu Swaga, ushauri wako ni mzuri kwasababu siku zote Umoja ni nguvu, ila una makosa ya kiufundi, wanaoamua kumuingiza mtu Ikulu sio wapinzani bali ni wapiga kura ambao ni wananchi.
Kama wananchi wanachotaka ni maendeleo na wananchi wenyewe wana macho na wanaona kinachofanyika, na pia wananchi hao wana masikio na wanasikia kwa masikio yao wenyewe, then October ni kazi ndogo tuu ya kukamilisha taratibu tuu za unachukua, unaweka...

Mimi niliuliza kama hiyo October kuna haja
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020? - JamiiForums
P
Ndiyo ,tuna macho tunaona sasa kwanini kila wanachokifanya mpaka watuonyeshe kwenye Tv!maendeleo huwa yanaonekana kwa macho, siyo kutulazimisha tuyaone kwenye Tv, ili hali hutaki wenzio nao waonekane.
 
Mkuu Swaga, ushauri wako ni mzuri kwasababu siku zote Umoja ni nguvu, ila una makosa ya kiufundi, wanaoamua kumuingiza mtu Ikulu sio wapinzani bali ni wapiga kura ambao ni wananchi.
Kama wananchi wanachotaka ni maendeleo na wananchi wenyewe wana macho na wanaona kinachofanyika, na pia wananchi hao wana masikio na wanasikia kwa masikio yao wenyewe, then October ni kazi ndogo tuu ya kukamilisha taratibu tuu za unachukua, unaweka...

Mimi niliuliza kama hiyo October kuna haja
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020? - JamiiForums
P
Hadi 2050 God bless our Presida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Swaga, ushauri wako ni mzuri kwasababu siku zote Umoja ni nguvu, ila una makosa ya kiufundi, wanaoamua kumuingiza mtu Ikulu sio wapinzani bali ni wapiga kura ambao ni wananchi.
Kama wananchi wanachotaka ni maendeleo na wananchi wenyewe wana macho na wanaona kinachofanyika, na pia wananchi hao wana masikio na wanasikia kwa masikio yao wenyewe, then October ni kazi ndogo tuu ya kukamilisha taratibu tuu za unachukua, unaweka...

Mimi niliuliza kama hiyo October kuna haja
Kwa Kasi hii ya Magufuli, kuna haja Kufanya Uchaguzi wa Rais 2020? - JamiiForums
P
Njaa mbaya, uteuzi umekwisha. Fanya kazi mkuu, muulize Kangi hawezi kusifia tena.
 
Ukiuliza wewe ndio basi tena! Hakuna mtu mwingine kusema kinyume na mawazo yako! Udikteta uchwara, unaopenda kuuliza kama namba moja anao kweli, umekuvaa. Mimi niseme na wewe useme! Paskali mwana wa Njaa ni nani hadi atusemee watz?
Kosa la kiufundi umelifanya wewe makusudi! Kwa wastaarabu wenye demokrasia ya kweli yenye utawala bora; hivyo na tume huru wakati wa uchaguzi, sanduku la kura ndilo linaamua nani atakuwa rais. Chaguo la wananchi linakuwa ndani ya sanduku. Jaribu kukumbuka sanduku la agano kwa Wayahudi! Wote waliliheshimu. Hakuna aliyelinajisi. Liliamua na kuhukumu kwa haki.
Vipaumbele vya wananchi na vya JPM wako ni tofauti sana! Wananchi wanataka katiba mpya, yeye kwake sio kipaumbele. Ananyoosha nchi bila rula( katiba). Kupinda ni lazima. Wote ni mashahidi ila tu kwa wale walioamua maksudi kujitoa ufahamu. Nchi imepinda vibaya sana katika kila sekta ya maisha. Tunayoyasikia ni mbwembwe tu za watawala na wapambe wao. Sheria ya takwimu ilimaliza kila kitu. Tunalishwa matango pori kila uchao!
Waziri alitangaza wenye corona 12. Kesho yake Bashite kaongeza mmoja kwa kumuumbua Mbowe ili kunusuru wakazi wake wa Dar yake. Waziri alikuwa hamjui huyo hiyo jana yake? Na rais naye sasa anajua ni hao 13 tu? Huyo waziri wake anayeumwa ni wa 10 kati ya hao 13? Au inatakiwa hao wananchi wanaomweka rais madarakani wajue tu hiyo namba ya bahati ya 13 tu? Matango pori ni mengi sana wakati wa masika( karibu na uchaguzi)!
Lakini kwa watz JPM ameishafanya hata nusu ya mazuri alokuwa amefanya Gaddafi kwa walibya tena bila ya ubaguzi? Vipaumbele vilitofautiana. Hata hapa vinatofautiana. Hiari yashinda utumwa. TWAWEZA wangekuwepo wakauliza ni wangapi wangetaka JPM aondoke kwa corona, ungejitia unafiki kushangaa jibu! Ndege, timu ya taifa hata ujio wa corona yenyewe umeona. Hujajifunza?
Stalini alisema ushindi wa kura unatokana na mhesabu kura na si mpiga kura! Ndio ukweli mchungu wa nec yetu yenye wasimamizi wa uchaguzi, wakurugenzi walokatazwa kutangaza wapinzani washindi!
Mwenye sikio na amekusikia...ubarikiwe...nimekuelewa sana kwenye kauli ya Stalin...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana, Africa tunahitji Rais mwenye busara kama JPM pigeni vigeregere mkizinguwa tunampatia miaka 10 zaidi mbele ainyooshe nchi hii kwa uozo uliokuwa umejengeka.
 
Wakuu nawasalimu kwa jina la aliye juu

Tumekuwa na huyu jamaa yetu kwa miaka mitano lakini hakuna jipya alilolifanya zaidi ya kuiingiza nchi kwenye chuki na mgawanyiko usio mithirika,ni wazi kuwa huyu bwana kwa anayotufanyia tukimpa tena miaka mitano tujue tumekwisha.

Ni rais mwenye kupenda kusifiwa na mwenye kutanguliza masirahi binafsi mbele,hana hata tone la huruma,viongozi wenzake wamekuwa na hofu dhidi yake,hawana maamuzi ya wao kama wao,ona Leo jinsi anavyoliweka taifa rehani kwa kuthamini uchumi huku akihatarisha afya za watu wake,ameweka sheria za kijinga dhidi ya Uhuru wa watu ,angalia huu ugonjwa unavyo uwa watu huko ngambo yeye huku kazuia taarifa za ugonjwa huu zisitolewe hafharani eti utalii utashuka,hizo fedha za utalii zina maana gani kwa raia millioni hamsini watakao kufa kwa uzembe wake ili tu upate watalii.

Rai yangu kwa vyama vya upinzani,musitangulize maslahi binafsi mbele ,naomba muungane mumutoe huyu anayenuka damu za watu,

covid 19 ni kipimo tosha kabisa kwa huyu kuwa hatufai pamoja na chama chake,let you unite to get back the lost freedom,hatufai ndo maana nchi inanuka damu,gharika linakuja hata kuwa na pakutokea.

Usiku mwema wapendwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Ungesema mapungufu yake katika kukabiliana na corona. Siyo unagusia nabhufafanui chochote.

Kuhusu maamuzi yake dhidi ya corona ni maamuzi sahihi ambayo nchi zinazoendelea inatakiwa zimuige. Kwa nchi zilizochukua uamuzi wa kuwafungia watu wake ndani kuna watu wanapata mateso hata zaidi ya wagonjwa wa corona.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom