Upinzani sasa Tufanye nini?

Nimeyapenda mawazo haya:

Vyombo vya dola, polisi, usalama wa taifa, mahakama havitekelezi majukumu yake kama vyombo vya taifa badala yake vinafanya kazi kama matawi ya CCM. Lengo ni kuibeba/kuibakisha CCM madarakani.

Viongozi wa Upinzania ni lazima sasa kupambana na haya:

1. kupigania kuwepo kwa tume ya uchaguzi iliyo huru.

2.Kuhakikisha na kupiga kelele za kutosha kwa vyombo vya dola ili vianze kufanya kazi
kama vyombo vya nchi na sio kama vyombo vya chama.CCM

3.Kususia Changuzi zote kama mapendekezo hapo juu hayatafanyiwa kazi.

Baada ya kufanya vibaya kwenye changuzi za udiwani ndiyo mmeshtuka.

Hivi Ikulu pia ni chombo cha dola? Siku hizi CCM huwa wanafanyia vikao vyao pale. Mbona Chadema hamjawhi kusema lolote kuhusiana na hili?

Tovuti ya Ikulu nayo siyo chombo cha dola? Mbona imetapakaa picha za chaguzi za CCM lakini Chadema hamsemi chochote?

Mpaka Ikulu inatumiwa kama chombo cha CCM lakini nyie Chadema mko kimya tuu. Labda na nyie mkiingia Ikulu mtakuwa mnafanya hivyo.


napata shida sana na watu kama wewe,

Hivi unajua mtu kujiidentify to kama mwanachadema inamgharimu sana?unaweza ukawajua wagombea waambie sasa wajiweke hadharani?

naomba tunapoongelea kitu tupime pande zote,wagombea wapo ndoyo mnawajua,waambieni wajitokeze waanze kupimwa na wananchi?
Kumbuka wagombea wengi kama si mfanya bihashara ni mfanyakazi,sasa ajitambulishe leo maCCM watamuokoa,tusiwafananishe na wagombea wa CCM,waowanalinda sana.

Naomba tu endelea kuwatia moyo na kuwajengea ujasiri hiyo ndiyo kazi kubwa inayotakiwa.

unapokuja kwenye swala la hela,mungu wangu ivi umeshataka kujua gharama ya operation kwenye mkoa mmoja tu inagharimu shillingi ngapi?ukijua hili utajiuliza je Chadema wanarasilimali gani zinazowaingizia kipato?
halafu ndipo utafute kujua kila kata walipewa nini.

Ukishaona hivyo, jua watu hawako tayari kwa mabadiliko. Mtu ambaye yuko tayari kwa mabadiliko atakuwa tayari kwa lolote lile.

Suala la gharama ni la kujitakia tuu. Ziko njia bora na cheaper zaidi za kufikisha ujembe kwa wananchi badala ya hii mikutano ya hadhara ambayo so far mmekuwa mkifanya tokea miaka 1990s bila mafanikio.
 
Josephine, haya unadhani ndiyo yaliyosababisha upinzani kushindwa vibaya katika uchaguzi wa madiwani? Sidhani, nafikiri bado upinzani haujagundua mbinu makini ya kupata kura kutoka kwa wananchi. Hizi kampeni za majukwaani tayari mimi nilishazikataa. Nimezifanya sana mwaka 2005, nikiwa kada wa CCM na nilielewa what it means by kampeni za majukwaani na za nyumba kwa nyumba.

CHADEMA msipumbazwe na idadi kubwa ya watu wanaohudhuria kwenye mikutano yenu, halafu mkabweteka. Kampeni za ukweli ni zile ambazo CCM wamezigundua hivi sasa za nyumba kwa nyumba. Muone mtu personally na umashawishi akukubali, lakini kauli za jumla jumla za majukwaani hizi mtu anazisikiliza anazikubali lakini akifuatwa baadaye na mtu mwingine nyumbani, anashawishika kufanya vinginevyo.

Inafaa sasa CHADEMA wajifunze hii aina mpya ya kampeni, badala ya kutegemea idadi ya watu wanaojaa kwenye mikutano. Nimekuwa kada wa CCM kwa muda mrefu na nimepiga kampeni za CCM kwa muda mrefu, hivi visingizio vya mara polisi, mara sijui usalama wa Taifa au sijui tume ni kujipa moyo tu ili muonekane hamjashindwa sana, lakini ukweli ni kwamba strategy yenu ya kampeni bado si ya kutafutia ushindi.

Si lazima muige kila kitu kutoka CCM, mnaweza pia kubuni mbinu yenu nyingine lakini ambayo itakuwa ni constructive na si kutegemea hizi za majukwaani peke yake.

Ndiyo strategy aliyorumia Obama kushinda uchaguzi uliopita. Obama kama community organizer alitumbua the power of grass-roots campaigns. Tokea mwanzoni strategy yake ilikuwa sio kutafuta big endorsements kwenye mikutano ya hadhara but kujitambulisha kwa Wamarekani tena kwa kuanzia Iowa. Obama maintained that if he could win Iowa, it would generate enthusiasm and confidence throughout the rest of the country.

