nakubaliana nawewe,sasa tuingie kazini.
kususia si ndio tutakuwa tumewapa advantage?
Vijana ambao wametimiza miaka 18 tokea uchaguzi wa 2010 ni wengi mno sasa hichi chama kichakavu hakitaki hao kwasababu sio mtaji wao
Kabla ya kuwanyooshea vidole wengine jambo la kwanza kabisa ni Chadema kuandaa wagombea bora kwa kila jimbo na kata, mfano kata ninayoishi mimi mpaka leo sijaona mtu wa kuaminiwa kusimama kwenye udiwani mwaka 2015, sasa wakati ni huu.
Nawafahamu vyema Watanzania na akili zao. mwonekano tu wa mtu ni sehemu ya kuaminiwa au kama umewahi kushiriki shughuri za umma au kamati mbalimbali za maendeleo mtaani au katani. tuwe wakweli jamani kuna wagombea hawachaguliki.
Hakuna kitu kilichonisikitisha kwenye uchaguzi mkuu wa 2010 na mgombea Urais wa Chadema kuwa na posters chache mno na Chadema kuwadanganya watu kwamba eti vifaa vya kampeni vimekwama bandarini, uhuni huu haukubaliki na ujinga usijirudie tena, hakuna kampeni zisizokuwa na vifaa vya kampeni kwa ajili ya hamasa.
Labda ningeomba kuuliza tu kwenye hizi Chaguzi ndogo Chadema ilitowa kiasi cha pesa kwa kata zote kuwezesha kampeni na hamasa? naomba jibu sahihi kwenye hili.
hatujachelewa.Kazi ilishaanza,hapa tunaendeleza mapambano tu.