Na hivyo ndivyo inavyotakiwa kwa vyama vya upinzani hapa kwetu. Badala ya kung'ang'ania mijini wakajitambulishe vijijini kwanza. Wawaeleze wanavijiji watawafanyia nini kama wakiingia madarakani. Halafu siyo wanaenda kule na kuanza kutoa povu zito dhidi ya CCM. Wananchi wahusishwe zaidi, wapewe haki ya kusikilizwa, haki ya kuhoji, n.k.

Mtu anakuja kijijini kwangu na kuniambia kuwa mtoto wa kigogo fulani alikamatwa na madawa ya China. Ukishanimbia hivyo, so what? Mtu mwenyewe aliyekamatwa hata humtaji jina, unatarajia mimi kama mwanakijiji nifanye nini?
Kwanza huku kijijini kwetu bangi ni mboga ya kulia ugali tokea enzi za mababu zetu. If you want my vote tell me what you can do for me hapa hapa kijijini. Mambo ya mjini mkayamalize huko huko mjini.
 
Tafadhali,

usimfananishe Josephine na yeyote,mchukue kama alivyo na madhaifu yake,mkosoe,na mshahuru but never and i say never compare.
Haya 1st lady, leo huna cheo unatishia watu je ukipata si ndio mtazika watu kwenye garden za ikulu.
 
Ndiyo strategy aliyorumia Obama kushinda uchaguzi uliopita. Obama kama community organizer alitumbua the power of grass-roots campaigns. Tokea mwanzoni strategy yake ilikuwa sio kutafuta big endorsements kwenye mikutano ya hadhara but kujitambulisha kwa Wamarekani tena kwa kuanzia Iowa. Obama maintained that if he could win Iowa, it would generate enthusiasm and confidence throughout the rest of the country.

Na hivyo ndivyo inavyotakiwa kwa vyama vya upinzani hapa kwetu. Badala ya kung'ang'ania mijini wakajitambulishe vijijini kwanza. Wawaeleze wanavijiji watawafanyia nini kama wakiingia madarakani. Halafu siyo wanaenda kule na kuanza kutoa povu zito dhidi ya CCM. Wananchi wahusishwe zaidi, wapewe haki ya kusikilizwa, haki ya kuhoji, n.k.

Mtu anakuja kijijini kwangu na kuniambia kuwa mtoto wa kigogo fulani alikamatwa na madawa ya China. Ukishanimbia hivyo, so what? Mtu mwenyewe aliyekamatwa hata humtaji jina, unatarajia mimi kama mwanakijiji nifanye nini?
Kwanza huku kijijini kwetu bangi ni mboga ya kulia ugali tokea enzi za mababu zetu. If you want my vote tell me what you can do for me hapa hapa kijijini. Mambo ya mjini mkayamalize huko huko mjini.
Well said mkuu. Kwa kiasi kikubwa CHADEMA bado hawajagundua strategy ya kuichukua nchi. Na kama watafanya utani na mwaka 2015 wakashindwa kuchukua Ikulu, then they are gone. Watabaki kuwa historia kama wenzao NCCR na CUF. Kuna idara mhimu sana hazijatumiwa vizuri ndani ya CHADEMA, nazo ni idara ya propaganda na ile ya uenezi. Kama uenezi naona ndiyo kwanza kazi yake kubwa imekuwa ni kutoa taarifa za vikao vya viongozi wa chadema. Na ile ya propaganda imekosa ubunifu na sasa imebaki tu na kauli za ufisadi. Ni lazima mfike mahali mjifunza kusimama bila kutegemea mapungufu ya CCM. Semeni sera zenu ni nini na zitawanasuaje wananchi kutokana na umaskini mkubwa wanaoukabili.
 
Hoja ya kususia uchaguzi haina mashiko.Ni mpenzi sana wa mageuzi ya maendeleo na siasa,tunachotakiwa kuangalia upinzani siyo vita ni changamoto itakayofanya maendeleo yetu kwenda kwa kasi tunayoitaka,hivyo basi kama watu waelewa wa jamii yetu hii ya kitanzania ambayo chama tawala kinapenda kudanganya umma ni neno amani,sidhani kama kuna mtu asiyependa amani na ustaarabu.
Hivyo basi nini kifanyike?Vyama vya siasa viwe na vyomba vyake vya habari TV,magazeti na redio ili kumfikia mlengwa bila matatizo wala fujo za polisi.
Kama viongozi wa vyama vya upinzani au vyama vya siasa vitaweka kipaumbele katika hili basi sera zake zitaenezwa kilaini kwa kupitia vyombo vyake vya habari.
Vyama vya siasa visitgemee sana TBC,ITV au Channel Ten kupeleka ujumbe wake vyenyewe vikazane kuwekeza katika vyombo vya upashanaji habari.
 
Hoja ya kususia uchaguzi haina mashiko.Ni mpenzi sana wa mageuzi ya maendeleo na siasa,tunachotakiwa kuangalia upinzani siyo vita ni changamoto itakayofanya maendeleo yetu kwenda kwa kasi tunayoitaka,hivyo basi kama watu waelewa wa jamii yetu hii ya kitanzania ambayo chama tawala kinapenda kudanganya umma ni neno amani,sidhani kama kuna mtu asiyependa amani na ustaarabu.
Hivyo basi nini kifanyike?Vyama vya siasa viwe na vyomba vyake vya habari TV,magazeti na redio ili kumfikia mlengwa bila matatizo wala fujo za polisi.
Kama viongozi wa vyama vya upinzani au vyama vya siasa vitaweka kipaumbele katika hili basi sera zake zitaenezwa kilaini kwa kupitia vyombo vyake vya habari.
Vyama vya siasa visitgemee sana TBC,ITV au Channel Ten kupeleka ujumbe wake vyenyewe vikazane kuwekeza katika vyombo vya upashanaji habari.
Hela ya radio na TV imetumika kujenga nyumba ya Slaa.
 
Na sie tujipange kuwaelimisha wananchi juu ya haki zao na uelewa wa mabadiliko. hatuwezi kuendelea kama chama kilichopigania haki, usawa na maendeleo leo hii kugawa pesa kama njugu kwenye chaguzi zake. hii ni lazima kujenga uelewa au kuchagua viongozi bora kuanzia kwenye mashina na matawi yetu kila wilaya ili kujenga uelewa huu kwa wananchi. tusishabikie shindi zetu za chaguzi kwa rabsha, tutaeleweka vibaya kwa wananchi kama wenye fujo. Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika!
 
Siseme upinzani sema Chadema maana nyie mshasema ni upinzani rasmi bungeni na hamtambui wengine.
 
Nimeyapenda mawazo haya:

Vyombo vya dola, polisi, usalama wa taifa, mahakama havitekelezi majukumu yake kama vyombo vya taifa badala yake vinafanya kazi kama matawi ya CCM. Lengo ni kuibeba/kuibakisha CCM madarakani.

Viongozi wa Upinzania ni lazima sasa kupambana na haya:

1. kupigania kuwepo kwa tume ya uchaguzi iliyo huru.

2.Kuhakikisha na kupiga kelele za kutosha kwa vyombo vya dola ili vianze kufanya kazi
kama vyombo vya nchi na sio kama vyombo vya chama.CCM

3.Kususia Changuzi zote kama mapendekezo hapo juu hayatafanyiwa kazi.

4. Kuvuruga chaguzi zote zitakazofanyika mpaka hayo mapendekezo hapo juu yafanyiwe kazi.
 
4. Kuvuruga chaguzi zote zitakazofanyika mpaka hayo mapendekezo hapo juu yafanyiwe kazi.

Mkuu wangu, hiki ndicho wanachoomba kitokee (with a smile) ili wapate ground ya kuifuta CDM kisheria, na kudhibiti harakati za kisiasa. Tizama sasa wameanza kudeploy mpaka Jeshi la wananchi (zile ni salam tu)

I know CDM is better than that. Ni wakati sasa wa kutumia Constitutional Litigation ili kupambana nao
 
Mtu anakuja kijijini kwangu na kuniambia kuwa mtoto wa kigogo fulani alikamatwa na madawa ya China. Ukishanimbia hivyo, so what? Mtu mwenyewe aliyekamatwa hata humtaji jina, unatarajia mimi kama mwanakijiji nifanye nini?

...Kwi kwi kwi kwi...
 
  • Thanks
Reactions: EMT
...Kwi kwi kwi kwi...

Mbona wacheka? Kama una uhakika na huyo mtoto wa kigogo kakamatwa china na madawa ya kulevya na unadai umezipata hizo moja kwa moja kutoka chini si uniambie tuu mie mwanakijiji jina la huyo mtoto na jina la huyo kigogo? Kwa nini kunificha halafu hapo hapo unataka kura yangu?
 
Kuna Kanuni moja ya sayansi jamii inasema hivi
''Usitumie MABAVU kupambana na mtu mwenye nguvu zaidi yako bali tumia AKILI''

*CCM inatumia PESA, VITISHO na DOLA kama sehemu ya mabavu yake ili kuendelea kukaa madarakani. Na itaendelea kufanya hivi siku zote.

*Kwa kuwa upinzani hauna nguvu za kimabavu, inabidi wakazane kutumia akili zao katika mambo haya;

1/KUTAFITI(Chanzo, Sababu, Ushahidi)

2/HOJA(kuhoji, kupinga, kukosoa, kupendekeza, kuunga mkono, kushinikiza)

3/MIJADALA(Midahalo, kongamano, warsha)

4/HARAKATI(Mikutano ya hadhara, Maandamano, Matamko, Kampeni, Migomo, Matangazo, Semina)


Maneno kuntu
 
Back
Top Bottom